Ni Ijumaa Tena.Wakati mwingine wa kupata burudani tayari kwa kuukabili mchana wa siku,jioni au usiku. Si unajua tena mambo ya Ijumaa? Kila mtu yuko “bize”.Ni mwendo wa ujumbe kwenye simu za viganjani(au wewe unaziita za mkononi?).Simu za mezani ofisini na majumbani nazo zinakuwa bize pia.Ukipiga ile ya ofisini usishangae sana ukisikia katibu muhtasi akikujibu bila yale mashamshamu ya kawaida.Ni Ijumaa mchana na anasubiri kwa hamu “kutoka”.Ili mradi tu kila mtu yupo bize kwa namna moja au nyingine. Na ukiwa mwenzangu na mie,ukata umetanda,basi unajidai kuwa na miadi muhimu nyumbani.Unaaga wenzako na kukimbilia nyumbani upesi.Ukifika nyumbani,unajidai uko tena “bize” na mambo ya ofisini.Maisha yanakwenda.Hapo ndio unagundua kwamba kumbe hapa duniani kuna watu wanaishi huku wengine wakiwepo tu.
Kwa upande wa burudani leo tunahama kidogo.Tunaenda kwa jirani zetu Kenya.Pale tunawakuta Gabriel Omollo na mwenzake Omondi Jassor.Wimbo unaitwa Lunch Time.Huu ni mojawapo wa zile nyimbo ambazo hata zipigwe vipi au mara ngapi,bado ukiusikia utakuamsha kama sio kukumbusha jambo,sehemu au mahali fulani.Radio moja maarufu sana jijini Dar ilikuwa inapenda kuupiga kila siku mara majira yanayoitwa mchana au wakati wa lunch(Lunch Time) ukifika.Mimi nikisikia wimbo huu nasikia njaa lakini wakati huo huo napata cha kufanya(kuzuga na window shopping).Pata burudani.Ijumaa Njema.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 6 or above) is required to play this audio clip. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Feedback / Comments
7 Responses to “NI LUNCH TIME!”
Leave a Reply













Ninyi watu BC mnagusa hisia sana kila mara.
mpo makini kwakweli.
keep it up!
Thank you so much
haha okee
BC
Safi sana hahahaa
Naipendea Ijumaa hapa tuu!
Home sick.music unaoendana na mlo wa mchana ugali kwa nguru wa bahari ya hind.wakati wa kipindi cha mapunziko ya saa saba enzi zile za shule aya msingi duh
safi BC
CHAFOSA CHAI GODA
Its too old for me…….Bc tuwekee ule wimbo wa kasongo yeye….mobali nagai, kasongo ngalaleo…….hapo nilikuwa macho. Edwin, upo hapooo?
Du mimi siku zote nilidhani hii nyimbo imepigwa na watanzania kumbe wakenya? Mbona basi walitakiwa wawe juu kimziki leo hii pia ila naona wamepwaya kidogo. Nice song this is!!!
Siuongo,shida haina adabu ukiwanashida unaonekana chojo tu hata ukitoa wazo watu wataona lakijinga,na mwenye vijisenti hata akikohoa watu watampongeza………ah ndio vile yote maisha