Ingawa vyombo vya habari mbalimbali,katika nyakati tofauti tofauti,vimekuwa vikiandika habari zake na yeye kualikwa katika mihadhara mbalimbali kuzungumzia masuala ya kujitolea, umasikini,maradhi na mambo mbalimbali yahusuyo ubinaadamu,yawezekana kabisa ukawa hujawahi kulisikia jina lake wala kuiona sura yake.
Anaitwa John Mashaka (pichani),kijana mdogo wa miaka 30 ambaye kama walivyo watanzania wengine wengi, anakerwa na hali za umasikini,ujinga na maradhi zinazowakabili mamilioni ya watanzania hivi leo.Tofauti yake na watanzania wengine wengi ni kwamba yeye ameamua kujitoa mhanga kusema na pia kusaidia kwa hali na mali anapoweza.Kwa maana nyingine,John Mashaka ni kijana ambaye anajaribu kuamsha upya hali ya kujitolea bila kujali sana hali ya utajiri aliyo nayo.Anasisitiza kile ambacho tumekuwa tukiambiwa tangu enzi na enzi;Kutoa ni moyo na wala sio utajiri.
Pamoja na hayo,hivi karibuni, habari zake zilipotolewa kwenye blog maarufu ya Issa Michuzi, mjadala mkubwa ulizuka kuhusu anachojaribu au alichowahi kukifanya.Kama kawaida ya binadamu,wapo waliomuunga mkono na wapo waliompinga kwa nguvu huku wakidai kwamba huenda anajitafutia tu “umaarufu” au kujifagilia njia ya kisiasa.Wengi wakawa wamemhukumu bila kumpa nafasi ya kumsikiliza.
Baada ya kusoma ule mjadala na kutafakari mambo kadhaa,BC tuliamua kumtafuta bwana Mashaka ili kufanya naye mahojiano utakayoyasoma hivi punde.John Mashaka ni nani?Je,Mashaka anajiandalia tu njia ya kuukwaa “ubunge” siku za mbeleni?Je ni kweli anakerwa kwa dhati na matatizo yanayomkabili mtanzania wa kawaida hivi leo?Vipi,inawezekana na wewe ukamuunga mkono katika anachojaribu kukifanya?You will be the Judge!Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Mashaka,Shukrani sana kwa kukubali kufanya nasi mahojiano haya.Kwanza kabisa watu wengi wangependa kufahamu kidogo kuhusu historia ya maisha yako.Unaweza kutuambia ulizaliwa lini,wapi na kisha ukasomea wapi mpaka kufikia hapo ulipo hivi sasa?
JM: Nimezaliwa na kukulia huko Tanzania miaka 30 iliyopita, na hatimaye kusoma shule ya msingi na sekondari nchini Kenya kabla ya kujiunga na elimu ya juu nchini Marekani kwa shahada za kwanza na zingine za juu.
BC: Hivi sasa hapo nchini Marekani unajishughulisha na nini haswa? Unafanya kazi gani?
JM: Nafanya kazi kama Investment Banker. Ila, sitapendelea elimu yangu, au nafasi yangu katika jamii, ihusishwe na kazi zangu au wito kwa binadamu wenzangu. Sipendelei kuyazungumzia kwa sababu haya yote ni batili tunapolizungumzia suala la ubinadamu.
Let my character and deeds decide on who I am. Elimu isiyotumika katika njia sahihi ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kijamii inakuwa ni mzigo mkubwa, nafasi au cheo isiyo na manufaa kwa binadamu wenzetu inakuwa kero.
Wapo vijana wengi wenye elimu, na kazi nzuri kuliko mimi ambao wanahitaji msukumo au changamoto ili nao pia wasaidie nyumbani. Ila nikiingia ndani sana kuhusu kazi ninazozifanya nahisi kwamba nitakuwa nakiuka imani zangu na baraka za Mwenyezi Mungu, na kuikaribisha jeuri.
BC: Mara nyingi waafrika tumekuwa tukitupiwa lawama kwamba hatuna moyo wa kujitolea(volunteerism) ikilinganishwa na wenzetu wa nchi za magharibi. Je unakubaliana na lawama hizi na kama ndio unadhani ni kwanini waafrika hatupendi au hatuko mstari wa mbele katika kujitolea? Nini kinaweza kufanyika ili kubadili hali hiyo?
JM: Waafrika tumsilaumu shetani.Shetani ni sisi wenyewe. Kumsaidia mwenzio inakuwa shida kwa kuhofia atakushinda bila kufahamu ya kwamba shida inayomkabili mwenzio hivi leo usiposaidia kuitatua itakuja kukuathiri hata wewe mwenyewe kesho.Siyo lazima uwe na hela au tajiri ndio uweze kusaidia.Yeyote anaweza kusaidia. Kuna watoto wengi wanaoharibikiwa maishani kwa kukosa muongozo mzuri ili wawe raia wema, na hii inaweza kutekelezwa na mtu yeyote mwenye moyo wa kujitolea siyo lazima uwe na hela nyingi kama ambavyo wengi tunadhania.
Sioni kitu cha ajabu kwa mtu kujitolea kwani ni jambo la kawaida huku katika nchi za magharibi au Ulaya kama ilivyozoelekwa miongoni mwa wengi.Ajabu ni kwamba tunaporudi kusaidia nyumbani kila mtu wazo lake ni ubunge au siasa. Nadhani hii kasumba inatokana na mazingira mtu anayoishi ambayo yanatawaliwa na wanasiasa.
Maendeleo katika jamii hayaletwi na mwanasiasa, yanaletwa na watu kama mimi na wewe.Kujitolea hali na mali ndio dawa pekee ya kukomesha ujambazi, uzururaji na pia wimbi la watoto yatima wanaojitokeza kila kona,kila kukicha.
Hii ndio dawa pekee dhidi ya umasikini siyo kuwatazama macho viongozi tukidhania kwamba watatuletea miujiza. Uongozi lazima uanzie kwenye nafsi zetu. Sikuzaliwa na chochote, maishani nimesaidiwa, sikusaidiwa na mwanasiasa hata mmoja nilisaidiwa na raia wa kawaida.
BC: Tangu habari zako zianze kusambaa kupitia vyombo vya habari na blogs mbalimbali za watanzania, kumekuwepo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakidai kwamba wewe unasaidia yatima ili kujiwekea mazingira ya kugombea nafasi za kisiasa baadaye(kama ubunge) au kujipatia tu umaarufu na mambo kama hayo.Unasemaje kuhusu shutuma au habari kama hizo?
JM: Kuna umaarufu wa aina mbili.Umaarufu unaotokana na wema (vipaji maalum) na ule unaotokana na uovu. Sitapenda umaarufu wa aina yoyote, kwa maana nikiwa maarufu kutokana na wema, nitakuwa natekeleza jukumu langu kama binadamu.Wote tumeumbwa ili tupendane na kutenda wema. Namuomba Mungu anipe moyo wa unyenyekevu ili niepukane na tabia mbovu kama kiburi ambayo ni matunda ya umaarufu.
Nakumbuka mwandishi wa habari Tanzania aliniuliza swali kama hilo, lakini kwa kifupi ni kwamba mabadiliko katika jamii siyo lazima yaletwe na mbunge au mwanasiasa.
Wote tuna majukumu ya kuibadilisha sura za jamii zetu, nchi yetu, bara letu na pia dunia kwa ujumla. Raia wa kawaida anayeguswa na matatizo yanayoikabili nchi lazima atatafuta namna ya kusaidia.
Hebu niambie, utafurahi kumuona mtoto anakufa kwa kukosa matibabu ilhali hela unayo mfukoni? Ni lazime uwe mwanasiasa ndo uchungu ukuingie?
Haja ilipokuwepo Afrika Kusini, Nelson Mandela alijitolea na kupata mateso ili nchi yake iondokane na ubeberu. Haja ilipokuwepo nchini India, Mahatma Ghandhi alijitolea nafsi yake ili nchi yake iondokane na ukandamizaji toka kwa mwingereza. Kadhalika Marekani walibarikiwa kumpata Martin Luther King ambaye aliyatoa maisha yake kwa ajili ya watu weusi.
Unapoishi katika mataifa kama haya kwa kipindi kirefu na kurudi nyumbani kuiona hali ya kawaida, utajiona kama msaliti usiposaidia.
Nadhani hata Yesu alipokuwa duniani alitupiwa shutuma za kila rangi akafika hata kusulubiwa. Sitashangaa nikikimbiwa na ndugu hata marafiki kutokana na imani yangu. Hakika sitaweza kuikana ukweli kwa ajili ya urafiki wa kibinadamu.

BC: Je shutuma kama hizo huwa zinakufanya wakati mwingine utake kukata tamaa kuhusu misheni yako ya kusaidia ma-yatima na wengine wasiojiweza?
JM: Siwezi kukata tamaa kutokana na shutuma kutoka kwa watu wachache kwani mambo kama haya ni ya kawaida maishani. Wapo wanaokutakia mema, na wengine wanaoomba usiamke usingizini, lakini yote ni ya Mungu. Watu kama hao wapo, nawaombea Mungu awaguse nao wauone mwanga na kuweza kujitolea kuliokoa taifa lao na binadamu kwa ujumla.
Sidhani kama kuna shutuma, kwa maana sijaenda kwa mtu kuomba anisaidie chochote, yote nafanya mwenyewe kutokana na kipato changu kidogo. Na iwapo wapo watu wa aina hiyo, basi shutuma zao nitazichukulia kama msukumo wa kutafuta ufumbuzi zaidi ili nao pia waguswe ili badala ya kushutumu washirikiane na mimi katika hizi shuguli za kutafuta amani.
Nitafurahi sana kukutana na mtu hata mmoja mwenye rekodi ya ubinadamu ambaye anaweza kujadili maswala kwa ufasaha ili tutafute ufumbuzi zaidi wa matatizo yetu ya kijamii.
BC: Kwa mtazamo wako,kibinadamu na kisha kitaaluma kama mchumi, unadhani umasikini uliotapakaa hivi leo barani Afrika na sehemu zinginezo nyingi duniani, unatokana na nini? Nini kiini cha tatizo la umasikini?
JM: Sitaki niingie katika kundi la watu wanaobeza au kulaumu kila kitu, umasikini na vita barani Afrika kwa ukoloni au nchi za magharibi. Uhuru tumeupata miaka zaidi ya arubaini iliyopita. Mpaka leo hatujatambua kwamba nchi yetu ndio moja ya nchi matajiri katika bara la Afrika.Bahari ya India inatosha kuifanya Tanzania nchi tajiri kuliko nchi zote Afrika ikiwa tutaweka mikakati mizuri na uongozi mzuri wa kuitumia. Tazama Dubai, ina nini zaidi ya Tanzania? Kitega uchumi chake kikubwa ni bandari zake.
Vivutio vyetu vya kitalii na kihistoria vinatosha kuiweka Tanzania katika kundi la nchi zenye nguvu zaidi kiuchumi. Amani na utulivu tulionao nchini vinatosha kuwakaribisha wawekezaji toka pande zote za dunia.
Ukoloni isiwe kigezo. Kwani nchi kusini mwa Afrika kama Zimbabwe ilipata maendeleo makubwa chini ya utawala wa kigeni, hadi pale Mugabe alipoibuka upya na sera zake za karne ya kumi na saba na kusambaratisha uchumi na kuifanya Zimbabwe kuwa kicheko cha uongozi bora Afrika.
Vitu ambavyo ningependa kuvizungumzia ni , bidii ya kazi, uadilifu, uzalendo na upendo kwa binadamu wenzetu. Mzalendo hawezi kuiba mabillioni ya fedha toka nchi masikini kama Tanzania na kuzirudisha Uingereza, Uswisi na kwingineko zilikotoka ilhali watu wake wanakufa na njaa.
Mtu mwenye upendo katika nafsi yake, kamwe hawezi kuishi kama mfalme na kuzidi kuiuza nchi yake ilhali amezungukwa na ma millioni ya watu wasio na matumaini maishani, wanaoishi kwa miujiza siku hadi siku
Israel ni nchi ndogo sana, haina chochote (utajiri)kulinganisha na Tanzania. Hii nchi imezungukwa na “lethal and vicious enemies”, lakini licha ya haya yote , ndio moja ya nchi zilizoendelea sana duniani. This clearly tells us that, where there is need there is a way. If our leaders had the passion and love for their country, then we would have been far by now.
Rather than being pessimistic, I am optimistic, and very confident, that our current president will soon tap the talents he has at his disposal to implement his economic policies stagnated by the corrupt individuals who are giving him headache day and night.
BC: Sina uhakika kama unafuatilia kwa karibu siasa za Tanzania. Pamoja na hayo ningependa kukuuliza; unadhani Tanzania hivi leo inapiga hatua kwenda mbele au nyuma kunako suala zima la kuleta maendeleo kwa mwananchi wa kawaida?
JM: Kashfa ya Richmond imeleta matumaini makubwa kuona Bunge likijadili kwa uzalendo wa hali ya juu hili suala la aibu, ambapo chama tawala na upinzani vilishirikiana kwa maslahi ya nchi. Huu ni ukomavu mkubwa hasa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.
Kinachoididimiza Tanzania kwa upande mwingine ni mwananchi mwenyewe.Unapouza kura yako kwa chai kikombe kimoja, unauza haki za watoto wako kupata elimu bora, huduma nzuri za kiafya na mengineyo. Unapompigia kura kiongozi fisadi ambaye miaka nenda rudi anajilimbikiza utajiri unategemea nini?
Rais siyo mungu, ni binadamu.Lazima wananchi wampe viongozi wema wenye uzalendo na kujituma. Hawezi kufanya kila kitu mwenyewe, anahitaji usaidizi. Wananchi inabidi wamchague kiongozi kutokana na utendaji wake, siyo kutokana na chama chake cha kisiasa.
Tanzania ina mwelekeo mzuri chini ya uongozi wa rais Kikwete , ukizingatia, kwa mara ya kwanza, tunaona matangazo ya mali asili za Tanzania katika televisheni kama CNN , FOX, CBS etc. Kilichobaki ni kwamba sheria za Tanzania itabidi zibadilishwe ili Rais awe na uwezo wa kuteua mawaziri au viongozi ambao siyo wabunge kwa maana Tanzania ina watu wenye vipaji vya hali ya juu ambao siyo wabunge
Kadhalika, ingekuwa vyema ikiwa viongozi wote watalazimishwa kusaini mikataba ya utekelezaji kila baada ya mwaka mmoja.Yule atakayeshindwa itabidi aachie ngazi. Bila shaka kutakuwepo utekelezaji wa hali ya juu katika wizara na mashirika yote ya umma.
BC: Katika mahojiano yako uliyofanya na gazeti la Charlotte Observer ulionyesha kukerwa sana na chuki miongoni mwetu binadamu,vita na mateso mbalimbali yanayowakumba binadamu duniani kote. Ungeshauri nini kifanyike?
JM: Binadamu wa karne ya ishirini na moja amepiga hatua kubwa sana katika fani zote; Amefika mwezini, amegundua tiba dhidi ya maradhi mengi. Binadamu amerahishisha mawasiliano kwa kuifanya dunia ionekane kama kidude kidogo, lakini cha kusikitisha licha ya maendeleo makubwa tuliyoyapata,tumeshindwa kupendana.
Tunauana, tunachukiana kupita kiasi, wengine wanakufa kwa njaa ilhali wachache wamebeba utajiri wa dunia mikononi mwao, na hii ndo sababu kubwa hatuna amani.
Lengo langu kubwa au nia yangu kubwa ni Amani na upendo baina ya binadamu. Lengo langu kubwa ni kuleta matumaini kwa binadamu wenzangu bila ya kujali rangi wala mpaka. Sitapendelea kumtazama binadamu kutokana na kabila au tabaka lake. Rwanda, Sierra Leone, Sudan, Kenya etc. Ni mifano ambayo inaonyesha binadamu asivyo na hutu. Ni kwa nini tuuane, kwa nini watoto na wanawake wasiokuwa na hatia wachomwe moto wakiwa hai?
Huzuni, lakini kweli, ni kwamba amani ya aina hii haiwezi kudumu kwani anayeshindwa daima anakuwa na kinyongo cha kulipiza kisasi rohoni. Ila mbegu za upendo daima zitazaa amani. Kama binadamu mwingine, namuomba Mungu anipe nguvu na muda kidogo kuishi ili angalau niguse mioyo michache ambayo pia inaweza kuyasambaza hizi mbegu za upendo ili amani iwepo duniani.
Amani haiji kwa mtutu wa Bunduki au mapanga, amani haiji kwa mabomu. Amani inapatikana pale watu wanapokaa na kujadili namna ya kusuluhisha matatizo. Amani haipo binadamu anapokosa chakula, amani haipo pasipo tumaini, amani haipo pasipo haki. Ni lazima tuungane kwa pamoja ili tutafute ufumbuzi wa haya maswala.
Binadamu ndiye kiumbe pekee Mungu alimuumba kwa mkono wake akampa akili za kufanya maajabu, na kwa bahati mbaya ndiye kiumbe hatari kuliko wote. Suluhisho ni kuibadilisha mioyo sugu kwa kuitendea mema.
BC: Kila mwaka wewe hupenda kutembelea Tanzania na kutoa misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto yatima na pia kusaidia watu wengine wenye shida.Ni vituo gani mpaka hivi sasa ambavyo huwa unavipelekea msaada kule nyumbani?Je ungependa kutoa ujumbe gani kwa watanzania.
JM: Ni bahati mbaya kwamba kila ulifanyalo katika hii karne ni lazima itapatikana katika vyombo vya habari. Ningekuwa na uwezo ningejaribu namna ya kufanya haya mambo kimya kimya. Kwani nimeanza hizi shughuli mwaka 2000 nikiwa chuo kikuu.Lakini pale nilipoanza kushirikiana na watu, basi habari nyingi zikawa zinaenea kila kona.
Nakumbuka msaada wangu wa kwanza ilikuwa ni kwa watoto waathirika wa ukimwi mwaka 2000 huko Bukoba.Na huo msaada niliutoa kupitia kwa masista wa kikatoliki.
Nisingependa kutaja ni vitu gani au hela ngapi nimetoa, nimetembelea vituo vingi Dar es salaam. Kijijini, huko Musoma, mara nyingi nimewapelekea chakula na kusaidia katika matatizo mbalimbali, nimesaidia wajane, wazee na watu wasiojiweza lakini nisingependa kutaja vitu nilivyofanya.Nadhani jamii itanihukumu kwa kusaidia kwa malengo tofauti. Mimi ni mtumishi wao, chochote ninachokifanya, nakifanya kutokana na ukweli kwamba walijinyima na kunituma kutalii na kujifunza namna ya kuwakomboa. Kwa hiyo sioni sababu ya kuyazungumzia niliyoyafanya.
BC: Utawashauri vipi wengine wenye uwezo wa kufanya hivyo, kuhusu umuhimu wa kusaidia watoto yatima na masikini wengine nyumbani Tanzania?
JM: Kusaidia katika jamii siyo swala la utajiri. Mimi siyo tajiri na siwezi kuwa tajiri kutokana na majukumu niliyonayo.Sina lolote, nafanya kazi kama vijana wengine wa kitanzania wanaohangaika pale Kariakoo. Sina tofauti na vijana wengine wanaoishi kwa kubahatisha huko vijijini, ila najiona kama mwakilishi au mtumishi wao waliyemtuma kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.Kinachohitajika ni kuwa na moyo wa kujituma bila kutegemea chochote kwa kutenda wema.
BC: Kuna msemo usemao kwamba “Nipe samaki na utakuwa umenilisha kwa leo.Nifundishe jinsi ya kuvua samaki na utakuwa umenilisha milele’. Sasa unapoangalia suala zima la kusaidiana na kutoa misaada hivi leo, unadhani ni juhudi gani zinaweza kufanyika,kwa upande wa serikali na watu binafsi na taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali katika kuhakikisha kwamba misaada inayotolewa inalenga zaidi katika kuwafundisha watu “kuvua samaki” na sio kuwalisha kwa siku moja tu?
JM: Ili binadamu azidi kuwa hai na mwenye afya bora na akili timamu ni lazima apate chakula, mavazi na sehemu ya kujisitiri. Lengo langu siyo kuja kila mara na kugawa chakula, nitakuwa sisaidii ila nawadanganya wana jamii. Ila, kila kitu kina mwanzo wake, na huu ndo mwanzo na haya mahitaji ni muhimu
Natafuta mbinu au suluhisho za kudumu. Panapo majaaliwa, nitatumia baraka alizonipa Mungu, angalau niweze kutafuta usaidizi wa kudumu kama vile kujenga zahanati, shule na pia kuanzisha mfuko maalum wa kuwawezesha vijana wachache wenye vipaji wasio na uwezo waweze kupata elimu.
Mungu anatupa nafasi kama hizi pamoja na uhai kwa sababu zake; nina imani kwamba mipango yake itakuwa dhahiri pale tutakapoleta mabadiliko katika maisha ya wengine. Na ikiwa vijana waliobahatika watajitolea kusaidia mmoja mmoja, nadhani dunia itakuwa tofauti.
Suala la watoto yatima nafikiri serikali ingelitafutia suluhisho la kudumu, kwani kuwaona wanaandamana kama ilivyotokea huko Temeke, mwanzoni mwa mwaka huu wakidai haki yao, ni swala la kuhuzunisha, hasa ukizingatia kwamba misaada wanayopewa inaishia katika mifuko ya watu wengine.
Ni laana kwa mtu wa kawaida kuwachukulia watoto wasiokuwa na namna kama kitega uchumi. Licha ya hayo, taifa kama Tanzania ambalo limejengwa katika misingi ya undugu isingekuwa na vituo vya watoto mayatima, kwani ndugu na marafiki wange wafungulia hawa watoto milango yao.
BC: Kuna hii habari kwamba kuna wakati uliwahi kuuza gari lako binafsi ili ukawasaidie watu waliokuwa wamekumbwa na njaa kutokana na ukame huko kijijini kwenu Tanzania. Unaweza kutuambia kidogo hii ilikuwaje? Nini kilitokea mpaka ukachukua uamuzi wa kishujaa namna hiyo?
JM: Sioni ushujaa au kitu cha ajabu kwa mtu kuuza gari yake, kwani hivi ni vitu vya kidunia ambavyo tunakufa na kuviacha. Sipendi kuzungumzia hili swala kwa sababu ni jukumu langu kusaidia. Gari halina manufaa yoyote kwangu ikiwa watu wangu wanakufa kwa njaa.
Kumbuka kwamba, chochote chaweza kutokea na hiyo gari kuniua, au kunifanya kilema nisiweze kuitumia tena. Lakini binadamu mwenzangu anaweza kutoka katika baa la njaa na kunisaidia au kuninunulia magari mengine kumi. Au weka picha ambapo umezungukwa na na masikini kila kona, kila unapotembea na hiyo gari yako unaowaona ni watu wenye njaa, je amani ipo kweli hapo?
Nitakuwa mtumwa wa kiitikadi na wa kifikra nikikumbuka kwamba nilimuacha mtoto akafa kwa njaa ilhali nilikuwa na uwezo wa kuokoa maisha yake. Mungu amenibariki na akili timamu ya na bidii ya kazi, kwa hiyo thamani ya gari nisingeweza kuilinganisha na uhai wa binadamu.

BC: Tumesikia kwamba hivi sasa uko mbioni kuanzisha taasisi yako binafsi ambayo itashughulikia masuala mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania katika mambo kama vile elimu, afya nk. Unaweza kutuambia kidogo mipango inakwendaje mpaka hivi sasa?
JM: Maswala kama haya yanachukua muda, na pia yanafanywa kwa uangalifu kutokana na sheria za nchi. Suala hilo lipo mikononi mwa wanasheria wanaonisaidia, ila kila kitu kikiwa tayari nadhani mtafahamu kwa maana nitaisajili Tanzania pia, ila isije kutokea uzushi kwamba napata misaada toka kwa watu, hapana kila kitu ninachotoa ni kujinyima kwangu mwenyewe.
BC: Je umeshaoa bwana Mashaka?
JM: Bado!
BC: Mwisho una ujumbe gani kwa watanzania? Na kwa wale ambao wangependa kuungana nawe au kushirikiana nawe katika jitihada hizi wanawezaje kufanya hivyo?
JM: Development in a country is not a political leader’s responsibility; it is a common man’s work. Greatest achievements in the history of the universe, have been made by common men. Farmers, carpenters, teachers, businessmen and many others, cornered without a way out of their problems, are the ones finding ways, which in turn makes life easier for all of us. Therefore, our poverty should not discourage us, but propel us to strive higher.
I am sure, our society has people, who can leave memorable deeds, if only we could utilize our skills, talents and social potitions positively . Politicians, controlling their lust, civil servants being honest in their dealings, and those in the private sector working diligently, our country can re-write another chapter in the world history.
Those that we envy especially the western world, prospered through passion, discipline and hard work.
To my fellow young people, we are the future of Tanzania. We must not disappoint those who look up to us, by returning back to them with rotten cultures and behaviours. We have our own culture, which we should be proud of. We must sacrifice, and give our lives should the need be, in order to make the needed change.
Those privileged to have education, should share their knowledge with a broader society and not center their talents on themselves. The future of Tanzania, and peace for humanity lies in our hands, and this can be possible if only we could embrace each other not hate one another.
My harms and heart are open to anyone willing to join me in the effort to reduce suffering amongst our people, and I do believe, even though we can’t change the world, we make a difference by making the world more liveable and a peaceful place.
Feedback / Comments
163 Responses to ““KUTOA NI MOYO,SI UTAJIRI”-JOHN MASHAKA”
Leave a Reply


These are honest comments from a man with a mission for humanity and especially the poor and helpless people.
Hongera sana Bwana John Mashaka; asante kwa changamoto tosha ubarikiwe, keep up the good work.
Jeff na timu nzima ya BC shukrani kwa kazi nzuri mnayofanya
Mashaka ingependeza kama ushauri wako kwa watanzania ungekuwa katika lugha ya kiswahili.
Ni hilo tu, nakupa pongezi.
Nimefurahishwa na mpangilio wako wote hata kama ungekuwa unafanya vitu for ur own interest still u have done a very gud job and Iam very proud of u ,keep ur kareji dont let anyone put u down,ur wonderful sasa mbona umejiletea matatizo ndugu yangu unatangaza hadharani ujaoa ohhhhhhhhh kuna wakina MANKA- G luck
good interview big up!! would like to join your effort
Mimi binafsi nampongeza kwa kuwasaidia wasiojiweza kwa nafasi aliyonayo. lakini upande mwingine namuona kama msanii flani, maana si anaishi marekani huyu? sasa unajua wenzetu wamarekani baadhi yao matajiri wanapenda saana kusaidia mtu ambaye wanaona anaweza fikisha msaada kwa walengwa, na bila kujifanya kama anavyofanya hawezi pata pesa anayopewa. kwa maana hiyo kwa kuji-publishize magazetini, tv nk, inampa nafasi kubwa ya kuchota pesa zao. kwa kawaida ukimwelezea mtu maisha tuliyokulia katika jamii zetu ni ajabu mno kwao wanaweza hata watoe machozi wakati sisi kwetu ni kawaida. hivo mimi nasema Mashaka anafanya hivo ili ajiweke katika position ya kupewa misaada na hao wanene through which na yeye ananufaika humo, tunampongeza maana ni wachache wanaweza fanya kama yeye. It is not a big deal anyway, nafikiri baadaye arudi bongo agombee ubunge kijijini kwao ili awe karibu zaidi kuwasaidia watu wake. hayo ni maoni yangu.
MMMh JM
Haya mahojiano yamenigusa saaaana,
Mwanzoni nilisoma juu ya wewe kidogo kwenye blog ya bwana Michuzi…and I wanted to know more and more….
Mashaka ,Mungu akusaidie uweze kutimiza yale unayopenda kufanya kwa jamii.
Nakubaliana kabisa na mtizamo wako juu ya jamii inayotuzunguka,hasa nyumbani Tanzania.
Watanzania wakati umefika wa sisi kusimama na miguu yetu,kuhakikisha tunasaidia jamii kwa namna tunayoweza ili kujenga Tanzania isiyo na masikini,isiyo na yatima wasiojiweza,isiyo na majambazi wa kulazimika,Tanzania inayoweza kutoa maisha ya furaha kwa kila mtu….Inawezekana
I am very inspired, this guy sound intelligent and humble. I am ready to join the team and make changes in our lovely country Tanzania.
People like John are center point of poor country like Tanzania. He sound like a man of his words, charismatic and intelligent.
John, unaweza kunipata kupitia mtanganyika01@yahoo.com. Nipo US, and i can contribute anything to the portfolio. Poor Tanzania.
Tunakutakia mafanikio mema na jitihada zako, ni hayo tu lakini usije kufanya kitu kwa kutengea ,kitu fulani
ni kweli tupu na mwenyezi mungu anzidishie maisha marefu!
endelea na kaza buti…kama wanavyosema,
ok tumeona ushirikiano wake swali langu inakuaje anakuja Tanzania kwa mwaka mara moja hapo sijamwelewa, kwa misaada yake anayotoa
Swali lakujiuliza mimi na wewe “umefanya nini kwa jirani yako asiyejiweza kwa kadri ya vipawa ulivyobarikiwa” Kama kila mtu akiwa kama huyu mshikaji tutafika… Ila mafisadi mtu wa kawaida unapiga hatua mbili yeye anakurudisha hatua kumi.
Sikubaliani na JM aliposema, “…To my fellow young people, we are the future of Tanzania….” We the youngs,energetic, the workforce, we’re not the future.That’s too political n’ utopian thinking. We’re the ones to shape the future in different capacities….
Big up Mashaka.
What I can tell today is “May God bless you at this energitic age.” Ni wachache sana wenye imani kama yako
Be blessed.
Haya ni mahojiano mazuri sana BC, nimefurahia mtiririko wa wa maswali na majibu ya kaka Mashaka. Truly MZALENDO!!
Sina sababu ya kusita kutoa pongezi zangu kwa bwana mashaka,na ni mfano wa mtu mmoja katika watanzania 1000 kwa sasa,hii yote ni kwamba watanzania tumejaa na ubinafsi na kukosa upendo wa kweli miongoni mwetu.
Cha msingi kila anayeguswa basi ni vyema akatenda kama anayeyatenda bwana mashaka,pia kuna haja ya hata kushirikiana na bwana mashaka ili tuweze kupata amani ya kweli kwani ilipo njaa hakuna amani ya kweli.
Ushauri naomba BC utupatie contacts za karibu za bwana mashaka ili yeyote anayetaka kushirikiana katika hili akawasiliana naye ili kutatua matatizo kwa ujumla.
Zaidi ya yote namuomba Mungu azidi kumpa moyo wa kujitolea bwana mashaka na ampe watu wa kweli wa kumsaidia kiutendaji ili tupate tanzania yenye misingi ya haki,upendo na amani ya kweli
I am so proud to have read the good news fo what John is doing! I have known John since he was interning at ICTR here in Arusha and he is determined to end poverty in Tanzania. i recall meeting him when he visited TZ last yr and I was moved by his concern! As a person who has a legal background and now practising here in TZ, I would also like to help John in setting up the NGO that will assist our community as a whole. John I will mail you personally and congratulate on such an understanding beginning I wish you all the best
MMMh JM
Haya mahojiano yamenigusa saaaana,
Mwanzoni nilisoma juu ya wewe kidogo kwenye blog ya bwana Michuzi…and I wanted to know more and more….
Mashaka ,Mungu akusaidie uweze kutimiza yale unayopenda kufanya kwa jamii.
Nakubaliana kabisa na mtizamo wako juu ya jamii inayotuzunguka,hasa nyumbani Tanzania.
Watanzania wakati umefika wa sisi kusimama na miguu yetu,kuhakikisha tunasaidia jamii kwa namna tunayoweza ili kujenga Tanzania isiyo na masikini,isiyo na yatima wasiojiweza,isiyo na majambazi wa kulazimika,Tanzania inayoweza kutoa maisha ya furaha kwa kila mtu….Inawezekana
Hello Mr. Mashaka,
Hii ni mara yangu ya kwanza kusoma bongo celebrate yako, yaani nimeadmire sana sana sana, hongera sana kwa kuwa na moyo ambao Mungu wa kujitolea, ingawa wengi wanadhani unatafuta umaarufu while wakati si kweli, i cant just differentiate u na wale wanaotafuta umaarufu. Anyway keep it up i real admire ur mission and i wish u all the best.
Here we go.. Here we go again..
The guy writes an article, then he compliments himself with written comments in other people’s blogs…
Kama ni kweli una machungu, achana na hiyo kazi yako, then njoo bongo uanze kuuza cv yako. Kuliko kutafuta cheap publicity in Tanzania, while hapohapo ukiwa unakumbatia kazi uliyo nayo huko US.
Acha kutuchezea akili bwana mdogo.
Hivi huyu mtu anajitangaza kwa kazi anazozifanya au anatangazwa? Kama anatangazwa hongera kama otherwise mungu atakulipa duniani na sio akhera.
Oh dear A’m so proud of u. I will join you and try to help our beloved one in Tanzania. keep up bro Mashaka. Nakubaliana na Kutoa ni Moyo Si Utajiri. utaavyo ndivyo ubarikiwavyo. yaani niko so touched for what ur doing ndugu yangu. Be blessed
Mr Mashaka, you are a hero. Be blessed and let our Almighty GOD bless all you are planning ahead for your future and others’ future life as you always do.
Biblia inasema kutoa ni moyo na wala si utajiri kama ulivyosema mwenyewe kwenye mahojiano na Bongocelebrity Blog.
Once again I say Keep it up!!
Kwa kweli awe msanii flani , awe anaishi marekani , awe anakuja bongo mara moja kwa mwaka, awe anajipublicize NONE OF ALL THOSE REALLY MATTER TO me sababu how many so called Leaders (Rais,waziri au mbunge) amefanya anayoyafanya?
Serikali inapewa misaada mara kibao je walifanya kama alivyofanya huyu JM?
Acheni kumhate Jamaa wa watu unless mmefanya the same as he did or more than he did…. mi nawaona wadumisha maendeleo sababu badala ya kuangalia the positive side nyie mnaangalia negative side.
mbona hamwambii wazungu/EU/USA gov au wajapani waje bongo na misaada yao mnaipokea.
unafiki tu na michuki binafsi …
Edwin Ndaki tutafika kweli?
Kaka Mashaka.
Hongera sana kwa moyo wa upendo na ukarimu uliyouonesha na unaoendelea kuuonesha, kweli nimepata changamoto kubwa sana kutokana na maelezo yako, mtu wangu inatia moyo sana, kweli kutoa ni moyo sio utajiri. Binadamu tuliowengi kwa kawaida hatupendi kuona maendeleo ya mwingine na ndiyo maana tunatumia kila sababu kukwamisha maendeleo ya mwingine na badala yake tunatafuta kujikweza sisi wenyewe.
Mpendwa mashaka hii ni vita iliyoko ndani ya mioyo yetu ni shauku ambayo kila mmoja wetu anayo lakini, ni sehemu tu ya maisha ya mwanadamu anaweza kuilekebisha na kuipa sura mpya tabia hii ya kuwa na wivu usio wa maana na hatimaye kuwa chachu kwa maendeleo ya jamii na Taifa.
Mpendwa mawazo yako na maelezo yako yamenitoshea nimejifunza kitu kutoka kwako na Naomba Mungu anijalie uzima nami niwe chachu kwa wahitaji. Nilisadiwa na watu na ndiyo maana nipo hapa nilipo kila siku najiuliza hivi ni kweli baba na mama yangu, pasipo msaada wa watu wengine ningeweza kufika hapa nilipofikia? Na mwomba Mungu akujalie uzima na Afya ili chachu yako iweze kuwasadia na wengine kulikuomboa taifa letu na wahanga wake. Leo umenigsa mimi kesho utamgusa mwingine, kwa njia hii Taifa linaweza kubadilika pole pole kama kweli watu wataweka masilahi mbele ya kusaidia na sio kutafuta umaarufu na sifa. Nakutakia mafanikio mema.
Anaonekana mkubwa na hajaoa. paper zimemchelewesha maskini.
Nimeguswa, ninamshukuru Mungu sana kwa kaka huyu Mungu akuangazie uendelee. Nipo nasoma kozi ya kunisaidia kurudi nyumbani kupambana na swala la umaskini na mengine mengi.
Nina mipango mingi kwa ajili ya nchi yangu na nimekuwa nakerwa na mengi ambayo ameyagusa kaka ninashangaa, nina mpango wa kufungua shule, na mikakati mingi mno..ikiwezekana naomba tuwasiliane ili nieleze wapi nilipo, ninakwenda wapi, kwa ajili ya swala zima la kulikomboa taifa letu.
Ni ajabu siku moja mwanafunzi mmoja toka Malawi aliniita akaniambia jamani kuna kitu kimenishangaza! nikamuuliza nini ….akasema nchi yenu?? kwa nini ninyi ni maskini?? mna bahari, mna maziwa makubwa , mna mito, mna mbuga za wanyama, mna mlima kilimanjaro, mna madini, mna vyakula, mna watu wazuri na wema, mlibahatika kuwa na kiongozi wa ajabu sana Raisi wenu wa kwanza…..mhhhhh kaka huyu ni kama alikuwa amenipiga kibao cha uso…kweli shime kizazi kipya tuungane, tuamke tufanye kitu kwa ajili ya Taifa zuri la ajabu katika uso wa dunia, mwenzenu nImechokwa na kutukanwa na hawa……..tunatamani ufike wakati sasa watusifu na si kututukana na kutudharau. Unakaa darasani unaambiwa …tena na lecturer…lakini…mna vita Africa, mna njaa, viongozi wenu wala rushwa …kweli mwenzenu nimechoka na matusi haya ninatamani …tubadilishe hizi kauli kutoka kwenye vinywa vya hawa watu. Ninaomba sana tuwasiliane kaka Mashaka tuko wakereketwa tuko tunaweza kufanya kitu …kikaitikisa jamii na kizazi cha leo.Mungu ibariki Tanzania. Mungu akubariki kaka Mashaka songa mbele, kazi yako si bure na Mungu atakulinda na kila baya. Asifiwe
JM Be careful man! wanadamu ukiwapenda sana mwisho wanakusulubu halafu baadae
wanaanza kukuabudu!!! si unakumbuka walivyomfanya YESU!
Inatia moyo, wabongo wote tuache ubinafsi na tujifunze kusaidia walio masikini zaidi yetu. Nakuja kusoma mahojiano kwa undani.
Kila la kheri
Mr Mashaka….isije ikawa mashaka yako juu ya jamii ya kibongo ndio imekufanya ufanye ufanyayo…..mana’ke majina nayo utata mtupu (a joke)
Mary: You are an absolute IDIOT
This guy is being interviewed by a well known and reputed Journalist. He did not copy any comment from any blog, to me his words seems genuine than yours full of hate and envy. He does not own this site, this site is owned by Bongo Celebrity. How can we prosper in life while we can not appreciate simple things in life? His actions seems simple, yet of great impact for true humans
I work for a daily paper in the UK, and very suprised how stupid and ill minded our people are. I suppose, most of these haters, are the ones whose fathers looted the country, and now stuck in the west without education; with never end factory work. Wake up Mary, I very much believe this is a force to recon with. Atleast he can puclicise himself with good work, what of you?
Hongera sana Bw. Mashaka, nimevutiwa sana na moyo wako wa upendo. Ni kweli ni watanzania wengi tupo nje ya nchi tukijitafutia riziki zetu, ila tumejisahau na kuona kwamba matatizo tuliyoyaacha nyumbani hayatuhusu tena!! Nina uhakika kila mmoja wetu akifunga macho ataona picha ya kama sio ndugu basi ni jirani ambaye watoto wake wanashindwa kumudu mlo zaidi ya mmoja kwa siku achilia mbali kuwasomesha na kuwavisha nguo. Kweli ni jukumu letu kusaidiana kama majirani zetu wanavyofanya. Kwa sababu mwisho wa siku ni kwamba tutakosa amani tutakaporudi nyumbani tukiwa na mali huku tumezungukwa na watu wasiojua kwamba kesho watapata wapi chakula. Tushikamane, tusaidiane na tupendane. Haitatupunguzia lolote zaidi ya kutupa amani sisi wenyewe!
jamaa mzushi anaonekana kama mwanakjj. tutaamini vipi kama kasaidia watu na yeye anasema siri? mama Thereza alisaidia wazi hakujificha tuliona kazi zake.
kama anafanya kwa siri mbona yeye katoa kwenye vyombo vya habari? wako wengi wazushi kama jack pemba. alisema ni wakala wa mpira kumbe uongo tu.
mzalendo nakubaliana na wewe, wasanii wa aina hii wapo wengi hata kama anasaidi watu ujue nayeye ndo anapopati akula hapohapo tena nyingi zaidi ya hizo anazozitoa..watu wanaakili sana yani mtu analala usiku anawaza afanye nini asubuhi,umefanikiwa baba hongera
mzalendo nakubaliana na wewe, wasanii wa aina hii wapo wengi hata kama anasaidi watu ujue nayeye ndo anapopati akula hapohapo tena nyingi zaidi ya hizo anazozitoa..watu wanaakili sana yani mtu analala usiku anawaza afanye nini asubuhi,umefanikiwa baba hongera…..halafu mkwara wake anatia na kingereza hehehehhe
na hilo swala la kuuza gari ameuza ili anajua anapata jingine kwa pesa za msaada hivi nyie mnadanganywa mnakubali
Watanzania wapenda maendeleo watampongeza JM because of his revolutionary thinking and ideas.Wale watanzania wanaosinzia ambao wanatafuta negative points in everything na ambao wana roho mbaya ya kutopenda kuona Mtanzania mwenzetu on the high levels wata mkashifu na kumsimanga.I’m glad that 90percent ya comments zinamuunga mkono JM.For those who are still sleeping,wake up to the smell of coffee!its a new day downing.The whole world is changing.Its no longer survival of the Fittest,but survival of the willing.We Africans have suffered for so long and young revolutionary academic thinkers like JM is what Africa in general needs.I dont know him personally but as a concerned African I like his thoughts,they seem to be His genuine.
Correction on my last sentence to”……they seem to be genuine”.
Jamani hivi watanzania tumelogwa na nani jamani… JM anafanya kazi ambayo nilitegemea wote tungemuunga mkono lakini kuna watu wengine eti wanamwita msanii mara tapeli hivi hukuna kitu kizuri mtu anafanya akaungwa mkono 100% mi nasikitika sana, kama hamuwezi kutoa basi anaetoa tumpe moyo jamani. Jamaa anafanya kazinzuri, eti arudi bongo alafu hizo hela za kuwasaidia atazitoa wapi? Mbona watu wengine wanaroho mbaya hata shetani anawashangaa. John jitahidi uwasaidie wasiojiweza wale wanaokupinga ni wale ambao wana account za EPA hawana shida. Na siunajua alieshiba hamjui mwenye njaa!!!!! Unapofanya jambo zuri usijali wanadamu watasema nini kwani mara zote kwenye kutoa Mungu anakuwepo pembeni. Na sisi tusio na uwezo tunakuombea. Hao wanasiasa si ndio wamejichotea EPA na Richmond? ni wangapi walisaidia wapiga kura wao kwa utajiri waliojichotea? Ambapo kuna watanzania ambao kula milo mitatu kwao ni msamiati. TANZANIA BILA UMASKINI INAWEZEKANA ANZA NA KUMSAIDIA JIRANI YAKO MWENYE SHIDA AMBAE HATA KUMLIPIA MTOTO ALIEFAULU ADA YA ELFU 20 HAWEZI.
“Ningekuwa na uwezo ningejaribu namna ya kufanya haya mambo kimya kimya.”
hapo tu ndo amenichosha…kwanini kakubali haya mahojiano……
We need more humanitarians like this guy to achieve what we always deem to be a dream. Together we can definately make it possible. Count me in on this, im ready to help. Mashaka when you can, kindly contact me so we can set up what exactly to do. my email add is babra72@yahoo.com
Ohh thanks Lord. Sikufahamu kama kuna watanzania wenye moyo wa kujitoa hata mali zao kwa ajili ya watu wengine. Mungu akutie nguvu uendelee na mipango yako ya kuwasaidia watanzania wenzako. Na imani Mungu atakuwezesha kufika pale unapopataka.
I admire the this interview.. the guy is serious..nilikua natafuta sana watu kama hawa ambao wanamuelekeo mmoja na fikra zangu..thank god mr John is one of them.. hey John we can communicate through this email sidevok@hotmail.com, lets together save our beloved country..our ideas and efforts will bring this country to the top… we have to beleave.
solange ndo umshangae,huyu ni tapeli..afanye tu kimya kimya
God bless you John, you are doing a great job. Keep it up!
Yes….I took time to go through all comments. It would be very surprising if there could not be even a single negative comment on John Mashaka.
Now it clearly shows that he is a real human being who have to be hated and loved for what he is doing and trying to do. I am not blaming those who despised what Mashaka is trying to do by calling him “tapeli”, after all they are the minority. They have that freedom. It sometimes worths to think twice before you critisize what a fellow Tanzanian is doing.
My piece of advice to Mashaka….be just like that deaf frog who was climbing the coconut tree in a competition and managed to reach the top simply because it did not hear all the shouts and ultimately won the race.
Hamry-Tendambwe
See what you wrote: “to me his words seems genuine than yours full of hate and envy”
I wonder “daily paper in the UK” would hire a Maimuna like you….
Ha ha ha!!!!!!
Fanyeni sirini na Bwana atawabariki! sio kutangaza kihivyo!
Mashaka habari yake ina mashaka. hakuna evidence kama amewahi kusaidia sehemu nani ana proof?
jack PembA alituhangaisha sana. lakini sasa hivi hatudanganywi. kazi kubwa anayosema kachimba kisima hilo nalo ni ushujaaa?akaulize Mkono amefanya nini jimboni kwake then ndio aje kuleta ujinga wake hapa.
kama mnakubali kudanganywa na hii story vipi wakija waNIGERIA? acheni ujinga comments nyingi hapa kaweka mwenyewe.mara kajipeleka kwa Michuzi.
nasema tena huyu ni JACK PEMBA NAMBA 2. TIME WILL TELL.
KAMA YEYE MTU WA MSAADA MBONA HATUJAMSIKIA KWA KANDORO MCHANGO WA MADARASA?
JAMAA NI MZUSHI HANA JIPYA KWANGU. NAKUBALI KULA LAWAMA ZOTE.
AMANI KABURU ALITOKA MAREKANI NA AKASEMA HAWEZI KULETA MISAADA HADI APEWE UBUNGE WANANCHI WAKAMPA UBUNGE-KIGOMA HAKUNA CHOCHOTE KILICHOTOKEA.
NADHANI BWANA MASHAKA IPO HAJA KINA COMEDY WAKUJUE NA WAWEKE KIPINDI CHAKO.
WATANZANIA JACK PEMBA ALISEMA NI AGENT WA MPIRA ATAPELEKA VIJANA ULAYA. WAKATI WEBSITE YA FIFA HAKUNA JINA LA PEMBA KAMA NI AGENT WA MPIRA.
TUNANUNUA STORY KIJINGA SANA.SORRY MASHAKA I CAN’T BUY UR STORY.
mashaka,keep it up bro,i know you very well since way back in segerea,you are a good person,ambitious and hard working,najua utapenya tu turudi home kujenga na kuendeleza vijana.
Mzalendo, Ninakubaliana na wewe kwa asilimia 100.
Unajua, ni rahisi sana kustukia wapenda misifa. Nakubaliana nawe kua huyu jamaa ingawa hayuko katika magnitude ya Jack pemba kiuongo wala kipesa, lakini inaonekana anamkaribia kwa kasi in terms of kupenda misifa.
Nilifikiri kwamba ni mimi peke angu ndie niliemstukia kua bwana Mashaka ana-initiate kujibandika kwenye blogs za wenzie, then anakuja baadaye kuweka michangio kibao chini ya habari zake kujisifia sijui eti “Mashaka anasifiwa na wazungu” – So what? Don’t he know that wazungu ni hypocrites?. Mara sijui “Mashaka anafanya kazi wall-street” – So what? There are so many people working in wall-street as junior eployees. Kwani wall-street ni nini? Watu wasiojua the meaning of wall-street wanaweza babaika. Ila ile wall-street tunayoisikia CNN sio wall-street mashaka anayoizungumzia. Wall-street ya CNN iko very competitive for a person like Mashaka to get into. Kama mtu haamini, basi fanya general research online na utapata majibu yote.
Watanzania inabidi wawe makini na hili. Kwa maelezo zaidi nawashauri waingie wikipedia ama waangalie dictionary; Watajua kila kitu kuhusu wall-street.
Ilikuwa ni rahisi sana kwa Richmond Development kuwaghilibu watz kwa sababu sisi watz tukisikia mtu katoka ulaya tunaona kwamba huyu kweli ndio mtu kikwelikweli. Be careful, msije mkastukia kwamba huyu Mashaka ni Ridvedco mwingine in terms of his content, not in terms of his pocket.
Naishia hapa.
Ndugu watanzania wenzangu,yatubidi tuwe macho kuhusu habari mbalimbali tunazosikia,tusiwe wepesi wa kupigia debe habari zinapotolewa kama hizi za JM.Tunahitaji kufikiri na kuzipima (critical thinking) na kuelewa mwelekeo wa habari zenyewe.Nampogeza jamaa aliye shauri kuwa tunahitaji kuwa na uthibitisho (evidence) wa shughuri na kazi aliyofanya mtu na si kukubali moja kwa moja.Wamisionari waliingia Afrika kwa gia ya kutoa misaada ya chakula,nguo nk ili kupandikiza imani ya dini ya KIKIRISTO na walifanikiwa wakafanya waliyotaka na kuchukua walichotaka nchini mwetu .Na wemefanikiwa sana kuuwa utamaduni wetu wa kuabudu.Tunahitaji kutafakari zaidi.Pili bwana JM amehusishwa sana na sera za sisa za Tanzania ,kwa sababu siasa za Tanzania zimetawaliwa na zawadi miongoni mwa hao wapiga kura hivyo basi ni vyema tukaelimishana kuwa kunipa msaada si mwisho wa matatizo tunahitaji njia nzuri zaidi ya kuondoa matatizo na si hiyo ya kutoa msaada.Nifundishe kuvua samaki ili nile samaki kila siku na usinipe samaki maana sitawapata na kuwala ninapohitaji kwani nitasubiri kupewa.Namanisha kuwa sioni mtu kutoa msaada ndo chanzo cha kumaliza matatizo ya Watanzania.
Majibu mengi ni ya kisiasa tu, just dancing around and playing with words. ameniuzi kukaraktaizi sisi wote kuwa shetani!
I am pissed.
Huyu mshkaji Kanumba hana lolote alilofanya la maana baki ya kutoa $70 za msaada. Acheni kumtukuza, Jamaa yuko kwenye movie na yeye streling. Si mnajua sterling hauawi!!!
Haiwezekani akawa anasifiwa na mamia ya watu namna hii. Mimi naona BC comments za wanaokandia anabana.
Kwanza kwa nini hajaoa na anaonekana umri umeenda, au karatasi imemchelewesha ndoa ya kweli? hihiiii! pole, mdau US
Tatizo moja nimegundua kwa watanzania kwasababu ya lugha ya kigeni imepinda kidogo basi mtu akitupia kivocaburary basi utasikia jamaa amesoma ile mbaya nilikuwa namwangalia Lilian Abel kwenye miss tanzania kwasasbabu aliongea kitasha na alitumia maneno ya vocabubarury ambayo yanaingia kwenye kitu chochote unachotoa sifa in a speacil occasion sio ya kutumia kila siku.basi bwana alivyomaliza kujielezea umati ulivyopiga kelele .basi kila sehemu utasikia demu alijielezea vizuri sana .ni kweli alijielezea vizuri
huyu bwana anatafuta antention ya JK TU. ANAJUA JK HUWA ANAPITA HUMU SASA ANATAKA KUJIUZA. ANALAZIMISHA KUWA RAIS ACHAGUWE WABUNGE HATA WATU WASIOPIGIWA KURA. INAONEKANA MTUPU WA SIASA, HAJUI KAMA RAIS ANA VITI KUMI VYA KUWATEUA WATU ANAOWATAKA?
MASHAKA NJOO UJIBU HAPA USIKIMBIE.
As an interlect, I have gone through a number of stories in regards to this young man. I carried some follow ups in his previous Michuzi’s posting, and I can assure you. It cant get real than this. We must learn to appreciate good things in ife
In the entire interview, he has not claimed to be anything. He has not mentioned any of his positive deeds, he only prayed for humility. Why do we have to judge him so negatively?
What do we want for our country, what kind of leaders do we need?
I have also analyst the comments, and seeminlgy, only a handful have criticized his work. We must accept this, because in life nothing is 100% unless something wrong, there must be a room for error. Thus, the majority gets the 95% while the 5% goes to the few negative.
Can I ask any of you who know this guy in person, i have read quite a number of peolple who know his gave positive comments. In this interview, I guess he was being interviewed, and i do hope that he never initiated it, if he did then I must take off some credit
BC… Good Job, this is the kind of interview we want to read and know about our country. These young people loves to read about ma Miss, and some crap, they dont need challenges in life.
Thanks Hidaya
MAELEZO YA JM NA FLOW YAKE,KUTOKUTAJA MAJINA YA SHULE/CHUO ….STATE….CITY ,MASWALI MENGI YA MSINGI KUTOKUYAJIBU KWA UWAZI.NIKIANGALIA SIZE YAKE YA MWILI INAFANANA NA SAUTI YA M.M. MWANAKIJIJI KULE KLH NEWS. NINAONA UMEANZA KUJITOKEZA KWENYE MAPAMBANO YA ARDHINI. KARIBU FRONT LINE.
125th ST.,HARLEM.
Watanzania nani aliwaroga? Yani mnashindwa kutofautisha kati ya uvumi na ukweli? Mtu anasema yeye ni msamaria mwema basi pongezi zinamiminika bila hata kuuliza alishafanya usamaria kiasi gani unaostahili kijifaragua kiasi hiki?
Mimi nilifikiri baada ya Kikwete kutulaghai basi watu watawapuuza watu wanaouza maneno matupu lakini wapi..ugonjwa bado upo palepale!
Tuwe makini jamani hasa katika mambo muhimu zaidi ya hili la huyu JM anayejitaftua umaaru kwa bei nafuu!
Asanteni!
mi nilimkuta kwenye blog ya mroki nikampinga weeee liliibuka kundi la watu kunishambulia humo nikakoma
na kweli inawezekana comments kajiandikia mwenyewe maana naona kuna majina mageni sana yanayomfagilia wkt tumeshazoea wachangiaji wengi humu huaga ni wale wale,halafu za kuponda mnabana
tena mtoeni mi anavyoniudhi
mezeni vipande vya chupa basi!
na hapo kwenye kuuza gari atoe msaada…mhhh kweli ana moyo basi…ukute una hako kagari kamoja then ukauze ili utoe msaada mhhh ngumu kuelewa……..haya mambo yana wenyewe bana na ndo wakina mzee mengi……wewe unatoa sadaka kama mie hapa ninavyotoa sadaka kanisani.
125th St., Harlem
Umenikuna sana. Inawezekana JM akawa ndio MM Mwanakijiji? Inabidi Mwanakijiji naye afanyiwe mahojiano na atoe picha tumwone. Tumesikia sana na umemsoma sana. Sasa tunataka kumwona
Haswa ndiye Mwanakjj hata coments alizoweka kwenye Jf forum za kumjenga bwana Mashaka kuwa aliandika barua kuhusu richmond.naona ameamua kuja hadharani.
shule yake ya mashaka sana na pia ni mtu wa musoma na mwanakjj anatoka musoma.
mimi naona kutoa ni moyo hivyo kaka we toa tu kama unacho Mungu atakubariki na kukuongezea wala usijali ya watu!
Hivi watanzania mnataka nini jamani! Richmond au watu kama hawa, mimi nafikiri huyu kijana ametumwa na Mungu tu na si vinginevyo. Tuwasiliane Mashaka haya yote hayana budi kutokea kwani wewe unafanya yaliyo mema hata Yesu alifanya mema lakini aliishia kuuwawa. Mimi nasaidia na nafanya kama anavyofanya Mashaka tatizo la wabongo ni Uchoyo tu na kupenda rushwa hawajui kama mtu unaweza kujitolea bila kujali umepanga, hujajenga bado, huna gari hawaelewi lakini kwa sisi tuliosaidiwa na sasa tuna kazi nzuri tunaelewa kwani waliotusaidia mbona hawakuwa na maisha mazuri ila baadae Mungu amewajalia na wamefikia hali nzuri kimaisha na wanaendelea kusaidia jamii bila kupata mchango kutoka popote ni kwa bidii yao tu na wala hawahitaji vyeo serekalini. ACHENI MANENO KWA NJIA HII ITAKUWA VIGUMU SANA KUJIKWAMUA KWENYE UMASKINI TULIONAO.
MASHAKA PLEASE EMAIL ME: totoob@yahoo.com
Its very impressive enough to change p’ple’s mentality toward the negativity attitudes which normaly led to the increasing of selfishness ‘n’ poverty in our community, according to my opinion regarding to JM’s comments, i think, in order to overcome such obstacles, p’ple should create synegy to tackle serious issues ‘n’ also the actions must be taken immediately according to the provided solutions, this will encrease humanity to the p’ple who think for themselves(“does’nt have a sense of human”) as well as more peace ‘n’ love in our country ‘n’ africa in general, in result the problems such as poverty, street children, corruption the areas that am so concern may it be easly solved.
mungu akubariki sana.
Hahaha u-celebs wahitaji moyo wa chuma otherwise unaweza usitoke nje ya nyumba yako au usiingie tena BC.
Naomba kusaidia kidogo kwa vile mimi binafsi namfahamu Mwkjj vema, huyu bwana sio M.M Mwkjj.
Kusaidia sio lazima ujitangaze uite na waandishi wa habari waje kuandika na kupiga picha kuhusu kile unachokifanya, wale wanaojitolea kwa moyo na sio sifa mara nyingi hufanya hivyo kimya-kimya.
Huitaji kuwa Miss au kwenye macho ya jamii au even kuishi Magharibi kusaidia sehemu ya jamii inayokuzunguuka, unaweza ukaishi hapo mtaani kwako, unauza samaki wa kukaanga na kukakusanya (save)Tsh. 500 kila mwezi kununulia mtoto mmoja madaftari na kalamu au sare ya shule kila zinapomuishia au kununua Pain killer kwa jirani yako ambae ni mgonjwa lakini hana senti za kununua dawa ya kupunguza maumivu.
Mashaka next time uje na vithibitisho vya uliyoyafanya hata kama ni home vid au picha ili wabongo wakuelewe vinginevyo ndio kama hivi….hawataki kabisa kukubali unachokifanya….mwee!
Kila la kheri MshaK
john Mashaka ni nani?Ni mwanakijiji asituzingue
Habari za kawaida
Posted Date::4/3/2008
Ufisadi wa EPA, Richmond wadhalilisha Watanzania Marekani
Na James Magai
�
BAADHI ya Watanzania wanaoishi Marekani, wamesema kashfa ya ufisadi iliyoibuka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na Kampuni ya Kuzalisha Umeme wa dharura ya Richmond Development Company LLC, imewadhalilisha.
Katika barua pepe aliyotuma kwa Mwananchi kutoka Jimbo la Carolina kwa niaba ya wenzake, John Mashaka alisema, kutokana na kashifa hizo, wamekuwa wakijiuliza kama wahusika ni wazawa au majambazi kutoka nchi za nje.
Mashaka alisema kutokana na hali hiyo, lazima wahusika wote wakamatwe na isipofanyika hivyo, itakuwa ni kejeli na matusi makubwa kwa walimu, polisi na wafanyakazi wengine wanaofanya kazi katika mazingira magumu.
�Ni jambo la kusikitisha na kutoa machozi, unapowaona watu wachache waliopewa dhamana ya kulinda nchi, wanajaribu kuifilisi na kuchezea jasho la Watanzania wengi, huku watoto wakifa hospitalini kwa kukosa tiba,� alisema Mashaka.
�
Kuhusu ufisadi, Mashaka alisema unasababishwa na watu kukosa uzalendo na kufanya uamuzi ambao hauna maslahi kwa Watanzania.
�Mtu mwenye ubinadamu katika nafsi yake na mwenye uzalendo na uchungu kwa nchi yake, kamwe hawezi kushiriki vitendo vya aibu kama vile vya Richmond na BoT,� alisema Mashaka.
Akitoa mfano wa Israel, Mashaka alisema nchi hiyo ina uwezo mkubwa kitaaluma kuliko mataifa makubwa yenye uwezo wa uchumi, kutokana na viongozi wake kutanguliza maslahi ya taifa mbele.
Mashaka alisema, Watanazania waishio Marekani, wameridhika na juhudi za Rais Jakaya Kikwete kuboresha maisha ya wananchi na kuweka Tanzania katika ramani nzuri.
Pia, alielezea kuridhishwa na jinsi wabunge wa chama tawala na vyama vya upinzani, walivyoungana na kushirikiana katika sakata la Richmond na kufanikiwa kuwang’oa mafisadi.
Licha ya ufisadi, Mashaka alisema wamefurahishwa na juhudi za serikali kutangaza Tanzania kimataifa hasa vivutio vikubwa vya utalii vilivyopo nchini.
Linalonitia mashaka juu ya Bwana Mashaka asije akawa kama Johnson Lukaza. Bwana Lukaza alimiminiwa sifa kemkem kule kwa Michuzi. Ilipoibuka EPA akabainika kuwa ni muhujumu uchumi mkubwa. Vijana wa aina hii wapo na watu wanapotoa maoni yao wanakuwa na marejeo. Nendeni mkaangalia kwa Michuzi maoni yaliyotolewa juu ya Johnson Lukaza mtaona ni kama haya mnayoyatoa hapa.
http://issamichuzi.blogspot.com/search?q=lukaza
Huu ujanja ujanja wa kujikwezakweza upo miongoni mwa watu. Wapo ambao wamejikweza kweza kiujanja ujanja na sasa hivi wamekwea madaraka na hatamu mbali mbali na hata kuwa maarufu katika jamii. Lakini ukiwachunguza undani wao unakuta kwamba siyo yule ambaye anafikiriwa.
Na sasa anapoanza kuwa de facto spokesperson wa Watanzania huko US kama inavyoonekana kwenye gazeti la Mwananchi ndiyo anazidi kunitia mashaka. Anyway, siyo jambo baya kujitolea kusaidia watu lakini jambo baya kama unadanganya kwamba unasaidia watu.
I think there is a miscompehension here. JM did not initiate the interview, he did not praise himself to be rich and did not either promise to supply everyone here with all necessities of life.
He is is a person with his own ambitions towards the society from which he is coming! Let him do what he thinks is right for him to do. He has not invited anybody to coontribute financially to what he is planning to do. Do you think even those who are trying to praise what Mashaka is doing are gaining something?
These blogs are created to be the only platform where various ideas surface and everybody is free to do that. Now, it is evceryone’s choice to embarace the isea or reject it, but not to convince others to do what you think is right! Most of the critical comments are not accompanied with any valuable substance!…People keeping on critisizing Mashaka without putting any substantial substance on the table!
In the country there are many poor people, yet people urguing without putting anything new to arrest the situation, it is really a disappoint phenomena. I would expect those ones who doubt about what Mashaka is saying and trying to think of would critisize him and come up with a better alternative than that, but unfortunately there have empty words!
I think Tanzanian minds have been so much affected by corruption in such a way that anybody who comes up wth an ideas seems to be corrupt. This is a grievious sickness. Some have even termed him as someone who seeks cheap popularity. Yes…It is not bad to think of any idea critically, but I think it is also reasonable not to convince others to follow your critics, which are not backed with any evidence.
Hey Bro, keep it up ma men, really this is what we all need to be. If you had be blessed by God of Heaven, you better split what you had been blessed with the other who are really on need.
I am also the one who need to join your effort in order to make this dear country on peace and harmony. Let we keep contact Mashaka through this email, mpandacharls@yahoo.ie I am at Tanzania but I got the possitive altitude like yours and we must share also what I am doing……
Mimi naona kama yuko serious angekuja hapa Bongo kimya kimya akasaidia maeneo kibao yanayotatiza wazalendo kwa vile ufisadi umezoa kila kitu. Bila kusahau nampa sharti moja aoe ili akili itulie.
Kweli mwenzenu inanishangaza kidogo kuona wanaochangia mada au maoni, baadhi yao kutumia Lugha za kejeli na dhihaka, naomba ni hoji hivi hawa watu hawasomi kwanza maelezo kuhusu mtu mwenyewe, na wakapata ufahamu kidogo wa kumjua ?
Mbona mahojiano hapo juu yanaeleza hadi maeneoaliyotoa misaada na mahojiano hayo yameandikwa na Mtanzania mwenzetu aliyemhoji kwa kina na kuzileta habari hizi hapa.
Je, unakosa imani hadi kwa huyu aliyefanya naye mahojiano hadi tunathubutu kumtusu na kumwandikia mambo ya ajabu ajabu humu kudai anataka sifa, amejieleza sana “Namnukuru anasema ningependa mambo haya niyafanye kwa siri lakini kila nilipojitahidi kufanya hivyo mambo yalizidi kusamba kwa watu”.
Na ni kweli kitu kinachofanywa kwa wema na kwa manufaa ya watu hakiwezi kufichika, kwani watu wanatoa shukrani na kwa njia hiyo taarifa zako zinasambaa ingawa wewe mwenyewe hupendi sitoke.
Nawasihi watanzani wenzangu tubadilike na tuone upande mwingine wa shilingi sio kila siku kusema mabaya tu juu ya wengine.
Kumbuka hakuna mwanadamua aliye mbaya kwa asilimia 100% kila moja wetu anamema na mabaya yake, lakini kwa upande wa mashaka ameonesha mema mengi, hivyo tunapasika kumshukuru kwa wema huu alioutenda na pale atakapoonesha kukosea basi tumsaidie kwa ushauri kurudi kwenye kundi pasipo kutumia Lugha za kashifa kama zinazotolewa na baadhi yetu. Ina uma sana.
Mimi sio mashaka lakini nasikitishwa sana na kitendo hiki cha baadhi yetu kusaga kama kwamba sisi ndiyo tunafanya mazuri zaidi na yamaana zaidi kuliko mashaka. Tubadilike Watanzania wenzangu.
Oh My goodness!!! Mashaka did it again!!!!!
Oh my God!!!!
Kwahiyo sasa anahesabika kama ni msemaji wa watz waishio marekani, duh!!!. Kama ni hivyo basi watz wote wa marekani hamna akili nzuri. Kumweka huyu jamaa awawakilishe kutoa maoni yenu kunaonyesha kwamba mnamuamini kama kiongozi wenu dhabiti. I wonder he’s taking you into the right direction. Oh my God!!!!!
Jamani watanzania. Sijui shida yetu ni nini. Tumelaaniwa kusema kweli, Nani mtanzania ambaye yupo katika anga za kimataifa ambaye tunamsifia, au nani kati yetu katenda wema tukamsifia.
Huyu kaka hata kama alitoa tu $100, hajajisifia, mahojiano ni mazuri kweli anachokilia ni ubinadamu kati yetu na upendo. Kaka wa watu hajaomba hela, kasema hicho kidogo chake ndo hicho anachotumia, nyie shida yenu ni nini kama siyo majungu
Sote tunaopiga makelele humu ni nini tumekifanya. Jamani wivu umetushinda. Mwenzenu kawashinda.. na ukweli ni sawa na abc.. au 1234…. Tumpongeze angalau siku moja atamsadia babu yako na bibi yako. Hajuae nani, pengine atamnunulia mkeo Chupi.
Na wewe XXXXXXXXXXXXXXXXX naona jamaa kakutia kiwewe kumuona anapanda chati, vipi alikutelekeza nini? Comments zako zinaongoza kwa madongo.Punguza hasira dada. Mashaka, u celebrity usikuingize kiburi.Mwombe mungu akuongoze wakina Jovita wasikuparamie
There cannot be any better story to read. This is quite insipirationl and motivating. John, I met you in Dar at Mkuranga along with the Bongo Celebrity Crew. i sat besides you the whole time we travelled to and from Mkuranga, please keep up the good work, and my the good LORD guide in all that you do
Let these people say all they want, I know you in Person. You touched my heart when you carried the little orphaned boy and wiped his tears, very few of your equals would do that. dont let pride stalk you, fight to the end.
For those who dont know this young man, I wish you had a little knowledge of his passion. He is passionate, and briliant I worked with him in Dar. He paid for everything during that trip. Donated food and other necessities along with Khadija Mwanamboka
Mrs. Tigo DAR
Naona vichwa vinaanza kufanya kazi. Huyu Kaka hakuomba interview. BC.. ilimtafuta kama anavyosema jamaa. Madongo anayomwagiwa ni wivu tu. Bwana mashaka, usiwaache hawa wachache wakuvunje moyo. Mungu yupo endelea na kazi yako
Kingine nnachoona ni kwamba aliyesoma majibu yake, kwa kweli hawezi kuwa na baya kumhusu Mashaka. WABONGO tumieni akili kuliko midogo Duuuh mmevuka mipaka, hata kijana mwenzenu badal ya kum support mnamimmininia matusi tu. ni vizuri kuwa na watu wachache ambao ni brilliant kama alivyo bwana mashaka. Shida ni kwamba hauwezi kugombea urais Marekani kama Obama, rudi Tanzania uitumikie jamii yako. Kura tutakupa ukiamua kurudi tumeone unamwelekeo mzuri sana.
Weusi tabia zetu ni sawa duniani kote, ndo maana tunazidi kuwa wesui.
weee mashaka mbona unaomba kura mapema hivyo? suria 2010. ila nimependa sana hiyo interviw yako, ni kiboko.
hivi wewe ni kabila gani ,mkurya nini. Angalia nyuma yako Jovinata anakuja. Kosa sona mdogo wangu kusema huko single , watakusumbua sana
kazi ipo
kaka ake Mary
Naona unashida na bwana mashaka, alikunyanganya mke nni. Madongo yako yamejaa hii blog kuliko mt mwingine. Ndugu yangu, dunia n mviringo. Tuliza wivu, wivu mpaka machzi, umevuka mpaka
Mashaka, wala usijali, hawa ni kama chura ndani ya maji, endelea na shuguli zako, kwani wafuasi ni wengi kuliko haya milevi ya EPA inayoshinda baa kia siku. Waache wanywe kwa mara ya mwish kabla hawajaleplewa Keko….
Kweli Kabisa, hawa wenye kejeli na matusi kama kaka ake mary au mary mwenyewe ni watu wanaomfahamu mashaka, ambao wameishi ulaya na kamba za mzee bushi miguun mwao. Hawawezi kutoka marekani. Wakitoka ni ticketi one way. kazi wanafanya masaa 23 na moya ya kulala, wakiamka hasira kibao hasa wakimuona yanki kama huyu anawashinda. Wabongo tuacheni wivu…. kaka ake mary hacha wivu rafiki yangu dogo kakushinda kubali yaishe…….. au twende mahakamani ndo ukweli upatikane?
someni kama alivyosema mshikaji hapo juu, ila mnapokuja kwenye blog kama hizi na hasira zenu bila kujua vyanzo vya mambo, jamani mnajidhalilisha sana, hasa mnapofungua vnywa vyenu. Huyu kaka hajaomba hela zenu, na wala hamjamsaidia, ni hela zako mwenyewe, hataki misaada yenu, sehemu alikotoa misaada yake yametajwa dar. Goji Bushi wape makaratasi hasira ziishe warudi bongo wakawannulie mama zao vimini…… kila la kehri kaka ake mary na mery wako msichelwe kazini shifti ya pili …. tete..tete…tete…..
Mkuu John Mashaka, heshima mbele, I am impressed na ninakutakia mafanikio na kama nikiwa of any help tutafutane mkuu, maana bongo tunahitaji viongozi vijana wenye muelekeo, maneno yako yanatosha kusema wazi kuwa wewe ni mtu wa namna gani, maana wengine tunahitaji ku-read betweeen the lines tu, I am impressed,
Na salaaam pia kwa wananchi wote katika hii blogu, maana ni mara yangu ya kwanza kutinga huku, wakuu vipi mpo?
BC:
I am particularly commeding you for a job well done of hunting Mr.Mashaka down, and handing him such a well thought interview
Of course, there are negative minded persons, who never take time to read, while their lips are burning with hateful words. You have done a good Job, can only suggest that you need to have a talk show in Bongo so that those corrupt leaders can be pinned down
I am a Tanzanian with a psychology phD from Univesity of Georgia and can read between the lines, this is a honest young man.He has responded to your questions very honestly and briliantly, he is brilliant and should turn on a deaf hear to these hooligans stuck up in the US and elsewhere.
Tanzania truly needs the likes of Mashaka’s mind. We are people who need to e pushed in everything and that is we sleep for so long while our country is being looted by a few persons. We talk too much and do very little, and those who talk the truth are being seen as enemies.
To You Mr. Mashaka, keep up the good work, let your passion be the torch in your endeavor. Dont let the Corporate America money corrupt you, on the other hand, know that your peers are going to hate your accomplishments.
Good Job, God bless you. The word needs more of you especially at these times of turbulance in the hearts and minds of fellow hman beings.
ILA NAWAOMBA WATANZANIA TANZANIA BADALA YA KUROPOKA I DONT SEE ANY FLAW WITH THE INTERVIEW, THE WHOLE THING IS WELL ORGANIZED
Namsifia John Mashaka kwamba ni mtu mwenye kujua namna ya kujipamba na kujaza threads zinazomzungumzia yeye. Namsifia hivyo kwa sababu kwenye blogs zote ninazosoma zinazomzungumzia yeye, mara zote utakuta “watu” wanaomsifia mara zote, kitu ambacho hakitokei kwa watu wengine.
Ebu ngoja niwaulize; Hivi huyu kijana ana level gani ya elimu? Jibu ni kwamba ana “Bachelors Degree” kutoka University moja uko Carolinas. Swali la pili; Hivi yeye ni msomi wa kwanza wa kitanzania kupata hiyo degree mpaka awe anajipamba mno kama yeye ana usomi wenye kutukuka? Jibu ni HAPANA. Swali la 3; Hivi Tanzania kuna watu wenye PhDs ambao wanasota kutafuta kazi na hazipatikani? Jibu ni Ndiyo; Swali la nne; Sasa kwa nini yeye anahangaika kujiuza usomi wake na kujifanya kwamba ana elimu kubwa mno kiasi cha kukurupuka kwenye blogs kujitangaza kwa kutumia gia ya kwamba yeye ni mtoa misaada kwa masikini? Jibu ni – SIJUI!!!. Swali la mwisho; Je una ushauri gani kwa huyu ndugu Mashaka? Jibu – Atafute gia nyingine ya kujaribu kuingia kwenye system bongo kwani bongo waingiao kwenye system wana majina makubwa yasito tia MASHAKA hata kidogo kwa mabosi waajiri. Ninamshauri kwamba afanye kazi kwa bidii kujiendeleza maisha yake na ya watanzania wenzake, na kwamba tumeshaona watu wakitoa sadaka za mabilioni ya dollars na kutaka majina yao yawe anonymous, just wakitegemea malipo kutoka mbinguni. Hivyo, simkatazi kuendelea kutoa misaada, ila akitoa hiyo misaada ajaribu kufanya hivyo vitu anonymously kwa sababu hii ni njia pekee ambayo itamwezesha kupata fadhila mbinguni.
LAKINI, SIONI SHIDA IKO WAPI NDUGU WATANZANIA, KWANI MUNGU AMEUMBA WATU TOFAUTI SANA . MAHALI POPOTE KUNAWEZA KUWA NA WATU MILLION LAKINI MWANDISHI WA HABARI AKAVUTWA NA MTU MMOJA AU WAWILI KUONGEA NAO. KUNA NAFSI AU WATU WENGINE WAMEZALIWA NA KUWEKWA DUNIANI KWA MAKUSUDI MAALUM, KAZI MAALUM NA MAHALI MAALUMU.
WEWE UNAYELAUMU AU USIYEPENDELEA HIKI ANACHOKIFANYA HUYU KIJANA UNGEKAA KIMYA NA KUSUBIRI UONE MWISHO, USIKIMBILIE KUHUKUMU. KILA MTU ANA MALENGO MAISHANI, SIJUI WEWE ….LAKINI MASHAKA ANAONA MBALI ANA MALENGO, MIMI SIMJUI LAKINI NAJUA ANA LENGO ANA UCHUNGU NA WEWE TUAMBIE UNA NINI, UNATAKA KUFANYA NINI KWA AJILI YA TAIFA LAKO. MIMI NAONA HAKUNA HAJA YA KUTUPIANA MADONGO WAKATI HUU WAKATI TUNAHITAJI KUONA MABADILIKO KATIKA MAMBO MENGI KATIKA TAIFA LETU.
NILIFIKIRI KWA WALE WALIOKO NJE YA NCHI LABDA WANGEONA TOFAUTI ILIYOKO NA SHIMO KUBWA KATI YA TANZANIA NA NCHI HIZO ZILIZOENDELEA NA KUJARIBU KUJAZIA HILO SHIMO KWA HATA MAWAZO AU KUTIANA MOYO.
NINASHANGAZWA SANA NA WAHINDI, JINSI WANAVYOINUANA NA KUSAIDIANA NA KUPEANA HATA MKOPO KUANZISHA BIASHARA ONA LEO WAKO WAPI.WENGINE TUNAO KATIKA NCHI YETU ANGALIA WALIPO. MUNGU ATUSAIDIE SISI WATANZANIA JAMANI ..NILIPENDA MTU ALISEMA NI NANI AMETULOGA???? KWELI TUNAHITAJI KUBADILIKA …LAKINI KAMA MASHAKA MWENYEWE ALIVYOSEMA “mabadiliko yataletwa na mtu wa kawaida kabisa…..” ni nani huyo mtu wa kawaida ni mimi na wewe. TUSIANDIKIE MATE ,….TUNGOJE, TUONE TUWE NA SUBIRA NA UVUMILIVU TUONE KITU MUNGU ALICHOWEKA NDANI YA WATU ….WENYE MAONO NA NCHI YAO. HUNA MAONO WAOMBEE WENYE MAONO YAO.
MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA NA MUNGU BARIKI WATU WENYE MAONO NA KULIPENDA TAIFA LAO KWA NJIA IWAYO YEYOTE….AMEN.
Mr. Tigo: I do agree with you, but has one question for you? Have you read the stry in entirety?
Sioni mashaka kajitangaza, nadhani BC: kama wanavyosema ndio waliomtafuta. I wanted at the beggining to criticize him, but after reading the whole story nilituliza mapozi. I think you should read everything.
Maybe we should blame him for accepting the interview. Mr. Mashaka, come out in the open and explain yourself,
Mr.Tigo, vipi Mashaka mnafahamiana? Ungemsifia ingekuwaje? au ungempa moyo ingekuwaje? Watanzania mbona kazi yetu kubwa ni kubomoa, kwa nini tusijenge, jirani zetu wote wanatucheka tusivyo na ushirikiano na kupenda starehe.
Kwani asingekua na bachelor degree asingekuwa mtanzania anayeijali nchi yake, c’mmon man. Pengine ni darasa la saba, lakini anafanya vya maana
Bila shaka, naona umekwama huko ulaya, kweli unaweza kurudi nyumbani Tanzania bila shida?
Au kubeba boxi ulaya ndo kumeletea mvi mapema? makubwa endelea kuosha mavi mwenzio anapaa.
Bushi analegeza kamba utapata green kadi angalau upate u-store manager badala ya kulia machozi ya damu
kila la kheri
Jamani mbona hamna huruma, Mr. Tigo kachoka, mtu amefanya kazi kutwa karudi nyumbani inabidi ajipikie na kujitayarisha mzigoni kesho. Duhhh
Ana kila haki ya kumchukia bwana mashaka, kwani ni mdogo kwake lakini anamshinda ki ujanja. Kaka yangu umechezewa kete molaaaaaaaaaaaaaa
Za Comedy Snr
Nilichogundua ni kwamba wachangiaji wakubwa humu ni Vihiyo, wakina mahimuna na matahira yenye hasira. Wabongo tupanuene mawazo siyo hasira za kuingia na kuchafua hali ya hewa kwenye blogs. Wasomi hawanaga mida michafu kama za wakina Mr.Tigo na wakina Mary
Wangu wamadaa
Yaani siku ya kwanza niliposoma mahojiano ya Mashaka, nikasema, subiri watanzania waamke huko walikolala watakavyo anza kumchamba kaka wa watu. Na kweli nimepitia humu leo nilichokiona astaghfirullah, sasa naelewa ndio maana BC ameweka wimbo wa Mwanahawa ‘Viumbe Wazito’ kuwapiga madongo watanzania!
Bwana Mashaka sikiliza huo wimbo wa taarabu ulioandikwa ‘Viumbe wazito’ hasa viumbe wenyewe kama wanatoka Tanzania. Ukishasikia huo wimbo wala hutakata tamaa katika shughuli zako. Hawa waTZ wengu wao wamechoka na maisha na tena ni watu wa kususpect kila kitu, hata ukiwa ndio hiyo kazi yako umeajiriwa uifanye ya Philanthropist na unalipwa mshahara wangesema unaifanya kwa sababu ina ulaji ili upate kuiba hapo misaada ya watu seuze wewe unaejitolea pesa yako mfukoni.
Ushauri, mabadiliko yanaletwa kwa namna mbali mbali hata ukiona ukiingia kwenye ulingo wa siasa unaweza kuleta mabadiliko katika jamii yako, ingia ili ulete mabadiliko. Tena kagombee ubunge kabisa kwenye jimbo lako ili uweze kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini katika sehemu ya nchi yetu, Na mwingine mwenye mawazo na uwezo kama wako akishika jimbo mwishoe nchi itapata viongozi wenye uchungu na nchi hii. Hao wotee waliokupiga madongo ni hofu tu waliyonayo kuwa waweza kuchukua majimbo yao si ajabu wanakufahamu vizuri na hayo unayoyafanya yanawapa changamoto na hofu kuu kuwa sasa malengo yao hayatatimia.
Keep up the good job nabii huwa hakubaliwi kwao hata siku moja! Ama atasulubiwa au kupigwa mawe!
MAMBO VP WADAU ?nimemsoma kwa makini mr tigo nadhani hastahili kulaumiwa mi naamini mawazo yake hayaokani na yeye bali mfumo mzima wa fikra na masahibu yanayomzunguka ndio yamemfanya kutoa maoni aliyotoa katika jamii yetu sisi waTz watu wamezungukwa na maoni ya vjiweni na ukosefu wa mawazo yenye ubunifu katika kujenga hoja ila niliporudi likizo bongo nilijaribu kukaa vijiweni kuona watu siku hizi wanaishi vp na nini wanachofikiria na namna wanavyochukulia mambo kwa ujmla kattika jamii yangu kuna vitu vingi niligundua ambavyo vinapelekea watu kuwa na mawazo kama ya kaka yake mary, mr togo na wengine wenye mawazo kama yao 1Ni ukosefu wa upendo miongoni mwetu na kutokupendana hususani mtu anapoonekana kwamba anagangamala kutaka kutaka kuinuka kimaisha(kama hauniamini nenda ongea na vijana wengi uone mawazo yao wengi hawapendani) 2.kuwaiwa kiutelezaji, utakuja kugundua wengi ambao wanawaponda J MASHAKA NA JACK PEMBA kwa mfano wengi wangependa kuwa kama wao ila wamekosea mahesabu na haijawezekana ,kutokana na kukukata kwao tamaa wanapoona kuwa mawazo waliyokuwa nayo watu wametoka nayo tayari ,wanaanza kuwaka na kuingiwa na KIWEWE na CHUKI ,wanasahau ni swala muda kujiri ,yaani ni vema wakakomaa ili na wao siku wawe kama hao JMASHAKA , kwani kumponda hakukuongezei kitu zaidi ya kuleta msuguano na kupotosha ukweli, 3WIVU WA KIKE , MAWAZO NA KUKOSA UUNGWANA ,ni mapema mno kumtuhumu JMASHAKA kuwa anautaka UBUNGE au UCELEBRITY na katika habari zake hakuna sehemu yoyote aliyo onesha kuwa yupo interrested na POLITICS (kama ipo waliotoa hoja ya ubunge naomba ushahidi) 4,Namaliza kwa JMASHAKLA mweyewe MENGI tumeskia juu yako wadau waliokutolea maoni MSIMAMO WANGU,KAMA KWELI UNA DHAMIRA YA DHATI NA NI MWANAHARAKATI MTIIFU KATIKA KUTOKA MFUMO CHANYA WA MAISHA KATIKA JAMII YA WA TZ NAKUUNGA MKONO NA NAKUPA HONGERA , ILA IKIWA UNAFANYA HAYA KWA MASLAHI YAKO BINAFSI YA KUJIPATIA FAIDA FLANI MBELENI ,NAKUPATIA ONYO WATZ SIO WAJINGA KAMA ZAMANI ZAMA ZINABADILIKA NA WATU WANAFUNGUKA MAWAZO ,SO KAMA UNAFANYA GHILIBA BASI MUNGU BABA NA AKUTIE ADABU KAM KWELI UNATUPIGA TAFU MUNGU BABA AKUBARIKI NA AKUZIDISHIE UPENDO NA AMANI,mwisho sijawahi kumuona JMASHAKA zaidi ya kuona habari zake kwenye blogs mbali mbali, maoni niyotoa yanatoka moyoni bila chuki nimedhamiria kumtendea haki JM na wa WADAU wote SIKU NJEMA
Mr Tigo Hoyeeeeeeeeee, Mwaga lazi baba. Nakubaliana nawe kiasilimia mia moja. Hawa wanaokubishia hawajui walitendalo baba.
Mashaka hakuna ushahidi wa shule au sehemu aliyosaidia, nyie mnaoingia kwenye mitandao ambao ni asilimia ndogo sana ya watanzania mnaamini.itakuwaje watu wa kijijini ambao hawana exposure watakapoingiliwa na matapeli? kama wajanja mnanasa kijinga bila kupewa kofia na fulana,mnawalaumu nini waliopewa kofia?
mtu analeta story anaaminika bila proof.mnaulaumu nini mikataba mibovu au richmond
Mods huo mchango # 91 sio wakwangu ni mtu ametumia jin alngu wa kwangu ni ule wa # 86 ebo kumbe huku mtu anaweza kutumia jina la mwingine? duh!
kiushaidi tushazoea kuona watanzania wanaanzisha vitu kwa maslahi yao binafsi hiyo”lakini kuna kitu naamini hasa wasomi wa ngazi ya falsafa”wanakuwa na ukweli fulani”na wapo binadamu wa kawaida nao pia wanakuwa na ukweli akiwemo huyu bwana”tusimdharau kwa kuwa tumezoea kuona ubaya.
Tomaso,
Au utomaso ndio tatizo letu. proof, proof, vitu vingine wala hamuhitaji proof ila huwa mnashabikia tu, lakini hili la huyu bwana mdogo mmekuwa wakali kwetu tunataka proof! Mbona wanasiasa kila siku wanawaambia maneno mradi tu ndio mnayayotaka kuyasikia hamuwaulizi proof. Au kwa sababu wanapinga kila kitu basi hawana haja ya kuleta proof.
Proof, proof, ukisaidia yatima leta proof, ukimpa mtu msaada leta proof. Huu sasa si ubinadamu hata kidogo kila kitu proof.
Yeye mwenyewe kasema anaguswa na anatoa misaada, sasa mimi sihitaji proof ya kujua kuwa anatoa misaada kwa sababu kwa wengine ukitoa kwa mkono wa kulia basi mkono wa kushoto usijue, na hautakiwi kutoa kwa RIYA, yaani utoe msaada basi dunia nzima ijue huko ni kujionyesha ni riyaa hiyo. Wako watu DSM wanatoa misaada lukuki tena kwa yatima na wasio yatima lakini huwasikii hata siku moja redioni wala gazetini wala kwenye luninga. Sasa nao hawa utawadai proof. NI dhamira tu. Na hata kama huyo Mashaka anatoa sina haja ya proof, ni dhamira yake tu inatosha midamu mwenyewe kasema anatoa misaada.
Wengi wetu hapa ni maneno makali kwa sababu tumeshindwa hata kuwasaidia ndugu zetu wa karibu wako choka mbaya wanasota hata wengine pesa za ada za shule zinawashinda, au wengine wanahitaji matibabu au dawa tunashindwa kuwasaidia kwa sababu hatutakuwa na proof ya kuonyesha kwa watu kuwa nasi tumetoa msaada. Pfhu!
Ingekuwa mimi sitahitaji kuonyesha proof kwa mtu yeyote ambaye ni ndugu yangu au si ndugu yangu niliyemsaidia wala ikitokea Mungu akanipa uwezo wa kumsaidia binadamu mwenzangu mwenye shida sitahitaji watu wajue, itakuwa kati yangu mimi na Mungu wangu, wala huyo niliyemsaidia sitataka ajue msaada umetoka wapi ajue tu ameupata kwa uwezo wake Mungu. Basi!
wee jamaa acha ujinga, mtu anakuja kwako na kukwambia nikopeshe milioni tano nina matatizo, huwezi kumpa bila kujua ana proof vipi kuzirudisha, yaani ana source zipi za funds za kumfanya arudishe mkopo si kumkubalia tu.
alikuja Jack Pemba akasema ana uwezo wa kupeleka timu ya Taifa ulaya na kuwatafutia timu watanzania nje ya mipaka. waTanzania hatukuhoji tukakubali kauli yake. TFF wakaweka timu kambini na wakatengeneza pasipoti za wachezaji wakimsubiri Jack Pemba aje kuwachukua, akaingia mitini,
kutokana na kutapeliwa na Jack Pemba inabidi hivi sasa tuwe wakali na tuhoji sana, kama Mashaka (mwanakijiji) ni Mcha Mungu kama anavyodai sasa kama mtoaji kwa ajili ya Mungu kwanini aje kujieleza humu?
hakuna mtu mwenye chuki na Mashaka lakini lazima tuhoji ili baadae tusije kuonekana wajinga kama kwa Jack Pemba.
kuna siku alikuja mtu toka Uinngereza akawapigia simu FAT akasema anataka kuja kuchezea timu ya Taifa kutoa mchango wake, kwani yeye anacheza na Beckham =UK na yuko timu ya READING.
FAT(CHAMA CHA MPIRA) HAKIKUHOJI WALA KUFANYA INVESTIGATION wakamwambia njoo akapelekwa kambini moja kwa moja KIBAHA, siku hiyo akasema amechoka hatacheza siku ya mechi akapangwa na umati ukajaa, kumbe jamaa hata kugusa mpira hajui, ikawa aibu.
Mwaka jana mwishoni kaja mchjezaji mwingine kasema anacheza DENMARK MICHAEL Chuma kuwa yuko daraja la kwanza akaitwa timu ya Taifa kufika home hata kukimbiza mpir a hawezi.
kama tungekuwa tunahoji sana hayo yasingetokea.
Mashaka hajasema kama primary alisoma shule gani, sekondari shule fulani au kazaliwa kijiji fulani, au digrii kasoma university fulani mwaka fulani hadi fulani.
interview yake ina mapungufu mengi mimi simkubali sababu naona ni DODGE.
MAMA Thereza hakusema kasaidia wapi ila sisi tumejua kutokana na athari za michango yake.
Mashaka angekuwa mtoaji watu wangemtangaza kuwa kuna kijana yuko marekani katusaidia hiki na hiki, lakini ukiona anajitangaza ujue kuwa tapeli.
waswahili wanasema kuwa CHEMA CHAJIUZA NA KIBAYA CHA JITANGAZA.
Bakhresa anajulikana kwa ukarimu wake na michango mikubwa kwa jamii huwezi kumsikia akijitangaza ila kazi yake inajulikana.
Nazidi kushangaa watu mliopo majuu mnakuwa na upepo mdogo sana wa kutafiti mambo.kama hili limewashinda mnamlaumu nini LOWASSA kubambikiwa mkatabata wa Richmond?
Mzalendo,
Umesema yote. Nabadilisha mwelekeo wangu. Naungana na usemi wako. Tunapaswa kuwa makini mno na huyu kijana Mashaka. Nakushukuru kwa kueleza kinagaubaga.
Shukrani kwa kunifumbua macho.
Heshima mbele.
mnaomtetea wote kawapa pesa mumfagilie au?au mna nidhamu ya uoga,waswahili tatizo letu tunapenda kufagilia vitu hata kama kuna kasoro..kisa yupo majuu/au anawadanganya msomi mhhhhhh eeeh ehhh tatu bila tatu bila tatu bila,nawewe subby wewe ndo kiumbe mzito usiejijua
Hongera Mashaka ukiwasikiliza waafrika hutofanya kitu majungu kibao ndio maana maendeleo ya kikonokonooo, achana nao wasidie watu usife moyo kabisa… kwa kuwa wao hawezi hata kupeleka sukari ya 2000 kwa watoto yatima, mawivu ya kijinga ndio hayo. Mawivu ya kimaendeleo zero,achana nao wanakijiji ni wao. alaaaaaa badala ya kumpa moyo mwenzenu tupige kahatua tuigwe na nchi nyingine za Africa mnatoa madongo…. mwaego jitoleee kwa raha zako.
hakuna kitu tutamwamini vipi kama anasaidia watu?anapata pesa kupitia mgongo wa watu,olalaaa hapa siyo swala la wivu tatizo lenu mtu akitolewa kasoro basi ni wivu,tumuonee wivu tunamjua sisi?tumpe moyo nasisi tutaishi vipi?mioyo yote tumpe yeye?
naona ameanza promotion mapema maana taasisi binafsi ni miradi kama maduka,, kama anataka kuwasaidia watanzania, achague maeneo kama mawili na akawasaidie walengwa moja kwa moja hakuna haja ya kuanzisha NGO yatakua yaleyale…..ebwana usitufanye bado tumelala bro tunaelewa sana lengo lango…kama inawezekana tueleze umesaidia wangapi ktk ukoo au familia yako maana hizi longolongo za kutaka kuingia bungeni tumeshazistukia toka siku nyingi kama hutajipanga we bora uangalie mradi mwingine na uachane na huu wa Nothing Going On (NGO) lasivyo mwisho wako utakua mbaya sana……msomi sio vidato na pia husifiwa hajisifii kama weye mashaka na mashaka ya mahojiano yake
I know this guy quite well. I covered him (Star-TV) during his trip to Tanzania in 2007.His family lives in Dar. Sina ushusiano naye, kwa hiyo msizushe kwamba kanilipa sina haja ya kulipwa
I met him when he went with a group of young people celebrities to Mkuranga village,ambapo watoto wengi wameacha bila wazazi. Lunch was prepared for everybody kwa courtesy yake. He is very humble and very polite.
Alitoa vyakula vingi sana kwa wanakijiji.He hired a minibus, along with Khadija Mwanamboka. There were several radio personalities, Dinah Mario Nancy sumari, Jokate etc… niliongea naye sana kwa zaidi ya masaa manne siku hiyo
Katika kituo cha New-Life Orphanage cha Magomeni, aliwanunulia pampu ya maji, magodoro, mablanketi vyakula na mahitaji mengine muhimu.pigeni simu 0754-202-216 ili mthibitishe the so called investigative journalists
In 2006, katika hicho kituo cha New-Life alienda kwa muda wa siku 5 bila kula kwa jili ya hao watoto, alikuwa akilala nje ya jengo. STAR-TV tuna uthibitisho ya haya yote
Kituo cha mayatima cha Safina cha mwananyamala pale alikaa siku tatu bila kula akawanaunulia vyakula vingi sana. Kitendo ambacho wengi wetu hawajakifanya
I think we are posting so many unnecessary comments; He has been doing charity for a long time for those who know him, and never publicized anything. I think jealousy is on the works here, in a very high gear. What is quoted here is a single instance from one of the hospitals in Musoma where he helped two wards
The last writer, rather than criticising his work, why can’t you work with him or show at least what you have done? Watanzania, wenzangu watu kama hawa inabidi tuwape moyo na kuwahimiza badala ya kuwacheka. Kikazi anafanya na Benki Moja kubwa la marekani jina sikumbuki nay eye ni investment banker Ni jamaa mtaratibu sana, na haya yote yalitokana na investigative work niliyofanya.
Nyie msijifanye kumjua. Mimi nilikaa naye kiti kimoja kwa masaa mawili, na pia kumhoji sana Dar. Nilipiga simu hadi kwa mkuu wa wilaya Tarime Stanley Kolimba, ambaye alinithibitishia kazi zake wilayani Tarime.
Katika kijiji kimoja cha wilaya ya Rorya, amechimba maji kwa ajili ya kijiji kizima. Wazee wote, wanawake wajane anawalisha kwa kuakikisha hawakosi chakula. Tunajidhalilisha sana kutokuchunguza mambo hau kutokuelewa ni vitu gani tuna comment.
I have done lot of research regarding this guy therefore wonder why some of you gets these under cooked stories. Mwananchi Feb, 29 a well written, those who read it would be touched, kwa kifupi ni kwamba tuacheni majungu na wivu !!!!
Mashaka:
Usiyasikie ya hawa watu, wamechoka hawa, hawana jipya endelea na shuguli zako, wala usikate tamaa Kwani Mungu atakulipa tu. Mike safari ya Mkuranga kama utanikumbuka.
Mike…
Sina mashaka na Mashaka John! Ninacho weza kusema ni kuwa mungu amzidishie katika utoaji wake. Nimesoma comments nyingi walizo changia wadau hapo juu nikaona kasumba ile ya kitanzania bado ipo inaendelea, wengine hata kumtusi ndugu huyu. Wengine wanadai kapewa misaada huko USA, wengine wamelaumu kwanini amekubali mahojiano, mara anataka ubunge na nk. Vyovyote vile mimi nasema inawezekana kwakuwa ndugu huyu amekaa muda mrefu (Kenya) kwenye jamii tofauti na yetu hivyo hana kasumba tuliyo nayo wa TZ ndiyo maana tunaona haiwezekani. Tuitumie nafasi hii kujifunza mambo mazuri aliyoyafanya nasiyo kuponda na kumkatisha tamaa. Kama kapewa msaada bado katoa kwa walengwa, kwanini sisi kila kitu kizuri tunakipindua kuwa kibaya?. Maneno yetu, hisia na mawazo yetu ndiyo vinachangia umaskini katika nchi yetu. Ifike wakati tukubali kuwa ya kale yamepita, tuanze upya, tuhusike kuto potosha ukweli kwa wengine na kuhamasisha jamii katika kuijenga nchi yetu tena bila lawama. Kinacho nifurahisha kutoka kwa Mashaka haja itumia nafasi hiyo kuponda uongozi wetu kama wengi ambavyo wangefanya wangepewa nafasi kama hiyo lakini ametoa mwelekeo na nimuwazi kuwa nchi haijengwi na viogozi bali ni wananchi ambao ni mimi na wewe. Viongozi ni kuandaa mazingira bora ili wananchi wasipate vikwazo au ugumu katika kufanya maendeleo yao ya kila siku. Kwa wale tuliyopo nje ya Tz hasa Ulaya na Marekani tunafahamu ni kwa kiasi gani nchi yetu ni maskini ukilinganisha na chumi za nchi hizi, tena tuna nafasi kubwa ya kuiletea maendeleo nchi yetu kupitia kuwafugulia milango ya kibiashara jamaa zetu kule nyumbani(networking). Tz imepewa nafasi ya kuuingiza baadhi ya bidbaa USA na UK bila kodi lakini bado hatujaweza kuzitumia nafasi hizo kwa kukosa network ambayo mimi na wewe tunaweza tukafanya kwa kuwaunganisha. Pia nasi kuwa na mitazamo ya kuwekeza kwenye nchi yetu kwa kile kidogo tunacho pata, tuache kuweka mbele matanuzi na anasa vitu vinavyo pita bila kuleta thamani kwa jamii yetu. Kutokomeza umaskini inawezekana nchini Tanzania inawezekana, simama kwenye nafasi yako bila lawama. Let us be envious to do good things when we see our fellows like Mashaka John doing . Mungu ibariki Tanzania!!!!!!
Hi Y’all
HUYU NI FISADI. HII NI PUBLICITY STUNT. AKINA ANGELINA JOLIE, WANAENDA KWENYE VIJIJI REGULARLY LAKINI HAWAJITANGAZI KAMA WEWE. NIMI NILIANGALIA OPRAH W SHOW SIKU MOJA, 2 HOT CELEBS WAKASEMA LAST YR WALIENDA KIGOMA AND I WAS LIKE WHAT!!! MBONA HAIKUTANGAZWA KWENYE VYOMBO VYA HABARI. WE ARE TIRED OF ALL TALK AND NO PLAY. NJOO BONGO UJICHANGANYE UONE JUA LILIVYO KALI. I’M SPEAKING FOR ALL TZ’s (TUNAOISHI BONGO) TUMECHOKA KUDANGANYWA KAMA WATOTO WADOGO!!!!!!!!!!!!! SCRAAAAAMMMMMMM!!!!!!!!!!
Nyie watu, sijui mna mashetani au nini. Huyu kaka hana kosa, nadhani mnempa moyo. Nyinyi ambao siyo Fisadi mmefanya nini ?
Wakena Chnege wanamaliza nchi, yeye anatoa hela zake na marafiki zake kusaidia Tanzania nyinyi mnamsema, sasa mnasema nini? Ni kijana mdogo, akiamua kufanya starehe hizo zote anaweza kufanyia atakalo yeye. You guys must reason a t a time, dont wivu control you too much, control it.
Well, ikiwa ni publicity Stunt basi kaipata na wewe Je? Nimesoma kila kitu hapa lakini naweza kusema kwamba naionea nchi yangu hurma ikiwa vichwa kama hivi ndo vnategemewa kuiokomboa nchi.
Sasa nyinyi mnaopewa data zenye kueleza ukweli kuhusu huyu mtafuta misifa na mnabisha, je mnasubiri hadi Dr Slaa aje awaeleze ukweli? Ngoja nimnukuu kama ilivyotoka kwenye gazeti la leo la mwananchi:
“Alisema kitendo cha Uingereza kuanza kuchunguza akaunti ya Chenge na jinsi alivyozipata fedha hizo, ni dalili ya kuelekea kuumbuka kwa kiongozi huyo ambaye aliwahi kushika cheo cha uanasheria mkuu wa Serikali.
Alisema tabia ya Watanzania kutowaamini wenzao wanaposema jambo, ndiyo iliyoifikisha nchi hapa ilipo, kwani kama Watanzania wangesikiliza maoni waliyoyatoa wapinzani, Chenge asingeweza kuchaguliwa katika nafasi hiyo.
“Sasa gazeti la Uingereza na taasisi ya nchi hiyo ndivyo vinafanya uchunguzi kuhusu kashfa ya Chenge na hapa ndipo Watanzania tunaamini kuwa kuna ufisadi. Hii ni aibu,” alisema Dk. Slaa. ”
Inabidi watz muanze kuwaamini wenzenu wenye kutoa data za uhakika.
WE MIKE UMEKUJA NA HUKU KUTOA USHAHIDI?TUTAKUAMINI VIPI NAWEWE?MWANSISHI WAKE SIJUI MSHKAJI WAKE…HEBU JIKATE STAR TV UNAFANYA KAZI GANI?Nyie msijifanye kumjua. Mimi nilikaa naye kiti kimoja kwa masaa mawili, na pia kumhoji sana Dar. Nilipiga simu hadi kwa mkuu wa wilaya Tarime Stanley Kolimba, ambaye alinithibitishia kazi zake wilayani Tarime. HE MAKUBWA UKIKAA NAE KITI KIMOJA NDO NINI?KUMEINGILIWA HAPA MAMLUKI HUYO
Eugenio;
Bwana umevuka mpaka sasa, hivi bwana mashaka kakufanyia nini? mbona hakuna Amani, kakunyanganya mke nini, kwa maana kila sehemu upo unampondea. Mike kayasema anayoyafahamu, wewe unafahamu nini au nini inakuhuma
Naona mashaka kamwaga chawa wengi kupita kiasi. Punguza majungu utaja kufa
Kisura
we kisura vipi?kaninyanganya mke wakati mi mwenyewe mwanamke,unakuruopuka tu kuingilia ya watu,we mfagilie kimpango wako sawa..mi sifanyi majungu hapa wala hakiniumi,wewe ndo utakuja kufa siyo mimi..tumemshtukia jamaa anatafta ubunge
Dah, kama ni mbunge basi atakuwa mbunge tosha, kwa maana mtiririko wa majibu yake ni ya kisomi na staili za kimarekani. ila nashangaa kwa nn mtu aache kazi nzuri za wallstreet kwenda kuenyeka na madafu za bongo, hatujui ngojeni tusibiri
Eugene, lakini naona imekuuma kidogo, mnafahamiana, mna undugu? Naisi wewe na jamaa kuna undugu kati yenu kwa maana kuponda kwako siyo hivi hivi
Kisura
we kisura nakuona mropokaji coz kila mtu anauhuru wa kusema kile anaona,kama najibu kwa staili ya kimarekani ndo tumbabaikie?tatizo la wabongo mtu akikaa nje tu anaweza akawafanya lolote na kumwangalia,huyu ni tapeli tu na sina undugu nae mi siyo mtu wa bara
Rafiki yangu mbona matusi kwangu tena? Waafrika tuna laana. Sasa angekuwa ameandikwa kwa mabaya ingekuwaje? Hawa wameandika vizuri tu, kijana hajajigamba na hajasema kwamba kafanya hili na lile, kasema anaomba moyo wa unyenyekevu na kuepukana na jeuri sasa hapo kosa ni nini?
Wewe ndio mropokaji, unamuona bwana mdogo anakushinda ilo linakuuma kupita kiasi. mimi hoja zangu zimetokana na niliyoyasoma, na siwezi kumhukumu mtu kiupuuzi staili yako lazima tutumie busara kabla ya kutua hukumu na matusi. WEWE ni mpuuzi kwa maana hauna hoja zaidi ya utapeli usio na ushahidi nao
Huyo kaka haumjui, na wala mimi simjui, ni ushahidi gani ulionao unaokufanya uniite mimi mropokaji au yeye tapeli kama siyo wivu na majungu?
Aliyemhoji ni mwandishi, na mwingine hapo namuona ni mwandishi (Mike) wote wametoa hoja zao, sasa wewe mtu haumjui na matamshi yako yanakuwa ya chuki kiasi hicho, kivyovyote vile lazima tutakushuku kuwa mwana majungu! Get a life… Umepambana na Mike, yemekushinda, sasa unanirudia mimi, wewe una lako jambo humu. Huyu kaka alikutelekeza ndo maana unampinga kwa kila namna, ila utaumbuka tu
Remember all that you do in the darkness comes out in the light at the right time , it is just a matter of time !
we subby unasema nini wewe/wote tunaoponda humu tumechoka na maisha/labda wewe ndo unabembeleza vimsaada hapa..hili tapeli
Wala msimjali huyo Euginio, wao kila kizuri wanapindisha kuwa kibaya, hayo ndo yale majizi mafisadi. Mashaka amewashinda ndio chanzo cha majungu majungu. Hacheni kumfutafuata huyu kijana. Mimi nimependezwa naye, mahojiano yake mazuri sana, na kweli inabidi wamuige
Kinje
Waliochoka na maisha inabidi wafe, siyo kutuletea zao !
huyu tapeli…na mimi sijachoka kimaisha coz hamjui mimi nani?huyo mike muandishi tutamwamini vipi kama kweli mwandishi?mi zaidi ya huyo mashaka ila sijisifii na kujitangaza!na mike hakunishinda mbona amekaa kimya ye mwenyewe kwani kajibu tena humu?tunachotakiwa ni kila mtu kutoa comments zake siyo mara ohh mara ehh nawewe sindo ulieanza kujidai kunipasha..nyie mmetumwa mje mumfagilie,mi simwonei wivu coz hanihusu,inamaana vyama vya siasa vinavyompinga jk pia ni kumwonea wivu?
Wee Euginio, hacha zako. Hacha wivu, mbona kila mtu huku kakushtukia? una tabia za Kichawi, badala ya kulumbana na sisi mtafute Mashaka ulumbane naye, umevuka mpaka sasa. Heri ningekuwa nina undugu naye, ningemwambia ajitaadharishe na wewe
Hakuna anayetaka kukujua, hata kama wewe ni Jena Bush. Heri yake tunamjua kua tapeli, ww anakujua nani? kijini kwenu hawakujui, hata na mbwa wenu hakujui jina !!!
Ushauri wangu! kajitie kitanzi, mashaka anamke tena wanaishi hapa Houston, mchaga mwenzake toka machame (Jovinata Kileo) demu bomba ka binti kiziwi uliza wadau kwa michuzi watakuadithia
Mi sina taste ya wanaume kama mashaka,huyo jovi mwenyewe siyo kitu kwangu…mi simtafti mashaka ila nakupasha wewe mpambe uliekurupuka na kujidai kunisahihisha mimi,huyu tapeli mnamfagilia sababu anawadanganya kasoma mnaingia mkenge,na kwa tarifa mi nimeolewa simtamani mashaka hata kidogo….mimi kijijini kwetu wananijua,na mitaa ya jiji la dar yote wananijua ninavituo.utajiju
Wewe Eugino, hauna lolote. Alafu hacha kujifanya mtoto wa mjini wewe pia kachaga tu au katoto ka fisadi fulani. Hii ni karne ya technolojia, kujua huko wapi syo noma, alafu kwa taarifa yako naweza kukupata tena hii wiki
Unajidai na sura kama kiatu, heti taste ya wanaume kama mashaka hauna, mbona basi swala lake linakusumbua? haya basi mzuri kuliko Jovi, mwambie Jovi mumwwe ni tapeli email yake ni jovinatakileo@yahoo.com. Ningekupa ya Mashaka, bahati mbaya sina. kama unajuana naye au kala alikutelekeza mwambie basi anitumia ukwacha kidogo, njaa kali mwanangu!
Mtu wee haumjui, lakini umemkazania kaa chonde! duh, huyo mumeo namuonea huruma, ila Jovinata kakuwai. Mimi ni mbeba boxi, na kwetu hatuna chochote lakini pale mtu anapofanya mema, lazima tumpongeze, nashangaa umejaa jazba mpaka kila mtu anakushangaa
Hakuna anayekujua, pengine magengeni au posta feri wateja wako. Niite mpambe, au mbeba boxi, yote nitakubali lakini wewe pia kubali dogo kakushinda. Wewe unadhani wazungu wajinga, hadi kumuweka mtu kwenye luninga zao, wamekukubali.
Sababu yangu ya kukuita fisadi na mchawi ni kwamba, mbona jamaa hajazungumzia elimu, hiyo umeitowa wapi? au alikutapeli chupi? Nadhani bangi zako unazivutaga na msokoto mbaya, kanunue makaratasi ya blunt, nzuri kiasi!
Heeeheee naona unabwabwaja,kwani we umekua nani humu kwenye bc?na hiyo anwani ya jovi unayonipa we mwenyewe umeitoa kwa michuzi nawewe ndo wale mliomtukana huyo jovi sasa unaleta nini hapa?hajawahi kunitelekeza mashaka kama nilivyokuambia sina taste nae kwanza pozi zake tu za kishamba…wewe ndo mchawi maana unachokitaka wewe ndo unataka watu wote wakubali,nani kanishangaa humu/kwani mi pekwe yangu ndo nimemponda?mbona wengi wamemkandia?sijajaa jazba ila huyu ni TAPELI MKUBWA NA ATAWAPATA WAJINGA KAMA NYIE WA KUMFATILIA
Na kwanio mzungu nio nani hadi akikuweka kwenye luninga ndo ujione ni mtu?yaleyale…tatizo la wabongo mnababikia ujinga..kwani mzungu ni mungu? hehehehe holllllllllla
Mimi sioni ajabu ya Eugenio kutokupenda maendeleo ya Mashaka. Hii ni kawaida ya wabongo na ndio ile kasumba wengi wetu wamekuwa wakiipinga ya kutokupenda maendeleo ya wenzao.
Wakina Mashaka, ni wachache sana, kwa hiyo mbongo lazima atashngaa na kuleta wasiwasi wake
Kinje
we uliejibadilisha jina na kujiita kinje ndo siwezi hata kujibishana nawewe
Hivi huyu karudi tena?
ni moja ya hazina bora, na kupitia john tukue tukijenga fikra njema ndani ya nchi yetu, tupendane na kuheshimiana, na hasa kwa wale tulioweza kufika ngazi za juu kielimu, kuna wenzetu hawakupata fursa hii, tuitumie vema na tukumbuke yote hii ni juhudi za jamii yetu, tusisahau tulipotoka, MUNGU ATUBARIKI.
Bc Funga mjadala sasa, naona wanaojibishana hamna kitu kabsa
Mwanakijiji au Mashaka kaumbuka na hapa anatumia majina mengine kama haya ya MIKE NA KISURA kujifagilia.
kule Jambo Forums anatumia majina ya kike kama Mwafrika wa kike, bi senti 50,madela wa madilu, koba na BEN kujifagilia au kuunga mkono hoja anazoziandika.
ni mpuuzi , kama angekuwa na pesa angemsaidia Zitto Kabwe kwenye jimbo lake. amekuwa akizurura nae tu. kwenye ziara ya marekani ya zitto. ni tapeli mkubwa.
Jamani haya ndo yapi tena mzalendo? Naona kazi ipo, hivi mashaka na zitto kabwe wana uhusiano gani?
hawana uhusiano wowote zitto ni mtu wa kule kwa akina brother K Kigoma na John ni wa Musoma huko…but all those guyz ni mfano mzuri sana sana wa kuigwa.
my dear fellow tanzanians dont be stupids like the old people in the bible who wanted to build a tower to reach heaven,it does need for you to graduate from oxford,cambridge or other big universities to know that there’s no way you can reach God by simply climbing the ladder,what i have discovered here is that tanzanians are very easy to be cheated cause they trust people so easily with no cost.now let me tell you the truth,namjua mashaka vizuri sana,huyo kwanza sio mtanzania hilo moja lakini hilo la uraia sio kubwa sana kwani yeye anadai anajitoa kusaidia watu wa tanzania hivyo mambo ya uraia tuweke pembeni.mashaka ni mtoto wa segerea tabata hilo hawezi kubisha hata kidogo na huwa tunamuona akija dar na kuondoka na tunajua mitkasi yake yote,huyo hana cha kusaidia wala nini he’s after the money and fame,hana lolote,mimi hata akija dar i will tell him openly kwamba yeye ni muongo na asiwaibie watanzania kwa michango yao aende kuwaibia wakenya wenzake.nasema haya yote sio chuki binafsi no!!!! bali nina uchungu na watanzania watakao toa michango,huyo mtu tunamjua wadogo zake wapo tu dar hapa,wezi tu.ni hayo tu kwa leo kama una masikio na usikie,kama huna toa mchango halafu utaona.jina lenyewe mashaka
Hamry-tendambwe huna jipya,
Acha kumtetea huyo jamaa kwani hana tofauti sana na wanasiasa wa BONGO.
Maneno miiiiiiiingi lakini hakuna kitu…..fix tu.
Atende kwanza ndio tumpambe kwa mapambio na sifa za haleluya eboh!!
Mchungu wa Bongo,
Mbona jamaa hajaomba hela toka kwa Watanzania. Dah.. mnaponda kweli, kama kweli ni mkenya basi ni mkenya mwenye uzalendo mkubwa kwa watani wake wa Jadi
Kwa hiyo ana wadogo zake ambao ni wezi? Nadhani wewe na JM ni mandugu na wivu unakunyonga.
Basi wewe Huyuhaumjui siyo mkenya, ndio wale wakina Mabere Marando ambaye ni mjomba wake
Hivi Huko marakani anafanya kazi gani? au huko pia anaiba?
Wanamuita na vile vile na kuhisi kwamba yeye ndiye mwanakijiji ambaye anamiliki KLH News, ambaye pia anasumbua na kuwafanya watu kujikuna vichwa kwenye Jambo Forum, usomi wake ni vipi?
Mashaka endelea na kazi zako, hawa wenye machungu ni wengi. Umewashinda kwa hiyo watazidi kukuchafulia hali ya hewa. Hongera na kila la kheri
Sasa nyinyi mnatuita wabeba boxi alafu mnamleta humu kuturingia? Mnatuona kama mbwa heti?
Huyu naye ni fisadi ndio maana tuna mahasira naye. Lazima tuone wivu mlidhani nini, tokeni zenu hapa na hilo li mashaka lenu mambo ni Obama bwana.
mimi nampongeza huyo kijana
sasa kunakitu kimoja vipi naweza kupata contact zake bro? kuna wakati na mimi nilijaribu kufanya hayo ingawa ni kwa mtu binafsi sio kikundi cha watu na pia siko njema kiuchumi ila napenda sana kujishughulisha na mambo hayo,
Vipi naweza kumpata kaka huyo (contact) ili anisaidie ushauri najinsi ya kufanya kwani nia na myo wa kutoa ninao jambo amabalo namshukuru sana Mungu kwa kunipa moyo huo.
Pia namuombea kaka John aendelee na moyo wake huo na Mungu atamjaza pale anapotoa mara saba sabini
WATANZANIA NAONA MMEATHIRIKA NA UFISADIMANIAC NA HAMUWEZI KUPONA TENA MKO ICU MNAPUMUA KWA MASHINE HEEEEEE,POLENI UNAJUA NIWAAMBIE KITU,EXPOSURE BROADNED YOUR HORIZON…….HATA YESU WATU WALIMWONA PIMBI 2 SI MTOTO WA FUNDI SELEMALA FLA 2 VIPI AJIFNYE MASIHA…..MSULUBISHE…………MNAMSULUBISHA MASHAKA AMBAYE ANAWASAIDIA NDG ZENU WA HALI YA CHINI……MNATAKA AWASHIKISHE KWANZA NDO MUMKUBALI?AMKENI WATOTO WA VIGOGO WANA HELA ZAIDI YA MSHKAJI LKN WAO WANAOTA KURITHI UDIWANI UBUNGE NA KUFANYA KAZI KULEEEE BIIIIIIIIIOOOOOOOTTIIIIIIIIII MPOOOOOOOOO.SHHHHHHHHHHHAAAAATTTTT………UP,BRAVO MASHAKKKKAAAAA.
John masaka. Jina lako limekuwa msukumo na pride kwa tanzania. Ila tumia muda wako magharibu kujifunza zaidi. usijiingize katika siasa kwa maana pamoja na upeo wako, mafisadi hawatakuacha. kadhalika usijali maneno ya hawa wachovu ambao hawatoi majina kamili. Endelea na kazi nzuri ongera sana Masaka na mungu akubariki
so… ur not married yet, what next……….
Jamani, Kaka yangu Bongo Celebrity, mimi ni dada mzuri tu,tena mstaarabu, nafanya kazi zangu za modelling Afrika kusini na jamii inanifahamu vizuri tu, sina kashfa ya aina yoyote na bila kuficha au kuzunguka mbuyu, huyu kama nimempenda.
Shida ni kitu kimoja, umaarufu unakuja na matatizo yake. Umaarufu wangu umewafukuza mabwana wote ambao wangeweza kunioa. Kwa sasa hivi kila anayeni approach ni watu tu wa kunichezea. umaarufu unafunika kila kitu isipokuwa watu wa kukuchafulia jina
Jamani mimi namtaka Joni Mashaka, najua hajaoa na hana mchumba, kwa hiyo naomba mnipe njia ya kuwasiliana naye. nimesikia habari zake kwa watu tofauti, ni kijana mstaarabu sana
M O
Wow..its very amazing to see this from our braza who live in America coz there are a lot of them but they cant do or think like u.am proud of u my braza..i know, they will be a lot of obstacles and critizes from haters but guess what if God put u into this no man will stop u. Am supporting u 100% and i will give u my email we will keep in touch n i will join u on this ,i live in Washingtn DC.
Its fine Mr Mashaka!
mashaka maelezo yako yananivutia sana na nina mambo mengi sana ya kuongea na wewe naomba tuwasiliane kwa kupitia mobbasi2000yahoo.com
mobbasi2000@yahoo.com nafanya marekebisho ya hapo juu
Mtu wangu nakufagilia, you are incredible. Kweli bongo Celebrity huyu ni mfano wa kuigwa..
do what ur doing, dont give up however, learn to deal with people like US based blogger who is now known to us in the utamu and jamii forums. we know his intent. keep it up
[...] mie nimemsoma “KUTOA NI MOYO,SI UTAJIRI”-JOHN MASHAKA – BongoCelebrity …..unajua wengi wakitoka majuu wanatuambia mengi na sisi huku tunawaamini kwa kuwa wanajua [...]
Lisemwalo lipo kama halipo basi liko njiani.
I would like to take this opportunity to thank Mchungu. Although I am not sure about his comment concerning Mashaka but my fellow Tanzanian open your eyes be visionary Mchungu has a point so at least he has warned you in one way another.
Nowadays there are so many crooks worldwide that are educated finding every means of making money. Pretending they are good Samaritans. He is on his way to ask donation from Tanzanians that’s why he came up with all fake explanation by knowing that they will be a lot people who would be attached and interested to what he is doing like I read some comments people want to keep in touch with him be carefully be wise enough (visionary) every human being have capacity of doing so
One might wonder Tanzania its one of the African countries with wealthy natural resources. When Americans or whoever come and sign agreement with (VIZITO) I mean readers about the utilization of Diamond plantation etc do you know how much % of money does the indigenous benefits from that resources and % taken by Americans. Or because they promise to build up clinics, schools that do not even cost 10% of the amount of money they generated and still indirect from our recourses we are just happy while they are making themselves rich and richer plus few minority Tanzania (wakubwa) and leave the majority without knowing what is happening?
Open your mind Mashaka might be one of few or many trying to rob Tanzanian who knows someone is behind him pumping him money when they will get what they want you will never hear about Mashaka you can prove me wrong at the later stage.
Asiyesikia la mkuu…………………malizia
I please to go and do more research about that.
Cheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeers!
Watanzania acheni Ujinga,Anaye stahili sifa mpeni sifa.mnajijiona ninyi ndio mnajua na mmesoma sana mbona hamsaidai?
Hongera bwana JM kwa mchango wako Mungu akubariki sana.Watu kama ninyi ni wachache sana katika dunia hii,Hivyo usiache kutoa mchango wako brother.Achana na hao mafisadi,
Km,
This guy must have chilled and get his skills pale kwa Azam (coping & paste)several articles put together and here we are! My advice is “you can fool the fool but not all the time” ngoja wanakijiji wakushtukie? ni Wall Street au samora Ave the one u r talking about? To me u r broker working at ur apt if any? Find another gear bro!!
on my view you have hidden agenda which is powerremember your country most of the people are under privilege
on my view you have hidden agenda
WEWE MR J MASHAKA UNAFIRI HICHO KINGEREZA CAKO UTADANGANYIA WANAINCHI? LISTEN YOU FAKE POLITICIAN MYSELF IM KEEP EYE ON YOU. AND MAKE SURE YOU WILL NEVER BE POLITICIAN.
majitu mengine majinga sana, sasa mbona manleta vitisho? kwani yeye siyo mtanzania au mnadhania kwamba hana haki ya kuwa kiongozi?
Hongera Mungu akubariki kama kweli unafanya unayoyafanya naomba email yako please kuna mambo nataka kudiscus na wewe,asante.
mashaka mie sitaki mengi au makuu. mimi nataka tujuane tu, kwani hapa dili italipa sana. nasikia swahiba wako january kamaba naye hajaoa, basi hapa lazima nijishindie mmoja, kwani alama za $$$$$$ ziko nje nje, na umaarufu juu yake nitake nini zaidi, wanainchi wenzangu?
mashaka napenda sana makala yako, na tunakusihi usihache kuandika kutokana na wivu wa watu wachache waliopoteza mwelekeo. wewe ni shujaa wangu, na ninakuombea kila kukicha, mungu akuzidishie na akubariki. sina shaka ukiwa kiongozi, nchi yetu itapata umeme kila kata na kila kijiji
Mashaka i wish you all the best,Mungu akujalie kutoangalia watu wanaokurudisha nyuma kwa maneno ya kukatisha tamaa.Songa mbele na Mungu wako pia muweke mbele.If God is with you who can be against you.
bless you
Huyu mtu alifanyiwa tambiko ndo maana kila alipo atu wanamfuata as if he is a little god. mambo ya kikurya, mura nakakotheme, thiga niche. Siyo kwamba ana akili kuliko wote, ni bahati tu