MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

 

Ukimtaja kwa jina la Henry Cele watu wengi watapata shida kidogo kutambua unamuongelea nani.Lakini ukimtaja kama “jamaa aliyeigiza kama Shaka Zulu” katika filamu maarufu ya Shaka Zulu kila mpenda filamu atakuambia “ahaa…yule”.Filamu hiyo ambayo ilikuwa inaelezea historia ya mfalme Shaka Zulu wa huko kusini mwa Afrika ni mojawapo ya filamu ambazo zipo kwenye lile kundi la “all time favourite movies ever made”.

Habari za kusikitisha ni kwamba muigizaji huyo aliaga dunia ijumaa iliyopita ya tarehe 2 Novemba huko Durban,Afrika Kusini katika hospitali ya Mtakatifu Augustine alipokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki mbili akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua. Amefariki akiwa na umri wa miaka 58.

Henry Cele au maarufu kama Shaka Zulu alizaliwa huko Durban mnamo mwaka 1949. Mwanzoni mwa maisha yake alikuwa ni mcheza soka wa kulipwa akiwa mlinda mlango kabla hajaingia kwenye masuala ya uigizaji. Kutokana na umahiri wake kama mlinda mlango (golikipa),wenzake walipenda kumuita “Black Cat” yaani paka mweusi. Hii ilitokana pia na weusi wake ambao ni ule unaoitwa “weusi tii”.

 

Ingawa katika maisha yake kama muigizaji filamu ameshiriki katika filamu mbalimbali kama vile Point of Impact ya mwaka 1993 na The Last Samurai ya mwaka 1990, filamu ya Shaka Zulu ndio atayokumbukwa nayo milele. Filamu hiyo aliyocheza na waigizaji maarufu kama Edward Fox na Christopher Lee.Kama hujawahi kuiona filamu ya Shaka Zulu, pata kipande kidogo katika video hii ya youtube;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Mpaka anafariki dunia inasemekana Henry Cele alikuwa amekuwa kama “chizi” hivi akipiga watu na kutukana watu ovyo. Mauti yamemfika huku akiwa amefungwa minyororo ili kumzuia asidhuru watu. Mke wake, Jenny Hollander, alikuwa pembeni ya kitanda chake hospitalini wakati mauti inamfika.Mkewe huyo amemuelezea kama mtu mpenda watu na aliyethamini sana kuishi karibu na watu wake na kuwasaidia.

Henry Cele alikuwa na watoto wanne ambao aliwazaa wakati wa ndoa yake ya kwanza. Hakubahatika kupata mtoto na Jenny Hollander ingawa walikuwa wameoana kwa zaidi ya miaka kumi.Anatarajiwa kuzikwa huko kijijini kwao Kwamashu,Durban wiki hii.R.I.P Henry Cele.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

12 Responses to “R.I.P “SHAKA ZULU”.”

  1. Comment by Dinah on November 6th, 2007 1:25 pm

    Dah! watu muhimu mbona wanazidi kupungua tu…tunabaki na maguluguja tu.

    RIP Cele.

  2. Comment by lilian on November 6th, 2007 3:33 pm

    kifo cha huyu jamaa kimenisikitisha sana. one of my favourite movie is Shaka Zulu, on top of that he is one of my favourite actor in general. Mambo mengi muhimu yamo katika hii movie, hasa jinsi wazungu walivyoingia na kutawala kiakili wazee wetu wa enzi hizo, mpaka kuja kuwa watumwa wao, most of all how smart Shaka was, even though mwishoni alishindwa nguvu. He did the best job potraying Shaka, I was conviced that he was the really Shaka. His death felt like loosing Shaka all over again. RIP. You’ left a mark in me and lot of people.

  3. Comment by hombiz on November 6th, 2007 5:50 pm

    Nimesikitishwa sana na kifo cha msanii huyu mahiri. Kwakweli sinema yake ninayoifahamu ni moja tu, nayo ni Shaka Zulu. Aliigiza wa ustadi mkubwa sana. Wala hakubahatisha. Yaani mtu yoyote aliyekwishaiona sinema ile, sidhani kama atapingana na kauli yangu. Na kwa ambaye bado hajaiona hii sinema, basi ningemshauli akaione ili aweze kutoa tathmini binafsi.
    MOLA amrehemu Henry Cele a.k.a Shaka Zulu, apumzike kwa amani, AMINA.

  4. Comment by veronica on November 7th, 2007 2:20 am

    natoa pole sana kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na funs wake wote inauma pale anapotutoka mtu muhimu na hasa hawa vioo wa jamii
    RIP Cele

  5. Comment by Bob Sankofa on November 7th, 2007 7:51 am

    Cele pia aliwahi kucheza filamu ya SIMBA WA TSAVO kama mnaikumbuka wadau. Alicheza kama kibarua mjenga reli ya Kenya kipindi cha ukoloni.

    Katika kazi zake zote naiheshimu zaidi triology ya SHAKA.

    R.I.P Mzee.

  6. Comment by Walter on November 9th, 2007 10:37 am

    Nilimpenda mcheza filamu huyu, kwa kweli filamu zake zinafundisha mengi ya asili ya kiafrika.

    Mwenyezi Mungu amempenda zaidi, tumwombee apunzike kwa amani.

    Amen

  7. Comment by jnjr on November 10th, 2007 12:22 pm

    RIP man of action…….AMEN

  8. Comment by Mama wa Kichagga on January 19th, 2008 12:56 am

    I’M SORRY TO HEAR THAT HENRY CELE “SHAKA ZULU” HAS DIED. IT HAPPENS THAT HE BECAME ONE OF MY HEROS WELL OVER 30 YRS AGO AFTER AFTER I WATCHED HIS MOVIE “SHAKA ZULU”.

    HE WAS AND STILL IS I AM SURE MUCH LOVED BY THE PEOPLE IN AFRICA AND OTHER CONTINENTS THROUGH HIS OUTSTANDING WORK (ACTOR).

    MY SYMPATHIES TO HIS FAMILY AND OTHERS WHO WERE CLOSE TO HIM. R.I.P.

  9. Comment by Andrew on April 30th, 2008 4:51 pm

    Hello Africa World!!!
    Shaka Zulu soundtrack needed for all time!!
    Pls

  10. Comment by byron denhere on December 17th, 2009 10:17 am

    can you pliz send me shaka zulu films

  11. Comment by Daniel Cruz on January 16th, 2010 1:25 am

    the great movie i see in my live ,i remember Shaka Zulu ,RIP Henry Cele i never forget you .

  12. Comment by sipho madlala on March 11th, 2010 9:35 am

    he was a good man the is now one how will cloused the space

Leave a Reply