
Tunapoelekea kuimaliza wiki hii, pengine hakuna habari iliyokuwa ya kusisimua nchini Tanzania kuliko ya HARUNA Pembe Mgombela (54) pichani juu, ambaye ni mfungwa katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam ambaye hivi majuzi alihitimu rasmi shahada ya kwanza ya Sheria kutoka kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania aliyosoma akiwa gerezani humo. Haruna anaingia kwenye vitabu vya historia nchini Tanzania kwa kuwa mtanzania wa kwanza kufanya hivyo.Kweli Impossible Is Nothing kama wasemavyo Adidas.
Feedback / Comments
16 Responses to “HISTORIA MPYA IMEANDIKWA!”
Leave a Reply













big up man¡¡¡¡¡¡¡¡¡¡¡¡
BC can you brief us for what charges is he serving 50 years in prison?…he looks to be serious and determined for revenge!
Kimori,
Our efforts to know what is he serving the years in jail for have been fruitless.No one is ready to talk about that,not even himself.We will keep asking.
Please tell us why his he serving 50years in jail.
He has shown the way that you can still learn even if your in prison.Keep it up and remember God
mhhh sasa kama yeye mwenyewe ana miaka 54 na anatumikia kifungo cha miaka 50 sasa hiyo degree ataitumiaje? akitoka hapo gerezani nathani atakuwa na miaka 104……je mnajua life expectance ya watanzania ni miaka mingapi?
haahaahaaa……this is a joke “they better set him free as congraturations to him”
Gazeti la Mwanachi la leo limetabanaisha wazi… soma Mwananchi la leo…02/11/2007
http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2689
Haruna Pembe:
Mfungwa wa kwanza nchini kupata shahada akiwa gerezani
Na Mwasu Sware
KWA mtazamo wa wengi hasa wale ambao hawajapitia maisha ya jela, mfungwa hana nafasi ya kufanya jambo jingine mbali ya kupangiwa na wanaomlinda na kamwe hawezi kujifanyia jambo lolote kwa maslahi yake.
Lakini Jumatano iliyopita, Haruna Pembe alidhihirisha kuwa kauli hiyo haina ukweli wowote. Aliweka historia ya kuwa mfungwa wa kwanza nchini kuhitimu shahada ya chuo kikuu akiwa gerezani.
Akiwa amevalia suti yake nyeusi na joho la jeusi lenye ufito wa bluu, Pembe ambaye anatumikia kifungo cha miaka 50 katika Gereza la Ukonga, alitunukiwa shahada ya kwanza ya sheria na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, John Malecela.
Shughuli za sherehe hizo zilianza rasmi majira ya saa 10:03 asubuhi katika Bwalo la Maofisa wa Magereza kwa tamko la Malecela: �Kwa mamlaka niliyopewa natangaza kuwa mkusanyiko huu ni wa Mahafali ya Chuo Kikuu Huria.�
Tamko hilo lilifuatiwa na risala na Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Tolly Mbwete ambaye alisema kwamba mhitimu huyo ni wa kihistoria kwa kuwa ameweza kuhimili vema mikiki mikiki ya kusoma akiwa gerezani na kuwa tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961 haijatokea mfungwa kutunukiwa shahada akiwa gerezani.
�Kuhitimu na kuweza kutunukiwa shahada ni sifa kubwa… gerezani si mahala pa kutumikia adhabu bali hata kwa mtu kujiendeleza ili kutimiza malengo katika maisha yake,� alisema Mbwete.
Ilipofika saa 11:10 Mkuu wa Chuo alitangaza kwamba umefika wakati wa kumtunuku Pembe shahada… Aliitwa na mara moja aliinuka kitini alikokuwa ameketi chini ya ulinzi akitembea hatua za kuhesabu, taratibu hadi mbele ya Mkuu wa Chuo na kisha kupiga magoti.
�Kwa mamlaka niliyopewa nakutunuku shahada ya kwanza ya sheria,� alisema Malecela ambaye wakati akisema maneno hayo alivua kofia yake na kumvisha Pemba kisha kuivua baada ya kumaliza maneno hayo.
Baada ya kitendo hicho, Pembe alipata wasaa wa kuvaa kofia yake nyeusi ambayo wakati wote huo alikuwa ameishikilia mkononi. Tukio hilo lilifuatiwa na kukabidhiwa cheti na ripoti ya utafiti (research) alioufanya ikiwa ni sehemu ya kozi ya shahada yake hiyo. Utafiti huo aliufanya humo humo gerezani akijikita katika sheria na utaratibu wa wafungwa wakiwa gerezani na jinsi ya kukata rufaa.
Baada ya kutunukiwa alikumbatiwa na watoto wake wawili waliofika kushuhudia hafla hiyo, Halima (28) na Leila (23). Pembe ana watoto wanne, wengine ni Abuu (18) na Jaffar (24) ambao hawakuweza kuhudhuria hafla hiyo kutokana na masomo. Mkewe alifariki mwaka 2000 kwa maana hiyo, Pembe hakuwahi hata kumzika.
Wakati wakimkubatia, mabinti hao walibubujikwa na machozi kabla ya baba yao kuwanyamazisha… Baadaye watoto hao walieleza kwamba imekuwa ni kawaida yao kutoa machozi kila wanapokwenda gerezani kumuona baba yao na kwamba mara zote amekuwa akiwakanya kwamba wasifanye hivyo.
Baada ya shughuli hiyo ya kupewa shahada kukamilika, mfungwa huyo alipata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari. Alisema kwamba aliamua kusoma akiwa gerezani kwa kuwa hakuona sababu ya kupoteza muda kusubiri hadi atakapotoka gerezani. Alisema kwamba mwaka wake wa kumaliza kifungo ni 2025. Ameshatumikia kifungo kwa miaka 16.
�Nilianza kusoma nikiwa hapa hapa gerezani mwaka 2003 na sikuona sababu kwa nini nisubiri hadi nitakapotoka kwa kuwa niliona ni kupoteza muda. Niliona kwamba wafungwa wengi hawajui sheria, nikaona ni vema nikasoma ili niweze kuwaelimsiha hata wenzangu,� alisema.
Pembe anasema utafiti wake umejikita zaidi kwenye matatizo ya kisheria, utaratibu wa wafungwa wakiwa ndani ya gereza hususan kukata rufaa.
Anasema kuwa amepata misaada mingi kutoka kwa watu mbalimbali wakiwamo wanafunzi wenzake hasa baada ya kuonyesha nia ya kusoma.
Alijiandikisha rasmi kuanza masomo yake hayo mwaka 1998, lakini alianza kusoma mwaka 2003 kutokana na kutokakamilika kwa taratibu za kumruhusu kusoma hasa ikizingatiwa kwamba alikuwa mfungwa wa kwanza kusaka nafasi hiyo.
Wakati wote wa masomo yake hayo, alipanga muda wake vema ambao alitumikia kifungo kwa maana ya kufanya kazi za gerezani na kisha muda wa kujisomea. Kazi za gerezani alizifanya asubuhi saa 12:00 mpaka saa 10:00 jioni na baada ya hapo alikuwa anapumzika kabla ya kuanza kujisomea.
Katika moja ya mambo ambayo anayakumbuka katika kipindi chake cha masomo amewasaidia wafungwa wenzake katika masuala mbalimbali ya kisheria. Anakumbuka kwamba zaidi ya wafungwa 90 wamepata msaada wake wa kisheria kutokana na elimu hiyo aliyoipata akiwa jela.
“Mmoja wa wafungwa niliowasaidia alifanikiwa kutoka gerezani. Kwa furaha aliyokuwa nayo aliniuliza anilipe kitu gani, nikamwambia anilipie ada yangu ya chuo. Akanilipia mwaka mmoja,” anasema Pembe ambaye muda wote alionekana imara na mwenye utulivu.
Alikuwa akisoma kwa kufuata muongozo aliokuwa akipelekewa gerezani kila baada ya siku mbili… �Nikishaletewa yaliyomo kwenye kozi, kazi yangu ni kuagiza vitabu kutoka Maktaba Kuu ya Taifa, vitabu ambavyo naletewa na askari na wakati mwingine uongozi wa wanafunzi wa chuoni.�
Naye Mkuu wa Kitivo cha Sheria chuoni hapo, Paul Kihwelo anasema kuwa matokeo ya Pembe ni licha ya kuwahi kurudia mitihani.
�Matokeo yake ni mazuri na hata utafiti wake alioufanya katika kuangalia sheria na taratibu kwa wafungwa wakiwa gerezani ameweza kupata alama (B+),� anasema Kihwelo.
Mshauri wa wanafunzi Chuoni hapo, Daphina Mabagala anasema kuwa alikuwa karibu na mwanafunzi huyo wakati wote wa masomo yake kujua matatizo yake na kumpatia msaada.
Anasema alikuwa kiunganishi kati ya Pembe na uongozi wa Chuo ikiwa ni pamoja na kufikisha matatizo yake katika vikao.
�Mimi ndiyo mshauri wa wanafunzi kwa hiyo muda wote nilihakikisha ninakuwa karibu naye kubaini matatizo ili kuyapatia ufumbuzi, alichokuwa anakifanya ni kuniambia mimi mahitaji yote kisha nayapeleka kwenye utawala wa chuo,� anasema Mabagala na kuongeza:
“Anaweza kusema hana kitabu fulani au manual au kamusi hivyo nafikisha kwenye utawala kisha anafanyiwa utaratibu wa kufikishiwa vifaa vyote hivyo.”
Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi Vincent Magendela na Kiongozi wa wanafunzi katika masuala ya mikopo, George Mtega wamempongeza mfungwa huyo kwa uamuzi wake aliouchukua wa kusoma akiwa gerezani na kuwa ni mfano wa kuigwa hata kwa wafungwa wengine.
�Pembe ni wa kuigwa na wafungwa wengine, hii ni dalili kuwa mtu unapokuwa gerezni si mwisho wa kujiendeleza kielimu,� alisema Magendela.
Akielezea kufurahishwa kwake na hatua ya mfungwa huyo, Malecela alitangaza kuwa, Chuo hicho kimejitolea kumlipia ada ikiwa atapenda kuendelea na masomo ya shahada ya uzamili ofa ambayo, Pemba alisema kwamba ameipokea kwa mikono miwili na kwamba ataanza mara moja hatua za kuanza kujiandikisha kwa masomo.
Katika mahafali hayo, Pembe alisindikizwa na mfungwa mwingine Mukrimu Semoyoga ambaye naye anasoma katika chuo hicho akiwa mwaka wa kwanza akisomea sheria. Mfungwa huyo anatarajiwa kumaliza kifungo chake mwaka 2010.
Wakizungumzia sherehe hizo, Halima na Leila walisema kuwa wanakosa mapenzi ya baba yao na wazazi wao kwa ujumla hasa ikizingatiwa kwamba hawana mama.
�Licha ya kuwa kila siku za Jumapili tunakuja kumtembelea na kupata fursa ya kuzungumza naye, na hata kumletea vitu mbalimbali, lakini bado tunakosa mapenzi ya baba yetu hivyo tunaiomba Serikali imfikirie kumsamehe ili tuweze kuwa naye karibu. Ameshakaa jela muda mrefu� Anasema Halima.
Mpendakeroro,
I hve gone through the article thoroughly, but I could hardly find the reason as to why Mr. Haruna Pembe is serving 50 years in prison!
Kwa kweli kwa nchi kama Tanzania,hii ni historia imeandikwa na bwana huyu.Hongera yake. Na inadhihirisha kwamba Tanzania ni moja ya nchi zinazozingatia haki za binadamu.Maana ni dhahiri kwamba si kazi rahisi kwa nchi zisizothamini haki za binadamu kwa mfungwa kufanya jambo la kimaendeleo kama alivyoweza kufanya bwana Mgombela.Lakini tatizo kubwa ni kwamba nimekuwa na shauku kubwa sana ya kutaka kujua huyu bwana anatumikia kifungo cha nini hapo ukonga.Miaka 50 ni mingi sana.Kwa tafsiri ya harakaharaka ni kwamba ni sawa na kifungo cha maisha hasa kwa umri wake kuwa mkubwa.Lakini sasa kwanini hamtuambii ni kifungo cha nini? tangu nimeanza kuisoma habari ya huyu bwana katika karibu magazeti yote ya Tanzania yalipo kwenye mtandao,sijaona hata gazeti moja likiandika habari kifungo chake,sielewi ni kwanini.Kama aliua si waseme tu? kwani ni wangapi wamefanya hivyo? BC hebu tusaidieni jamani.Haya sio maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kuwaacha wasomaji wakiwa na kiu ya majibu kutokana na habari husika.
amefungwa kwa sababu ya manslaughter
Imenisikitisha sana hali wanayokabiliana nayo watoto wa huyo bwana.Mama yao alishaga dunia…Baba yao yupo kifungoni…Kati hali nyingine wanajikuta wako peke yao kama yatima.
Ingawa sifahamu nini kilipelekea huyo bwana kutumikia hicho kifungo kikubwa,namtakia kila la kheri na jema awe na ujasiri kutumia vema muda wake kutubu katika makosa kama alifanya…
Hongera kwa kupata shahada yako maana wengine wako huru lakini wanashindwa kuipata hiyo shahada.
Watanzania bwana wanajifanya watu wa huruma sana eti unawaonea huruma watoto wake….Nyie ndo huwa mnakuwa wa kwanza kupiga wezi hamjui kama wana watoto wala nini mkiulizwa mnasema haki yao kupigwa leo wale waliobahatika kuokolewa na polisi ukajua kuwa wana watoto unajifanya unawaonea huruma this is Crazzyyyy……
Mi nampongeza tu kwa kuamua kupoteza muda wake kwa kusoma maana atleast anakuwa anajipa majukumu ambayo sio yake indeed….
Nway hata kama ni mimi ningekuwa nataka kuweka history ofkoz ningesoma hadi masters mradi tu niingie kwenye vitabu vya history….Pamoja.
amefungwa manslaughter
watoto tuwachangie wasome,wasije wakajikuta wanaingia kwenye mambo ya hatari…sex trade
Mungu amsamehe,lazima katoa ROHO ! ya mtu hai
BIG UP MAN.
Nampongeza Mr Haruna kwani ameacha historia.Pia ameweza kuwasaidia wenzake ambao walikuwa hawajui haki zao.That is a challenge.
REMEMBER ONE THING; NOT ALL WHO ARE CONVICTED AND SENTENSED BY COUNTRY LAW ARE WRONG DOER!
THIS IS BECAUSE THE SITUATION CAN COM UPON YOU JUST AN TEMPTATION FOR THOSE WHO GO THROUGH SCRIPTURES.
SO I WOUNDER WHY OTHERS TRIES TO QUESTION ABOUT HARUNA BEING IN JAIL FOR LONG PERIOD BUT I ADVICE YOU TO PRAY FOR HIM AND HIS COLLEAGUES.