Tunapoongelea muziki wa kizazi kipya siku hizi hatuongelei bongo flava pekee bali pia muziki wa injili (gospel).Aina hii ya muziki inazidi kupanda chati na kujipatia wapenzi lukuki.Cha kufurahisha zaidi ni kwamba vijana ndio haswa wanaupa nafasi muziki wa injili.Miongoni mwa vijana hao ni hao pichani Mary Fue na Matha Fue(tumeshindwa kutambua yupi ni yupi). Vijana hawa ni mapacha ambao wanasema wamedhamiria kuipeleka gospel kutoka Tanzania kimataifa.BC inawatakia kila la kheri.

Feedback / Comments

19 Responses to “BONGO FLAVA YA GOSPEL.”

  1. Comment by Dinah on November 17th, 2007 8:06 am

    Ni vema kumkumbuka Mungu na kumtukuza kwa kumuimbia. Bila yeye tusingeweza kufanya tunayoyafanya.

    By the path….mnamacho mazuri alafu mmepatia kuchonga nyusi zenu kufuatana na ukubwa wa macho.

    Keep it tight gals.

  2. Comment by daya on November 17th, 2007 11:28 am

    Mbalikiwe sana na mungu azidi kuwabaliki, Ni vizuri kumkumbuka MUNGU BABA

  3. Comment by HOLM on November 17th, 2007 8:55 pm

    Hey guys keep it up. We are praying for you and please stand still in the Ministry. We know what you are going through. We are Tanzanians doing the same thing here in America. For more Info you can visit our website at http://www.themissionband.org

  4. Comment by ZeMdau on November 19th, 2007 7:46 am

    Wameolewa hao?
    Wengine tunatafuta Wachumba hapa.

  5. Comment by Cathhbert Angelo on November 19th, 2007 9:39 am

    Hawa wadada wanajitahidi sana ila naamini watakapomaliza chuo. Big Up! kazi yenu ni njema.

  6. Comment by bdo on November 20th, 2007 2:03 pm

    dinah may be y’re making fun of them “….mnamacho mazuri alafu mmepatia kuchonga nyusi zenu kufuatana na ukubwa wa macho….” but i beg your assistance, maan hadi sasa sijaweza kutofautisha muziki wa gospel na “kiwanzenza” however gospel songs inspire

  7. Comment by Dinah on November 20th, 2007 6:26 pm

    bdo! Hapana sijawadhihaki nimemaanisha kabisa kutoka moyoni kuwa macho yao ni mazuri na wamepatia kuzichonga nyusi zao.

    Kuhusu Gospel nafikiri (sina uhakika na sijawahi kusikia kazi zao) ni kama anavyoimba Jide (kama kwaya hivi)ila tu wanatumia maneno ya kumsifu Mungu au Yesu Kristo :-)

  8. Comment by bdo on November 20th, 2007 11:21 pm

    Dinnah, afadhali umenena hujawadhihaki kuhusu umodo wao that japo ni wapendwa katika kumwimbia Bwana but nao wamo katika mambo ya kwetu…kwa kweli hata mie sijapata kusikia kazi zao, ila kuhusu “gospel songs” kwa ujumla, my perception is ..nahisi its like other musics/genre hasa kwa sisi wabongo&E/Afr.umekuwa na tune ya kizaire-dance like than insparation,kama ulivyosema JIDE huimba kikwaya zaidi(kikanisa zaidi) than others-musics..its my view

  9. Comment by Furaha on November 21st, 2007 3:41 am

    Jamani hawa wadada nawafahamu vizuri saana, guys these girls sing vizuri yaani wana sauti nzuri saanna. Kazi yao moja inaonekana EATV yaani utapenda. Big up girls.. Ukimtangaza Kristo hutakiwi kuwa mshamba au outdated lazim auwe presentable hata ukisema YESU ANAWEZA uvutie watu waje kwa Yesu anayefnya watu wapendeze.. Iende mbele injili!!!

  10. Comment by bdo on November 21st, 2007 9:30 am

    Furaha true japo sijaona kazi yao naamini wanaimba vizuri,naamini hata wewe japo si mwanamuziki naamini upo presentable, but nauliza nisaidie what gospel singers’ dance is spiritually or just a style?or a congolize mood?

  11. Comment by Mwampetha on November 22nd, 2007 12:53 am

    bdo,
    Swali lako halieleweki. Afadhari utumie kiswahili kuliko Kingereza ambacho hujui unauliza nini. Au nenda shule ukajifunze lugha upya halafu utarudi BC kuuliza swali lako.

  12. Comment by Flojoma on November 23rd, 2007 6:53 am

    ooh! sis Dinah uko right sana maana msema kweli ni mpenzi wa Mungu ama kwa hakika wamepependeza sana ama kwa hakika Bwana anaweza maana amewatengeneza. Mary and Matha mm nawaombea mungu azidi kuwabariki katika kueneza injili kwa kuimba.Bwana awabariki sana Jina la bwana libarikiwe.

  13. Comment by irene Eusebi on January 28th, 2008 6:45 am

    Hi!
    mary na pacha mwenzio!!!!!!!
    Nawapa big up mnaimba bomba mnapendeza sauti nyororo.
    Nakumbuka tulipokuwa zoo iringa ulikuwa unapenda kwaya sana mwana.Usikate tamaa endeleza libeneke la Gospel kwenda mbele big up mumy!!!!!!!!!!!!!!!.Its me irene classmet wako.

  14. Comment by mary on February 11th, 2008 4:41 am

    Nafurahi sana ninapoona vijana wanamtukuza Mungu kama nyie nawatakia heri,Mbarikiwe sana, pia mzidi kumuomba Mungu ili msirudi nyuma.kazi yenu nzuri

  15. Comment by shi on March 26th, 2008 9:29 am

    keep it up gals
    God bless you

  16. Comment by Lily Victor on July 15th, 2008 5:52 am

    Kila la heri katika kazi ya Bwana na Mungu awabariki sana. awape afya njema. Mnapotunga wimbo naomba muwe makini sana kwani kuna nyimbo nyingi sana hazimtukuzi Mungu ila ni kulalamika na mipasho kama nibebe wa Rose Mhando na wa Bahati Bukuku wa majaribu. Kuweni Makini Mungu anastahili kilicho bora.

  17. Comment by eliud on September 10th, 2009 9:24 am

    Kwa kweli kwa ujumla wangu ni kwamba ninawapongeza sana wakina dada hawa kwa kujishughulisha na gospel, kwa kweli mimi mwenye ni mwana kwaya na ninapenda sana gospel. kwa hiyo Mungu wa Upendo awazidishie maisha mazuri na kila la hery katika kazi ya Bwana.

  18. Comment by Marco Mlacha on November 1st, 2009 12:18 pm

    KUSEMA KWELI SIJAWAHI KUONA AU KUSIKIA GOSPEL MUSIC AMBAYO NI MBAYA AU ISIYOVUTIA,
    NI DHAHIRI KWAMBA KAZI HIZO NI NJEMA SANA.
    TWWAPA MOYO SANA KWANI WANATUPA DAWA ZA KIROHO.

  19. Comment by JOSEPH BALEKE on July 31st, 2010 11:24 am

    nina wapongeza sana kwa kuendelesha injli
    kwa njia hii ya myimbo.

    NAMI PIYA NINA PATIKANA HAPA CAPE TOWN AFRIKA KUSINI PIA NINA IMBA NYIMBO ZA INJILI. ILA NINAWAHITAJI KWA UDHAMINI WENU ILI NIWEZE KUENDELEA NA KAZI HII YA KUPELEKA INJILI.
    TAYARI NIME TOWA: ALBUM YA NYIMBO 8
    ALBUM INAITWA: SIMAMA KWA DHAMU YESU YUWAJA

Leave a Reply