IVO MAPUNDA

 

Hapo zamani kulikuwa na majina kama Athumani Mambosasa, Juma Pondamali,Joseph Fungo,Sahau Kambi, Iddi Pazi, Mohamed Mwameja na wengineo. Hao wote walikuwa ni walinda milango (makipa) waliojizolea sifa kemkem kutokana na umahiri wao katika kuzilinda nyavu zao zisitikiswe na timu pinzani.

Hivi sasa, huku watanzania wakiwa wamepata upya mwamko wa kupenda soka na kuunga mkono timu za nyumbani(hususani Taifa Stars), tunaye Tanzania One,Ivo Mapunda (pichani). Huyu ndiye kipa nambari moja wa timu ya taifa ya soka kwa upande wa wanaume,Taifa Stars na pia klabu maarufu na kongwe ya Yanga ya jijini Dar-es-salaam. Ameshatwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa mwaka nchini Tanzania mara mbili. Ushauri kwa Ivo Mapunda?

Page 1 of 3 | Next page