
Pichani ni Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania na miongoni mwa wanasheria mahiri ambao Tanzania inajivunia.Pamoja na hayo katika siku za hivi karibuni amekuwa akitoa kauli mbalimbali ambazo kwa kiasi kikubwa zinawachanganya wananchi.Mfano ni kauli yake ya hivi karibuni kuhusiana na suala la kujiuzulu kwa Lowassa na jinsi ambavyo tume ya Mwakyembe “haikumuita” EL ili kumpa nafasi ya kujitetea.
Jaji Warioba alizaliwa tarehe 3 Septemba mwaka 1940 huko wilayani Bunda mkoani Mara. Alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuanzia tarehe 5 Novemba mwaka 1985 mpaka tarehe 9 Novemba mwaka 1990 alipompisha John Samuel Malecela.Unaweza ukapata zaidi CV yake kwa kubonyeza hapa.
Page 1 of 3 | Next page