TUMESHINDWA!

Pichani Raisi Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na wachezaji wa Taifa Stars na makocha wao alipowatembelea kambini kwao katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar hapo juzi.

Pamoja na kuungwa mkono na kila mtanzania, timu yetu ya taifa ya soka, Taifa Stars, imeshindwa kututoa kimasomaso katika iliyokuwa kampeni nzito ya kutaka kutupeleka nchini Ghana hapo mwakani kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika.

Matokeo ni kwamba Taifa Stars imechapwa goli moja kwa bila (1-0) na timu ya taifa ya Msumbiji,(Mambaz). Kwa maana hiyo kampeni zetu kuelekea Ghana ndio zimefikia kikomo kwa mwaka huu.

Unadhani nini kimetokea? Kwa maoni yako kwanini Taifa Stars imeshindwa? Nini kifanyike kwa siku za mbeleni? Unauongelea vipi utaratibu mzima wa shirikisho la soka la Tanzania (TFF) katika uuzaji wa tiketi za mchezo wa Taifa Stars na Msumbiji? Ungepata nafasi ya kumhoji kocha mbrazili wa Taifa Stars, Maximo au raisi wa shirikisho la soka la Tanzania, Leodgar Tenga, ungependa kumuuliza swali/maswali gani? Tunaomba maoni yako.

Page 1 of 3 | Next page