Raisi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Chilla Tenga(pichani), amechaguliwa kuwa Raisi mpya wa Shirikisho la Soka la Nchi za Afrika Mashariki (CECAFA).. Kufuatia uteuzi huo Leodgar Tenga hivi sasa anakuwa Raisi wa TFF na CECAFA kwa mpigo. BC inampongeza na kumtakia kila la kheri katika majukumu yake mapya.

Picha kwa hisani ya Maggid Mjengwa

Feedback / Comments

9 Responses to “RAISI MPYA WA CECAFA NI LEODGAR TENGA.”

  1. Comment by TanzanianDream on December 7th, 2007 6:20 pm

    Hata mimi nampongeza….Sasa ni kweli unaongoza East n’ central lkn pliz TAnzania ipe kipaumbele maana bado ni Rais wetu…Pamoja.

  2. Comment by TanzanianDream on December 7th, 2007 6:27 pm

    Dina nimeona comment inasema una blogu embu ukipita hapa weka link ili niweze kuibookmark hapa….

  3. Comment by John. on December 7th, 2007 11:12 pm

    Nampongeza, asilewe sifa,akaze buti ili Mwaka 2010 Cecafa itoe timu hata mbili kwenye word Cup.Sio kila siku West and Nort Africa ndio zitambe.”Kama wao wameweza wa nini hata sisi tushindwe tu nanininiiii?”

    John.

  4. Comment by Kekue on December 8th, 2007 1:02 am

    Hongera sana, umetufanya wantanzania tujisikie tuko juu juuu zaidi.

  5. Comment by Mchunguzi on December 8th, 2007 3:53 am

    Mweeh!
    Mbona ka Msomali!?!
    Khaa!

  6. Comment by any on December 8th, 2007 7:33 am

    ana smile nzuri,

  7. Comment by Subira on December 8th, 2007 12:31 pm

    Sio kama msomali tu ni kama mkikuyu, mmasai, mnubi. Nimeona wachaga wengine wengi wako hivyo kama wamachame, na wakibosho wengi wanafanana kama hayo makabila hapo juu, haya ma-anthropologists watuambie wachaga walitokea wapi kiasili north au south au central? Wana ujamaa na wakamba au wakikuyu? Ni wabantu au wahima?

    Haya yote hayana umuhimu cha umuhimu ni kuwa Tenga umetufanya tumalizie huu mwaka vizuri hongera sana, tunataka tuone mabadiliko ya kweli katika CECAFA kama mdau alivyosema hapo juu angalau timu zetu ziingie fainali ya kombe la dunia.

  8. Comment by any on December 9th, 2007 12:11 pm

    Ivi tenga mchaga?
    wachaga hatu belong kwenye yote uliyotaja apo juu Subi,nachojua wachaga ni jamii ya karibu sana na wamasai wa Kenya.

  9. Comment by Mama Wawili wa K'nyama on December 9th, 2007 4:20 pm

    Sir Tenga,
    Hongera sana.
    Big up. Asante kwa kupeperusha bendera ya Tanzania vema. Tutakuombea mwenyezi mungu akutangulie katika kila jambo.
    Bidii, uadilifu na uongozi bora viendelee kuwa katika vipengere vya dira yako binafsi katika wajibu wako huu mpya.
    Uzalendo uwe karibu sana nawe.
    Nimalize kwa kusema tena hongera and keep the big fire burning.
    Pia anza kuwabeep CAF n FIFA. The sky is your limit boy. Keep going
    Mama Wawili

Leave a Reply