MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kama bado hujapata muda wa kuisoma ripoti ya kamati teule ya bunge kama ilivyowakilishwa jana bungeni na mwenyekiti wa kamati hiyo,Mbunge wa Kyela,Dr.Harrison Mwakyembe,tunashauri uisome.Ripoti imeanisha mambo mazito na pia kutoa mapendekezo muhimu.

Baadhi ya majina ya wanasiasa maarufu(celebrity politicians) na watendaji wengine muhimu serikalini ambao wametajwa kwenye ripoti hiyo huku wakihusishwa,kwa njia moja au nyingine,na Richmond Saga ni PM,Edward Lowassa,Ibrahim Msabaha,Rostam Azizi,Karamagi,Daniel Yona,Arthur Mwakapugi na wengineo kibao au kama wanavyoonekana pichani juu.Unaweza kuisoma ripoti hiyo kwenye post ya hapo chini ukibonyeza pale kwenye (more).Ni ndefu lakini worth reading.Ni wazi kwamba hivi sasa swali sio tena tunakwenda wapi bali tumefikaje hapa?

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

26 Responses to “WALIOTAJWA”

  1. Comment by Liz Baraka on February 7th, 2008 1:34 am

    Ushahidi umeshapatikana hakuna cha kusubiria, waachishwe kazi kwa manufaa ya umma.

  2. Comment by NYAKATAKULE UNYILISYA ECHALO on February 7th, 2008 2:07 am

    TANGAZO
    NDUGU WATANZANIA WENZANGU NA RAFIKI ZETU WOTE,

    BADO TUMEPIGWA BUTWAA NA TAARIFA YA WAZI YA KAMATI TEULE YA BUNGE ILIYOCHUNGUZA ZABUNI NA MKATABA NA KAMPUNI YA RICHMOND YA HOUSTON MAREKANI.

    BAADA YA UCHUNGUZI WA KINA, TUMETHIBITISHIWA KUWA HATA BAADHI YA VIONGOZI WETU WA NGAZI YA JUU SERIKALINI WALIAMUA PASIPO AIBU WALA KUJALI MASLAHI YA UMMA NA TARATIBU ZA KIUTENDAJI KULAZIMISHA KUINGIA MKATABA NA HII ASASI FEKI .

    TUKIO HILI LIMETUINGIZIA HASARA KUBWA KATIKA TANESCO NA ZAIDI KWA MWANANCHI AMBAYE BADO ANAENDELEA KUHANGAIKA KUKIDHI MAHITAJI YA KAWAIDA YA MAISHA YAKE.

    AIDHA CHOMBO KAMA TAKURURU PIA KUSHINDWA KUWEKA HADHARANI HILI RADHI LA UFISADI, BADALA YAKE WAKATUELEZA KUWA MAMBO NI SHWARI WAKATI SI SHWARI NI DALILI ZA KUWEPO MNYORORO WA UOZO KATIKA KUZIMA NURU YA MWENGE WETU PINDI UFISADI UNAPOMILIKWA.

    KWA NGUVU NA MAMLAKA YA UMMA TULIYONAYO SISI WANANCHI, LEO TUNASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MAADILI YA UONGOZI NCHINI MWETU KILICHOTOKEA KUANZIA OFISI YA WAZIRI MKUU.

    KWA UHURU WA KIKATIBA WA KUJIELEZA NILIONAO KAMA RAIA MMOJAWAPO NILIYEGUSWA NA HUU MSIBA, BINAFSI NAPENDEKEZA TUWE NA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO KATIKA BLOGU HII NA KWINGINEKO KOKOTE WAANDISHI WA HABARI NA WADAU WATAKAPOTUUNGA MKONO ILI TUTAFAKARI JUU YA HUU MSIBA NA ULE ULIOTUSIBU HIVI KARIBUNI WA BOT AMBAPO BADO TUNATAFUTA MCHAWI LICHA YA WATAALAMU KUTUELEZA WAZIWAZI SABABU YA KIFO NA JUU YA TAARIFA ZA MAHUTUTI MBALIMBALI TULIZONAZO AMBAZO BADO ZINAFANYIWA UCHUNGUZI.

    TUKIWA KATIKA SIMANZI HII TUTOE MAWAZO YETU KWA HEKIMA KWA MIHIMILI MITATU YA NCHI (SERIKALI, BUNGE NA MAHAKAMA) NINI KIFANYIKE WAKATI WA MAZISHI NA KATIKA KUTUOKOA NA BALAA HILI LEO NA KWA VIZAZI VIJAVYO.

    HIVYO NAPENDEKEZA KUWA TUKIWA KATIKA MAOMBOLEZO HAYA NDANI YA HIZO SIKU TATU, BENDERA YA LIBENEKE YA BLOGU IPEPERUSHWE NUSU MLINGOTI KWA KUPOSTI PICHA NA MAANDISHI YANAYOHUSU MISIBA HII TU NA SI VINGINEVYO.

    AZIMIO LA ARUSHA LILIWEKA, AZIMIO LA ZANZIBAR LIKATWAA,
    JINA LA MAADILI YA UONGOZI CHINI YA
    NGAO ZETU ZA UHURU NA UMOJA LIDUMISHWE.

    NAWASILISHA,

    MDAU,

    NYAKATAKULE UNYILISYA ECHALO

  3. Comment by amina on February 7th, 2008 2:19 am

    mi nakwambia wote wajjiuzulu na huyo karamagi ndo nilikua namtamani sana walimnyasinyasi zito bungeni sasa kiko wapi?miwani mbaya

  4. Comment by khadija on February 7th, 2008 2:53 am

    Jamani jamani hawa watu hawana hata haya hivi hela zote hizo wanazipeleka wapi? yaani wananchi wa hali ya chini wanaishi bila hata kuwa na uhakika wa maisha wao wanakusanya mijihela yote hiyo, hivi wataenda kusema nini mbele za mungu? kwa kunyonya jasho za watu ambao hawajiwezi? sasa jamani muwe makini sasa hivi watu wamechoka wako tayari kwa lolote kwa hiyo nyie mafisi mjihadhari kwani mambo ya Kenywa yatakuja Tz na ya kenya itakuwa cha mtoto kwa maani tumechoka.

    Yaani mtu unapokea kamshahara kadogo lakini katakatwa kodi hadi unasema hiki nini, matokeo yake wanakuwa watu ambao wameshashiba, hivi huu ni uroho gani? Ila kwa upande wangu nawapongeza sana wabunge, wanatupa matumaini wananchi, na bado uchaguzi ujao tunataka tuingize wasome zaidi huko bungeni ili waweze kutusaidia.Hongera Mwakyembe yaani wewe nafikiri utakuwa mbunge hadi wewe mwenyewe useme basi, kwa maana unatukosha sana wananchi kwanza unaongea kwa kujiamini na una wasiwasi kabisa sasa tungepata wabunge hata japo kumi kama mwakyembe tungesonga mbele kidogo. Lakini watanzania tuzidi kuomba mungu tu tutawapata wabunge kama mwakyembe.

  5. Comment by scritygospel on February 7th, 2008 3:26 am

    Hongera sana Dr.Harrison Mwakyembe kwa kutueleza ukweli.
    Watanzania tumekukubali kweli ulituahidi utafanya kweli leo yametimia.

  6. Comment by mkata issue on February 7th, 2008 3:50 am

    Lowasa amejiengua tayari kesho anapandishwa kizimbani na atakuwa huko magereza kwa muda maana hakuna dhamana. Huyu ni mkosefu mbaya zaidi kuliko hata akina maumba maana athari zake ni kwa watu karibu millioni 40.

  7. Comment by Hassan on February 7th, 2008 3:53 am

    One step ahead in our liberation struggle, to gain independence toward accountability and Responsibility. We must know there is no one above the law. We must all know that no stone will left UNTURNED!

  8. Comment by Chris on February 7th, 2008 5:02 am

    This is what we were waiting.Akina Msabaha, Karamagi, Yona, Mkapa wajumuishwe pamoja na Lowassa ili kuwajibishwa sasa. Kumbe tunaendelea vizuri sasa,tutafika tuu.Bado Kikwete tu kutumia lungu lake, i mean kukunja sura…

  9. Comment by kijiwe on February 7th, 2008 5:07 am

    Kuna watu dunia hii wana roho mbaya sana kweli hawa jamaa walivyo na pesa bado wakaona ni poa kujiongezea pesa kwa kuwatesa wananchi.
    Haya ndiy mabo yanayoleta ethnic violence duniani mimi sitaki kutabiri hilli ia the way it is now kama hawa jamaa hawapelekwi mahakamani then tunaelekea direction nyingine yaani violence inanukia and siyo jadi yetu but believe me hii itawakasirisa watu wengi sana

  10. Comment by kijiwe on February 7th, 2008 5:43 am

    kumradhi maneno yameteleza kidogo nawasilisha edited version hapo chini.

    Kuna watu dunia hii wana roho mbaya sana kweli hawa jamaa walivyo na pesa bado wakaona ni poa kujiongezea pesa kwa kuwatesa wananchi.
    Huyu Lowasa mimi nina machungu naye personal maana namjua yeye na familia yake kwa undani zaidi sista wangu alikuwa anasoma na mtoto wake na pia jamaa alikuwa anakuja botswana kuzitumbua pesa zake yupo underground sana anaoperate like some sort of mafia hivi kwa hiyo he is not what people think he is. Haya ndiyo mambo yanayoleta ethnic violence duniani mimi sitaki kutabiri hili ila the way it is now kama hawa jamaa wote especially Lowasa hawapelekwi mahakamani then tunaelekea direction nyingine yaani violence inanukia and siyo jadi yetu but believe me hii itawakasirisha watu wengi sana

  11. Comment by Kimori on February 7th, 2008 5:57 am

    Waw!…..Lowassa has already tendered his resignation and I expect others to follow the suit…no joke in this 21st century! We need at least a clean government, which can bring obout tangible changes to the citizens…we are really tired of fake leaders!

  12. Comment by Edwin Ndaki on February 7th, 2008 6:05 am

    Duu…mmhm..hii ndio tz.

    Safari moja uanzisha nyingine.

    Edo kajiuzulu,hio ni safari kaanzisha.Nafikiri itakuwa busara wengine kufuata nyayo zake .

    PCCB ..aibu hiyo inawakuta ,kudondosha taulo ukweni.Edo hosea na wewe jiuzulu.

    Yaani mwaka huu ni Edo Ndaki tu ndio nabaki madarakani nikitoa maoni.

    Ene wei..tutafika tu.

  13. Comment by daniel on February 7th, 2008 6:15 am

    naomba hao watu wahukumiwe kunyongwa

  14. Comment by Revo on February 7th, 2008 6:27 am

    “Kioo, kioo, alikivunja nani?, sijui sijui, wa mwisho akamatweeeeee!”

    Nawasilisha.

  15. Comment by olivia on February 7th, 2008 6:30 am

    Fisadi karamangi anasubiri nini ku stepdown. I’m sick seeing his face. Fisadi mkubwa. mmenyonya jasho la wazazi wetu sana.

  16. Comment by Mtanzania Mkereketwa HHH on February 7th, 2008 8:00 am

    Inanishangaza sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
    Kuwaona ninyi viongozi wetu tuliowachagua kwa kura zetu za siri kuwaona mnatabasabu hapa pichani wakati sisi twafa kwa njaa sababu ya uchu wenu wa utajiri.

    Kabla ya yote naipa pongezi kamati ilioundwa kutuletea ukweki wote kuhusu Rich mond(richmonduli) kwani inaonyesha kweli hizi ni zama za uwazi na ukweli.

    Mimi kama mkereketwa nawasi sana na majukumu walionayo baadhi ya viongozi wetu sijui ni kujisahau au ni kutokujua kilichowapeleka madarakani na kuanza kufanya mambo ya aibu kama alilofanya Lowasa na wenzake samahani kwa kumwita hivyo kwani mpak sasa sio PM tena kwa kashfa hii.

    Lakini amejaribu kujitetea mi naona is 2 leti kama wanvyowakorapt wengine kwa nini asingeikorapri kamati mapema mpaka amedhalilishwa namna hii?kama anavyodai? halafu anatudanganya watu wazima eti hawakumtendea haki wangemuuluza. Yeye kwa mawazo yake anafikiri angeulizwa angekubali au? hii ndio maana kamati ikafanya kazi wangemuuliza ukweli usingepatikana lakini pamoja na hayo kuulizwa au kutokuulizwa hakubadilishi ripoti kama wewe fisadi ni fisadi tu.

    SIKU ZOTE MFA MAJI HAISHI KUTAPATAPA.
    Tujihadhari san na hizi ngozi nyeupe wengi wao hawtupendi hata kidogo nikujineemesha tu
    Nawasisi hata na huu ujio wa raisi wa marekani tanzania kama sio kuwatafutia watu wake ambao amewachoka nchini kwake makazi nasi tuwapappatikie kumbe hawana lolote ni kama mateja wetu nao ni mateja marekani. lakini tungojee matokeo yake

  17. Comment by Kidon'goi ole Kiteytey... on February 7th, 2008 8:25 am

    Kwi kwi kwi tugawane mali zake mimi naanza na lile shamba la Ngómbe 3000 la Handeni….

  18. Comment by lala on February 7th, 2008 8:52 am

    Jamani nimefurahi sanaa sana tu,maana niliingiwa wasiwasi kwamba labda watanzania tumekua malimbukeni kulifumbia macho swala zito kama hili.
    ni muhimu wahusika wote kuwajibishwa ipasavyo ili waliobaki wajue kwamba watanzania tumechoshwa na upuuzi wa muundo mzima wa serikali yetu,na mambo ya kiholela kama watu hawajaenda shule bwana!!!
    its about time kilaza wastep down and watu wenye uchungu na nchi yao wastep in.

  19. Comment by ola on February 7th, 2008 8:59 am

    MWALIMU NYERERE ALIKUA NA MAANA SANA NA ALIONA MBALI WAKATI ALIPOKATA LOWASSA KUGOMBEA CHEO NYETI KAMA HIKI.
    MWALIMU ALIONA MBALI SANAA JAMANI,MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI.

  20. Comment by MAZWIGANG'ONDI on February 7th, 2008 10:05 am

    Pamoja na hayo yote, tukumbukeni kuwa yalishasemwa na wapinzani tukabaki tunawashangaa. Sasa nadhani rais ivunje balaza la mawaziri lote na awaondoe wale wote wanaotuhumiwa na wanaonuka rushwa. Wananchi tukichoka hatutakuwa na subira tena. Kama TAKUKURU wanadanganya, je wanayoyachnguza sasa watayaleta kwa usawa?

  21. Comment by hasira on February 7th, 2008 2:22 pm

    huyu Dr. Harrosin Mwakyembe asipoangalia watamu-Amina Chifupa. Na wakimu-Amina Chifupa ndio hapo watakapokiona kivumbi chake

  22. Comment by mstari on February 7th, 2008 5:12 pm

    MUNGU mkubwa na leo hii ndugu zangu wote mmeyaona,ila hayo tisa na kumi yaja muda c mrefu,kuna watu wanaona wao ndio tanzania km yao,km huyu lowassa,na km tungewaacha huko mbeleni wasingeshikika kabisa mana ingekua km mafioso vile,tunamuombea MUNGU bwana mwakyembe ili wasimdhuru,mana sijaona jasiri kama yeye kwa kizazi hiki na kujiuzulu haitoshi tunataka kuona wanafikishwa panapostahili na watulipe hela zote walizochukua,km hawana wafilisiwe,ila km nimngekua rais nafikiri adhabu ya kwanza kufikiri ni kifo kwa hawa wote waliohusika,ndio mana mwl.jk nyerere aliuliza hawa wahindi wanatafuta nn bungeni,na leo tumeona ya rostam aziz yani kila soo kubwa linalohusu hela bongo lazima kuwe na wahindi,nafikri wkt umefika sasa kufanya km ya iddi amini dada hapo uganda,maombi ya wabongo sasa yanajibiwa na si ajabu siku hata rais ambae na yeye anajifanya msafi akavuliwa nguo bungeni,naomba tuwaombee wale walio kwenye kamati ya madini nao wawe na nguvu na kuthubutu km kulikoonyeshwa jana na dr.harrison,ahsanteni sana.

  23. Comment by Peter M on February 7th, 2008 8:40 pm

    Siku zote uongo na ukweli vinajitenga, na siku za wezi ni arobaini, halafu bado na mengine yatakuja. Wanyan’ganyi wote lazima wafilisiwe na washtakiwe. AIBU KUBWA. Lakini afadhali tunaanza kupona. Na wabunge wetu safari hii wamekataa kupigwa sindano ya ganzi; Walikuwa wapi siku zote hizi jamani, mbona kuna watu wangepona au wangepeleka watoto wao shule kama wangekuwa makini namna hii miaka yote! Tusaidie kuwauliza hao walikuwa wapi siku zote wakati tunaibiwa na watu amabao wanatucheke kila siku. Ndugu zangu, mlikuwa wapi?, mlilishwa nini? Hebu mtujibu na nyie!! Kama wafidhuli wasingeiibia nchi hii kwa miaka 40 Tanzania ingekuwa mbali sana. Bara bara zote kubwa zingekuwa za lami, hospitali zingekuwa super, mashule yetu yangekuwa mazuri sana. Na ajira ingekuwa tele tele, wamachinga wangepungua kwa asilimia 80%. KIKWETE amaekuwa Garbachovu wa Tanzania, HONGERA SANA. JE NA CHAMA CHETU nacho je? mara ngapi kimekumbatia huo ududu? Je kinataka kujisafisha au nacho kijiuzulu? Haki bin Haki tu!! ??

  24. Comment by amina on February 8th, 2008 3:07 am

    waende zao….ila bado kuna safari ndefu kwa watanzania watakaoteuliwa nao watakua walewale

  25. Comment by yunginfamous on February 8th, 2008 4:12 am

    hehehheh….. hizo zote kelele za mbu nje ya neti :)
    So guys, are you gonna bark all day or you gonna bite??!!

  26. Comment by Matty on February 8th, 2008 7:56 am

    Bora nchi iuzwe tugawane mshiko!!!!!nawatania jamani eheeee.
    Ona wanavyotabasamu??coz wanajua washatunyonya wanyonge, wengine hapo sura wamekunja!!!utafikiri wako serious na maendeleo ya nchi yetu kumbe wamejilimbikizia mimali ya kufa mtu!
    WAFILISIWEEEEEEEEEEEEEE

Leave a Reply