Yapo mambo ambayo pindi yakitokea kila binadamu hushikwa na butwaa na kutokutambua mara moja kwamba nini kimetokea,kinatokea au kinaelekea kutokea. Mojawapo ya mambo kama hayo ni kama kitendo kilichotokea hivi majuzi pale katika hospitali ya Muhimbili ambapo mtoto mwenye umri wa miaka 12 ajulikanaye kama Ramadhani Mussa(pichani) alikamatwa akiwa na kichwa cha mtoto mdogo, Salome Yohana (miaka 3) alichokuwa amekibeba kwenye mfuko wa Rambo!

Tukio hilo la aina yake,la kusikitisha na hata kuchosha akili limeandikwa na blogs mbalimbali na pia vyombo karibuni vyote vya habari nchini Tanzania.Kwa sababu habari yenyewe bado inazua mijadala mbalimbali, tumeona sio vyema kukunyima wewe msomaji na mtembeleaji wetu, fursa ya kutoa maoni yako kuhusiana na tukio hili.Nini maoni yako kuhusiana na tukio hili? Ni uchawi, imani za kishirikina, matatizo ya akili au ni nini hasa? Kwanini watoto?
Isitoshe,mtoto Ramadhani Mussa, ambaye hivi sasa anashikiliwa na Polisi Mkoa wa Ilala, Kanda Maalumu ya Dar-es-salaam akiendelea kuisaidia polisi na uchunguzi, yawezekana ndio jina au tukio lililotawala vinywa vya watu wengi hivi sasa.
Kama hujapata fursa ya kusoma habari mbalimbali kuhusu tukio hili,unaweza kufanya hivyo kwa kubonyeza hapa na hapa na hapa.
Wakati huo huo,gazeti la Uwazi(mojawapo ya magazeti ya Global Publishers), hivi leo wametoa habari ya kina ya tukio hili kama ambavyo unaweza kuiona katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo hapo chini.Unaweza kuisoma habari hiyo kamili kwa kubonyeza hapa.

Page 1 of 3 | Next page