
Prof.Jay (kulia) na Lady Jaydee(kushoto) ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao wamejijengea heshima sana katika fani.Mara nyingi nyimbo zao zimekuwa zikiweka bayana mambo ya kijamii ambayo hugusa wengi kwa njia moja au nyingine.
Kwa bahati nzuri Prof.Jay na Lady Jaydee wameshawahi kushirikiana katika nyimbo kadhaa.Mmojawapo ni ule wa Bongo-Dar-es-salaam.Usikilize kwa kubonyeza hapa.
Prof.Jay tuliwahi kufanya naye mahojiano ya kina siku zilizopita.Bonyeza hapa kuyasoma.Mahojiano na Lady JayDee yatawajieni wiki ijayo.Stay tuned.
Feedback / Comments
8 Responses to “BONGO-DAR-ES-SALAAM!”
Leave a Reply


sending...
Muimba Rap mwenye muonekano wa kiofisa!! hahaha si mchezo!
Prof J anaheshima yake pekee ktk historia ya muziki wa kusema(rap). Huyu ni Kijana aliyeilazimisha jamii ya Kibongo na Wazazi/wazee wanoko kuukubali mziki huo wa kufoka/sema(rap)……hasa alipotoka na kibao fulani hivi kinahusu maisha halisi ya bongo wa kawaida…..yaani alikiimba kutoka kumoyo nakuanzia hapo wazee “wanoko” wakaanza kuzoea na kuchukulia “rap” sio uhuni, “rap” sio matusi…”rap” sio utovu wa nidhamu.
Msanii huyu anastahili Tuzo maalum na ya pekee kabisa kwa uwepo wake ktk soko hili la muziki wa kusema(rap) a.k.a Bongo flava.
Prof J naheshimu kazi yako.
Lady J Dee wewe nadhani ni mfano mzuri kwa wanawake wanamuziki kwani sijawahi kusikia una “skendo” za kipuuzi, alafu ukifanyiwagwa mahojiano huwa umetulia sana yaani huna makuu.
Nafurahishwa sana na Uvaaji wako wa kibunifu……kaza kamba mamaa!
Keep it up guys, i luv your works!actually you rock my heart…luv you!
Namuheshim sana profesa kazi zake nazikubali hata dada yetu jidee yuko juu ila apunguze kula kijiti!!!hahaahhah,pro fanya tizi mkubwa naona kitambi kwa fujo !!!!!!!!!!!
Namfagilia Prof J. Kwanza sijawahi kusikia kashfa kuhusu yeye
best mc ever to blaze bongo period!!!kwa maoni yangu jay ni mc pekee wa bongo ambaye akija kiwanja naweza kutoa pesa yangu kwenda kumuangalia, wabongo state wanamrespect jay to the fullest, unakumbuka hardblasters crew, washikaji wengine wa hard blasters wako wapi na wanafanya nini?
Heeee huyo dada anakuwa kama bibi flani, au amelewa nini? mwambieni aache kujikondesha asije akafa ni magonjwa ya kukonda,Man!
sana toka kitmbo i sulute much