MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Ijumaa nyingine imewadia.Mwezi wa pili ndio unakatika hivyo.Naona kama vile mwaka huu unaenda kwa kasi sana.Wewe unaonaje? Pamoja na hayo sisi wanadamu hatutakiwi kwenda kwa haraka sana kwani mwenda pole huwa hajikwai,au sio?

 

Kwa ujumla ujumbe huo ndio uliomo kwenye burudani yetu ya leo.Leo tunalo jina kubwa katika muziki wa dansi nchini Tanzania.Juwata Jazz Band.Wimbo unaitwa Msafiri Kakiri ukiwa ni utunzi wake Marehemu TX Moshi William(jina halisi Shaaban Ally Mhoja Kishiwa) ambaye alitutoka mwezi Machi 2006.Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

 

Ukisikiliza wimbo huu utakiri jambo moja muhimu sana.Utunzi wa nyimbo enzi zile ulikuwa sio lelemama.Ilikuwa ni lazima wimbo uwe na ujumbe mzito na unaoeleweka.Burudani ilikuwa inakwenda sambamba na kuelimishana haswa.Nadhani wanamuziki wa leo wanaweza kujifunza mengi kwa japo tu kusikiliza tungo za wakongwe kama TX Moshi na wengineo wengi.Asikudanganye mtu,nyimbo zenye ujumbe wa maana na unaoeleweka bado na zitaendelea kuwa na nafasi sana katika mioyo ya wapenzi wa muziki.Kwa hiyo,wanamuziki wa leo au wa kizazi kipya,jitahidini basi,au sio?

 

Katika wimbo huu,gitaa la solo lilipigwa na Abdi Ridhiwani(Totoo) Rhythm na Pishuu,bass guitar na Issa Ramadhani huku saxophones zikiwa chini ya usimamizi wa Mnenge,Abdi Mketema na Hagai Kauzeni.Mnaojua zaidi mtarekebisha kama kuna makosa.Kama kawaida,bonyeza player hapo chini upate burudani.Ijumaa Njema

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

9 Responses to “MSAFIRI KAKIRI-JUWATA JAZZ BAND”

  1. Comment by majuto Kitobo on February 29th, 2008 1:51 pm

    Asikudanganye mtu…muziki wa TZ ndo huu hapa. Hizi kele za kitoto ama Bongo Flava ni ujinga mtupu tu. Sijawahi kusikia wimbo wowote wa Flava wenye maana, zote ni masuala ya pipipi tu na ujinga wa kuchukuliana mademu, Hii yote kwa sababu kila mtu aliyeshindwa maisha Bongo anataka aimbe Flava matokeo yake ndo hivi…ujinga wa kujifananisha na kina black americans na kuimba porojo. BC leteni raha kamili tuwekeeni nyimbo zetu za asili.

  2. Comment by Emmanuel-kingsstudio on February 29th, 2008 5:59 pm

    Hongera sana BC.
    Hayo ni mambo ya kiutuuzima.Sanaa ya muziki ina raha yake.Hapo umetuwekea miongoni mwa sauti adimu za dhahabu zenye maadili yasiyo kifani,ambayo ubora wake hautakoma…

  3. Comment by jomaeli on March 4th, 2008 9:14 am

    majuto kitobo nakukubali..kweli bc huu ndo mziki

  4. Comment by Saidi Situ on March 6th, 2008 11:20 am

    Yeyote anyeupenda huu mziki lazima ni mtu mzima. Yaani umri umeenda na nyimbo hii inamkumbusha mbali sana. Ni haki kupenda huu mziki na sio bongo flava maana ni kitu ulichozoea.

    Vijana wa siku hizi tunaokuwa na bongo flava mziki kama huu lazima tuone mbaya. Kwa maoni yangu kitakachokufanya huu mziki uupendi kuliko mavituz ya Alikiba na wengineyo ni umri.

    Kama unaupenda huu mziki kwa dhati basi jijue kuwa umo miongoni mwa watu wazima.

  5. Comment by Fred on March 7th, 2008 6:00 am

    jina la wimbo ni msafiri kakiri au kafiri!

  6. Comment by Kamanzi on March 9th, 2008 5:25 am

    Jina la wimbo ni MSAFIRI KAKIRI sio KAFIRI. Yaani amekiri kuwa mwenda pole ajikwai upo hapo Fred?

  7. Comment by DUNDA GALDEN on April 2nd, 2008 3:20 pm

    NITAIWEKA BC KUWA HOME PAGE KILA NIKIWA NA FIKRA KUH MYUMBANI NAWEZA KUSOMA NA KUBURUDIKA HASWA KWA UJUMBE NA MAWAZO YA WANA WA BC HATA VIBAO VIKALI KAMA HIKI MSAFIRI KAKIRI TOKA NYUMBANI BONGO MPAKA HAPA AUSTRALIA DARWIN NDUGU ZANGU YOTE MAISHA LAZIMA TUKILI REMEMBER HOME IS HOME
    CHAFOSA CHAI GODA NEVER DIE

  8. Comment by yohana francis on May 9th, 2008 7:46 am

    Napingana na mawazo ya said situ kuwa muziki kama huu ni wawatu ambao umri umesha kwenda, sio kweli kabisa, muhimu hapa ni kujua maana ya kuwa mwanamuziki. mwanamuziki anatakiwa kuelimisha jamii, kuburudisha na kuonya sasa mambo hayo sio suala la umri na suala la ujuzi. vijana wengi wa sasa awajui muziki wanakimbila uko katika namna ya kuganga njaa.
    wanaona raha kuonekana katika luninga tu. awana vipaji vya muziki, na ndio maana tungo zao hazidumu. hakuna wimbo unaoweza kukaa kwenye chati kwa miaka 5 kwa kuwa tungo azilengi jamii na tungo nyingi zinalenga watu wachache tu, si ajabu kuwa na wimbo unaotaja majina ya marafiki wa mtunzi tu.

  9. Comment by Sally on June 23rd, 2008 2:19 am

    Oooh gosh……This song is one of those can’t get enough of when playing, goes straight to to “the” heart.

Leave a Reply