Swali lililopo kwenye kichwa cha habari hii ya leo linaweza kuwa na majibu chungu mbovu.Tunaweza kuendelea kujiuliza kama tunapenda.Pamoja na hayo,jambo moja lililo wazi ni kwamba mazingaombwe ni mojawapo ya sanaa kongwe sana ulimwenguni.Kama una tafsiri yako kuhusu mazingaombwe usisite kutuambia wenzako.Tupo hapa kujifunza na kuelimishana pia.

Vilevile kama unazikumbuka enzi zile ulipokuwa shule kisha matangazo ya kuhusu ujio wa mwana-mazingaombwe yakaanza kusambaa, jamaa akaja mstarini akawapeni sample kidogo ya mazingaombwe yake,utakuwa pia unakumbuka jinsi ambavyo ulikuwa unaenda mbio ikitokea kwamba mazingaombwe yanakuja shuleni kwenu na wewe huna kiingilio.Sema ukweli,ulikuwa unafanyaje ili usiyakose mazingaombwe?

Lakini si unakumbuka kwamba kulikuwa hakuna wana-mazingaombwe wanawake? Jadi hiyo siku hizi imevunjwa na Akanashe Joan(pichani juu).Huyu inasemekana ndio mwanamke wa kwanza mwanamazingaombwe Afrika Mashariki. Sanaa hii yeye amejifunzia au kuisomea nchini China. Hivi leo ni mwanamazingaombwe maarufu nchini Tanzania akitoa burudani popote walipokusanyika watu.

Feedback / Comments

13 Responses to “MAZINGAOMBWE NI NINI?”

  1. Comment by Dinah on November 20th, 2007 8:16 am

    Akanashe wewe endeleza fani, safi sana.

    Nasikia hata Odemba ni mwanamzingaombwe au “karitaya” :-)

  2. Comment by Dinah on November 20th, 2007 8:16 am

    Mwanamazingaombwe*

  3. Comment by Pope on November 20th, 2007 10:34 am

    Huyu kama ndio demu wako ukimkorofisha anaweza kuhamisha hamu zako akapeleka ndiko kuliko siko nomaaa
    ila Big Up Dadaa

  4. Comment by bdo on November 20th, 2007 1:56 pm

    but she needs some innovation to make her job reputable,sio vizuri kufanya maonesho kila kwenye kusanyiko la watu…let her find special venue for special audience..sio kila akiona watu anandunduliza au labda siajelewa

  5. Comment by danieli on November 21st, 2007 9:14 am

    Akiingia Shinyanga wanamchoma moto fasta, wana usongo sana na wachawi au kile wanachodhania ni uchawi! Ashauriwe a-stay put kwenye sehemu zinazorecognize art and talent as just that, basi.

  6. Comment by ney on November 21st, 2007 2:35 pm

    HUU SASA UCHAWI WA KINAIJERIA. HII ELIMU YA MAZINGAOMBWE HIVI INATOFAUTI GANI NA UCHAWI AMBAO WATU WANARUKA KWA UNGO? HIVI HUYU NI MZALIWA WA TANZANIA AU KATOKA NIGERIA? USIKUTE NI MPOPOZZZZ(NIGERIAN) NA WASI WASI NA URAIA WAKE.

  7. Comment by Lohhy on November 21st, 2007 2:37 pm

    aiseee hii dili kweli, maana kama unaweza badilisha karatasi zikawa pesa, shida ya didi watu kubomoa mabenki, si wakusanye karatasi wakamuone awabadilishie jamani, nikija bongo nitamtafuta.

  8. Comment by Key on November 21st, 2007 2:39 pm

    NO COMENT! ney nakusupport- she is totally witch

  9. Comment by lim on November 21st, 2007 2:42 pm

    mmhhhhhhhhhhhh

  10. Comment by Betty Boop on November 26th, 2007 10:03 am

    Jamani Huyu Dada Sio mchawi kaanza mbali hajaanza jana wala leo. Kwa kifupi yule anaetake kujua chochote muulizeni atawaambia……Si mpompo ni Mbongo mzawa kabisa!!!

    Na kuhusu uchawi, uo sio uchawi its called illusions…..a misinterpretation of an experience of sensory perception, especially a visual one, where the stimuli are objectively present and the mistaken perception is due to physical rather than psychological causes……..Siwezi kuexpalin kwa kiswahili

    Kazi kwenu kama hamtaelewa……..Jua Facts kwanza kabla hujameka Comment.

    Akanashe endelea na Art yako……….Represent.

    Mwanao!!…”

  11. Comment by Akanashejoan on July 2nd, 2010 11:33 am

    Duh!
    bado Tupo nyuma watanzania kisanaa huh!,
    sijawahi kuview hii page.watu wanachonga.I wish ningekuwa na muda wa kuwaeleza waliocoments wasiyoyajua ili kufumbua uelewa wao kuhusu mimi,nimeanzaje,nimefaidikaje na sasa nipo wapi na sanaa hii ya mazingaumbwe….ULILOLIJUA……….!!!!!!!!!!!!!!

  12. Comment by mimi on July 2nd, 2010 10:07 pm

    Ni uchawi.

  13. Comment by mtam on May 9th, 2011 2:16 am

    hivi uchawi unavuka bahari?

Leave a Reply