MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

kikwete-libya

Hivyo ndivyo anavyoelekea kusema First Lady wa Tanzania,Mama Salma Kikwete alipokuwa akisalimiana na Rais wa Libya,Muamar Gaddafi hivi karibuni. Anayeshuhudia ni Rais wa Tanzania,Jakaya Mrisho Kikwete.

Rais Kikwete alikuwa nchini Libya kuhudhuria Mkutano wa 13 wa wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika.Rais Gaddafi ndiye Mwenyekiti wa umoja huo hivi sasa.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

vijana-jazzbcKama unaishi katika dunia hii hii tuijuayo sote,basi bila shaka umeshawahi kusikia kuhusu ugomvi kati ya mke wa kaka na dada zake kaka.Kwa maneno mengine ugomvi kati ya fulani na wifi yake au wifi yao.Mimi nimeshawahi kusikia na pia kuona mtu na wifi yake ambao hawapikiki chungu kimoja.Kila kukicha “kesi za ukoo” zilikuwa haziishi.Amani hakuna,kila mmoja anadai kuwa malikia wa boma.

Je ni kwanini huwa kunatokea ugomvi ugomvi hivi kati ya mtu na wifi yake au wifi zake?(sio wote lakini.Wapo mtu na wifi yake au zake wanaoiva kupita maelezo) Hili swali pengine limeshaulizwa mara milioni kidogo na bado majibu yasipatikane.Tunaweza kujaribu kutafuta majibu mapya kama tunataka.Mimi sitochangia.Sijui.

Pamoja na hayo, miaka kadhaa iliyopita bendi ya Vijana Jazz walijaribu kulijibu swali hilo katika kibao chao maarufu kilichoitwa Wifi Zangu. Aliyeongoza mashambulizi alikuwa mwanadada Kida Waziri.Nakumbuka kuwaona Vijana Jazz wakiuliza swali hili pale katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro enzi hizo.Kwa kweli ilikuwa ni burudani ya aina yake.

Nakuomba usikilize kibao hiki kisha,baada ya burudani, tafakari kisha jaribu kutupa majibu yako.Kwanini unadhani huwa sometimes inatokea rabsha kati ya mtu na wifi yake?Nani alaumiwe?Nakutakia weekend njema.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

** Wimbo huu sio original.Ni remake tu.Pata burudani.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

ijumaa-front-pgbc

Kwa undani wa vichwa hivyo vya habari, bonyeza hapa au jipatie nakala yako mitaani.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

mbilia-spikabc

Bila shaka tunakubaliana kwamba ukiongelea wanamuziki waliowahi kutamba barani Afrika na duniani wakiliwakilisha bara la Afrika,huwezi kumuweka pembeni mwanamama Mbilia Bel kutoka DRC(zamani Zaire).

Hivi karibuni alikuwepo nchini Tanzania ambapo alipata nafasi ya kuwaburudisha ‘waheshimiwa” pale Dodoma katika viwanja vya Bunge.Naamini waheshimiwa waliburudika zaidi kwani lets face it wengi wao walikuwa vijana zaidi enzi Mbilia Bel alipokuwa akitikisa majukwaa kwa nyimbo zake motomoto kama vile Nadina, Nairobi nk. Unaweza kujikumbukusha kidogo wimbo Nadina kwa kubonyeza player hapo chini.

Pichani ni Mbilia Bel akilisakata rumba na Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania,Samweli Sitta.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Photo/Jube Tranquilino

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

jose_juma_naturebc

Mojawapo ya mambo ambayo yanaweza kukufurahisha kama unapenda muziki kutoka Afrika Mashariki ni pale wasanii kutoka nchi zinazounda Afrika Mashariki wanapoamua kushirikiana katika kazi zao. Mifano ipo mingi kuonyesha jinsi gani mipaka iliyowekwa na mtawala wa enzi hizo inaweza kuvukwa japo kwa kutumia muziki.

Nimewahi kuandika siku za nyuma kwamba wakati viongozi wetu wanasuasua katika kukamilisha muundo wa jumuiya ya Afrika Mashariki(ukiniuliza mimi nitakwambia ni kwa sababu kila mmoja anaweka mbele maslahi binafsi badala ya faida nyingi za muungano makini) wasanii wao wameshavuka kizingiti hicho.Wanashirikiana.

Miongoni mwa mifano ya ushirikiano huo ni huu wa Juma Nature akimshirikisha Jose Chameleon(Uganda) katika wimbo unaokwenda kwa jina Mikiki Mikiki. Kama ujuavyo hawa wote ni ‘majina makubwa” katika muziki wa ukanda wetu. Wanaposhirikiana tunategemea kitoke kitu makini.Nakuomba uwe muamuzi.Sikiliza Mikiki Mikiki hapo chini.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Picha na Muziki kwa niaba ya GetMziki.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

hasheem

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

hasheemt1bc

Kama uliwahi kutabiri kwamba siku moja mtanzania Hasheem Thabeet atakuja kuchezea katika ligi ya mpira wa kikapu ya NBA, unayo sababu ya kujidai kwani utabiri wako umetimia jioni hii(saa za New York).Hasheem Thabeet amechaguliwa kujiunga na timu ya Memphis Grizzlies yenye makao yake makuu huko Memphis katika jimbo la Tennessee nchini Marekani.

Hasheem anakuwa mtanzania wa kwanza kufikia hatua hiyo.Kama nchi tuna kila sababu ya kufurahia mafanikio yake na kumtakia kila la kheri. Hivi sasa anakuwa,bila shaka, “balozi” wetu katika ulimwengu wa michezo hususani mpira wa kikapu. Kila la kheri Hasheem.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

michael-jackbc

Habari za uhakika ambazo BC imezipata zinapasha kwamba Mfalme wa muziki wa Pop,Michael Jackson,amefariki dunia huko Los Angeles nchini Marekani mchana huu.

Mfalme huyo wa Pop alikimbizwa hospitali mchana huu baada ya kuzimia akiwa nyumbani kwake maeneo ya Holmby Hills huko Los Angeles alizimia baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo kitu ambacho kinasemekana ndicho kilichomaliza uhai wa Michael Jackson katika Kituo Cha Afya cha UCLA ilipotimia saa nane na dakika ishirini na sita (2:26pm) kwa saa za Los Angeles.

mj-jackson_1972b

Michael Jackson akiwa na umri wa miaka 13

Michael Jackson alizaliwa huko Gary,Indiana nchini Marekani tarehe 29 August mwaka 1958 akiwa ni mtoto wa saba kati ya watoto tisa wa Joseph na Katherine Jackson(wazazi wao). Alianza  kujishughulisha na masuala ya muziki akiwa na umri wa miaka minne(4) katika kundi la familia lililojulikana na kutamba kama Jackson 5(pichani).

jackson5

Kabla ya kufikwa na mauti,Michael Jackson, alikuwa anapanga kufanya show za mwisho huko London mwezi July mwaka huu.Tiketi kwa ajili ya show hizo zilikuwa zimeshakwisha(sold out)!

garyindianabc

Pichani ni nyumbani alipozaliwa Michael Jackson na ndugu zake huko Gary,Indiana nchini Marekani.Nilipiga picha hii December mwaka 2006 nilipotembelea maeneo hayo ili kujionea alipozaliwa Mfalme wa Pop.Mtaa ilipo nyumba hii unaitwa Jackson Street.

BC inapenda kutoa pole kwa wote ambao wameguswa kwa njia moja au nyingine na msiba huu.Tunaamini kwamba Michael Jackson alikuwa sio tu mwanamuziki maarufu ulimwenguni bali muziki wake uligusa wengi.Wengi walicheza,wanacheza na wataendelea kucheza miziki yake.

Hapa chini unaweza kusikiliza simu iliyopigwa kutoka nyumbani ikwake kwenda kwa watu wa huduma za dharura(Emergency)

Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

hasheem-thabeetb

Kwa mapana na marefu,jina la Hasheem Thabeet litatawala vichwa vya habari wiki hii.Swali au maswali ambayo wengi wanajiuliza ni je Hasheem Thabeet atajiunga na timu gani?

Mambo mengi yanasemwa kuhusu Hasheem.Wapo bado wanaoendelea kusema kwamba bado hayupo tayari kwa sababu alianza kucheza mpira wa kikapu “ukubwani’! Pamoja na hayo,wote wanaosema hivyo wanakubali pia kwamba Hasheem ataleta “impact” kubwa katika NBA.Wapo ambao wamefikia hata kumbeza kwamba hatoweza kutamba kama ilivyokuwa kwa Mzaire Dikembe Mutombo na badala ya yake atakuwa kama Msenegali Mouhamed Sene (Mo Sene) ambaye kimsingi hafanyi vizuri katika NBA kama alivyotarajiwa.

Waache waseme.Kwetu sisi muhimu ni kwamba kijana wetu atakuwa mtanzania wa kwanza kucheza katika NBA. Ni matumaini yetu kwamba Hasheem atafungua milango kwa wengine wengi ambao kupitia kwake wataamini kwamba “inawezekana”.Binafsi naamini Hasheem atafanya vizuri.Cha msingi ni kwamba ni lazima awe msikivu kwa makocha wake,wachezaji wenzake na daima azingatie mazoezi na kujiweka mbali kidogo na “mambo ya ujana”.

Watabiri wa mambo wanasema kuna uwezekano mkubwa  kwamba Hasheem atajiunga na Memphis Grizzlies ingawa yeye mwenyewe inasemekana hangependelea sana.Je atajiunga na timu gani basi? ESPN wataonyesha zoezi hili. Tizama ratiba ya hapo ulipo.Kwa sasa mtazame Hasheem na wenzake ambao ndio “wapo juu” katika pick ya mwaka huu.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

shaa2bc

Kama unafuatilia Bongo Fleva kwa makini bila shaka hivi sasa umeshalisikia jina la Sarah Kaisi au Shaa (pichani) kama ambavyo anajulikana kwa mashabiki na wapenzi wa B Fleva.

Shaa ameingia kwenye game kwa kishindo.Uwezo wake wa kumiliki jukwaa,kuimba na kwa ujumla kukidhi haja ya mashabiki wa muziki huo wa kizazi kipya,ndivyo vitu ambavyo vinamfanya azidi kupanda chati na hivyo kuungana na wasanii wengine wa kike ambao wanafanya vizuri.

Hivi sasa anatamba na nyimbo zake Zamu Yangu na Pambazuko huku akiwa anapika kitu kingine studio ambacho mwenyewe anasema ni zawadi aliyopewa na Judith Wambura aka Lady Jaydee.Tunasubiri.

Leo tunao wimbo wake Pambazuko. Katika wimbo huu amemshirikisha msanii maarufu wa B Fleva,Ambwene Yessayah au AY. Usikilize. Kama kawaida maoni yanakaribishwa(ila jitahidi kutoa maoni yanayojenga badala ya kubomoa au kuonyesha chuki na dharau).Umeupenda wimbo? Unasemaje.Shaa atazidi kushika chati?Karibu.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

shaa1bc

Shaa on stage!

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • E-mail this story to a friend!
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page