Kwa wapenzi wa filamu za Bongo ni jambo la faraja kuona kwamba hatimaye,kwa mara ya kwanza,mwaka huu kutatolewa Tuzo kwa sekta hiyo ambayo inazidi kukua siku baada ya siku.Tuzo hizo zimeitwa Tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania au Tanzania Vinara Film Awards.

Kama ambavyo mmekuwa mkifuatilia kupitia vyombo mbalimbali vya habari,kampuni ya One Game Promotions ndio waandaaji wakuu wa Tuzo hizi.Baada ya mchakato mzima wa kuwasaka vinara hao wa filamu,majina rasmi ya walioingia hatua ya mwisho ya kuwania tuzo hizo yametangazwa.Here are the nominees;

TUZO ZA VINARA WA FILAMU TANZANIA (TANZANIA FILM VINARA AWARDS) 2007 – 2008

Muigizaji Chipukizi wa Kike (Up coming actress)

Irene James – Miss Bongo II

Irene Uwoya – Diversion Of Love

Fatuma Makame – Karibu Paradiso

Jennifer Mwaipaja – Silent Killer

Grace Michael – Malipo ya Usaliti

Muigizaji Mwandamizi wa Kike (Best Actress in a Supporting Role)

Irene Uwoya – Diversion Of Love

Mama Frank – Yolanda

Irene James – Miss Bongo II

Susan Lewis – Behind the Scene

Tecla Mjata – Macho Mekundu

Muigizaji Bora wa Kike (Best Actress)

Lucy Komba – Diversion Of Love

Grace Michael – Malipo ya Usaliti

Halima Yahya – The Stranger

Elizabeth Chijumba – Copy

Riyama Ally – Fungu la Kukosa

Muongozaji Bora wa Filamu (Best Film Director)

Gervas Kasiga – Fake Pastors

Jimmy Mponda – Misukosuko II

Kulwa Kikumba – Macho Mekundu

Haji Adam – The Stranger

Halfan Ahmed – Copy

Mtunza Sauti Bora (Best Soundman of The Year)

Adam Wazir – Fungu la Kukosa

Cleophance Ng’atingwa – Kolelo

David Sagala – Copy

Camillius Kanuli – Fake Pastors

Swalehe Juma – Fungu la Kukosa

Mpiga picha Bora wa Filamu ( Best Cameraperson of The Year)

Mbalikwe Kasekwa – Misukosuko II

Sylon Malalo – Kolelo

Rashid Mrutu – Copy

Nicholaus Mtengwa – Kilio moyoni

Sylon Malalo – Simu ya Kifo

Adui Bora wa Filamu (Best Film Villain)

Mohamed Aziz – The Body Guard

Irene Uwoya – Diversion Of Love

Sebastian Mwanangulo – Misukosuko II

Ahmed Ulotu – Silent Killer

Elizabeth Chijumba – Copy

Mhariri Bora wa Filamu (Best Film Editor)

Moses Mwanyilu – Misukosuko II

John Kalage – Miss Bongo I

Rashid Mrutu – Copy

Hassan Mbangwe – Malipo ya Usaliti

Sylon Malalo – Kolelo

Mwandishi Bora wa Filamu (Best Script Writer)

Seleman Mkangara – Malipo ya Usaliti

Hammie Rajab – Kolelo

Kulwa Kikumba – Diversion Of Love

Lucy Komba – Utata

Elizabeth Chijumba – Copy

Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kiume (Best Actor in a Supporting Role)

Aliko Tshmwala – Segito

Single Mtambalike – The Stranger

Adam Kuambiana – Fake Pastors

Halfan Ahmed – Copy

Emmanuel Muyamba – Fake Pastors

Muigizaji Chipukizi Bora wa Kiume (Best New And Upcoming Actor)

Emmanuel Muyamba – Fake Pastors

Laurent Anthony – Karibu Paradiso

Hassan Nguleni – Body Guard

Yussuf Mlela – Diversion Of Love

Uswege – Malipo ya Usaliti

Muigizaji Bora wa Kiume (Best Actor)

Single Mtambalike – Agano la Urithi

Nurdin Mohamed – Utata

Jacob Steven – Copy

Haji Adam – Miss Bongo

Yussuf Mlela – Diversion Of Love

Mapambo na Maleba Bora (Best Costume And Makeup of The Year)

Misukosuko II

Macho Mekundu

Kolelo

Utata

Copy

Mtunzi Bora wa Filamu (Best Creater of The Year)

Lucy Komba – Utata

Nicholaus Mtitu – Diversion Of Love

Single Mtambalike – The Stranger

Halfan Ahmed – Copy

Hammie Rajab – Kolelo

Filamu Bora ya Mwaka (Best Movie of The Year)

Behind the Scene

The Stranger

Diversion Of Love

Macho Mekundu

Misukosuko II

Simu ya Kifo

Copy

My Sister

Silent Killer

Miss Bongo I

Agano la Urithi

Malipo ya Usaliti

Utata

Kilio Moyoni (Crying Silently)

Fake Pastors.

Ungependa kuona nani anashinda?BC inawatakia kila la kheri all the nominees.

Feedback / Comments

19 Responses to “AND THE NOMINEES ARE…”

  1. Comment by Nina on May 22nd, 2008 2:41 pm

    Mhmh hii kali mbona waigizaji tunaowajua sisi, kama kna kanumba na kin aRay hawamo.. mhmh sijui kazi kwelikweli.. na hii award ni za movies zote zilizotoka ama ni za wmaka jana?

  2. Comment by Mtukwao on May 22nd, 2008 3:07 pm

    Jamani wana kama nitakuwa nimekoea naomba mnirekebishe.

    Hilo jina la “Tanzania Film Vinara awards” mie naona kama haileti maana “in a professional level” kwanini wamechanganya kiswahili na kingereza/english?? kwanini wasinge andika ktk “lugha” moja kiswahili au kingereza?

    but nikitu kizuri kwa Tz!

  3. Comment by michelle on May 22nd, 2008 4:36 pm

    Mbona akina Kanumba hawamo, au ndo mmeshaanza mambo yenu ya huko Bongo mpaka uhonge mambo ya kujuana, vinara juu juu zaidi wabongo bwana.

  4. Comment by Pearl on May 23rd, 2008 1:49 am

    no comments for sure.

  5. Comment by Chala on May 23rd, 2008 3:33 am

    jamani hii inakuwaje tena? kuna watu kibao mmewaacha, Ray Kanumba, Mzee kipara na wengine kisha kuna filamu ya shumileta ni nzuri sana mbona haimo? au lazima kitu kiwe kimetoka mwaka huu sielewi kdg jamani!! uigizaji wa hiyo filamu ni mzuri mno.mmh haya….

  6. Comment by binti-mzuri on May 23rd, 2008 8:15 am

    mi simjui mtu hata mmoja hapo

  7. Comment by baker on May 23rd, 2008 10:49 am

    Duh ebwana wee kweli bongo wameamka sasa! lakini mbona apo kuna kama kuchemsha kidogo? Kiswahili + kingereza???????
    kazi ipoooo bongo.

  8. Comment by Meremeta on May 25th, 2008 9:17 am

    Jamani, mbona majina makubwa kama Kanumba hawaonekani hau ndio stahili za kibongo za kuhongana? Na yule kaka Mtanzania wa Holy-Wood Jonie Mashaka, mbona hayumo? alafu hizi awards zina maana gani kwa sabubu hawa wote ni waganga njaa hapa mjini

  9. Comment by Mdau Halisi wa Filamu on May 25th, 2008 11:54 am

    Binafsi nina hakika kabisa kuwa One Game wameanza gwaride kwa mguu usio sahihi, labda pengine walikurupuka bila kufanya utafiti wa kina katika tuzo kongwe zitolewazo kwa wenzi wetu waliotangulia katika tasnia hii, kwa sababu wamelipuka tu na kutangaza tuzo bila ya kuweka bayana vigezo vitakavyotumika ima kumfanya muigizaji kuwa mshindi au filamu kuwa na kiwango stahiki; jambo ambalo litachochea ubora wa kazi zetu, kwani kila mmtayarishaji atakuwa akijitahidi kufikia vigezo ili ushindani uwe katikati ya viwango vya ubora. Nimesema wameanza sivyo kwa kuwa kuna kila dalili ya upendeleo na rushwa ya waziwazi katika mchakato mzima mpaka sasa kuna baadhi ya watu wanayo majina ya filamu itakayoshinda na mwigizaji bora wa kike wa kiume n.k. Kwa ujumla lilikuwa ni wazo zuri sana, lakini “hata mawazo mazuri yakifikiwa kwa sababu za kipuuzi huwa ni mawazo ya kipuuzi pia.” Tuombe Mungu wawe na nia njema ili baadae wajirekebishe!

  10. Comment by mamapinoh on May 26th, 2008 4:23 am

    mimi naona kwakuweka majina mapya ni poa sana,sio kila siku hao hao kina kanumba kwani hakuna wengine wanaofanya vitu vizuri mtawafanya wajione kuwa wao tu ndio wanajua pia sifa ziki zidi zitawaharibu watajiona wamemaliza

  11. Comment by aisha on May 26th, 2008 10:20 am

    jamani jamani,tukubari tukatae unapozungumzia filamu za kibongo tanzania na africa mashariki huwezi kuacha kutaja majina haya kanumba,ray,johari na monalisa,vijana hawa ndio wameleta mapinduzi ya film bongo baada ya tasnia hiyo kufa miaka ya nyuma wao wameamsha mpaka sasa,hata sisi wa huku ughaibuni tunawajua wao,hasa kanumba mchango wake unaonekana wazi toka alivyoanza kuigiza na wanaijeria mpaka sinema zako twaziona through dstv,sasa hao waandaaji na majaji wana macho kweli??kueno wa kweli watendeeni haki wasanii wanaostahili nasi kupeana tu,mfano asilimia 60 ya majina yote hapo juu hatuwajui…think…vigezo gani mmetumia?

  12. Comment by binti-mzuri on May 27th, 2008 8:18 am

    mi aisha naona rushwa tu hapa au chuki binafsi

  13. Comment by Robert chale on May 28th, 2008 4:14 am

    kweli hii ni movies star search, hizo ni tuzo za ma-underground pamoja na story butu, poleni Watanzania kwa kurubuniwa na watu wanaotaka umaarufu

  14. Comment by ttwalibu on May 28th, 2008 4:36 am

    aliyetangulia katangulia, kulikoni kushika njia ili hali huna macho ya kuona wakati watu wengine wakiona movements zako? hizo tuzo zina walakini nadhani hata ninyi waandaaji mmeshaanza kuona aibu, coz hao nominees na movies zao ni kama gunia chakavu na pumba za mpunga, siku hizi watu hawaishi kwa kudanganywa kiasi hicho, ninyi ni wasanii wachanga katika industry ya Tz ila mwataka umaarufu ila njia mlioitumia ni ya aibu, hakika mnajimaliza, nendeni mkaziangalie hizo movies upya ndipo mtakapojua kuwa mmechemsha, hata kuna movie moja nilipoiangalia hata nilicheka sana eti mwanamke anamtambulisha rafiki ya kuwa HUYU NI UBAVU WANGU…tangu lini mwanaume akawa ubavu wa mwanamke? but ndo hivyo tena mmeshaliletea aibu Taifa

  15. Comment by Burton on May 28th, 2008 1:22 pm

    Inashangaza kuona macho ya majaji ni tofauti na ya waliowengi.Sisemi kwamba mliowateua hawafai ila najiuliza hivi uzoefu hauna nafasi katika masuala ya filamu?Iweje kwa mfano waigizaji kama akina Kanumba,Johari au Ray wote kwa pamoja wasiwemo katika orodha yenu?Ni vigezo gani mlivyotumia kuwapata hao mliowachagua?Ikiwa sisi tunaonunua kazi zao tunazikubali inakuwaje nyie mwone sio nzuri,Je, hata mchango wao kwenye fani hii hauonekani?Ni vema kama mngetuambia kuwa lengo lenu ni kuwa’promot’ ma’underground’ tungewaelewa na tungewasifu vilevile.

  16. Comment by MAMII on May 29th, 2008 3:23 pm

    HIYO NI TANZANIA RUSHWA AWARD,,NYAMAYAO MBONA HAYUMO,MAMA ABDUL PIA

  17. Comment by MAMII on May 29th, 2008 3:25 pm

    TANZANIA BWANA

  18. Comment by Lily Victor on August 4th, 2008 7:54 am

    Namjua hapo huyo dada mahiri wa fungu la kukusa, Jacob Steven, hao wengine labla mpaka kidole

  19. Comment by mumy on March 15th, 2010 4:40 am

    tunamtafuta david sagala

Leave a Reply