
Sio jambo rahisi na wanamuziki wasio wengi duniani wanaweza kufanya.Tunazungumzia kuimba na kutumia kifaa chochote cha kimuziki (kama gitaa,piano,ngoma nk) wakati huo huo.
Carola Kinasha(pichani) ni mmojawapo miongoni mwa wanamuziki tulionao nchini Tanzania ambao wanaweza kufanya hivyo.Carola anaweza kuimba na wakati huo huo kucharaza gitaa kama anavyoonekana pichani hapo juu.Habari za undani za Carola Kinasha unaweza kuzipata kwa kutembelea tovuti yake kwa kubonyeza hapa.
Halafu bado kuna ule ubishi/mjadala kwamba mtu anayejua kuimba tu huku akiwa hawezi kutumia kifaa chochote cha kimuziki, hastahili kuitwa mwanamuziki bali mwimbaji tu peke yake.Ni kweli? Wewe unasemaje?
Picha kwa hisani ya Bob Sankofa.
Page 1 of 3 | Next page