MH.ANNA KILANGO MALECELA

Pichani ni Mbunge wa Same Mashariki,Mheshimiwa Anna Kilango Malecela.Mbunge huyu katika siku za karibuni ametokea kuwa miongoni mwa wabunge wanaoonekana kuwa na dhamira nyoofu katika kuupinga ufisadi nchini Tanzania.Inatia moyo kiasi fulani kuona kwamba kumbe wapo wabunge au viongozi ambao angalau wanaonyesha kukerwa na hali halisi(hali mbaya) ya mambo nchini mwetu.

Yupo msomaji wetu mmoja ametuuliza;hivi ufisadi ni tabia inayoanzia ukubwani au ni tabia ambayo mtu anakua nayo tangia utotoni?Mazingira ya kazi ya mtu yana mchango gani katika kuendeleza au kuamsha tabia za kifisadi?Tunaomba msaada wa majibu ya maswali hayo kama unayo.

Page 1 of 3 | Next page