Kwa mpenda soka ya Tanzania yeyote yule, hususani mnamo miaka ya themanini,jina Lawrence Mwalusako sio geni hata kidogo. Alikuwa sio tu kipenzi cha wapenda soka bali beki wa kutumainiwa wa timu zote alizowahi kuchezea, zikiwemo Waziri Mkuu Dodoma, Pan African, Yanga na timu ya taifa,Taifa Stars. Ndio maana yanapotajwa majina ya wachezaji soka nchini Tanzania waliowahi kuwika na jina la Mwalusako likakosekana,wadau wa soka,wanaoijua vyema historia ya soka la Tanzania,watakuambia wazi,something is missing.

Lawrence Mwalusako ni wa sita kutoka kushoto waliosimama.
Waliosimama kutoka kushoto: Marehemu Daktari wa timu Peter Manyika,Meneja John Manongi,Abeid Mziba “Tekero”,Athumani China,Yusuf Ismail Bana,Lawrence Mwalusako,Said Mrisho,Edgar Fongo,Isihaka Hasan,Golikipa Joseph Fungo,Kocha Mwinda Ramadhan.
Waliochuchumaa kutoka kushoto: Marehemu Lucias Mwanga,Rashid Idd Chama,Moshi Majungu,Allan Shomari,Ali Mchumila,Freddy Ferix Minziro,Abubakar Salum “Sure Boy”
Picha hii ilipigwa Mwaka 1987 uwanja wa taifa wakati wa mechi ya premier kati ya Yanga na Maji Maji.
Safari ya Mwalusako katika medani ya soka inaanzia kule Kyela mkoani Mbeya alipozaliwa mnamo mwaka 1960.Tulipofanya naye mahojiano hivi karibuni,Mwalusako ameongelea mambo mengi yakiwemo mtazamo wake wa soka la bongo hivi sasa,washambuliaji aliokuwa anawaheshimu,ushauri kwa wanasoka chipukizi nk.Pia anagusia jinsi “juju” ilivyo katika timu kubwa na pengine hata zile ndogo. Fuatana nasi katika mahojiano haya ambayo hata yeye mwenyewe anakiri,hajawahi kufanya na chombo chochote cha habari duniani akiwa kama mchezaji na hata baada ya kustaafu. Hivi sasa yeye ni Corporate Affairs Manager wa kampuni ya Sumaia Group Tanzania.Anaishi Dar-es-salaam.
BC: Unaweza kukumbuka wakati ulipokuwa mdogo ni nani alikuvutia katika mchezo wa soka? Kulikuwa na mtu yeyote maalumu ambaye ulimuona kama role model wako katika soka?
LM: Mimi nimekuwa mpenzi wa timu ya Yanga tangu mdogo. Hivyo basi nilikuwa navutiwa sana na wachezaji wote wa Yanga hasa Maulid Dilunga na Sunday Manara. Kwa upande wa timu ya Simba, nilikuwa navutiwa sana na uchezaji wa Haidari Abeid na marehemu Willy Mwaijibe. Willy Mwaijibe alikuwa ni home boy wangu na akija likizo nyumbani nilikuwa nabahatika kuwa naye kwani tulikuwa tunatoka kitongoji kimoja. Willy alikuwa ni role model kwangu kwani alikuwa anatoa demonstration ya uchezaji mpira katika kiwango cha kimataifa. Alinifanya niupende mpira sana kwa sababu wakati huo yeye alikuwa anasoma secondary school huku akichezea Simba Sports club. Ila hakuweza kunishawishi nibadilike kuwa mpenzi wa timu ya Simba.
BC: Je wazazi wako waliyachukulia vipi mapenzi yako ya kucheza soka?
LM: Wazazi wangu walipenda sana niwe na soma hasa mama yangu.Alikuwa ananikataza kucheza mpira wakati niko shule ya msingi. Hata hivyo kwa sababu alijua kuwa nafanya vizuri shuleni aliniruhusu kucheza chandimu baada ya masomo hapo kijijini kwetu. Sikuweza kuchezea timu ya shule ya wakati nasoma primary school kwa sababu nilikuwa mdogo sana pamoja na kwamba wengi walitabiria kuwa nitakuwa mchezaji mzuri wa mpira wa miguu nikikua.
BC: Mbali na soka uliwahi kucheza aina zingine za michezo? Kama ndio ikawaje basi ubobee zaidi kwenye soka?
LM : Soka ni mchezo unaopendwa sana hapa duniani. Hata vijijini utaona vijana wengi wanajishughulisha na mchezo wa mpira wa miguu kuliko michezo mingine yoyote. Katika ujana wangu nilibahatika kuupenda mpira kwa sababu kaka zangu wengi wa kijijini walikuwa wanacheza mpira katika kiwango kikubwa sana. Kuna baadhi ya wachezaji wengine wa kijijini walifanikiwa kuchezea timu kubwa kama vile Marehemu Yusufu Ambewne (CDA) na Marehemu Awidson Mwafongo (Maji Maji) ukiachia mbali mrehemu Willy Mwaijibe. Mpira wa miguu huwakutanisha watu pamoja na hujenga mahusiano mazuri miongoni mwa wachezaji.

Lawrence Mwalusako alivyo hivi sasa.
BC : Mchezo wa soka katika bara la Afrika ikiwemo Tanzania huwa imetawaliwa sana na imani za kishirikina.Unaweza kutuambia kidogo ni kwanini na ilikuwaje enzi zako ulipokuwa unachezea vilabu vikubwa kama Pan Afrika na Yanga?Kuna tukio lolote la “juju” unalolikumbuka?
LM : Katika nchi nyingi zinazoendea hapa duniani utaona kuwa watu wake wanatawaliwa na imani za kishirikina tangu enzi na enzi. Sio tu kwenye maswala ya michezo, ni katika masuala yote ya kijamii. Hizo imani zimejengeka ndani ya mioyo ya kila jamii. Hata kwenye michezo, watu wamejenga imani za kishirikina. Timu nyingi za Tanzania huwa zinaamini kuwa pamoja na kuwa na wachezaji wazuri, ushindi wa timu hauwezi kupatikana bila juju kuwepo.Pan Africa na Yanga ni timu ambazo nimezichezea na ni timu ambazo zina imani na juju kuwa ni mojawapo ya nguzo ya ushindi. Kwa sababu mchezaji ni mwajiriwa katika timu hizo analazimika kufuata kanuni na taratibu za uendeshaji mpira kwenye klabu. Hata hivyo kitu cha msingi katika kuleta ushindi kwenye timu ni kuwa na wachezaji wazuri wenye kufuata maadili ya mchezo wa mpira wa miguu na kufanya mazoezi ya nguvu. Sijawahi kuona viongozi wa timu hizi wakiwaamuru wachezaji kukaa bila kufanya mazoezi ya nguvu huku wakitegemea juju kupata ushindi. Mechi kati ya Yanga na Simba hutawaliwa sana na imani za ushirikina kiasi cha watu kushinda makaburini na kusoma dua siku nzima kabla ya mechi. Kuna kipindi hata wachezaji hawapati nafasi ya kulala usingizi kwani usiku kucha mnaamshwa na kila aina ya watu wakidai tunakuja kusoma dua.
BC : Kabla ya kuingia uwanjani katika mechi kubwa kwa mfano kati ya Simba na Yanga ulikuwa unajiandaa vipi kisaikolojia huku ukijua fika jinsi mashabiki wa timu yako wanavyoutamani ushindi?
Page 1 of 6 | Next page