
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange, akirejea katika jukwaa kuu mara baada ya kukagua gwaride la heshima leo katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Picha kwa hisani ya Freddy Maro.
Feedback / Comments
8 Responses to “UHURU DAY KITAIFA”
Leave a Reply


Presidaa safi anatembea akitafakari maono ya Watanzania miaka mingiiii baada ya uhuru. Mhusika Ikulu angepaswa atoe ushauri kwa rais ili avae tu angalau tai yenye rangi za Taifa na suti inayolandana kwa siku kama hii. Mpambe wa Mama wa Kwanza anastahili kupokea huu ujumbe wangu wa pongezi na nyongeza mbili za heshima kwa hekima na ubunifu wake wa leo.
Afande Mwamnyange nakusifu kwa utanashati lakini kumbuka askari akiwa anatembea siku zoteeeeeeeeeee MACHO MBELEEEEEEEEEEEE! muachie mnusaji aliye nyuma yako kazi ya kuangalia chini na kunusa kila kona!
Mkata Issue
Tarehe 09.12(9 Disemba) Uhuru Day?????????
Ok.Ni Uhuru Day.Swali Je ni Uhuru wa Nchi gani???Mimi Masikini wa watu najua ni Uhuru wa nchi moja inaitwa TANGANYIKA. Sijui wewe mwenzangu unasemaje.Lakini vilevile nijuavyo mimi kama ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika,basi inatakiwa tuienzi Tanganyika.Nilitegemea kuona bendera ya Tanganyika ikipepea kuashiria kweli Tanganyika ilipata Uhuru tarehe hiyo.Kuashiria ni ile bendera Cap.Nyirenda aliyoipeleka pale kileleni kilimanjaro.Mmmmmh! Changa la macho.
Siyo kuwa Siitaki bendera ya Tanzania. Hapana.Bendera ya Tanzania nayo ingepeperushwa siku Tanzania ilipozaliwa. Naamini inafahamika siku ya Muungano.
Nimepata shida sana kujua sababu za kwa nini Bendera ya Tanganyika haipepei wakati ya Zanzibar inapeperushwa.Huko Zanzibar si bendera tu bali hata wimbo la Taifa la Zanzibar pia unaimbwa.Napata kigugumizi kusema labda kabla ya Muungano nchi ya Tanganyika haikuwa na Wimbo wake wa Taifa.Rais alikuwa akipandishiwa bendera kimya kimya tuu.Lakini wapi.Nawakumbuka wale MANJU wa enzi hizo walivyokuwa mahiri kwa fani zao.
Inasikitisha wakati wa Sikukuu ya mapinduzi kuimbwa zile nyimbo za mapinduzi.Lakini Tanganyika NO nyimbozz wala bendera shinanizzz.Kwa niniii?????
Naogopa nikisema kuwa Watanganyika wametawaliwa na wazanzibari.Lakini huo ndo ukweli.Hapa nilipo kuna mgahawa mmoja wa wachina,kuna wapishi 2 WAZANZIBAR. Kamwe sijawahi kusikia wakijiita watanzania.Nami nikapata hasira nikaanza kujiita mtanganyika.Loooo!!!Nilichekwa na watanganyika wenzangu wote wanaojiita watanzania.Mbali ya yote
MTIKILA UKO WAPI UTUJUVYE MAMBO HAYA????
Mungu Ibariki Tanganyika
Waongoze viongozi kuturudishia uhuru na heshima yetu ya kitaifa (Tanganyika) iliyosaritiwa siku nyingi,ndipo tuew watanzania.
Majita
anaonekana kachokaaa huyo kikwete na anajuta kwa nini kawa rais
Zanzibar kila mwaka wanasherekea ..MAPINZUDI…tena wana kamsemo katamu.MAPINDUZIIIIIIIIIIIIIII..Daimaaaaaaa.
Siye watanganyika..yaani ndio maana lile lizungu lilisema lina mashaka na kauwezo ketu ka kufikiri na kungamua mambo.
Sasa tunakomaa uhuru dei wa Tanzania…
makubwa.
TANGANYIKA ndio tumeitosa sio…
Jumatatu njema.
Muunganao uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar hauna maana yoyote kwa Watanganyika na huenda anayejua siri yote ni Marehemu Nyerere ila nadhani kwenye mafaili hizo siri zipo vile vile.
Mimi huwa nakerwa sana na hawa Wazanzibari wanapokuwa huku nje ya nchi ambavyo hawataki kabisa kuitwa Watanzania kwa kuonyesha utengano wa wazi wazi na mara nyingi hujiita wazanzibari….na ni kweli. Sijui kwa nini nchi yenye watu zaidi ya milioni 36 itawaliwe na kakisiwa kaliko na watu sijui milioni 2 tu! Nafasi zote huwa tunagawana nao sawa kule bungeni, katika balozi zetu nje lazima wawepo wazanzibari, hata nakumbuka ilikuwa ni lazima chuo kikuu cha Dar es salaam kichukue idadi fulani ya wanafunzi kutoka Zanzibar, nk
Ningefurahi kama hivi visiwa viwili vingeachiwa na vijitawale vyenyewe na tubaki kuwa watanganyika na kuzingatia mipaka ya ki-utaifa. Haiwezekani kuwa tuko kwenye muungano wakati Zanzibari ina wimbo wake wa taifa na bendera yao. Ukiangalia viongozi watano wakubwa wa serikali ya Muungano watatu wote wanatoka Zanzibari (makamu wa rais, rais wa zanzibar na waziri kiongozi)…sisi huku tunabaki na rais na waziri mkuu tu!…..hivi ni kwa nini lakini?
Nauchukia sana muungano basi tu!
tanzania ni nchi ya amani, all the best watanzania endeleeni na mshikamano kw anjia mbalimabli kama vile sanaa, maonyesho na maneno ya busara.
Joseph acha zako, unataka Zanzibar wajitawale ili iweje??unajua sisi wabara tunaoishi hapa Znz wasivyotupenda kisa kitabu kimetupitia na ajira tunazo si haba kama wanavyosema wenyewe, tatizo ni kwamba wao elimu wengi wao ni zero na hawana wanachofanya zaidi ya kukaa the so called “MASKANI”usiseme kitu usichokuwa na experience nacho hasa ukizingatia ajira ni ngumu wakijitawala ujue sie wengine ni migration within 24hrs inatupitia.
Wewe mwenyewe umeshuhudia wakijiita zanzibarians while they are Tanzanians…it is ubaguzi tosha.
I am not really happy seeing a lot of mess around!…It is very unfortunate that every high government post needs a single person!