
Wiki chache zilizopita tulipoweka picha ya mtangazaji Dina Marios wa Clouds FM, mvua ya maoni ilianza kumwagika. Wasomaji wengi wakaonyesha kutamani sana kusoma mahojiano kamili na Dina Marios.BC hatukuwa na jinsi bali kumsaka Dina ili kukidhi haja ya wasomaji na watembeleaji wetu ambao kimsingi ndio “wafalme na malikia” wa BC.
Kipindi maarufu anachoendesha Dina hivi leo kinaitwa Leo Tena kupitia Clouds FM kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa mida ya saa tatu asubuhi mpaka saba mchana. Umaarufu wa kipindi cha Leo Tena haujaanza leo.Ulianzishwa na marehemu Amina Chifupa.Haishangazi basi hivi leo kusikia watu wakimtaja Dina Marios kama “mrithi wa Amina Chifupa au anayekalia kiti alichowahi kukalia Amina Chifupa”.Lakini cha maana zaidi ni kwamba Dina anajitahidi kuendesha kipindi cha Leo Tena kwa kufuata yale yote mazuri aliyoyaanzisha AC na kuongeza mengi mengine.Ubunifu,kipaji na kiu ya kufanya vizuri zaidi kila siku ndivyo vinavyomsaidia.
Hivi karibuni,katika kuitikia hiyo “popular demand” ya wasomaji na watembeleaji wetu,tulifanya mahojiano ya Dina Marios.Tulipofanya hivyo tuliongelea mengi yakiwemo masuala kama anajisikiaje kuwa mrithi wa Amina Chifupa hivi leo hususani baada ya kufariki(Dina alimrithi Amina pale Clouds FM kabla hajafariki).Unajua Amina Chifupa alimuomba Dina ampigie wimbo gani ambao Dina anauona kama ndio ulikuwa wa kumuaga? Je ni kweli sauti yake inafanana na ya marehemu AC kama ambavyo wengi husema?Yeye mwenyewe anasemaje?Kwa hayo na mengine mengi fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kuna nyakati tungependa kuanza bila kukuuliza juu ya historia yako.Lakini kwa sababu hii ni mara yetu ya kwanza kufanya nawe mahojiano basi hatuna jinsi.Hivyo kwa kifupi tu unaweza kutueleza juu ya historia ya maisha yako?Ulizaliwa wapi,ukakulia wapi,ukasomea wapi,unatoka kwenye familia ya watoto wangapi nk?
DM:Kwanza asante kwenu BongoCelebrity kwa kuniweka karibu na wasikilizaji wangu kupitia kipindi cha Leo Tena.Mimi ni wa pili kuzaliwa katika familia ya watoto wanne nikiwa ni msichana pekee katika familia. Nimezaliwa mkoani Arusha tarehe 23 Novemba.Baadaye kidogo familia yetu ikahamia hapa Dar nikiwa na miaka 7.Nikaanza elimu ya msingi katika shule ya msingi Ushindi.Nilipofika la nne nikahamia boarding school huko Iringa katika shule ya Lyalamona na kuhitimu mwaka 1998. Nilianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Shauritanga mkoani Kilimanjaro na kuhitimu kidato cha nne mwaka 2002. Kidato cha tano na sita nikasoma Mkwawa mkoani Iringa nilipohitimu mwaka 2004.
Sikuendelea na chuo kipindi hicho kwani nilikuwa napenda sana kuwa mwanamitindo na pia mbunifu wa mitindo. Nilikuwa nachora na kutengeneza nguo zangu mwenyewe kwa hiyo nikawa nipo Nyumba ya Sanaa katika kujifunza masuala hayo ya ubunifu wa mitindo.
Ndoto yangu ilibadilika siku niliyokuja jingo la kitega uchumi mwaka 2005 nikakutana na jamaa mmoja tukaongea mengi na yeye akanishauri niwe mtangazaji kwa sababu aliona nina sauti nzuri inayoweza kufaa kwenye utangazaji.Nikavutiwa na wazo hilo na ndio nikajiunga na chuo pale Royal School of Journalism.
Wakati huo huo, huyo jamaa aliniombea Times FM niwe nafanya mazoezi enzi za Taji Liundi. Sikukaa sana nikasafiri nikaenda Arusha kwa babu yangu mzaa mama.Kule nikakuta radio moja inayoitwa Triple A nikaomba kujiunga nikakubaliwa. Napo sikukaa sana Clouds Fm wakanichukua kuja kufanya Leo Tena kipindi marehemu Amina amechaguliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalumu.Ndio safari yangu Clouds FM ilipoanzia.

Dina Marios akiwa kazini.
BC: Nini kilikuvutia kuingia kwenye fani ya utangazaji?Unakumbuka ulipokuwa mdogo ni watangazaji gani ambao ulikuwa ukipenda kuwasikiliza?
DM:Nikiwa mdogo huwezi amini nilikuwa najua kuimba nyimbo za wakati huo,matangazo yote ya wakati huo kupitia Radio Tanzania.Lakini kipindi nilichokuwa nasikiliza kwa wakati huo, tena kwa umakini, ni cha Mama na Mwana cha Bi Debora Mwenda…hasa simulizi zake za ua jekundu,binti chura nk.Nilikuwa nampenda vile alivyoweza kuteka akili zetu wakati ule.
BC: Umewahi kufanya kazi zingine mbali na utangazaji?Unaweza kututajia?
DM:Hapana, japo natamani nifanye pia kazi nyingine ila kwa sasa mawazo yangu yapo katika kuisaka elimu zaidi.
BC: Watu wengi siku hizi wamekuwa wakikutaja wewe kama “mrithi wa kiti cha Amina Chifupa” hapo Clouds FM.Sasa ingawa ulianza kuendesha kipindi hicho kabla hata Amina Chifupa hajafariki,wengi tungependa kujua ulikipokea vipi kifo chake na je unadhani kifo chake kimekuachia jukumu gani katika kuendesha kipindi kama “Leo Tena”?
DM:Si vibaya watu kuniita hivyo japo waliniita hivyo hata kabla Amina hajafariki.Ila nazungumza hivi japo sio vizuri kwa sababu ameshaenda na mungu aipumzishe roho yake mahala pema pepo. Mwanzoni sikuwahi kuwa karibu sana na marehemu Amina ingawa nyakati za mwisho alikuwa ananifuatilia sana jinsi ninavyoendelea na alikuwa ananiusia mengi,hususani kwenye mambo kama playlist nk.Alikuwa ananitumia message na kuniandikia nyimbo za kupiga.Ananitumia message na akawa ananiambia hakuna kitu kizuri kwa mtangazaji kama kuwa na good playlist ya miziki.
Unajua nini????mara ya mwisho nimechat nae aliniambia atakuwa mshauri wangu kwa kunifuatilia pale atakapokuwa na nafasi ili kipindi cha Leo Tena kiendelee kuwa kizuri. Nikamwambia sawa nitafurahi kwa sababu nilikuwa nataka mtu wakunifuatilia na kuniongoza ili kipindi kibambe zaidi. Akaniambia tutaongea zaidi maana siku hiyo hakuwa na furaha then akaniomba wimbo wa Show Me The Way wa Papa Wemba.Toka hapo naamini nina jukumu kubwa la kuendeleza yote aliyoyaanzisha katika Leo Tena na zaidi.
Mhariri:Unaweza kuusikiliza wimbo huo kwa kubonyeza hiyo player.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
BC: Baadhi ya wapenzi wa kipindi chako wamekuwa wakifananisha hata sauti yako na ile ya marehemu Amina Chifupa.Wewe mwenyewe ukijisikiliza unadhani kuna ukweli wowote katika hilo?Je Amina alikuwa ni mtangazaji ambaye ulikuwa ukifuatilia nyendo zake ili siku moja uwe kama yeye?
DM:Ha ha ha ha ha ha jamani yaani sijui nisemeje sijui kwa nini watu hufananisha sauti zetu. Hata nikipiga picha watu husema sura yangu inafanana na ya marehemu Amina.Lakini mimi mara nyingi husikiliza kipindi changu sidhani kama sauti yangu inafanana na ya marehemu Amina japo sio vibaya ikifanana. Unajua kipindi Amina anafanya Leo Tena na Kwa Raha Zetu sikuwa napata nafasi ya kusikiliza radio.Mtu niliyekuwa namuhusudu wakati huo ni Phina Mango.

BC: Kila kazi ina mazuri yake na mabaya yake.Kwa upande wako,unadhani ni mambo gani matatu unayoyapenda sana kuhusu kazi yako na yepi matatu usiyoyapenda?
DM:Ninachofurahi ni kwamba nina nafasi kubwa katika kuielimisha jamii.Huwezi amini sauti yangu huwafanya wengi wapate faraja ya kuja kunieleza matatizo yao yanayowasibu kwani hupata nafuu. Nina umri mdogo lakini nashukuru Mungu mpaka nashangaa kumbe jamii inanichukulia kama niliyekula chumvi nyingi kiasi cha kuyajua ya ulimwengu huu.Nashukuru sana kwa hilo na mimi bila kusita huwa nawashauri kwa uwezo nilio nao.
Pili napenda kwamba nina nafasi ya kuonyesha ubunifu wangu kupitia jingles za Leo Tena ambazo huandika mwenyewe,segment za kipindi topics za kuzungumza.Napenda mengi sana lakini tatu na mwisho napata nafasi ya kukutana na watu wengi ambao najifunza mengi kupitia kwao.
Sina ambayo siyapendi.Maudhi madogo madogo ni sehemu ya kazi.

Dina (wa pili kutoka kushoto) akiwa na watangazaji wenzake na mpenzi wa Clouds FM.Kushoto ni Gardner G.Habash,mpenzi wa Clouds(samahani jina hatuna) na Sakina Lyoka.Hii ilikuwa ndani ya Mkwakwani Stadium,Tanga wakati wa tamasha la Fiesta 2007.
BC: Kwa maoni yako,utangazaji ni kipaji cha kuzaliwa nacho au ni kitu ambacho yoyote anaweza akajifunza na kisha kumudu kuwa mtangazaji mahiri?
DM: Kwa maoni yangu utangazaji ni kipaji ndugu yangu na pia ukiendeleze na shule ili uweze kuwa wa ukweli ukweli. Ndio maana kila binaadamu ana ujuzi wa kufanya kazi fulani ambavyo naamini ni vipawa kutoka kwa mungu.

A usual charming face of Dina Marios.
BC:Lipo suala la jinsia kwenye kazi mbalimbali ikiwemo ya utangazaji au u-DJ.Jamii ya kitanzania bado haijazoea au haina DJs wengi wanawake.Unadhani ni changamoto gani ambazo DJ au mtangazaji mwanamke anakabiliana nazo ikilinganishwa na zile wanazokabiliana wanaume katika fani hiyo hiyo?
DM:Sipendi kuwashawishi wanawake wenzangu kufanya kazi isiyo na manufaa kwao kwa maana ya kipato,maisha magumu nk.Lakini kazi ya udj sio mbaya kwa mwanadada na si lazima iwe katika radio hata kwa kupiga katika kumbi mbalimbali za burudani na kwa jinsi ilivyozoeleka ni kazi ya wanaume iwapo wasichana watajifunza na kujitokeza belive me watazoa ajira tu. Hivyo cha msingi ni kukomaa tu kwani hakuna anayeweza kukuyang’anya maarifa yako.
BC: Mbali na utangazaji unapenda kujishughulisha na nini? Na ni mambo gani ya kijamii (mfano haki za wanawake,watoto,yatima nk) ambayo unapenda kujishughulisha nayo.Kwanini?
DM: Hivi karibuni nilipata na nafasi ya kuwa mwanachama wa kijiji cha watoto yatima cha SOS cha pale ubungo na nimepewa jukumu la kupeleka mtoto mmoja yatima kila mwaka kwa ajili ya kupata malezi yote muhimu ikiwemo malazi na elimu. Ni kijiji kizuri sana ambacho kinashughulikia ustawi wa watoto yatima.Wakifika hapo wanalelewa mpaka watakapoweza kujitegemiea wenyewe.Watoto hukuwa kwa heshima,usalama na upendo.Wanawake wengi hunijia na matatizo mengi ni vile sina uwezo natamani ningeweza kutatua tatizo la kila mmoja lakini sina uwezo ila ipo siku.
Sipendi niwe kama uwa lililokosa harufu kwa maana ya kuzungumza pasipo matendo ila mungu akinijaalia nitafanya mengi kwa wanawake wa jamii yangu.Hayo ndio mambo ambayo napenda kujishughulisha nayo zaidi ya kazi yangu ya utangazaji.
BC: Kabla ya kumaliza mahojiano haya tungependa kukuuliza kidogo swali binafsi.Je umeolewa au una mchumba?
DM:Jamani mhh..sijaolewa japo nina boyfriend.

Dina katika pozi tulivu.Anaelekea kusema “Pole,I am taken”
BC: Mwisho unatoa ushauri gani kwa vijana wanaotaka kuingia kwenye fani ya utangazaji hivi leo? Ujumbe wowote kwa wapenzi wa kipindi chako?
DM: Wanakaribishwa ila sio kazi ya kujaribu na ulelemama ni kazi ya kujitolea maana wengi hufanya wakidhani ni point ya mtu kupata umaarufu,kama una kipaji follow your dreams na kusoma pia ni muhimu.
Mwisho nawaambia wasikilizaji wangu tuwe pamoja kama kuna mengineyo wanapenda wanifahamishe kupitia dina@cloudsfm.co.tz
BC: Asante sana Dina kwa muda wako.Tunakutakia kila la kheri.
Picha zote kwa hisani kubwa ya MichuziJR.
Feedback / Comments
152 Responses to ““UTANGAZAJI NI KIPAJI,LAKINI…”-DINA MARIOS”
Leave a Reply




sending...
dina safi lkn gea habib nae ni nomaaa…ivi dina unaishi wp? nahisi gea anaishi uswazi sana au yeye mwenyewe kajichetua? lkn nasiia kaolewa na mbabu flani ivi tetetetee
Dina you deserve to have everything in life as per your kipaji, wishing you all the best and endelea kutuburudisha.
shavu dodo, rangi chocolate. Usijichubue dada baki hivyovyo usije jiharibu ngozi yao ukawa kama maimartha.
Aaa. Sijui nisemeje jinsi picha zako na life story yako vilivyokaa njema. Mbona umeficha mwaka wako wa kuzaliwa?
Yap Dinah!Ur so cute,Kazi yako nzuri sana.Elimu aina mwisho karibu tusome.
Nakukubali Dina.Tuwasiliane.
reen_minja@yahoo.com
Safi napenda kazi yake,ila bado Fina Mango.
una sauti nzuri na unatangaza fresh ila mnaharibu kipindi cha leo tena kwa kukifanya cha mipasho mnaongea sana ka waswahili tena mambo yasiyo na maana pale mnapo kutana na GEA na SAKINA,OTHER WISE ur GOOD
Kijana unajitahidi na unavutia ila punuza mipasho hua inapoteza maana halisi ya kipindi kinaonekana kama cha mipasho achana na akina dida wa mchops wale wamekubuhu keep it up dear
your cute
Dina,
Do not end up there…I would like to encourage you to go higher than that….more education will give you a brighter future, as most of the radio commentators in our country cherish fame and then forget to study further!…all the best!
All the best my girl, i really appreciate ur work!!
unafanya vizuri saana pamoja na crew yako (sakina & Gea)
Cheers!
Dina unamikono mikubwa! Hivi unaumri gani vile?
Well, niliwahi kukusiakia once nadhani unasauti nzuri ila ongeza ubunifu n au ujanja wa kujifunza mambo mapya ktk kazi yako sio lazima urudi shule…Kila lakheri.
Emmi, kutokana na historia yake ya shule…. mahesabu ya haraka haraka anaonyesha amezaliwa kati ya 1983-1984.
punguza kingereza mama,au umesahau kuwa clouds ni people’s station? otherwise umebarikiwa dada.nakushauri umchunge sana masoud kipanya atakuharibia kazi kama hauko makini.mwenzio ni malaya wa kiume huyo.
Mmh! Mikono mikubwa tena kivipi, watu wengine bwana. Wivu tu unakusumbua Dinah.
Keep it up mdogo wangu,una mvuto wa haja! Ila endelea kusoma hapo isiwe mwisho.
hey Marios ur good.just keep it up.Ila uswahili umepitiliza kwenye kipindi chako hasa mkikutana na Gea pamoja na Sakina.Otherwise the segment is good.Just keep it up
ALL THE BEST MDADA UNA BAMBA KINOMA
hey gal,u’ve got good voice,i’like ur vybez,keep it up.
eeeh bwana dinah umetulia, sio siri maramoja moja huwa naskiliza kipindi chako but uswahili unakuja mkikutana na best zako…..inakuwaje unajua? kipindi kinapoteza maana kwani kinasound kuwa cha kike zaidi 7bu ya mipasho,otherwise mshukuru mungu coz ua appearance sayz u av everything in a woman,cjui tabia…..take care pls
Hey mbona dogo kisha unaonekana mtu wamakamo?au maisha bongo yanakuzeesha?nakukubali dinah kwa kazi yako Big up lkn marehemu alikua bomba zaidi.
To all haters dont hate,appreciate,to all the supportes of dinah, big up thats what is required,helpin someone to grow,too many haters in Bongo and thats why many have sad lives,dinah is moving and haters you may not know but u r moving three steps abckward whwn dinah is moving 10 steps forward…learn to appreciate…..am out
huyu dada she is fine, to u dinah *mchangiaji*, she is cute and better than u, kama unabisha weka picha yako apa tuone wewe na dina mtangazaji nani bomba.
utamwambiaje mwenzako si lazima arudi shule? kama imekushinda wewe waache wenzako wasome, umri wake bado unaruhusu wee kama ulizeeka jana shauri yako.
Ajisifu akumilikae. Asikwambie mtu watoto wanaumbwa, nawe ni mmoja wao.
Dinah mama, hongera sana kwa kazi nzuri unayoifanya, kipindi kizuri sauti mashallah, kipaji pia unacho. Elimu ni muhimu kwani ndio itakayofungulia milango zaidi tunataka siku moja tukusikie na wewe ukitangaza BBC au Dutchwelle. Sky should be your limit, keep it up!
[...] “UTANGAZAJI NI KIPAJI,LAKINI…”-DINA MARIOS [image] Wiki chache zilizopita tulipoweka picha ya mtangazaji Dina Marios wa Clouds FM, mvua ya [...]
the one sawa kabisa huyo Dinah yuko kama chiriku yaaani kambea basi nikajua Dina huyu ndo huyo Dinah wa kuchamba wima eeeeeeeeeh umetokea wapi wewe mbona uko hivyo aaaaaah jamani punguza maana kila mtu anataka kumuwekea comment wewe aaaaaaaaaah umezidi……….Dina wewe wa kwenye picha sikujui ila kila la kheri kwenye kazi yako!
Yani huyo mchangiaji anayejiita Dinah ana kiherehere ile mbaya siku zote lazima atoe kasoro tu. Aweke picha yake tumuone na yeye. Halafu anajifanyaga ana point kweli kweli kumbe hamna lolote.Tumekuchoka sasa.Afadhali na nyie mmemuona. Big up Dina Marios!!
DINAH ni mzuri na sio mmbeya… mtembeleeni hapa…
http://dinahicious.blogspot.com/
tunaifahamu hiyo blog yake kuwa yeye ni “fundi” “mfundaji”.
mimi nawajua dina wote wawili! Dina mnayemuita anakiherehere wa dinahicious.blogspot ni mrembo sana kuliko huyu japo dina wa marios wa ukweli ukweli ana sauti bomba! kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake kwa jinsi akili yake inavyomtuma!
Dina yu r good japo kipindi chako as days go by mnakua na uswahili mwingi sana! punguza mama manake umbea umezidi, we nio binti tena mrembo sana, mwenyewe shavu dodo!!
Kaza buti kwenye hiyo fani yako, endeleza kipaji dina marios wa ukweli! Salam kwa Jasmine shoga yako wa mwananyamala
hamna lolote yeye na huyo mwizi wake wote walafi wa ngono! utawezaje mdhibiti mwanaume/ke? ata ukimpa kama dozi ya asprin bado atataka mengineyo, mwizi ni mwizi tu, hata umweke paradiso kwenye mema yote bado atataka na ziada.
GO DINA GO BABY GAL, MAKE US PROUD WITH UR LOVELY VOICE ON AIR. DONT MIND WHAT PEOPLE R SAYING, AS YOU KNOW THIS WORLD IS FULL OF HATTERS…………..
GO DINA GO
Kina Dinah;
Na mie nikiwataka nitawapataje????????
Duu!!1 kiwango acha wenyemeno wale bwana, ila punguza ancheche utahalibikiwa ukiwa bado bint.
Huyu dada ana sauti nzuri.Yasemwayo na watu mazuri endeleza ila yale mabaya jirekebishe ili uweze kufikia malengo yako katika maisha, wasalimie hapo clouds fm,, wote kina gea, sakina pamoja na kelly
mmh hawezi kumfikia amina chifupa hao wanaofananisha wanahitaji jicho la tatu mi ananiudhi mswahili sana akikutana na wale wenzie…….mshhzbhgxu
Wa ukweli ukweli tulia! utamegwa utaachwa.. dunia tambara bovu, endeleza juhudi SOS Mungu atakubariki.
Kazi yako naikubali, sauti yako mashallah ila punguza uswahili kwenye kipindi. Gea anakuharibu, You even sound kishangingi shangingi samtyms! But otherwise i appreciate!
wanaume zenu wenyewe vicheche sasa mnatakaje??hembu mwacheni mtoto wa watu…dina all da best dear tunakupenda na kuthamini kazi yako
nyie mnaotaka afanane na amina chifupa mna akili timamu au??wewe unaejiita amina hapo juu binadamu tumeumbwa tofauti sana ndio maana tumezaliwa na baba na mama tofauti kabisa,dina ataendelea kubaki dina na amina ataendelea kuwa amina milele so acheni upumbavu wa kushindanisha vitu,uswahili nafikiri ndio chachu ya hicho kipindi Amina alipokuwepo mlimsema kuwa alikuwa msahili na mbea leo hii amekufa mnakuwa wanafki na kujifanya mnampenda…binadamu wa ajabu mtu akiwa hai hamthamini mchango wako akifa mnakuwa wanafki na kusifia wakati haisaidii ashakufa,acheni hizo…dina marios ataendelea kuwa dina marios au mlitaka azaliwe na mzee chifupa ili awe sawa na amina chifupa??tuvipende na tuthamini tulivyonavyo kwani ni wanawake wachache waliopata nafasi ya kuongea na jamii kupitia radio…dina all da best watu watasema lakini wewe ndio wewe na umeumbwa kuwa wewe keep it up.
kumfananisha dinnah marius na amina chifupa ni sawa na kumfananisha nyerere na kikwete,.,.,.,. kueni na muone mambo kwa mwanga wa ukweli sio kuvaa miwani ya mbao na kujifanya dereva pumbavu nyie
KWI KWI KWI KWI!!! Mnanichekeshasana.
Amina hawezi kupata wa kufanana nae jamani!!! Hahahahah nimecheka kweli never n ever!
Amina will always be amina . You better be used to it Marios acha kujipa sifa na kujifananisha na ambao huwezi fanana nao kamwe!!
Otherwise unajitahidi ila punguza umbea na upashukuna.
wewe dada hapo juu zulha..nimefatilia mahojiano kati ya dina na bongocelebrity nafikiri sijaona any statement aliyotamka huyo binti dina ya kujifananisha na amina labda kama wewe uanachuki yako ya binafsi.Na kwanini umtukane mwenzako kwa kumuita mjinga??ujinga upi alioufanya??wanawake bwana mnanichosha ndio maana nilisema marehemu amina alipokuwepo wanawake wengi walikuwa hawampendi na mengi walisema juu yake..hayupo mnajikosha?wewe mwenyewe unanini ungekuwa muungwana na mwenye busara usingemuita mwenzako illitrate?wewe ulichokamilika ni kipi?acha chuki binafsi dina hatters will always be around kamua mama huo umbea sisi ndio tunautaka na ndio tuaenjoy sisi tunajua upo kazini..
ha ha haha ha aha ha nimeona comment nying za kumkandia dina zinatoka kwa wanawake,duniani kote wanawake huwa hawapendani ndio maana wataendelea kutawaliwa na wanaume milele wanawake wanamioyo dhaifu na wivu,chuki na kutojiamini na ndio maaana hawaendelei wanaoendelea niwale wanaoweka pamba maskioni na kupigana kiume,dina i like u, u r so cute,napenda macho yako na pua yako ya kama mnyarwanda hivi kwani wewe kabila gani??maana hujatuambia
bongo bwana?? mtu hata degree hana anajaziwa umaarufu sababu anasikika redioni kila siku. ana uwezo gani wa kuchambua mambo sasa??
angalieni huku marekani kuwa mtangazaji na kupata umaarufu lazima uwe na angalau degree and dedicate a lot of time kuonyesha jamii kweli unajua unachofanya.
haya nyie kaeni na USERE-UBWETE wenu unaotokana na multiple appearance kwenye jamii rather that what you have and you have done.
Heri yako wewe MWANZA ni mmarekani.
Wote wanaochonga juu yako Dina Marios wanakuonea wivu. Songa mbele mama usiwasikilize hao.
Dinah huyu mtangazaji ukikata kichwa ukaweka kwa msichana atakuwa bomba sana.Ana kisura kizurii cha kike.Ila mwili,mikono,vidole!!!mmmh
Dina muosha kinywa ni mzuri na ana midomo ya ganja.Midomo yake na ya mvuta wida sawasawa.Umbo lake linavutia.Ukikata umbo lake uliwekee kichwa cha dina mtangazaji atakuwa bomba sana.
Wasalaamu
Jamani makubwa haya, hii blog ina mambo nimecheeeeekaaaa mpaka basi.
wote hapo mnaongea huyo dina hamumjui kwa appearance mnaongea tu kwa kuona picha,dina mimi namjua ana shape nzuri kichizi na hips za kumtosha…kifupi ni mrembo na ana mvuto gud lucky dina.
He jamani, wanawake kweli hampendani, ila mtajiju. Dina watu ndo walivyo, you give them an inch they will go a mile! Ndo maana wengine wanajadili hata yasiyostahili. ila kama ni kicheche kweli kama wasemavyo acha. All in all you are so cute, don’t ever! ever! apply mkorogo utachekesha utakuwa kikatuni kama kMaimatha!
teh
Edna Peter Marios dina kifupi jama!a.k.a wa ukweli ukweli unavyojiita, hongera kwa kazi yako ila tulia mtoto… ukicheche haufai kwa mtoto mzuri kama wewe,, scandinavia umejaza katika umri huo shauri yako…
Jitahidi kujituma SOS kwa juhudi zote; haitatoka moyoni mwako zote ulizoshusha mama! when its done its done.
Punguza mipasho isiyo kua na msingi, rekebisha playlist zako na acha ukicheche!
daima kumbuka leo unamfanyia mwenzio kesho utafanyiwa wewe.
dina mzuri, sauti nzuri.. hongera.. yasemwayo na watu mazuri nenda nayo na mabaya yafanyie kazi…
hao wanaoongea ubaya juu ya dina ni mkosaji mmoja aliekosa pa kusemea ndio amekaa kusemea hapa,dina she always playing a very good music kulingana na walengwa wa kipindi cha leo tena ambao ni kina mama na watu wote wanaoishi uswahilini ndio maana ni kipindi ambacho kinasikilizwa zaidi ya vipindi vyote katika mikoa ambayo clouds fm inasikika katika muda huo,anayozungumza na kufanya na wenzake kama wewe si mlengwa wa kipindi hicho utaboeka kwa wale tunaolengwa tunaenjoy kichizi na kujifunza mengi keep it up dina kama kuna mtu kaachwa na bwana matatizo yake wenyewe wanayao ya binafsi yanawasibu na hamna mtu anawafatilia,mama kamua ndani ya leo tena wewe mzuri huna ubaya wowote.
We Mwanza wivu tu, name a radio presenter mwenye digrii hapa ughaibuni nitakupa £1000 myself. 90% of celebreties hawana elimu yoyote. Elimu kwa kazi nzuri ni bongo tu.
Dina wewe ni mzuri na sauti yako ni nzuri, lakini tatizo uswahili mwingi, yaani wewe ni mswahiliiiiiii hadi basi!
dooo! mola kakupendelea big up!
We mchangiaji namba 60.
Ulitaka asiwe mswahili awe nani? Mhindi???
katika watangazaji niliowafatilia kwa mwaka huu,dina ni kifaa simwenyeji sana katika fani lakini unakimbiza kichizi..si unaona wenye wivu wanavyochonga ha ha ha safiiiiiiii big up sweet
Nashukuru kwa maoni na support watanzania wenzangu ambao mmekuwa mkifatilia kazi yangu kupitia kipindi cha leo tena hapa clouds fm radio.Nimekutana na ushauri mwingi kutoka kwenu na nitayazingatia kwa sababu nahitaji kukua maana bado ni mchanga katika fani ya utangazaji.Mimi ni binadamu ili nifanikiwe nahitaji marafiki na ili nifanikiwe zaidi nahitaji maadui hilo nimeligungua kupitia maoni yenu.Ila napenda kuzungumzia kitu kimoja ambacho wengi wenu mmekizungumzia kuhusu kipindi kuwa na uswahili kila kipindi kina walengwa wake leotena inawalengaa wakina mama hasa wauswahilini nafikiri unapomzunumzia mwanamke kuna vitu vingi anapenda anapenda umbea,mitindo hasa nywele,mavazi,viatu..pia wanawake wanapenda kujua kuhusu mahusiano,afyazao,nini kinaendelea katika maisha ya watu maarufu kama wasanii,wanapenda kuangalia michezo ya tv na filamu za nyumbani,ninapofanya kipindi najaribu kuongea na Mama Habiba ambae anakaa Magomeni anapenda vyote nilivyotaja hapo awali pasipo kusahau muziki wa nyumbani hasa taarabu.Hapa ndipo inapobidi niwe katika ulimwengu huo mimi na yeye tunaelewana kichizi lakini wewe kama si mlengwa wa kipindi hiki huwezi kuvutiwa…nitarudi kufafanua zaidi nawapenda sena.
Mkerewe nakunukuu:
“Mkerewe Says: December 7, 2007 at 8:27 am
We Mwanza wivu tu, name a radio presenter mwenye digrii hapa ughaibuni nitakupa £1000 myself. 90% of celebreties hawana elimu yoyote. Elimu kwa kazi nzuri ni bongo tu”
labda swali lako lingekuwa “nitajie mtangazaji ambaye hana degree ughaibuni?” FYI mtangazaji ambaye hana degree na anafanya kwenye radio ni wale “ma-intern” sijui kama unanielewa vizuri “internship” wako college wanatangaza part time kupata experience otherwise hupati kazi kiubabaishaji tu hapa sio bongo hapa
Mwanza una uhakika na unachokisema?.Larry King na degree ya nini?Sasa sema radio na tv ipi inatakiwa uwe msomi zaidi?
huyo Mwanza si anataka kujifanya anajua!………..
50 cent nahisi ana degree si eti Mwanza pumbavu kabisa ujinga tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!!!
Mdada uko safi. Mvuto wa kutosha japo sijawahi kusikia sauti yako. Bamba lipo la kutosha. ciao
Nimerudi wajameni….sasa uswahili inabidiuwepo mimi na hawa walengwa wangu tunaelewana na huyu mama hapati hata muda wala hana huo mzuka wa kuja kwenye blogsport ndio maana wengi wanaolalamika nahisi sio walengwa wa kipindi cha leo tena.Wengi wamelumbana mimi kufanana na amina au mimi kujifananisha na marehemu Amina si kweli mimi sijajifananisha nae ni watu tu huniita mrithi wake kwa maana nafanya kipindi alichokiasisi aliesema mimi ni mjinga na wala sitakaa ni fanane na marehemu Amina amejikosea haki yeye mwenyewe maana hata yeye wahezi fanana na Dina wala yeyote katika ulimwengu huu kila mtu amezaliwa na karama yake na atakuja kuyafanya yale yaliyomleta katika ulimwengu huu na hakuna atakaefanana na mwenzake…kupitia kauli yake nimegundua binadamu hatujitambui laiti ungekaa ukatafakari na kujitambua wewe ndipo ungeweza kunyoosha kidole na kusema Dina ni mjinga!!mapungufu kwa binadamu ni lazima kwa sababu hatuna umalaika ndani yetu natumai hata wewe Majita,zulha,tatiana na amina mna mapungufu yenu lakini hakuna binadamu aliyepewa ruhusa ya kuhukumu wengine maana wote tutahukumiwa na aliyetuumba….lakini mmenipa changamoto ya kujua si wote watakaokukubali wala kukuunga mkono katika uyafanyayo na hiii ni nature inafaamika toka enzi lakini naamini ili nifanikiwe zaidi nahitaji kuwa na maadui.
Mwisho napenda niwashukuru wote kwa kunipa changamoto nipo bado katika safari ndefu ambayo imenileta hapa ulimwenguni natumai tutaendelea kupeana changamoto
Napenda nimwambie huyo anaejiita MAJITA nampongeza kwa uumbaji wake alioufanya kati yangu mimi na Dinah wa Dinahicious mimi naamini Dinahicios na Dina mimi tu warembo kwa namna ya tulivyoumbwa tunakila kitu ambacho mwanamke anapaswa kuwa nacho hivyo uumbaji wako hauna nafasi labda utafute udongo wako na upewe karama ya uumbaji ambayo huwezi kuwa nayo hata uzikiri uchi halafu umuumbe mtu wako mwenyewe na si sisi, tulishapendwa na muumba ndio maana tupo na tupo tulivyo….kabla hujafa hujaumbika wahenga walisema nizungumzapo huwa naona mbali na kuamini kile kitokacho moyoni mwangu.
ASANTE WOTE NA NAWAPENDA WOTE TUENDELEE KUWA PAMOJA..KILA LAHERI KATIKA KAZI ZENU.
mengine hujamalizia, tueleze yana ukweli au laah.
Any….nafikiri kuna mengi ambayo yanaendelea katika maisha yako na yanabaki kuwa siri yako,mimi ni mwanamke sina kasoro yoyote na kama binaadamu ninaweza kupenda au kupendwa na mwanaume yoyote…kunamtu humu ndani anawapelekapeleka na nyie mnakubali kwenda tu lakini kelele za chura hazimzuwii tembo kunywa maji ni sawa na mtu anaehara halafu ananitishia kujamba….nafanya kaziyangu vile inapaswa kufanywa mengineyo ni ziada…
Nashukuru kwa maelezo, apo umekubali kiaina, japo hukwenda kwenye details, umejibu kiutu uzima nashukuru,
But remember personal life inachangia sana kukubalika/kataliwa katika jamii. Na pia kigezo cha kuweza kupenda au kupendwa na mtu yeyote ni sawa, lakini uangalie na maadili ya jamii tunayoishi kama yanaruhusu huo uhuru, maana sisi ni binadamu na sio wanyama, ivyo we have limits kwenye mambo mengi hata kama moyo wako unakutuma kufanya hilo jambo, still unaangalia na jamii inanitazamaje, then unakufa na lako moyoni. Pia katika maamuzi tunayofanya katika maisha, watu tuwe tunajiweka kwenye position ya unaemwibia, kwamba ingekuwa wewe utajisikiaje? vinginevyo kama dini inaruhusu basi wahalalishe na mtu awe mke wa pili na watatu au sita kabisa kama inakubalika. Sina uhakika na wanayosema hawa wachangiaji wengine, so i cant judge you. ila ukweli unao wewe and u will be the judge mbele ya kiti cha hukumu. sisi tunaweza sema ivi kumbe sivyo, siri unayo wewe na demokrasia ni yako mama, ivo itumie utakavyo. Happy holidays. PEACE.
Dina,
Hongera dogo kwa kazi nzuri upeo wangu ni wa wastani kadri Mola alivyonijalia. Ninachoweza kusema ni kwamba “KIPINDI CHAKO NAKIPENDA SANA NA KINA NASAHA NYINGI SANA, USIKIBADILI HATA CHEMBE NA BADALA YAKE KIBOORESHE”!
Sikia, hapa maadui wako ni wengi sana “MAANDIKO YANASEMA HIVI “OMBEA MAADUI WAKO WAISHI SIKU NYINGI ILI UNAPOBARIKIWA WAJIONEE KWA MACHO” MAANA HAWANAHAJA YA KUFA KABLA HAWAJAONA BARAKA AMBAZO MUNGU AMEKUWEKEA MBELE YAKO”
Tafadhali sana usipoteze muda wako kuwajibu wee endelea na kazi zako walausitetereke hata dk moja kila ulalapo wasemee sala ya kuwabariki. WAACHE WASIME WAKITAKACHO KAMA KWELI WAO WAMEWEKWA NA MUNGU WAKUHUKUMU MBELE YA WATU BASI WAENDELEE NA KAZI YAO NJEMA.
Nawaombeni wadau mjaribu kutafakari na kuamua kuiendeleza jamii kwa michango ya kujenga na tuitumie blog kama njia pekee ya kuelimishana na SIO SEHEMU YA MIPASHO NA KUSUTANA – WEE KAMA WAJUA ANAKULA CHAKULA CHA WATU SI UMWAMBIE LIVE? AU NIAMBIE MIE NIMZUKIE HUKO HUKO AU MWENYE CHAKULA CHAKE ANA HABARI AU NAE KAKIACHIA CHAKULA BILA ULINZI NA KUKU WAPO WENGI?
Wakati mwingine maisha ni mapito hivyo Dinna songa mbele “yana mwisho” haya na jua kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake.
Cheki hapa:
1. Dinna kweli anachukua mali ya mwenzie
2. Watoa hukumu wanamuhukumu Dinna hadharani namna hii
Kati ya hawa wote (1 & 2 ) NI NANI ASIYEKUWA NA DHAMBI JUU YA HILI? Tusije kumnyooshea mwenzetu kidole cha shahada wakati “Gumba, cha kati, cha Pete na Kadada” vyote vinatuhukumu wenyewe!
USIHUKUMU USIJE UKAHUKUMIWA ………..
“WHERE THERE IS SHOUTING THERE IS NO TRUE KNOWLEDGE – Da Vinci, L “
challenge is always there for a human being.you should accept it.
kazi ipo
Uyo mwanaume nani jamani, au kipanya? Dina ukipendwa na watu lazima watapenda wajue anaechukua mzg pia, alafu umeanzaje mataarabu tena? Kipindi kizuri kilivokuwa mwaka jana.
dina first of all wacha nikupe hongera alaf nimependa vile ulivyowajibu watanzania wengi hasa wanawake wana majungu sana wanaweza wakacreate kitu cha uongo na kikasambaa alaf wale wanaopata wanaweka ok bila kuchunguza je ni ukweli au uongo mimi ni hapo tu huwa nashindwa kuwaelewa.mwisho naweza kukuambia usijali what people said about u do what u think is good to u is not a crime to love someone so let them talk !
kumbe umerithi kiti cha amiiiina,sasa kujishaua ooh wananifananisha na amina ..nani?humpati kwa uzuri wala bahati..lo…sasa unawaka nini usiongee sana hapa
wewe ni mswahili mh..na chaumbea mwenzio sakina ndo anaboa kabsa,hata mkizidisha mnaboa..amina alikua mpashu lakini hakuwa na papara kam nyie,mmezidi kujishebedua wakubwa wazima
halafu huyu mtu mzima asidanganye watu mhhhh…tatizo la waswahili mnataka kusifiwa tu mhhh
yeyoo! Dina!
wewe ni ni mswityii kama shuga mamaa!!!
nakupa shavu sana mamake! kazi nzuri!! sauti nzuri,
n’ plz kip it up baby!
NA USISAHAU KUMUOMBA MUNGU AENDELEE KUKUSIMAMIA KWA KILA JAMBO.
OTHERWISE’
TAKE CARE.
me dada’ko GIDECHU.
Dina mama sikiliza wimbo wa songa mbele wa Bahati Bukuku alafu utapata jibu ya haya yote yanayosemwa na watu. alafu wewe Mwanza Vijijini unajifanya uko ughaibuni. ughaibuni gani wanafanya umbea namna hiyo. kwanza wewe mwenyewe mbona una matege watu hatusemi.
Kha!!! hakika kazi ipo yaani watu badala ya kumtakia mema mwenzenu na kumu ecourage asonge mbele mnaanza kumkandia mara hivi mara vile, halafu wengi ni wanawake ptuuu!! Ila siku zote usitegemee eti mwanamke mwenzie akupe maneno ya kukutia moyo.
Inashangaza sana wanawake tuna vijiba vya roho na roho za korosho, lakini Dina dear usijali we angalia kazi yako na yule anaekupa support tu. Kuna wanawake wengine hajui kumsifia mwenzie amependeza hata kama ni kweli umependeza sasa huo ni wivu.
Mimi nasema songa mbele achana na hao kina mwanza wanaojisifia mambo ambayo hawana, mtu kama Dinah usitegemee hata siku moja akusupport cause hata kwenye profile yake amesema yeye ana tabia za namna hiyo kuwavunja moyo wengine ndio kazi yake lakini mwambie habari za ngono hapo mtakuwa marafiki nyoooooooo.
Thus why mi binafsi sina marafiki wa kike na kama wapo ni wachache.
MTAZAME MUNGU PEKEE ALIYEKULETA DUNIANI USIMTAZAME MWANADAMU KWANZA HANA MBINGU YA KUKUPELEKA!!
KEEP IT UP GAL!!
we linda unataka kusema nini kkila mtu ana mtazamo wake tumpe moyo halafu sisis tubakie na nini?anapewa ukweli na upashu wake,kipindi ana kiharibu siyo kama alivokuaga amina hayooooooooooooooooooo
Muacheni dada wa watu,anatimiza wajibu wake!!!!!!!! endelea kutupa vitu.
hongera Dina kwa sauti nzuri.
nakumbuka vizuri siku marehemu Amina alipoanzisha kipindi hiki alianza kwa kupeluzi maoni na tahariri za magazeti na kila siku alijitahidi kutafuta mambo mapya katika kuboresha kipindi chake. na mpangilio mzuri wa nyimbo na visimulizi vya hapa na pale, binafsi nilivutiwa nae sana sikukosa hata siku moja kusikiliza kipindi cha leo tena.
Mwanzo ulianza vizuri sana kipindi chako lakini kwa sasa kinaboa kina ujinga ujinga mwingi binafsi huwa nasikiliza power breakfast ikifika saa tatu nazima radio au nabadilisha station.
kipindi chako huwa kinaharibiwa hao wanaoingia katikati na kuanza kuleta habari za kipumbavupumbavu na kutufanya watu makini tuone kama tunasikiliza upuuzi.
we bado ni mdogo jitahidi kuwa mbunifu hata zaidi ya Amina mwenzako alibuni kipindi cha watoto cha chuchuuu na kilipendwa hata na watu wazima akiwa anasoma aliendesha kipindi kinachohusu mambo ya chakula na musiki laini kilipendwa na idadi kubwa ya watu.
sasa ww kipindi chako tayari kinagawa wasikilizaji wa clouds wengine tunakiona cha kipuuzi wengine wanakifagilia.kumbuka hii ni radio ya watu huwa tunasikiliza masaa 24.
jitahidi kuwa mbunifu na utaweza hao wanakuletea story za mitaani wapinge chini na buni k2 kingine
Thom
kinondoni
mh…kazi ipo!
Dinna mi nakukubali sana,sauti yako naipenda sana,Big up just keep it up.
haya dinna hizo ni challenge tu wanasema mti wenya maembe ndo unaorushiwa mawe usijali kazi yako imekubalika dada ndo maana unaona watu kibao tunavutiwa kucomment kuna macellebrates kibao wamewekwa hapa lakini hana comments nying i kama wewe kwa hiyo ujue huo mti una maembe. UYOU LOOK PRETY.
hata siku 1 sikufikiria kuwa dina atakuwa wa namna hii. nilijua atakuwa bonge la kifaa kwa jinsi anavyoponda wenzake na kujifanya mjuaji wa kila kitu. dah!
D UNAJUA kutumia position yako.n nimependa ulivyojibu kwenye interview
bigup buddy u are talented but keep working hard i think u know that success is the best
hahahaaaaa…nakufa mie!! mmenifurahisha wote mliochangia. naskia ncha kali wa clouds fm ni boyfriend hewa wa mdada!! sijui kweli! Ncha kali na wewe!! ama kweli ncha usicheze nayo..manake inaweza kutoboa au kuchana pabovu na pazima!
vp mzazi unatisha km vita vya darful endeleza mapigano bila ya kumwaga damu its mateja kerzman,mtoto wa tabata kimanga
i really acknowladge thee big up
uko juuuuuuuuuu
hivi nyie macelebrit wa kibongo lini mtaacha kudanganya umri kueni banaaaa
oooooooooyyyo nimekubali we ni nima
uko juu dada, ila yuo just go school kama ulivosema hao wanaokwambia sio lazima kwenda shule usiwasikilize. ur sooo cute! BIG UP!!
Dina unalipa m2 wangu keep it up!
hi dina,bigtime!u luk so cute,n very african.unawakilisha.nimfurahi sana kukuona.nlikuwa hapo bongo nakuskia tu kwenye leo tena.jamani nmiss chachandu la leo,kitchen party,na hekaheka.nawamiss mno mlipokuwa mkilichachandua hilo chachandu na kina gea.loooh!nyie ni noma.una rangi nzuri sana,itunze shostito
DINA upo juu achananao hawo hana maana.
yani sio siri dada dina,kwanza we mzuri hilo alina ubishi pili upo juu kama obama.mimi shabiki wako namba moja.
Mambo da Dina pole na kazi na penda saut yako na ze way ulivyo naunavyo tangaza endelea hivyohivyo leotena milele daima
good girl but mind u no body is perfect kasoro unazo unanenepa mno utakuwa kama sanamu ya michelin noma tutakuita bibi muda si mrefu but keep it on well done i appreciate your work
MAMBO VP DINA DU MWANANGU UNA JUA SIJA WAHI KUKU ONA KWASABABU HUA NAKUSIKIA TU? DU MWANANGU WE NI NOMA I APPRICITE YOU BY
aisee da dina ya good lov u keep it up na crew yote ya leo tena1
Unaweza dada unanifurahisha sana tena kwenye kipindi cha mipasho
kweli we nimkali vibaya vipndi vyako nina vikali kichizi kwani utangazaji wako umeanza lini kutangaza kabla ya hapo ulikuwa unatangaza redio ipi? nihayo tu.
DU!KIUKWELI WEWE NI ENGINE KATIKA LEO TENA HAO WENGINE GEA HABIB NA NI MAGURUDUMU HUWA MZEE MZIMA MNANIPA RAHA KWANZA HABARI ZENU ZINA UHAKIKA KWA SABABU HUWA MNATUPA NA USHAHIDI LIVE YANI I WISH NINGEWAALIKA HAPA MORO TUBADILISHANE MAWAZO HAYA CHACHA
Dah! i luv u Dina……ur so beutiful bby!
Dah! i luv u Dina……ur so beautiful bby!
eeeeeeeee jamani dina we ni kifaaa vibaya nilikuwa wapi ukiwahiwa?/ gooooooooood
WEB SITE YENU NI BOMBA ILA KUWE NA ANIMATION MANAKE ITACHANGAMSHA SI UNAONA MFANO KAMA MTANGAZAJI WA HABARI AKITANGAZA HABARI HUYO HUYO ATANGAZE MICHEZO HUYOHUYO ATANGAZE BIASHARA INA BOA AU VP WEKA ANIMATIONS WEBSITE IPATE UHAI
Dinnah beibi dnt mind abt ol haterz,jas muv on with yo lyf en du wat u thnk z best fo u..haterz ar there to gv challengez.jas tek wat suits u.u ril gud en actualy u ril drive me crazy wit yo kipindi.big up cutey.
Jamani binadamu hawakosi la kusema ukiwa mzuri ukiwa mbaya yote hayo kwao ni kawaida lazima wakutoe dosari hamchoki kusema Dinnah endelea tu na watilie wimbo (WACHA WACHA WASEME MTUSEMA MCHANA NA USIKU MTALALA)
mmh mi bwana sijawahi kumuona huyu mtoto “live” Kumbe mtu bwana! afaa….
dear dina
kwa mara yakwanza kukuona ilikuwa katika uzinduzi wa taarabu,ulimfunika dida vibaya mno,nakupendaa sana lait ungejuwa sikosagi kipind chako hata siku 1 labda niwe kazini na bosi kanisimamia hapo,take care all ze best
MIMI BINAFSI NAKUKUBALI SANA CSTA,CAUSE NIMEANZA KUKUSIKIA KITAMBO TANGU NINASOMA USHINDI PR. SCOOL, KULE MIKOCHENI B.TEACHER ALIKUWA AKITUPA STORI NA KUJIGAMBA KUWA WATANGAZAJI WENGI WA CLOUDS-FM AMEWAFUNDISHA.HE TOLD AS ALIMFUNDISHA MAREHEMU A.CHIFUPA AND YOU KWA MIAKA TOFAUTI.Hakuna muda ambao huwa nafurahi na kujifunza kama wakati nninaposikiliza kipindi cha LEO TENA. I LOVE YOU CSTA,UPO JUU. Your brother 4m another mother,DAUD.
Yeyyyaaaaaaaaaaa!!
Real like you girl!! Nakupa big up, upo juuuuuuuuuu. Kip it up gal’.
your so cute!Really i appreciate you and i like much to hear from you.All the best my dear.
niaje mzeiya,
real sister upo juu mbya mno,yani apa kwa offce daily early in 9:00 lazima ndani ya clouds nitege sikio,
wish to meet you,tichaoooooooooooo na leo tenaaaaaaaaaaaaaaa
ebwana dinno yan we na sauti yako ni tofauti kabisa nikajua utakua kmodo fulan hivi kumbe umejahaliwa mwili……..uko juu!
dina:ma sis
uko bomba u know i was not realise that u look like,
keep up
but be care cause kaumaalufu kabaya.
seeeee uuuuuuuu
sioni haja ya kumhukumu DINA wala mtangazaji yeyote. kila mwanadamu anamapungufu yake. na wahenga husema ; kila mwanadamu anavidole vyake na vidople havilingani;so kila mtu ajijaji kwanza ndo amtazame mwenzake; na mwanadamu hatupendani. bible said. mpende mwenzako kama nafsi yako. tufanye mambo yanayo tuhusu wacheni majungu. DINA NA WENZAKO MKO JUUUUUUUUUUUUUUUUUU YA MSAAAAAAAAARIIIIIIII’
hi u know wat i lv very much na ninackiliza pind every day.dada.
HASNATI FROM KIGAMBONINO
dina unatisha kinoma mwana, mimi mkufunzi mzima wa morogoro teachers college lakini nakuzimia. big up then mama
dina unatisha kinoma mwana, mimi mkufunzi mzimawa morogoro teachers college lakini nakuzimia. big up then mamaaaaaaaaaaaa…
Upo juu Dada
Hey Dina uko juu mama nakufagilia big up ongeza ubunifu km mwanamke. kazi njema
YAAAAH! UR SO CUTE BUT NAOMBA TUWASILIANE PLZZZZ USINIANGUSHE I WISH U ALL THE BEST
jaman nakupenda dina
Du!!! nilikuwa na hamu kweli ya kukuona ila leo nimekusoma kumbe uko hivyo
We ni mrembo na usiogope kelele za chura. kingine leo nashangaa kukuona kwani hua sijui nikamtu au mtu ila nimejua ni wa ukweli poa msiz .
jaman i love u and za work natamani nije kuwa kama wewe Dina uko juuuuu zaidi ya kigimbi cha mcheza mpira wa miguu
HI DADA DINA UPO JUU KINOMA NA KIPINDI CHAKO CHA LEO TENA,JUZI ULISAFIRI KIDOGO NIKAWA CSIKILIZI KIPINDI ENDELEA HIVYO UTAPANDA JUU
ZAIDI.
Aisee, nimefatilia comments nimecheka na kufurahi na kukasirika. sijawahi kuona mtu alopewa comments kama Dina.
dina u know what…hiyo interview ilikuwa 2007, imagine last commenter b4 me ni October 19th 2010, miaka mi3 watu wanakucomment…what a long thread…na pia watu wameanza kuponda kuponda hadi wamechoka..now ni comment nzuri..pengine walikuwa hawakujui vizuri etc..na nzuri u did not reply back..that’s nice. mara nyingi kizuri hakijisifii, chenyewe kinajieleza, ndiyo sasa hivi.
big up…mi nataka kukuona clouds TV…huna kipindi?
mambo dada, hongera na upo juu kwani umeweza kukiendesha kipind vizuri uckatishwe tamaa na wachache kwani kwa sasa umekubalika na vipingamiz vya wachache ndo changamoto za maisha ili uweze kujijenga na kujiboresha zaid katika kazi zako
dina, iam your fun.i like you a lot, so can we be friends? plz reply soon.
realy Dinnah i love u ile mbaya co kazi zako tuu bali hata tha way ua are………kip it up muyyyy.
Dah! aisee nilikuwa na hamu ya kufahamu kisauti kizuri cha mwadada mzuri DINA MARIOUS nimekuona na nimefarijika sana.
nakupenda sana mydada, kupitia kipindi chako cha LEO TENA, big up mdada!
yes dada dina nakukubali sana ukiwa kwenye moja na mbili clouds fm kwenye kipindi chako pia huu mrembo km bado dent wa chuo so nilitaka kujua tu umeshaolewa? na vp una mtoto?
DINAUKOBOMBAILEMBAYA,NAIPENDAKAZYAKO NA WEWEMWENYEWE PIA,NAIPENDAKAZ YAUTANGAXAJI BUT BADO NIPO SHELEN PUGU SECONDARY SCHOOL KIDATO CHA NNE,ILOVE YOU DN.MARIOS.
nice to see u, i like u’re voice more than much.but my dear uko TOFAUTI NA SAUTI YAKO.
hey Dina.hongera sana keep it up c6 and god bless u twice of much!kama hautojali naomba unisaidie coz mimi ni mtangazaji chipukizi wa radio info fm(MTWARA) Plz naomba nitafute kwa no 0718690794. halaaaaa!
jamani! sioni tatizo la DINA, kwanza ni msichana mzuri kwa sura, sina uhakika wa umbo lake lakini bado ni poa sana tu. Ninavomtazama dina anauwezo wa kufanya mengi makubwa na mazuri na jamii ikamkubali zaidi ya hapo, nakuomba ujitahidi usiishie hapo ulipo, unaweza kabisa hata kufikia ngazi ya kuwa WAZIRI fulani baadae. Huyo hapo juu anayesema kutangaza vizuri lazima uwe na DEGREE ni bwege, kwani dina anaonyesha uwezo mkubwa sana! jibadilishe basi uwe MMAREKANI. kama huwezi kusapoti kidogo anachofanya mtanzania mwenzio na kumpa moyo wa kufanya vizuri zaidi, sasa una maana au faida gani hata huko uliko kwa hao wamarekani. KEEP IT UP dada Dina, Kila la kheri
Kuhusu kipindi chake kuwa na uswahili ni kweli hasa part ya taarabu, ila nadhani kabla hajarusha kipindi chake utawala ulisharidhia na ndio maana tunakisikia hewani, taarabu ni uswahili sasa lazima aonyeshe uswahili huo, labda sivyo alivyo ila ana act ili kipindi kunogesha uswahili ktk taarabu. Dada Dina labda tu ufikirie jinsi gani utaboresha part hiyo ya uswahili ndani ya kipindi chako ili wapenzi wasikilizaji wako waridhike wote, ni sehemu ya jukumu lako kuridhisha wasikilizaji wako. Ila kwa GEA yeye hamna kitu, anaonekana wazi! hata kijijini anakotoka MAZINDE huko korogwe hakuna maendeleo ni uchawi tuuu wasambaa wanaendekeza! na shule haiwezi hata akishauriwa kwenda atachora zero vyeti vyote, na ndio anayezidisha uswahili kipindini.
mwanangu nimekutembelea leo umenifurahisha sana na kunifariji katika mahojiano yako yoe naamini mungu anakuongoza endelea hivo amina.
unikumbuke unasikia nina mengi nataka tuongee asante.
UKWELI NI KWAMBA MIMI SIJAWAHI KUMSIKILIZA AKITANGAZA ILA TUU KUPITIA MANDIKO HAYA NAAMINI HUYU ANAKIPAJI HICHO NA ANAHITAJI MSAADA WA UIMIRISHAJI WA KAZI YAKE .
Yani nlikuwa natamani sana kumuona dina, nimefurahi sn kwa sababu huwa nasikiliza leo tena. hongera,