
Ukimtaja kwa jina la Henry Cele watu wengi watapata shida kidogo kutambua unamuongelea nani.Lakini ukimtaja kama “jamaa aliyeigiza kama Shaka Zulu” katika filamu maarufu ya Shaka Zulu kila mpenda filamu atakuambia “ahaa…yule”.Filamu hiyo ambayo ilikuwa inaelezea historia ya mfalme Shaka Zulu wa huko kusini mwa Afrika ni mojawapo ya filamu ambazo zipo kwenye lile kundi la “all time favourite movies ever made”.
Habari za kusikitisha ni kwamba muigizaji huyo aliaga dunia ijumaa iliyopita ya tarehe 2 Novemba huko Durban,Afrika Kusini katika hospitali ya Mtakatifu Augustine alipokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki mbili akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua. Amefariki akiwa na umri wa miaka 58.
Henry Cele au maarufu kama Shaka Zulu alizaliwa huko Durban mnamo mwaka 1949. Mwanzoni mwa maisha yake alikuwa ni mcheza soka wa kulipwa akiwa mlinda mlango kabla hajaingia kwenye masuala ya uigizaji. Kutokana na umahiri wake kama mlinda mlango (golikipa),wenzake walipenda kumuita “Black Cat” yaani paka mweusi. Hii ilitokana pia na weusi wake ambao ni ule unaoitwa “weusi tii”.

Ingawa katika maisha yake kama muigizaji filamu ameshiriki katika filamu mbalimbali kama vile Point of Impact ya mwaka 1993 na The Last Samurai ya mwaka 1990, filamu ya Shaka Zulu ndio atayokumbukwa nayo milele. Filamu hiyo aliyocheza na waigizaji maarufu kama Edward Fox na Christopher Lee.Kama hujawahi kuiona filamu ya Shaka Zulu, pata kipande kidogo katika video hii ya youtube;
Mpaka anafariki dunia inasemekana Henry Cele alikuwa amekuwa kama “chizi” hivi akipiga watu na kutukana watu ovyo. Mauti yamemfika huku akiwa amefungwa minyororo ili kumzuia asidhuru watu. Mke wake, Jenny Hollander, alikuwa pembeni ya kitanda chake hospitalini wakati mauti inamfika.Mkewe huyo amemuelezea kama mtu mpenda watu na aliyethamini sana kuishi karibu na watu wake na kuwasaidia.
Henry Cele alikuwa na watoto wanne ambao aliwazaa wakati wa ndoa yake ya kwanza. Hakubahatika kupata mtoto na Jenny Hollander ingawa walikuwa wameoana kwa zaidi ya miaka kumi.Anatarajiwa kuzikwa huko kijijini kwao Kwamashu,Durban wiki hii.R.I.P Henry Cele.
Feedback / Comments
29 Responses to “R.I.P “SHAKA ZULU”.”
Leave a Reply


sending...
Dah! watu muhimu mbona wanazidi kupungua tu…tunabaki na maguluguja tu.
RIP Cele.
kifo cha huyu jamaa kimenisikitisha sana. one of my favourite movie is Shaka Zulu, on top of that he is one of my favourite actor in general. Mambo mengi muhimu yamo katika hii movie, hasa jinsi wazungu walivyoingia na kutawala kiakili wazee wetu wa enzi hizo, mpaka kuja kuwa watumwa wao, most of all how smart Shaka was, even though mwishoni alishindwa nguvu. He did the best job potraying Shaka, I was conviced that he was the really Shaka. His death felt like loosing Shaka all over again. RIP. You’ left a mark in me and lot of people.
Nimesikitishwa sana na kifo cha msanii huyu mahiri. Kwakweli sinema yake ninayoifahamu ni moja tu, nayo ni Shaka Zulu. Aliigiza wa ustadi mkubwa sana. Wala hakubahatisha. Yaani mtu yoyote aliyekwishaiona sinema ile, sidhani kama atapingana na kauli yangu. Na kwa ambaye bado hajaiona hii sinema, basi ningemshauli akaione ili aweze kutoa tathmini binafsi.
MOLA amrehemu Henry Cele a.k.a Shaka Zulu, apumzike kwa amani, AMINA.
natoa pole sana kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na funs wake wote inauma pale anapotutoka mtu muhimu na hasa hawa vioo wa jamii
RIP Cele
Cele pia aliwahi kucheza filamu ya SIMBA WA TSAVO kama mnaikumbuka wadau. Alicheza kama kibarua mjenga reli ya Kenya kipindi cha ukoloni.
Katika kazi zake zote naiheshimu zaidi triology ya SHAKA.
R.I.P Mzee.
Nilimpenda mcheza filamu huyu, kwa kweli filamu zake zinafundisha mengi ya asili ya kiafrika.
Mwenyezi Mungu amempenda zaidi, tumwombee apunzike kwa amani.
Amen
RIP man of action…….AMEN
I’M SORRY TO HEAR THAT HENRY CELE “SHAKA ZULU” HAS DIED. IT HAPPENS THAT HE BECAME ONE OF MY HEROS WELL OVER 30 YRS AGO AFTER AFTER I WATCHED HIS MOVIE “SHAKA ZULU”.
HE WAS AND STILL IS I AM SURE MUCH LOVED BY THE PEOPLE IN AFRICA AND OTHER CONTINENTS THROUGH HIS OUTSTANDING WORK (ACTOR).
MY SYMPATHIES TO HIS FAMILY AND OTHERS WHO WERE CLOSE TO HIM. R.I.P.
Hello Africa World!!!
Shaka Zulu soundtrack needed for all time!!
Pls
can you pliz send me shaka zulu films
the great movie i see in my live ,i remember Shaka Zulu ,RIP Henry Cele i never forget you .
he was a good man the is now one how will cloused the space
Its just come to sight that this shaka Zulu has passed away over 2 years ago. This is with sadness even though its two years later. This movie that was created showed the indigenious peoples especially New Zealanders that there is links to our past that we can not forget especially of the fights our ancestors had endure during the changes of time. This is so important for our children today to see that it was hardship that gave them a life today and especially the life that they will never experience ever. Hence this movies needs to be replayed in the cinemas so our children learn that its not shelfishness and ungreatful things that make us a people but the heart of our land that keeps us walking today is life.
kiaora naku noa Karlos
i read the story of shaka zulu for some years ago, but i still have interest in him dat i like him so much.i will like o know more about him as my herow i realy like may his soul rest in pieac may the good lord recieve him with warm hands.
Henry Cele fait parti de mes plus grands acteurs préférés tels que Gary Cooper, John Wayne, Henry Fonda, Harysson Ford. Pour moi Henry Cele restera toujours vivant dans mon coeur.
Il est parti trop tôt et cela me déchire le coeur car il n’ avait pas fini de montrer tous ses talents d’ acteur, dommage.
I Love you Henry for ever, I miss you.
h cele he was a hero from now the is now one
how can replse hes space
This is the a performance that has outweighed all what i have watch so far. Thanks “SHAKA” HENRY CELE for using your skills to portray the biggest man Africa has ever had. Just like Nkosi SHAKA ZULU, you will remain forever in our minds.
could you please translate that whole information into english as we the non-native speakers of that language cannot get the language spoken and written in that text
Glenn,
Thank you for visiting us.I would suggest you copy the information and then paste it into google translator to the language of your choice.You can have the information translated that way.
I was forced to watch Shaka Zulu as a young child. I was born in 1983. It is now 2010 my Grandfather still has it on VHS. I’ve been watching it for almost a week now.( I do a lot of rewinding Lol 2 get the full picture.) I googled it and am just now hearing of shakas death. I believe their is a new SHAKA! long live SHAKA!
Even though his passed on he’ll 4ever live as a hero in our Hearts. Thank You Henry 4 telling the wonderful story.
My son was doing a play about Shaka Zulu at school, we were forced to watch all the shaka zulus DVDs. From when I was a kid I trully believed Henry Cele was the real Shaka. MHSRIP we shall forever remember you for protraying one of africa’s great sons.
I have just acknowledged the death of HENRY CELLE. This man to my understanding did the most superlative job of potraying NKOSI SHAKA LIFE. As an African, Shaka made me proud of our past in many aspcts. In addition, I challenge Tanzanian movie industry& Ministry of Culture to produce films and movies which reflect the life of our heroes such as MTWA MKWAWA, MTEMI MIRAMBO, MANGI SINA, MELI,HOROMBO, KINJEKTILE…ETC so that we as Tanzanian can have something to look up to and be proud of oue noble ancestors
oh no my king i have watched that movie my whole entire life he became the cheif he was the great king we all know and love shaka
I love this Man he was a great actor.I still watch his movie over and over again I am mad because his passing wasn’t on American T.V.I love him none the less
I love him! I love him! I love him!I wish I could have meant him. I am mad because his passing wasn’t on American T.V. none the less I love him 4ever still
OMG took me almost 4 yrs to find out that he passed away, gulp well he will be missed by alot of his fans. i have watched his first Shaka Zulu movie back in late 80′s loved to. been watching the zulu movies and mini off and on for yrs. rest in peace bro you’re missed.
I am shocked and befuddled about the death of Shaka Zulu and wished that the media here in the U.S.could have been more informative in respect to this great man’s death.Iremember watching him as a child and I aspired to be like him someday.He will be sorely missed in the annals of Art,Culture,and Human History.We love you and miss you so much Shaka.May you rest in peace.
BEST MOVIE EVER