MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

 

Bila hiana wala ubishi, DDC Mlimani Park(Wana-Sikinde Ngoma ya Ukae) ni mojawapo ya bendi zilizowahi kutamba na kujizolea sifa kemkem nchini Tanzania. Pichani ni kikosi kizito cha Wana-Sikinde.Ili kupata majina kamili na nafasi zao katika bendi,tuliwasiliana na Fresh Jumbe ambaye siku za nyuma aliwahi kutamba na Sikinde. Biila kusita Fresh alitupa captioning nzuri kabisa ya picha hii ya Sikinde.Fresh hivi sasa anafanyia kazi zake za muziki nchini Japan.Mwaka jana tuliwahi kufanya naye mahojiano ambayo,kama yalikupita,unaweza kuyasoma kwa kubonyeza hapa.

WALIOSIMAMA NYUMA TOKA KUSHOTO:Habibu Abbas Mgalusi “Jeff” (Drums), Wa pili jina limenitoka, anayefuatia ni Shaaban Lendi (saxphone), Hamisi Milambo (Trumpet), Nyuma ya Hamisi Milambo ni Kalamazoo (Saxphone), Huruka Uvuruge (Rhythm guitar), Machaku Salum (Trumpet), Kassim Rashid “Kizunga” (Lead guitar), Charles Ngosha (Bass) na Ali Jamwaka au Ali “Tumba” (Congers).

WALIOCHUCHUMAA MBELE TOKA KUSHOTO:Wa kwanza simjui, wa pili ni Juma Shabani (Drums) (Huyu nilikuwanae Dar International, Anaefuata mwenye kofia ni Tino Masinge (Muimbaji) nae pia nilikuwa nae Dar International na nimeimba nae karibu nyimbo zote kule Super Bomboka, alijiunga na Sikinde baada ya mimi kutoka. Anaemfuatia Tino kwa nyuma kidogo simjui, anaefuatia mwenye viatu vyeupe ni Husein Jumbe (Muimbaji), nyuma ya husein Jumbe aliyeshikwa bega na Dede simjui, halafu Shaaban Dede (aliyegeuka nyuma na kumshika mwenzie bega (Muimbaji), baada ya Dede kwa mbele kidogo ni Adam Bakari “Sauti ya zege” (Muimbaji), Nyuma kidogo ya Adam ni Hassan Kunyata (Muimbaji), Baada ya Kunyata ni Joseph Bernard (Saxphone) na wa mwisho kabisa mwenye kipara simjui.

Picha kwa msaada mkubwa wa MichuziJR.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

11 Responses to “NGOMA YA UKAE”

  1. Comment by Nkwanga on January 8th, 2008 11:43 am

    Huyo mwenye upara anaitwa Mbaraka Othman ni mpuliza Trumpet.

  2. Comment by Edwin Ndaki on January 8th, 2008 4:32 pm

    Ndinge ukipenda ..sikinde wapo njema..ila wazee OTTU wapo juu zaidi…aaaa aaaa

  3. Comment by james on January 11th, 2008 5:50 pm

    NGOJA NI KUSAIDIE FRESH JUMBE KUNA WA2 MIMI NAWAJUA WAPILI TOKA KULIA WALIOCHUCHUMA NI SAUTI YA ZEGE(ADAM BAKARI) NA ALIEKUWA NYUMA YA DEDE NI KUNYATA HAO WOTE NI WAIMBAJI WENZIO.

  4. Comment by james on January 11th, 2008 5:54 pm

    SORRY. NIMEWATAJA WATU AMBAO WASHATAJWA SASA FRESH NGOJA NIKUFAHAMISHE HUYO WAPILI WALIOSIMAMA TOKA SHOTO NI MPIGA GITAA ANAITWA MJUSI SHEMBOZA

  5. Comment by Senyandumi on January 12th, 2008 6:17 am

    Baada ya Jeff ni mpiga solo “Mapessa” na baada ya Tino ni jina linakimbia kidogo marehemu huyu alikua mkristo afu akabadili jina alikua hana makuu kabisa alitunga na kuimba wimbo wa “nawashukuru wazazi wangu-najiona kama niko songea”nimemkumbuka “Lubua”.Doo nashukuru nimemkumbuka nilikua nampenda sana akiimba katulia hana mbwembwe wala maringo.Sasa BC nakupa kazi katika picha hii kama wachache wao hatunao tena kwa kutaja wachache Tino na Lubua,machaku na kassim Rashid,na katika picha wamefuatana pia Adam Bakari “sauti ya zege”kazi kwako nenda DDC kariakoo(old trafford)upate ukweli zaidi.umenikumbusha mbali sana.Tchao

  6. Comment by Senyandumi on January 12th, 2008 6:56 am

    Ngoja niongeze kidogo alibadili dini na kuitwa Nasir Lubua.Fresh Jumbe hupaswi kumsahau huyu ni mmoja wa waliokua waimbaji wenye sauti na kipaji cha hali ya juu,yeye na marehemu Mwinyikondo sauti zao ni kama Bitchuka.BC kama unaukumbuka hule wimbo wa “Easter asukapo rasta wanamuonea wivu”.Duuh,basi nisiendelee sana na kwaherini

  7. Comment by james on January 14th, 2008 4:34 pm

    DUUH MMENOA KABISA HII PICHA IMEPIGWA WAKATI WA WIMBO WA NACHECHEMEA WAKATI HUO NASRI RUBUA AU FRANCIS RUBUA ALIKUWA AMESHAKUFA.

  8. Comment by Senyandumi on January 15th, 2008 9:56 am

    Wewe bwana James yaelekea huijui Nginde tafadhali usijepotosha watu hatupo katika mashindano hapa ni katika kuelimishana na kuweka kumbukumbu sawa kwa ajili yetu na wengineo waliopo na wajao.Binafsi ninafahamiana na wanamziki wote wa Nginde mmojammoja na trupu zima pia ni friends wa nginde hivo sitoweza kubahatisha.Tafadhali elimika

  9. Comment by Anthony Angasisye Kisondella on January 18th, 2008 1:03 am

    Mimi ni mpenzi mkubwa wa Sikinde, ningependa kuirekebisha lineup ya wana sikinde kama ifuatavyo: -

    WALIOSIMAMA NYUMA TOKA KUSHOTO: Habibu Abbas Mgalusi “Jeff” (Drums), Ramadhani Mapesa “Solo dola”( Lead guitar), Shaban Lendi (|Saxphone), Hamis Mirambo (Trumpet), nyuma ya Shabani Lendi ni Mohamed Juma Banduki “Super Tall” (Keyboard) na SIO KALAMAZOO kama Fresh Jumbe Asemavyo, Huruka Uvuruge (Rhythm guitar),Machaku Salum (Trumpet), Kassim Rashid “Kizunga” (Lead guitar), Charles John “Ngosha” (Bass) na Ali Jamwaka (Congers). Aliyechuchumaa mbele na chini ya Machaku Salum ni Fadhili Uvuruge

    WALIOCHUCHUMAA MBELE TOKA KUSHOTO: Wa kwanza ni Gervas Herman (solo) huyu alitokea Magereza Jazz Band Pamoja na Mohamed Juma Banduki “Super Tall” (Keyboard), wa pili ni Juma Choka (Drums) SIO JUMA SHABANI kama Fresh Jumbe asemavyo, Tino Masinge “arawa”(Muimbaji), halafu John Malyanga (Bass guitar), Husein Jumbe (Muimbaji), nyuma ya Husein Jumbe aliyeshikwa bega na Dede ni Fadhili Uvuruge, halafu Shaaban Dede (Muimbaji), (aliyegeuka nyuma na kumshika Fadhili Uvuruge bega baada ya Dede kwa mbele kidogo ni Adam Bakari “Sauti ya zege” (Muimbaji), Nyuma kidogo ya Adam ni Hassan Kunyata (Muimbaji), Baada ya Kunyata ni Joseph Bernard (Saxphone) na wa mwisho kabisa mwenye kipara ni Mbaraka Othmani (Trumpet)

    Picha hii ilipigiwa siku ya “Summer Jam” (Dar es Salaam Fiesta) kule kwenye viwanja vya Leaders Club – Kinondoni kama sikosei ilikuwa Jumapili ya tarehe 11/08/2002 na mie kama mkereketwa wa sikinde nilikuwa pale.

    Aidha katika safu hiyo kuna mapungufu makubwa kwani baadhi yao wamefariki, mwenyezi Mungu aziweka roho zao mahali pema peponi nao ni Mohamed Juma Banduki “Super Tall” ambaye alikuwa anapiga kinanda, Machaku Salum ambaye aikuwa anapiga trumpet, Kassim Rashid “Kizunga” ambaye alikuwa anapiga gita la kuongoza (solo), Gervas Herman ambaye alikuwa gita la luongoza la solo pamoja na gita la kati (Rhythm), Tino Masinge “arawa” ambaye alikuwa muimbaji, Adam Bakari “Sauti ya zege” ambaye alikuwa muimbaji

  10. Comment by Anthony Angasisye Kisondella on January 18th, 2008 1:16 am

    Senyandumi nashukuru kwa kumrekebisha James, inaonekana James anahisi tu lakini hawafahamu vizuri wanamuziki wa sikinde, kwanza Mjusi Shemboza hayupo kwenye hiyo picha japokuwa kwa hivi sasa anapigia Sikinde, aidha Kama anamtaja Nasir (Francis) Lubua kuwa wakati wimbo wa nachechemea alikuwa amefariki, sivyo kumbuka album yote ya sikinde ya Nachechemea iliimbwa na waimbaji wafuatao Shabani Dede, Hussein Jumbe, Hassan Kunyata, Nasir (Francis) Lubua na Adam Bakari “Sauti ya zege”. Jamani kama mtu anataka kujua masuala ya sikinde basi tuwasiliane kwa email: aakisondella@yahoo.com ili tusipotoshe wadau

  11. Comment by shaban on October 28th, 2009 12:42 am

    nimefurahi sana

Leave a Reply