
Pichani ni kikosi cha kwanza cha Timu ya Soka ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars ambacho jioni hii kimetupwa nje ya Mashindano ya kugombea Kombe la Challenge kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati baada ya kufungwa magoli 2-1 na Timu ya Taifa ya Sudan. Kili Stars imetolewa katika hatua ya robo fainali katika mashindano hayo yanayoendelea katika vituo vya Dar-es-salaam na Arusha.
Majina ya wachezaji hao wa Kilimanjaro Stars ambo wote kwa pamoja ni “celebrities” wakubwa katika michezo (soka) ni kama ifuatavyo. Walio mstari wa mbele toka kushoto, Dani Mrwanda,Amir Mafta,Ali Mustafa ‘Bartez’,Uhuru Suleiman na Nizar Khalfan.
Mstari wa nyuma toka Kulia-Salum Swedi, Shaban Nditi,Michael Chuma,Erasto Nyoni,Meshack Abel na Castory Mumbara.
Safari ya soka la bongo bado inaelekea kuwa ndefu.
Picha kwa hisani ya Issa Michuzi.
Page 1 of 3 | Next page