Habari za kusikitisha zilizotufikia hivi punde zinapasha kwamba aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto Mheshimiwa Salome Joseph Mbatia (pichani), amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Kibena karibu na Songea. Habari zinazidi kupasha kwamba dereva wake naye amefariki kufuatia ajali hiyo. Mheshimiwa Salome Mbatia alikuwa ni mbunge kupitia viti maalumu. Amefariki akiwa na umri wa miaka 55.

Marehemu Salome Mbatia (kushoto) akiwa na Naibu Katibu Mkuu UN, Dr.Asha Rose Migiro enzi hizo wote wakiwa wabunge kabla Migiro hajateuliwa kushika wadhifa alionao hivi sasa.Hii ilikuwa katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Habari zaidi zitazidi kuwajieni kadiri tutakavyoendelea kuzipata.
Page 1 of 3 | Next page