Jina la Dr.Willibrod Peter Slaa (pichani),Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Karatu, hivi sasa linaweza kuwa jina ambalo linatajwa zaidi kushinda lingine lolote katika anga za kisiasa nchini Tanzania.Wananchi wengi wanamuongelea kama kiongozi shujaa,aliye tayari kudiriki kufanya au kusema chochote katika kutetea maslahi ya wananchi hususani wale wanaoitwa “wa kawaida” na wenye hali duni za kimaisha.Angekuwa anaishi katika nchi za magharibi,Dr.Slaa angeitwa “whistleblower” nambari wani jina ambalo hupewa mtu anayeamua kuwa mkakamavu na kukemea mienendo mibaya na isiyofaa ya watu walioko kwenye madaraka fulani nk, potelea mbali kinachoweza kumtokea kutokana na ujasiri huo.
Kwanini jina la Dr.Wilbrod Slaa liwe vinywani mwa watanzania wengi hivi sasa?Jibu ni rahisi;ni kutokana na mchango wake katika kufichua “ufisadi” uliokuwa unafanyika katika Benki Kuu ya Tanzania(BOT) na mambo mengi mengineyo ambayo anahisi yanakwenda visivyo.
Ingawa umaarufu wa Dr.Slaa haujaanzia na suala la BOT,ni wazi kwamba sakata hili ndilo limefanya jina lake liwe miongoni mwa majina maarufu sio tu kutoka kambi ya upinzani bali katika anga za wanasiasa kote nchini Tanzania.
Lakini Dr.Slaa ni nani?Anatokea wapi?Wangapi wanafahamu alikuwa akifanya nini kabla hajaingia kwenye siasa? Tangu ameingia kwenye siasa amepata mafanikio gani? Anasemaje kuhusu sakata zima la BOT?Ameridhika na maamuzi yaliyochukuliwa na Rais Kikwete?Ana ujumbe gani kwa wananchi?Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo, hivi karibuni tulipata fursa ya kufanya naye mahojiano rasmi.Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Dr.Slaa karibu sana ndani ya www.bongocelebrity.com. Ni heshima kwetu kupata nafasi hii ya kufanya nawe mahojiano.Jambo la kwanza kabisa ambalo tunaamini wasomaji wetu wangependa kujua ni kuhusu historia yako. Je, unaweza kutueleza ulizaliwa wapi,lini,ukasomea wapi mpaka kufikia hadhi ya udaktari wa falsafa?

WS:Historia fupi, nilizaliwa Kwermusl, Mbulu, Tanzania, tarehe 29.10.1948.Lakini ili kukidhi haja ya swali hili zima,labda tuambatanishe CV au BIODATA yangu kama ifuatavyo;
CURICULUM VITAE(BIODATA)
Full Name: Willibord Peter Slaa.
Date and Place of Birth: 29.10.1948,Kwermusl,Mbulu,Tanzania.
EDUCATION:
PRIMARY: 1958-1961 Kwermusl
1962-1965 Karatu Middle School.
SECONDARY: 1966-1969 Dunguyi Seminary
1970-1971 Itaga Seminary
PHILOSOPHY:
1972-1973 Kibosho Seminary
THEOLOGY:
1974-1977 Kipalapala Seminary
1974-1976 Makerere University,Diploma,Theology
HIGHER EDUCATION:
1979-1981 Pontifical Urba University,Rome,JCD(summa cum laude)
1980-1980 ADV.Diploma-Socio-Political Studies,Koln,Germany(KAF)
1981-1981 St.Thomas Aquinas University,Rome,AD.Diploma Rural Development
1985-1985 London COR.College, Principles and Practice of Management Certificate.
WORK EXPERIENCE:
2000-Todate Member of Parliament(MP),Karatu
1995-2000 Member of Parliament(MP),Karatu.
1991-1995 Executive Director,Tanzania Society for The Blind.
1986-1991 Secretary General,Tanzania Episcopal Conference(TEC)
1982-1986 Development Director,Diocese of Mbulu
1982-1986 Vicar General,Diocese of Mbulu
1977-1979 Development Director,Diocese of Mbulu (Catholic Priest 1977-1991)
MEMBERSHIP IN LOCAL AND INTERNATIONAL BODIES
2006-Todate: Deputy Leader,Official Opposition, Parliament of Tanzania
2000- Todate: Vice President, Forum of African Parliamentarians on Education( FAPED)
2004-Todate: Secretary General,CHADEMA.
2001-Todate: Member,Special Education Committee,MOEC/SADC.
2000-Todate: Shadow Minister,Legal and Constitutional Affairs.
1998-2004 Vice Chairman,CHADEMA
1998-2003 Chairman, Inter-Parliamentary Forum (SADC-PF)
1996-2000 Member,ACP-EU Joint Parliamentary Assembly
1994-Todate: Chairman,Comprehensive Community Based Rehabilitation Tanzania (CCBRT)
Page 1 of 8 | Next page