
Iwe ni uchaguzi, mechi kubwa ya mpira au chochote kile chenye mvuto au gumzo la kitaifa, Sheikh Yahya Hussein (pichani) atakifanyia utabiri bila kusita. Kitu chochote kikitokea pia iwe ni ajali mbaya, mafuriko nk, Sheikh Yahya atakitolea maelezo pia akiweka sababu za kutokea kwa kitu au tukio hilo. Hivi leo anabakia kuwa mnajimu au mtabiri maarufu kupita wote nchini Tanzania. Amekuwa akifanya hivyo kwa miaka chungu mbovu mpaka hivi sasa.
Alizaliwa mwaka 1932 huko Bagamoyo kwa wazazi wakimanyema. Alipata elimu yake ya awali katika shule ya Al-Hassanain Muslim School jijini Dar-es-salaam. Baada ya hapo alikwenda visiwani Zanzibar alipojiunga na chuo kilichojulikana kama Muslim Academy kilichokuwa chini ya Sheikh Abdallah Swaleh Al-Farsy aliyekuwa Kadhi Mkuu wa Zanzibar wakati huo. Baada ya kuhitimu alielekea nchini Misri alipoendelea kusomea masuala ya dini katika chuo kikuu cha Al-Azhar kilichopo Cairo.
Alirejea nchini mnamo miaka ya mwanzoni ya 60 ambapo alianza kazi yake ya utabiri . Sheikh Yahya Hussein ndiye mtabiri wa mwanzo kueneza utabiri wa kila siku katika magazeti mbalimbali ya Afrika Mashariki enzi hizo. Jina lake lilivuma zaidi alipokuwa akitoa utabiri kupitia radio kuhusu mashindano ya mpira kati ya nchi tatu za Africa Mashariki yaliyojulikana kwa jina la Challenge Cup au Gossage Cup.
Feedback / Comments
125 Responses to “SHEIKH YAHYA HUSSEIN.”
Leave a Reply


Kweli kabisa, watu wengi wanamtegemea kwa ajili ya uchawi tuu. utabiri ni cover up..
Sidhani kama kuna haja ya kuamini kila kitu anachokisema huyu bwana ila kwa vile sisi waswahili tunaamini sana nguvu za giza bado ataendelea kupata wateja! Hakuna ukweli katika haya mambo….watu wanaojua theory of probability wanajua anafanaya kitu gani!
Mh! Kwa jina la Yesu Toka! Ushindwe na ulegee, ukaangukie baharini umezwe na Nyangumi!(joke)
Kila la kheri ktk shughuli zako Shekhe(niliona mahojiano yako kwenye Luninda mwezi wa 4), naamini ni kipaji kamavilivyo vingine na umejaaliwa na mwenyezi Mungu.
Kuna kutabiri na kukisia, nadhani Sheikh anafanya hilo la pili zaidi.
Huwa naangalia sana mahojiano yake pale Channel Ten, huwa naona “ananiuzia chai tu”. Huwezi ukasema “Tarehe fulani ama jua litawaka ama mvua itanyesha” halafu ukauita utabiri, huko ni kukisia na hata mdogo wangu pale nyumbani ana kipaji kikubwa sana cha kukisia.
Lakini kwa sababu ni namna fulani ya kusukuma siku mbele kwa watu fulani fulani, nampa big-up Sheikh.
Bob hii kali mkuu.Natabiri utafanyika uchaguzi wa uraisi na wabunge mwana 2010.
Alishatabiri kifo chake?.Anyway nampa shavu
Natabiri Bongo Celebrity wataweka post nyingine baada ya hii!
Unabisha?
Natania tu , usichukie mpenzi wa watabiri!
BC wamemaliza kazi .
Au?:-)
Jamani mbona comment yangu imetolewa? au kisa sikuweka maneno mengi ya kumpamba na kusema “mchawi tu”….Nway kama mtu wa pili alivyosema maana nilikuwa wa kwanza ….Mchawi tu hana lolote
Sheikh yahaya ni mtu muhimu sana,profile yake sio tu east africa mpaka mbele huko alishatabiri vitu vikawa kweli.haya mambo yapo jamani someni histry ,encyclopedia inaeleza vizuri sana.Utabiri sio kubahatisha ni calculations (kucheza na namba) wanasema namba ni uchawi mkubwa kuliko kitu kingine.Mi nampabig up kubwa nilishawahi kumtembelea mara mbili hivi ,habahatishi ..Ila anachoniboa ni kutembea peku ndo mana watu wanasema mwanga..
Big kubwa shekh
Colin umenichekesha mpaka basi na kutembea peku. hivi ni kweli?? mi naomba siku nyingine ukimtembelea muulize kwanini anatembea peku? au mwambie akutabilie akiwa amevaa viatu…lol!!
kama anacheza na namba basi kasoma ipasavyo nampa big up sana cause hiyo shughuli inampa kukaa mjini ila hilo la kukaa bila viatu linanitia wasiwasi ila labda ni mazoea tu naomba atabiri siasa ya nchi hii inapoelekea cause napatwa na wasiwasi sana.big up sheikh kaza buti babu.
si wabongo wabishi mno.
Hivi kipaji huwa kina mrithi? Kama ndio je Mrithi wake ni nani? Kama hapana mnaomtegemea kiutabiri mtafanyaje?
Naona tumeshamgundua mchawi na wateja wake wanajitokeza…Pamoja
Hebu nisaidie na bahati yangu.Na nataa unitabilie kuhusu maisha yangu na nini natakiwa kufanya kwani maisha yangu huwa nna mtisha yakwamba sikutafika ambapo nataraji maitaji yangu yatatimika.Tafathari nipigie hesabu ya jina langu ili unitumie majibu.Unaweza kunitumia majibu kupitia simu ya rununu 0724038264.Asante kwa mda wako.
Nadhani anajaribu zaidi kuelimisha jamii kwa kupitia utabiri wake
Ispokuwa watu wenge hawaelewi nini anafanya
Jamani waswahili leo utabiri mnauita uchawi, kwa sababu ni utabiri umesemwa kwa kiswahili. Lakini ingekuwa kwa kiingereza mngemsifia sana kuwa ni kazi nzuri, kazi ya utabiri au unajimu inafanywa duniani kote sio Tanzania au Africa tu. Na watu wengi wanawatumia hao wanajimu au watabiri katika mambo yao, kuna wengine wako addicted kabisa hawafanyi kitu mpaka wawaulize wanajimu wao, tena watu maarufu hasa.
Ni kazi na biashara pia ndio maana hata kwenye website kama ya Yahoo, na msn, kuna kurasa za utabiri au unajimu (HOROSCOPES). Ndio hizo hizo zinatolewa magazetini kama nyota za kondoo, punda, nge na sijui nini. Na Wachina nao wana design zao za nyota kama mbwa, mbuzi, nyoka na kadhalika. Sasa sio kitu cha ajabu au ni kazi ya ajabu hayo mambo ya unajimu.
Ila ni juu ya mtu kuamua kufuata mambo hayo au kutoyafuata, kusoma horoscopes au kutosoma, wengine wanasoma for fun wengine ndio hivyo tena. Cha msingi ni kujua duniani malengo yako ni nini na wajibu wako kama mwanadamu ni nini.
RAHA RAHA UTAMU, ENDELEYAH MWANAUME, WHY? KWANINI? MBONA WATU WANAHOJI SANA KUHUSU UTABIRI WA SHEIKH, HICHO NI KIPAJI TU, NDIO NI KIPAJI KATIKA UJASILIAMALI, HATA MIMI HUWA NATABIRI, NGOJA NIWAPE UTABIRI WANGU KWA MWAKA 2008 1. UTAKUWA MWAKA AMBAO REDIO NYINGI ZITATANGAZA MATANGAZO YA KONDOMU, BIA, NA VIFO. WATU HAWATACHOKA KUNYWA BIA. RAIS ATAKUWA ANATOA HOTUBA SEHEMU MBALIMBALI ATAKAKO TEMBELEA, HAKUTAKUWA UCHAGUZI MKUU WA RAISI, ANYWAY KATIKA UPANDE WA SOKA, TIMU YA SIMBA ITAENDELEA KUITWA WEKUNDU WA MSIMBAZI. HAYA ATAKAYEBISHA NA ABISHE. KILA MTU ANAYO HAKI YA KUELEZA MAONI NA KUPASHWA HABARI KWA MUJIBU WA KATIBA. WENU KATIKA UTABIRI…..WAKUVWANGAVUNGA
I want to know the telephone number for Sheikh Yahya because I want to ask something
huyu mzee mi ananitisha
NAMPOGEZA SANA SHEIKH YAYHYA BIN HUSSAIN KWA YOTE ANAYO YAELEZEA KILA MARA. UTABIRI WAKE KWELI HAUNA SHAKA WALA KUTILIWA DOSARI.
HONGERA SANA TENA SANA SANA,,
JAMBO MOJA TUU NDIO LANIPA SHAKA NALO NI LA KUHUS ( FIMBO YA AJABU) NATUMAI SHEKHE ATANIELEWA,
NAMTAKIA DAIMA SWIHA NJEMA NA AENDELEE DAIMA KUTUPA MANUFAA YAKE YA HEKMA NA TAADHIMA,,
YOTE TISA KUMI UNAPOSOMA QURUAN TUKUFU TU MIE HOI SIJAONA KUSEMA KWELI YANI NIKIONA TU SHEKHE YAHAYA BIN HUSSEIN ANASOMA QURUAN YANI HUWA NATULIA KAMA MAJI YA MTUNGINI KWA USOMAJI WAKE HADI NATETEMEKA MASHALLAH UMEJAALIWA WIPAJI NA MWENYEZIMUNGU .
NAKUOMBEA UMRI MREFU.
Mimi namkubali huy bwana, na hasiye amini basi huyo hana dini make wapagani,wakristo,waislamu,waothodoksi,wahindu, n,k wana amimi majini,wanajua kazi zamungu na shetani sasa iweje wewe husiye jua kazi ya mungu na viumbe vyake umjue yeye….????????????
by the great samy
asalam alaykoum
mimi ninatakakujuwa hali yangu ya maisha ni nayo kwa siku hizi na nipite jia gani ili nifaulu maisha mazuri
achen kubania watu kila mbuzi atakula kutokana na urefu wa kamba yake big up sheikh
simwamini binadamu yoyote namiini Mungu aliyeumba mbingu na dunia…..people wake uo and open ur eyes.
simwamini binadamu yoyote namiini Mungu aliyeumba mbingu na dunia…..people wake up and open ur eyes.
Nina matatizo ya uzazi sheikh naomba msaada wako kupitia email address yangu hapo juu, ahsante sana
Da huyu mzee sio kigagu,bali ni hali flan ya meditation ambayo ata marastafari wanaweza kuipata na kuweka wazi.
Mzee wangu hicho ni kipaji.kitu ambacho kibaya ni kusema siri za Jah.mfano kutabiri kifo cha mtu,kiama na wapi mtu anakwenda baada ya kufa.
Mzee wangu,elimu uliyonayo ni yakitabu,na Jah alituambia kupitia prophet Muhamad.kwamba kila kitu cha chini ya jua na maelekezo mengine yapo ndani ya Kitabu cha Mwisho ,ambacho ni Quraan Tukufu.
Ndio naona comments zingine zina mlenga kumshambulia Sheik Yahya Hussein pamoja na kipaji alichopewa na mwenyezi Mungu mwingi wa rehma.Sheikh Yahya Hussein hakamati watu kwa nguvu kwenda kujipatia msaada wa mambo yanayo watatiza hapa duniani,yeye kazi zake ni halali na analipia kodi zote zinazo hitajika na serikali yetu.Yeye hamshurutishi mtu kwenda kwake kwa msaada wa kinyota.Watanzania huu ni wakati wa kujifunza na kwenda na wakati,Sheikh Yahya kafanya jambo kubwa sana kujenga web site kwa ajili ya shughuli zake, naona kaamua kurahisisha mambo, sasa audience yake inazidi kukua kwa kasi sana,tumuombeeni salama katika kazi zake.
mzee kutoka Ujiji
Ikiwa kam watu wanaotegemean mwenyezi Mungu. Utabiri kama huu ni shiliki na ALLAH AWEZI KUWAVUMILIA WATU KAMA HAWA SIKU YA KIYAMA.
KWA HAKIKA ELIMU YA GHAIBU( VITU VILIVYO JIFICHA) IPO KWAEKE (MUNGU) TU
Ima kwa wale wanaotegemea utabili wa nyota wapo ktk shiri na huo ni ukafiri wa wazi.
Mtabri yeyeote nwa wano mfuata hawapo katika uongofu (UISLAM) ila ni washirikina.
nakila mshirikina ajikadirie maisha ktk shimo la moto wa jehamam.
Acheni kupalilia shiriki. Muaminini Allah. tafadhali contact me Trmlee99@yahoo.com nikutumie kitabu |the right to destroy satanism” utabiri ni part ya satanism religion. wala sio kipaje ambacho UISLAM UNAKIKUBARI. acheni uzushi muogopeni Allah.
a real muslim never addicts to utabiri.
“Utabri ni elimu ya shirki na matokeo yake ni motoni”
Epukeni kutegemea sababu za kitabiri, mtegemeeni Allah huku mkichua hatua za sababu za kisayansi na sio utabri.
Enyi waislam ujieni uislam wenu . utabiri ni ushirikina.
Enyi wakristo. hakiak utabiri haupo ktk sifa za uslam.
utabiri ni ukafiri.
Bwana Yesu Asifiwe,
Mimi ni mama wa makamo,natafuta dawa mbadala ya kuzibua mirija ya kizazi na kupevusha mayai,nataka kuzaa na matatizo hayo yamegundulika hospital na siko tayari kufanyiwa upasuaji!!!!
Tafadhali nisaidie,naomba unitumie majibu kwa email address yangu hapo juu.
Ubarikiwe sana kwa Jina la Yesu!!!!!!
MZEE KIVUTIO KIKUBWA KWA NCHI YETU SERIKALI IMPE USHIRIKINO NI MTU MUHIMU SANA
sheikh yahya mungu akuongoze na akupe mke kijana wa miaka 18 mbichi mtamu mhhhhhhh mzee una mambo wewe.
wako
mkojani
habari yako mzee! mimi sina bahati ya kufanikiwa na kitu chochote ambacho kitaniletea manufaa hata mwanaume nikikaa nae antaniacha katika mazingia ya utatanishi nifanyeje na umri unapotea bila mafanikio ya malengo
Mimi sijawahi kutabiriwa na sheikh yahya, ila nilisha msikia akisoma Quraan. mashaallah, haki ya mungu sheikh huyu akiwa anasoma Quaan tukufu, utasikia madirisha na milango yakigongana kutokana na ile sauti nzuri ya na usomaji wake Quraan tukufu, basi malaika wanagombania madirishani kusikiliza na kuona nani asomae quraan kwa sauti nzuri kama hiyo ! mimi binafsi ninapo msikia sheikh akisoma Quraan mama yangu mzazi huwa natokwa na machozi!
Hongera sheikh wangu.
Namtakia afya njema Sheikh Yahya azidi kutusaidia
VIPI HALI YA INCHI YA R D CONGO VITA HUENDELEA ? MIMI NINA HITAJI KUPATA PESA YA KUNUNUA GARI.
kwakweli haifai kumsema mtu
Sheikh Yahya Hussein ni kiboka ya njiakuhusu masuala ya utabiri babu yangu yule si mtu wa mchezo yuko fit sana na anajua afanyalo,mwenzetu macho yake yanaona tusivyoviona sisi wengi.Muachieni babu yangu afanye vitu vyake,je mliishs msikia maalim Hussein pia (huyu ni baba yake sheikh Yahya na kafundisha wengi sana kusoma Holy Qraan pale nyumbani kwake mtaa wa Mafia.Hawa watu wamejaaliwa vipaji vikubwa vikubwa na hakuna mtu atakaye weza kivichukuwa kutoka kwao,wacheni midomo ya kitanzania maana wabongo tunasifa ya kujua matusi na upondaji watu.
wenu mgosi wa Ndere.
hiv mi naomba kujua ki2 kimoja utabiri umekatazwa katika kuran au haujakatazwa?second ni zambi za aina gan ambazo mwenyez munngu amesema hatozisameh mpaka unaingia kaburin?
sheikh yahaya ni kiboko wengine wote wanaiga upo juu baba
2be honest anatusave sana tu….wanaompinga wana yao!!nadhani kinachohitajika ni imani tu,ata kama unasali kama huna imani ua doing nothing.namfagilia kwa sana coz anawasaidia hata wasioweza kumpa chochote ki2.big up SHEKHE
shk yahy husein ni mushrik nina maana kuwa ni mshirikina kwa waislam wenye kufuata uislma wao ni haraam kujifunza na kuifanyia kazi mambo ya nyota yaani ni nujuu ni mambo ya shetwni mlaanifu aliefukuzwa katika rehema za mwenyezimungu na yeyote atakaemfuata na kuamini maneno yake japo kuwa anaweza kusibu basiatakuwa pale naye katika moto wa jahannam , maana mtume wetu hakuwa mnajimu wala mpiga ramli na mambo ya uchawi hafai kabisha sheke yahya hussein na wala hafai kuitwa shekhe. salim
Acheni kupalilia shiriki. Muaminini Allah. tafadhali contact me Trmlee99@yahoo.com nikutumie kitabu |the right to destroy satanism” utabiri ni part ya satanism religion. wala sio kipaje ambacho UISLAM UNAKIKUBARI. acheni uzushi muogopeni Allah.
a real muslim never addicts to utabiri.
“Utabri ni elimu ya shirki na matokeo yake ni motoni”
Epukeni kutegemea sababu za kitabiri, mtegemeeni Allah huku mkichua hatua za sababu za kisayansi na sio utabri.
Enyi waislam ujieni uislam wenu . utabiri ni ushirikina.
Enyi wakristo. hakiak utabiri haupo ktk sifa za uslam.
utabiri ni ukafiri. nakupongeza sana ndugu yangu kwa waislam wasioijua dini yao wana kokotwa tu na mshirikina
naungana na mchaniaji wa mwisho,
utabiri huendana na majini na ni moja kati ya shirki na muumba wetu anasema hakuna kosa kubwa kwake kama shirk na hasamehe kosa hilo!!
nachukua fursa hii kumkanya awache mara moja na arudi kwa muumba wake na kama hataki basi akome kuinasibisha elimu yake ya shirki na quraan tukufu na uislam; kwani uislam unakataa mambo hayo na quraan haikubali.
sorry naomba website ya Sheikh Yahya Hussein itanisaidia kwa kuwasiliana na shekh
please could you kindly give me the contract or information or the name of Sheikh who recovered stolen good in mombasa during the kenya election problem in December
huyu mzee zaidi ya utabiri ni mganga,na am sorry to say this, mchawi. zamani zile,nilikua namjua mama mmoja jirani yangu siku moja aliropokaga eti kaenda kwa huyu sheikh kugangiwa,kisa mumewe alikua anatoka nje ya ndoa.ndo nikashangaa,huyu mtabiri atagangaje,ndo nikapewa ‘habari ndo hiyo’ huyu sio mtabiri tu ila ni mganga na anaweza kukuchawia,kama huyo demu alivyomchawia mume wake. MUNGU tuongoze! hizi dhambi mwe!
Hello Mkolonjinji big up man! u these people they don seem to understand what they’re told! hilo halina ubishi kwamba utabiri huu unaofanywa na hawa mabwana ni njia za shetani tu! Ambao ni ushirikina mtupu lakini kwa bahati mbaya sana nafsi ya mwanadam inapendezwa sana na uovu (mambo ya kishetani) hilo linalofanywa na hawa wanaoitwa wanajimu (astrologists) haliungwi mkono na Quran wala biblia tuache hayo mambo!
Big up sheikh tena nna mpango wakukutembelea mwembechai ndio maana nikapitia habari yako kwanza. Wasiotaka kuku-visit ki vyao vyao. Nahitaji utabiri wa 2009 nakutegemea kwa ushauri
Binafsi utabiri wa nyota huwa unanipatia sana sheikh. Kaza buti
mwanga tu huyu hakuna nini wala nini!
Mimi ni mmanyema safi na watu wangu wamanyema wengi wanaamini hayo mambo ni kitu cha kawaida kwa wamanyema kuwa na imani kama hizo.Ni vizuri tumuogope m/mungu amekataza sirki kama hizi.Kila mwanadamu ni mtabiri wewe muombe m/mungu na kama siku ni yako utaona mambo yote uliyomuomba yanakwenda sawa,kwa hiyo mchawi wetu mkubwa ni subhana wa taala na sio binadamu au mitume.Mwenyezi mungu amesema kwenye holy qoran “niombeni na nitakusikilizeni”ni hivyo tuu ,simple sana haina haja ya kutegemea watu wengine kuzungumza naye,usitegemee watu wewe nenda moja kwa moja kwake na matokeo yake utayaona.Msisahau kuwa dua zinaambatana na rakaa ,ni lazima kusimamisha sala tano kwanza halafu ndio maombi.Kwa maelezo zaidi kuhusu deen wasiliana namimi through this address karenga@lycos.com hapo tutajadili kwakina kuhusu deen ya kiislam ni hayo kwa leo nawatakieni wote week njema popote mlipo.
Kulutu Willo
wasalaam
Allah knows best!
Hey punguzeni maneno yasiyona mpangilio,Sheikh Yahya Hussein ni bingwa wa utabiri Afrika Mashariki nzima na vitu anavyotabiri vina ukweli mtupu tofauti na hao watabiri wengine ambao wanaongopa bila haya machoni pao yani kazi yao ni wizi mtupu enziii za Mwalimu kulikuwa na watabili wa kweli ambao walitabiri mambo mengi na yalitokea lakini hivi sasa ni wizi mtupu,hata kipindi Kristo anazaliwa wale Mamajusi wa mashariki na magharibi walitabili kuwa kuna Mfalme wa wayaudi amezaliwa nao walienda kumsujudia lakini hivi sasa watu wamejazana kwa waganga wanataka mali na vitu vingi vya anasa wamemsahau Mungu,Sheikh Yahya ni mtabiri basi acheni atabiri atakae amin mwacheni aamin na asiyeamin basi nae mwacheni,ila fahamuni kuwa utabiri sio uchawi.Asanteni wote kama kuna maswali au unahitaji ufahamu zaidi niko kwenye hassbaby@gmail.com
Naomab niwasalimie kwa salaam ya kiislam,Asalam alikum, (Amani hiwe juu yenu)
Nawaomba mutembelee website hii http://www.alhidaya.com.
Utabiri kam wa huyu sheikh ni shirik hivyo yeye ni mshirikina pia. Kila mwenye kumfuata mshirikina ni naye ni mshirikina.
Allah asema kila mchawi (mshirikina) ajikadirie nafasi ktk moto wa JEHANAM.
Wote ninyi mnao mshabikia Yahaya ni wafuasi wa shirk. Ninyi na huyo mnaye mfuata nitaingizwa motoni bila wasiwasi. kisha mtashuhudia kwa yakini mpo moto.
Hivi mnajua nini kuhusu SATANISM? kijitawi chake kidogo MASONS. MNAJUA?
Siku moja nilikuwa nilifungua TV kipindi kilichokua hewani kilikuwa cha YAHAYA katika maongezi yake alionyesha kuwa Askofu mmoja naye anaendesha kipind star TV (sipendi kumtaja jina lake) Yahaya kaseam kuwa ni FREE MASON. akaongeza akisema kama yeye si FREE MASON aende mahakamani.
Siku ilifuata yule askofu alijibu kwa kufundisha mtandao wa shetan na akimtuhumu Yahay kuwa ni Mason lakini bila kutaja waziwazi.
NINI TWAJIFUNZA?
WOTE HAWA WAWILI NI FREE MASONS. ( WANAFUATA NADHARIA WAZI ZA MFUMO WA SHETANI WAKIJIEGEMEZA KATIKA DINI). YAHAYA AMEJIEGEMEZA KATIKA UISLAM kwa UHAKIKA wa mafundisho ya UISLAM Yahaya si Mwislam. Na huyo Askofu mmiliki wa kanisa amejiegemeza katika Ukristo akitumia Bibilia lakini si Mkristo.
Wenye akili wameelewa. kama bado unatatizo hapa.
Unawea kuniandikia nitakutumia kitabu kilicho andikwa kwa lugha ya kiingeleza juu ya SATANISM utawajua hawa.
Tumia email hii trmlee99@yahoo.com
Ninashangaa kuona watu wanachangia hoja za kusifu mtu wataiki wawajui mambo wanayo changia.
Ikiwa wewe ni mwislam acha kushabikia shiriki na washireikina.
Mwogope Allah.
Ukiwa wewe ni mkoristo. unahitaji maelekezo zaidi niambie nitakutumia makala zitakazo kusaidia kujua ukweli wa mambo.
Ukituma email elza wazi nini unahijaji. ucije ukaandika tu nitumie…., nini we unahitaji nini
HIVI UNAVICHWA VYA NANA GANI? YAHAYA MWENYWE ALIKUBARI KUWA ANATUMIA MAJINI.
ALLAH AMETUKATAZA CONTACT YEYOTE NA MAJINI. WAPO WATU WANAO SEMEA NA KULETA HOJA ZAO KUWA CONTACT NA MAJINI ZIMERUHUSIWA KTK DINI.
HOJA ZAO NI DHAIFU. MAFUNDISHO YA UISLAM HAYATUAMBII HIVYO. KOMENI KUUCHAFUA UISLAM KWA SHIRK. HAKUNA DHAMBI KUBWA ZAIDI KULIKO SHIRK.
ALLAH S.W AMEASEMA ATASAMEHE DHAMBI ZOTE ILA SHIRK.
MWOGOPENI MUUMBA WENU JAMANI.
nakupongeza mzeeee kwa kazi unayo fanya
Salaam.
Sheikh naomba unitabirie mimi nitaolewa na nani? Jina langu kamili lipo kwenye email address yangu.
Ahsante.
Salaam.
Sheikh naomba unitabilie mtu atakae nioa. pia naomba namba yako ya simu ya mkononi ili nipate kukuuliza maswali mengine.
Ahsante.
wewe mariam unachekesha sana..subiria mume utakayeletewa na Muumba,wanaume wa kuwavuta kwa uganga sio wazuri.. limbwata litakuishia na utakimbiwa
AMANI KWENU WOTE MLIOCHANGIA MAONI KTK SWALA La YAHAYA HUSSEIN!. Kwakweli tofauti lazima ziwepo kati yetu hii ni kutokana na mitazamo ya watu wenye imani tofauti! Lakini tusiendelee kubisha pasi na kuwa na hoja za msingi wakati tayari mchangiaji ameshatoa maelezo yenye uzito kutoka katika vitabu vitakatifu vya dini! Kwa kweli hata kama utabiri huo utaendana na ukweli lakini lazima tukubali kwamba linalofanywa halipo ktk njia sahihi! Kwani mimi mara nyingi nimeshamsiki Yahaya Hussein akisema kupitia vyombo vya habari kwamba utabiri anaoufanya ni uchawi mkubwa! Husema “HUU NI UCHAWI MKUBWA!” sasa tujiulize uchawi unakubalika ktk jamii yetu? au umepewa nafasi gani ktk vitabu vyetu vya dini! Hata kama anayoyafanya mnayapenda lakini mkubali kwamba hayakubaliki ktk imani za dini ni makosa makubwa! Ni kazi ya shetani! Ni vizuri sana myapime mambo kwa mizani ya mafundisho ya dini na msijiingize ktk malumbano msiyokuwa na elimu nayo bali mnategemea vichwa na mataminio ya nafsi zenu! Nafsi zenu ni zenye kupenda mambo ya anasa na amali zote za shetani ndio maana unaona leo hii wengi hawapo ktk kujibidiisha na mambo ya Mungu bali ni starehe na anasa! Anayoyafanya ni ushetani mtupu! muache ubishi lah mlete hoja zenye kueleweka!
huu niushirki wa wazi na huyu bwana kazizi yake kuwalahai wanawake na kuwalia pesa to na kama kasoma angefanya kazi ya chuo na si uganga kwani uganga ni ushirki wa wazi na mungu hayataki na kama kweli mtabiri ngekitabiri kiama lini,huu ni uhakika wazi utabiri ni wake m/mungu to subhana wataala na sibinaadamu kama sisi.
Sheikh,
Maombi yangu iko na wewe, upone. Na utuambie vile wafrica wanaweza kuishi vizuri.
Hakuna kitu hapo ni ushirikina na ubabaishaji( Pepo wa utambuzi)mengi ya mambo anayotabiri huwa hayatokei hiyo tu iantosha kuwafumbua watu macho kuwa yote yanawezekana ktk MUNGU na siyo uwongo wa binadamu ktk kutafuta riziki
DAH KWELI KILA MTU NA IMANI YAKE KWAHIYO SIWEZI KUSEMA KUWA ETI SHEKHE NI MWONGO NOOO HIVYO VYOTE VIPO NI HALI HALISI VINATOKEA NA VINAFANYIKA KTK DUNIA HII YETU KWAHIYO CHA MSINGI NI KUAMINI KILE UNACHOKIONA..NI HAYO TU.
WAPENDWA KTK KRISTU, PAMOJA NA MENGI YANAYOFANYWA NA SHEIKH YAHYA NA KUTHIBITISHWA KWA NAMNA TOFAUTI ANAZOZIJUA YEYE, TUSISAHAU IMANI YETU HASA SISI WAKRISTU AMBAO TUNAAMINI KUWA NI MUNGU BABA MWENJEZI PEKEE NA WALA SIYO MALAIKA WALA WATAKATIFU, NDIYE AJUAYE HATIMA YA LOLOTE KTK MAISHA YA MWANADAMU. KAMA BWANA WETU YESU KRISTU ALIVYOSEMA. HIVYO BASI HAYA YAFANYWAYO NA SHEIKH YAHYA NI MOJA YA YALE AMBAYO BWANA WETU YESU KRISTU ALITUTAHADHARISHA KUHUSU MANABII WA UWONGO AMBAO WATATENDA ISHARA NYINGI ILI TU KUJIHAKIKISHA, TUSIMKUYBALI WALA KUMSIKILIZA HUYU NI MWIBA KTK IMANI YETU SISI WAAMINI.
MATENDO YA MITUME KATIKA BIBLIA 8;9-13 YUPO MTU ALIITWA SIMONI ALIE WASHANGAZA WATU KWA MAUCHAWI YAKE NA MAAJABU, LAKINI BADO MUNGU HAKUPENDEZWA NAE,KWAHIYO FUNGUENI MACHO MSIJE KUPOTEZA PESA ZENU NA HUKU MKIMCHUKIZA MUNGU MWENYE WIVU KWAKU MWAMINI MWANADAMU BADALA YA MUNGU,JAMANI HAMUSHTUKI TU MPAKA LEO HATA KAMA HAMUMJUI MUNGU HATA ZAMA ZENYEWE HIZI HAZITOSHI KUWAFANYA MUSHTUKE HATA YEYE SHEIKH ANAJUA KABISA KWAMBA HIYO NGUVU ALIYO NAYO NI HARAMU KUWA NAYO, ILA TU AFANYEJE NI KWA AJILI YA KUGANGA NJAA
HATA HIYO PETE ALIYOIVAA INAONEKANA HAPO YE MWENYEE SHEIKH ANAJUA FIKA KWAMBA INAHUSIANO NA MAPEPO NA WENGI WANAOZIVAA KWA AJILI YA BAHATI NAWAELEZA MAPEMA KWAMBA HIYO NI CHUKIZO,PETE INAVALIWA KWA AJILI YA ISHARA YA NDOA NA PAMMBO ILA UKIVAA TU KWA AJILI BAHATI BASI UJUE TAYARI UMESHAINGIA KTK CHUKIZO HIYO NI PAMOJA NA KUVAA NGUO ZA RANGI FULANI KWA MAELEKEZO YA UNAJIMU HIYO NI CHUKIZO TAYARI MAANA NAJUA HAYO MAELEKEZO YAKE YAMETOKA KUZIMU HIYO HATA SHEIKH ANAFAHAMU
i challenge shikh yahya to see my future!!!!!
shikh if u can let me know…..!!!!!!
astaghfirullah!
“ENYI MLIOAMINI! BILA SHAKA ULEVI NA KAMARI NA KUABUDIWA (NA KUOMBWA) ASIEKUWA MWENYEZI MUNGU, NA KUTAZAMIA KWA MISHARE YA KUPIGIA RAMLI (NA KWA VINGINEVYO);(YOTE HAYA) NI UCHAFU (NI) KATIKA KAZI YA SHETANI. BASI JIEPUSHENI NAVYO, ILI MPATE KUFAULU” (quran 5:90)
kuna mshairi mmoja wa kiingereza anasema “LIFE IS THE PATH OF TEARS, AND MAYBE YOU CAN LIVE ONLY EIGHTY(80) YEARS! SO USE YOUR LIFE WELL FOR DEATH WILL COME SOON!”
mimi ni mwenyeji wa zanzibar, niko Dar kwa ajili ya kupata elimu, ni mwanafunzi wa IFM, kwa mara ya kwanza kumuona YAHYA akisoma QUR’AN TUKUFU tena ndani ya msikiti! huyu mtu anaejiita ‘SHEIKH’ nilishtuka sana!!! nikawa najiuliza hivi inawezekanaje kwa MSHIRIKINA NA MTU ANAEPOTOA WAISLAM NA KUZUWIA WALIOKUWA SI WAISLAM kurudi kwenye dini yao ya asili ya mwanaadam(UISLAM)ANARUHUSIWA kusoma quran tukufu ndani ya msikiti??!!! wallah waislam tumo kwenye hasara kubwa kupita kiasi! na Mwenyezi Mungu alietukuka ana haki ya kutuadhibu hapa hapa duniani! hivi wale wanaompa kitabu na wakamshikia mic asome quran kwa sauti hawana macho??! au hawasomi quran na mafundisho ya mtume wetu Muhammad (saw)? kwanini jamani???!! hivi hatuoni kama hii ni sababu tosha ya kuchekwa na wasiokuwa waislam? udhaifu wa hali ya juu kabisa! sote tunastahiki kukatwa vichwa! na JE hakuna katika muislam mwenye uwezo wa kutoa kipindi kwenye tv na kumlaani YAHAYA kwa mambo yake? na kwanini hawafanyi? Ilhali kuna AYA za wazi kabisa ndani ya quran zinazompinga huyu mtu?! hivi wanaogopa kupoteza mali ambayo kawapa ALLAH mtukufu? au wanaogopa kuacha vyeo vyao walivyopewa na ALLAH hapa duniani? tahadhar ndugu zanguni, wallah maisha ya duniani ni mafupi mno kwa kustarehe! tuseme wewe unaesoma hapa una miaka 40, umepata ziada basi ni miaka 15 ambayo utaendelea kuishi hapa duniani huku ukiwa na afya njema, vinginevyo ni kero na mateso kwa ndugu zako, mana utawapa kazi ya kukushughulikia ukiwa mkongwe!! YAHAYA una miaka 76, bado unamuasi Mungu kwa maaasi makubwa makubwa!!? ni kweli ALLAH aliposema “hakika mtu ataniasi mimi mpaka ghazabu zangu zitathibiti juu yake, na hatakuwa wa kumuongoa kamwe!” YAHAYA sisemi kwamba ni wewe katika waliozungumzwa hapo, ila nakunasihi ndugu yangu, MUOGOPE ALLAH aliekuumba, na urudi kwake, kwani huna maisha tena hapa DUNIANI, na ADHABU ya ALLAH ni kubwa kuliko unavyoifikiria, kwani hakuna yoyote kati yetu anejua machungu yake….”NA KAMA INGALIWAGUSA DHARUBA MOJA TU YA ADHABU YA MOLA WAKO, BILA YA SHAKA(WANGELINYENYEKEA MARA MOJA) WAKASEMA:”EEE ADHABU YETU! HAKIKA TULIKUWA MADHALIMU!” (quran 21:46)
please can u send me sheikh yahya hussein’s number because l need to ask him something????????????
mbona majini niliokua nayo mimi yakipanda nafahamu kinacho endelea ni kwa nini.mbona kama vitu vingine najituma mwenyewe au ni ujinga tu
huyo mzee anatutia aibu waislam tu.jamani ndugu zangu msiokua waislam.mjue kwa hakika uislam hauruhusu utabiri.atawapata wajinga tu.wapendao kuongopewa.na kama hajatubu moto wa jahanam unamsubiri.(ALLAH kasema hakuna kiumbe chochote kinachojua kiumbe chingine kitakula nini kesho)yeye mwenyewe hajui kama kesho atapata wajinga wangapi
Habari za jioni Sheikh mimi nina shida ya binafsi siwezi zungumzia kwenye comments hivyo nahitaji namba yako
Sheikh Mkuu, Mufti wa Tanzania. Asalaam Aleykum,
Tafadhali naomba nielimishe juu ya utabiri kama afanyavyo Mzee Yahya Hussein na msimamo wa Quran Tukufu.
Wabillah Tawfiq
Maamuma
could you please send me sheikh yahyas number i need to talk to him personaly, thnks
Would you please give me his phone # so that i can call him, Thanks
najaribu kwa muda mrefu kufungu website ya sheikh yahya lakini nisifanikiwe je kuna mabadiliko katika tovuti http://www.astrosheikhtz.com I was trying to open sheikh hussein yahya website couple days ago but it doesnt work. May be there is something wrong, I really dont know. Probably the webside could be changed let me know if there is something new
regards
kuna kijana nampenda,nisaidie niweze kumpata jina lake linaanzia na ‘L’.naamini jini Bacona atanifanyia kazi hiyo.
aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
asate nyote
hari yako sheikh yaya huseni mimi, nina watoto , kiume,wawili ,nilikuwa anaka wanameke jena una weza kunita biria ,naona unujibu kupitia anununi yako .masalam
naomba msaada wako wa kuumwa kila siku
kutoweza kuendesha gari inanivuta nini sababu
sheikh yahaya mwenyez mungu kakupa kipaji kikubwa sana,ninashida muhimu na wewe naomba uni2mie email yako kupitia email yangu hiyo hapo,natamani sheikh ungekuwa babu yangu.i like you sheikh.
PORE SHEHE KWA MARADHI YANAYO KUSUMBUA MUNGU KAKUPA KIPAJI KAMA ALIVYO WAPA WASANII WACHEZAJI NK,KAZI NJEMA NAKUTAKIA AFYA NJEMA.
nakuuliza wee mzee unawezaje kusoma quraan 5|90 (ENYI MLIOAMINI!BILA SHAKA ULEVI,NA KAMARI,NA KUABUDU MASANAMU,NA KUPIGA RAMLI, NI UCHAFU KATIKA KAZI YA SHET”ANI,BASI JIEPUSHENI NAVYO ILI MPATE KUFANIKIWA.)au unaparuka hapo?. na kama huparuki basi wewe ni munnafiki pia.tubu b4 2 late. na utangaze watu wajue kama umetubu. una tamaa ya dunia.na hao wanao kufata wanakumezesha kuni za moto na si zaidi. AYA INAANZA HIVI ENYI MLIOAMINI. AU WEWE HUJAAMINI SISI TUNAPOTEZA MDA WETU TU? TUFAHAMISHE TUELEWE TAFADHALI
mtu kama huyo hawwezi kuitwa sheikh nyinyi waswahili musiwe na ujinga you know define sheikh ndio uongee sio munampa kipaji baba la ujinga ,, mzandiki,,, mnafiki,, muongo ,, na allah amewasema watu wanaoshirikiana na mambo kama haya ya unafiki na allah atawatia motoni mmoja wapo ni yeye mnafiki yahya hussen
ninamatazu sex
jamani huyu mzee ni noma yani ni nuksi uwiiiiiii?????????????
MIMI NI suddi kassim wa picha sec …nipo na scofield………….iaaaaaa
nimesoma comment zote za kumsifia na kumponda hakuna hata moja ya maana nikinza na kumponda hili kwa kila binadamu ndo sifa zetu hasa kwa rangi nyeusi hatuna cha kufikiri ila ujinga na kuandika mineno ili uonekane nawewe umeandika na kumsifiakwa yule mwenye kwenda shule akiona jambo limekwenda shule kama yeye atalipa point unajua hakuna alokamiliak ilamuumbaji na shehe yahya husein amesoma na anjua nini atendalo hakuna hukumu ya uislam eti umkatie hukumu huyu mtu wa motoni kwa lile ulionanalo wewe kwanza jitazame wewe unaendika coment umekamilika huwenad hili la kukmatia mwenzio wewe wa motoni likawa dhambia kwa upande wako tunaoandika jambo na unapomtaja mungu haraka kwanza iulize nafsi yako nini mungu imemfurahisha halafu toa hukumu kwa mwenzio by mzee wa busara
MBONA ME C ELEWI CHOCHOTE KWANI MNAZUNGUMZIA KUHUSU NINI MAANA MIMI NIPONIPO 2
japo unajiita mzee wa busara,lakini ulioandika hayana ubusarara wowote.hakuna aliyesema binadamu kakamilika sisi wajibu wetu kukumbushana, sasa wewe kama unamtetea shatani basi nenda ukatabiriwe,allah kasema sio sisi,na wewe umesema mungu peke yake kakamilika.KASEMA UTABIRI NI KAZI YA SHETANI.AYA 5/90 QURAN TAKATIFU.mimi najua sijakamilika lakini naomba msamaha kwa m/mungu kila siku.allah pia kasema akitaka anaweza kusamehe Dhambi yoyote lakini sio SHIRKI, wewe mzee wa busara umeelewa nini hapo? maana kama hujatubu basi makazi ni motoni, kwa sababu allah kasema hasamehi, nafikiri umeelewa…………..
hi shekh yahya nakupa hongera kwa dem nilo kuona nae nairob
assalam alaikum, mzee wa busara umechemsha , huyu mzee ni mshirikina na my advise ni kwamba seeking knowledge is obligatory to any one, otherwise u can easly be misguided.ama kweli hii ni dunia ya mwisho!!!
Asalamualykum,i hope u are all fine n good health.Nimejaribu kusoma baadhi ya email ambazo kuna zinazoeleweka n wengine jst wanaandika.Ila ukweli ni kwamba huyo anaejiita shekhe Yahya akubali akatae k2 anachokifanya ni shirki,ambayo anasababisha some people kupotea kutokana na kumuamini yeye kuliko Allah anaejua vilivyopita na vinavyokuja.Jee yupo mwengine kuliko Allah? Big up Salum and Abdul Said.My Email-darshrey@hotmail.com.For all who need friend.
salama mze baada yasalamu nyingi nimependa kujuwa habari yako
mimi kijana wako wahapahap
Rwanda
kigali
naomba msada wauchunguzi wamaisha yangu
asalam alaykum sh.yahya mimi nimsomi wa sheria ya kislam mafaanikio shuleni sio mazuri tatizo shaytwan mahaba ninaomba mbinu za kumfukuza inshaalah
samahani naomba niulize dawa ya mtu anaye sahau sahau mambo mara kwa mara.
samahani naomba niulize dawa ya mtu anaye sahau sahau mambo mara kwa mara.pia naomba msaada wa mawasiliano yako.Yaani namba ya sim
Darish umshukuru allah kakupa moyo wa kufahamu wengi wengi bado wajaamka kuufahamu uislam, kama hapo juu kuna mtu ana shetani wa mahaba anataka msaada kwa yahaya hussein ili amfukuze huyo shetani,na yeye anasomea sharia ya kiislam.sasa watu kama hawa hii ni sickness.sharia ya kiislam inatoka kwenye quraan.ramadhani mimi sio mganga lakini ukitaka kumfukuza shetani sema hivi,(audhubillahi mina sheytan rajiim) very simple wallah.mimi sio msomi urnderstanding yangu inatokana quraan ya tafsir.na tfsiri ya maneno hayo ni (najilinda na mwenyezi mungu kutokana na shetani aliye laaniwa)mambo hayo inatakiwa wewe unaesoma uislam ndio utufahamishe.may allah atulinde wote ishaallah.AMIN.
HUWI MUISLAM KWA JINA.YAANI MIMI, SALIM, ABDULA, MOHAMED,ALI, OMAR, HUSEN, RAMADHANI, ‘NO’ UISLAM NI VITENDO.JINA HALIKUPELEKI PEPONI BALI NI YOURE DEEDS.MATENDO YAKO MEMA.LAKINI JE KAMA UMEFANYA MATENDO MEMA LAKINI HAPOHAPO UKAFANYA SHIRKI JE UTAINGIA PEPONI?.MFANO KAMA VILE UMETEGENEZA JUICE YA MATUNDA YA KILA AINA LAKINI UMETENGEZEA MAJI YA CHOONI JE UTAKUNYWA HIYO JUICE?.UISLAM SIO DINI YA MAKARATASI BALI NI NYIA YA MAISHA.ALHAMDULLILAH
ANY WAY,JAMMA ANAJITAIDI BUT MY PROBLEM NI MOJA KATIKA SIMULIZI ZAKE ZA MA-FREEMASOONS ANAWATAJA SANA VIONGOZI TU WAKIKRISTO. SIJAWAU KUSKIA HATA KIONGOZI MOJA WA KIISLAMU INA MAANA AKUNA FREEMSON WA KIISLAM,,,.MMMMMMH NAMASHAKA SANA ISIJE IKAWA NDO JANJA YA KIINI MACHO NA MFUMO WA KUUA UKRISO KAMA HUKO ALIPOPATA ELIMU YAKE EGPT….
huo ni utabiri2 wa huyu jamaa na amepewa na
mwenyeezi mungu kwa hiyo tusimseme vibaya
Assalaam alaykum; Mimi kama mfuatiliaji mkubwa wa Sheikh Yahya nakiri kuwa hana mpinzani katika suala la utabiri kwa sababu kila analotabiri mara nyingi huwa ni la kweli.
Watu wanaokuandama kwa sasa wengi wao hawafuatilii na hawajifunzi kupitia utabiri wako kweye tovuti,tv na redio-wao wanaropoka tu. Wataisoma namba mwaka 2010. mwinyi.hms8@gmail.com
mwambie akutabirie wewe utakufa lini.acha ujinga.soma uislam ujue mtume kasema nini kuhusu utabiri.by the way.mimi sijui kama yeye ni mjuzi katika utabiri hilo wewe unajua.lakini sisi tupo hapa mwenyezi mungu kakataza au hajakataza.soma quran 5/90 hapo.aya hiyo inasema hivi enyi mlioamini bila shaka ulevi,kucheza kamali,utabiri,kuabudu sanamu hiyo ni kazi ya SHETANI hivyo jiepusheni nayo ili muweze kufaulu.TENA naipenda hii aya sana kwa sababu hakuna kitabu cha dini zaidi ya quran inateketeza mashetani wanne kwenye aya moja. 1 ulevi wa aina yoyote, 2 kamali ya aina yoyote,3 utabiri wa aina yoyote, 4 kuabudu chochote zaidi ya ALLAH…. kuna wengine wanasema eti hicho ni kipaji basi kama ndio hivyo hata kunywa sana pombe pia ni kipaji,au kuwa na mademu wengi ni kipaji, au kusema sana uongo ni kipaji,Hivyo tunajua kwamba yoyote anaye fanya mambo hayo anafanya kazi ya SHETANI.na anaye fanya kazi shetani ni SHETANI, NA MAKAZI YA SHETANI NI JAHANNAM.MAY ALLAH atulinde na moto wa jahhanam,AMBAO mafuta yake ni mawe na watu. AMIN
Namuomba sheikh arudie jinsi ya kutumia alama za kijini na nina omba azioneshe kwa michoro yake.
Na mimi nina tatizo moja la uoga mimi ni muoga sana naomba uniambie nifanye nini ili uoga upungue
maoni yangu wale wanaoponda naona upeo wao ni mdogo wakuelewa kwa sababu mzungu ameficha ule ukweli na kutangaza yale matokeo ya kisababtshi yaani kile chanzo cha yeye kutuacha gepu kubwa asili ni kujua hayo mungu aliyomficha mwanadamu.Na huko kwao wanaheshimu sana mambo hayo ya nyota,kwa hiyo mnaoponda ni malimbukeni tu na mnakurupuka tu.
ENYI MLIOAMINI BILA SHAKA ULEVI NA KAMALI NA KUABUDU MASANAMU NA KUTIZAMIA KWA MISHALE NI UCHAFU KATIKA KAZI YA SHETANI BASI JIEPUSHENI NAYO ILI MPATE KUFAULU……QURAN 5/90.WEEEEEEEEEEEEEE Yusuf hapo juu umefahamu? sasa nani limbukeni sisi tunaopondea au wewe unaetetea? amka tena una jina zuri sana la nabii yusuf yeye hutii kila anachoambiwa na ALLAH
HE SASA MBONA MNAZUNGUKA TU,NAOMBA UFAFANUZI,.JE?MFALME SULEIMAN HAKUWA AMEBARIKIWA NA MWENYEZI MUNGU?NA YALE MAJINI ALIYOKUWA ANAYAPA KAZI VIPI?TUMUWEKE NA YEYE KATIKA KUNDI GANI?HUYO YUPO KATIKA VITABU VYOTE VYA UKRISTU NA UISLAMU.
VIPI WALE WATABIRI WALIOTABIRI UZAO WA BWANA WETU KRISTO(mamajusi),NA WALIWEZA KUIONA MPAKA NYOTA AMBAYO WALIIFUATA NA KWENDA KUTOA ZAWADI KWA MTOTO ALIYEZALIWA?
mimi naona hii ni elimu tu,.kama zilivyo elimu nyingine.,ilikuwepo na na bado ipo miongoni mwetu./,kuielewa na kuipata ni maajaliwa kutoka kwa muumba.
Hongera sana kwa kazi unazo zifanya.Mimi ningebena ufafanuzi kuhusu nyota yangu.
Hongera sana Sheikh Yahaya kwa ELIMU yako ya UTABIRI unayoitoa mimi nimenufaika nayo sana na ninafuatilia sana.
Ombi langu kubwa ni kupata hatua za kutabiri matokeo ya mpira, pia namna ninavyowezakutafuta namba zangu za bahati ikiwa nacheza bahati nasibu.
Pia kama kuna uwezekano sheikh naomba nitumiwe vitabu vyako vyote ulivyovitunga vinavyoendana na mambo ya utabiri, nitajie bei na gharama za kusafirishia toka Dar hadi Mbeya ambako mimi nipo, pia nitajie njia salama za kulipia feha hizo.
NAKUTAKIA KAZI NJEMA NA MAFANIKIO ZAIDI,WANAOKUKASHIFU HAWAJUI WATENDALO WASAMEHEWE TU>
hongera sana sheikh yahaya kwa kutuelimisha na utabiri unaoutoa. ombi langu kubwa ni kutaka kunisaidia kunitabiria mume ambaye nitaweza kuishi naye kwani kwa sasa niko katika njia panda kwani yupo anayenitaka lakini mimi siko tayari kuishi naye kutokana na kabila lake.
hey .mzee asante sana mungu akubarikisana uishi maisha meme.mwaka 1998 .tulikuja ofissini .kwako maisha yalikuwa magumu sana.lakini .ulitutabiria .tulikuwa 3 wasichanauliniambia ntaendakuishi mbali sana .na ni kweli .nimepatamaisha sweden.ubarikiwe naomba namba yako nikija bongo nikupe zawadi asnte.so watakao amini usemayo .haya wakipuuza haya .mimi umenitabiria bila malipo .mana tulikuwa hatuna pesa .tukasema tufanyaje .ukatushauri kila mmoja .na wenzangu sijui walipo .nipe namba yako ya simu.
Nataka kuajulisha kama nasi sisi tupo RWANDA tuna wafatilia sana kipindi chenu je ikiwa mtu akiwa idje ya tanzania mnaweza kumtabiria utabiriwake? naikiwa kama inawezekana basi mtujulishe kupitia anuani hii (nsabedi1@yahoo.fr).asanteni sana.
mimi binafsi siamini kama mtu unaweza kutabiri kitu then ukasema ni lazima kiwe hivyo kama ulivyosema, ila ninachofahamu utabiri ni kama kubashiri mambo yajayo na yanayotarajiwa kutokea but si kwa uhakika wa asilimia mia moja.so mzee wetu sheikh most of the time anachemka
no comment but l want to give big up sheikh yahya for good work,thats talent which delive from GOD,so even me l believe.
Asalaam aleikum sheikh. Utabiri wako naukubali. Mimi nimezaliwa tarehe 15 Julai ni mama mwenye familia ya watoto wanne. Naomba unitabirie maisha yangu ya takuwaje kwani najitahidi kusoma nafanya vizuri katika masomo lakini nafeli mitihani yangu mwishoni hadi wenzangu wanashangaa. Nifanyeje ili nifanikiwe?
Mariam,
Tunajaribu kumfikishia Sheikh Yahya haya maombi yako na pia ya wenzako wengi waliotangulia kwani ni dhahiri kwamba Sheikh hapitii hapa BC mara kwa mara.Asanteni
sheikh naomba uniambie kazi inayonifaa nimezaliwa 28/07/1992
naomba numba yako ya simu
namba yangu ya simu ni 0714 276397
Wapendwa katika kristo ningependa ningependa tumuombe mwenyenzi mungu atusaidie kuelewa juu ya mambo haya ya utabiri unaofanywa na sheikh biblia takatifu inatueleza wazi kuwa tusiwaendee watabiri,wapiga ramli na watu wengine kama hao vilevile katika quran 5/90 tunaambiwa ya kuwa kuwafuata watu kama hao ni sawa na kuabudu miungu ama wapiga ramli hivyo mwenyenzi mungu amsaidie huyu mzee aweze kutubu na wale wajinga wote aliokuwa amewateka.JINA LA BWANA LIBARIKIWE SANA
Assalam alalkum wa rahmatullahi wa barakatuh,
Mie ni kijana ambapo kwa sasa nipo katika chuo kikuu cha Islamic University of Imam Muhammad bin Saud mjini RIYADH ( SAUDI ARABIA ).
Nilikuwa na suali langu moja ambalo ningependa kupata ushauri kutoka kwako sheikh Yahya,yupo msichana ambae ni rafiki wa dada yangu na tumezowea kuongea kwa kawaida na huyu msichana umri wake kidogo ni mkubwa kwangu ila kwa sasa kanidhihirishia kuwa ananipenda na kaniandikia ujumbe kuwa anasubiri mie niwe mume wake yaani nimuowe.
Kwa upande wangu sina mapenzi nae na nili mueleza kuwa mie bado sijajiandaa kuowa na kama ataweza atafute ambae ataemuowa sababu mie nisije kumpotezea muda kwa yeye kukaa ananisubiri.
Hapo ndipo ikawa ugomvi kati yetu hadi kakata mawasiliano.
Sasa,nilikuwa napendelea kufahamu kuhusu qadhwia yangu kwa jibu ambalo nililompa,ninaweza kuwa nilifanyiza vibaya kumueleza jibu lile moja kwa moja ama inakuwaje?
Sababu mie kwa kweli hanivutii na niliokopa kumueleza kwamba hanivutii sababu niliona kuwa anaweza kunichukulia kama nimemdhalilisha.
Nasubiri usemi wako Sheikh
Kazi njema.
MOHAMED ( SAUDI – ARABIA )