HAPPY MOTHER’S DAY TO OUR SWEET MOTHERS.

Katika nchi nyingi za magharibi,leo ni Mother’s Day au kwa maneno mengine Siku ya Mama.Leo ni siku maalumu ya kumkumbuka,kuutambua na kuuthamini rasmi mchango wa mama yako katika maisha yako.Huu ni utamaduni wa kimagharibi ambao unazidi kuenea kwa kasi ulimwenguni kote zikiwemo pia nchi zetu za kiafrika.Sasa hii sio kumaanisha kwamba katika siku zingine usimkumbuke,usiutambue wala usiuheshimu rasmi mchango wa mama yako.La Hasha!Kila siku,kwa walio wengi, ni siku ya mama. Kwetu sisi waafrika ndio kabisaa.Ndio maana kuna ule usemi kwetu wa Nani Kama Mama?

Itumie siku ya leo kumkumbuka mama yako.Kama kwa bahati mbaya alishaiaga dunia,basi chukua muda maalumu kumkumbuka,kumuombea na muhimu zaidi kumuenzi.Kama upo karibu na mama yako,basi mkumbatie na umkumbushe kwamba unampenda na unamtakia kila la kheri katika maisha.

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, kama binadamu,huwa inatokea wakati mwingine tukakosa kuelewana.Ndio.Huwa inaweza kutokea tukakosa kuelewana hata na mama zetu! Kama hali ipo namna hiyo katika maisha yako,itumie siku hii kusameheana na kuweka mambo sawa na mzazi wako.Jinsi moja nzuri ya kuweza kusamehe ni kujiuliza swali;Je kuna ulazima au manufaa yoyote ninayoyapata kutokana na kutokuelewana huku? Usiwe mgumu wa kusamehe ili nawe upate kusamehewa.Sote tunakosea katika maisha.Kama leo basi ni kesho.Usisite kutenda lililo jema leo.

Katika kuisindikiza siku hii,tumekuchagulia wimbo maalumu kutoka kwa mwanamuziki mkongwe wa nchini Nigeria, Prince Nicco Mbagga.Wimbo unaitwa Sweet Mother. Huu ni wimbo maalumu kwa kina mama wote.Kinamama,tunawapenda na tunawathamini.Bila ninyi dunia si dunia.Bonyeza player hapo chini upate burudani,sikiliza ujumbe uliomo ndani ya wimbo.Happy Mother’s Day!

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Page 1 of 3 | Next page