
Mrembo Amanda Sululu(pichani) jana aliibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Miss Universe Tanzania 2008. Shindano hilo lilifanyikia jana usiku katika ukumbi wa Hoteli ya Movenpick jijini Dar-es-salaam.Kwa maana hiyo Amanda ndiye anarithi taji kutoka kwa Flaviana Matata mrembo ambaye mwaka jana alifanikiwa kuiletea sifa Tanzania baada ya kufanikiwa kuwemo katika tano bora ya mashindano hayo katika ngazi ya dunia yaliyofanyikia nchini Mexico.

Tatu bora-Katikati ni Amanda Sululu,kushoto ni Jamila Nyanga(mshindi wa pili) na kulia ni Eva Babuely(mshindi wa tatu)
Mashindano ya Miss Universe mwaka huu yanatarajiwa kufanyika tarehe 14 Julai katika ukumbi uitwao Crown Convention Center(Diamond Bay Resort) mjini Nha Trang nchini Vietnam.Zaidi ya washiriki 80 kutoka nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki.
BC inampa hongera Amanda na kumtakia kila la kheri mbele ya safari.
Feedback / Comments
20 Responses to “MISS UNIVERSE TZ 2008 NI AMANDA”
Leave a Reply


sending...
Mabint wa kibongo.hawana mchezo wana ng“ara kama wataliano wenye asili ya kimakonde na kizaramo.si rahisi kubainisha sina budi tuseme mashallah,
chafosa
BC VIPI LEO WIKI ENDA?
HAMNA HOME SICK
MSIALIBU MAMBO TUNATAKA MUSIC AU MAMBO
YA NET BINT MITAMBO KIDOGO IMELETA SIVYO NDIVYO
chafosa
Hongera dada, hivi c alikuwa ktka kambi ya mamiss ya kina Richa au nimemfananisha? Hivi umiss una umri wa mwisho mtu kushiriki au hata kama una miaka kama yangu unaweza shiriki??
Tanzania ni nchi yangu naipenda sana.
Mbona miguu imepauka sana? mamodo wa bongo oyeeeeeeeeeeee.
jamilla kajitahidi hakutaka tamaa baada ya kushindwa kwenye kisura.good keep it up,one day u will win.
Hongera dada kwa ushindi ..unaonekana unaconfidence plzzzzzzzzzzzusituangushe kule Vietnam…kila la heri!
Kekuu umenivunja Mbavu umri wako ni upi???au kama wangu?maana mimi najua mwisho ni miaka 24, zaidi ya hapo hiyo sio miss labda ni fashion show nyingine.
Kekue umiss hauna umri maalum mana hao mamiss wengi wao unakuta ameshasoma na kumaliza vidato vyote na kazi anafanya na wengine wanawatoto wao nyumbani,akiona mwili umekaa kushiriki anaenda kushiriki na kusema anamiaka 18,19,20,21 wachache sana unamsikia nina 22 hapo ujue ni miaka 50 na nusu.
Samahanini lakini mamiss wenzangu mwenyewe umri miaka 40 ila stejini nasema miaka 11 na nusu olaaaaaaa.
dunda anasumbua bc muwekee basi hiyo nyimbo anaitaka jamani
Matty nishavuka 24 rafiki huko hakunifai tena, Jenas ni kweli kuna warembo wanadanganya umri wao ili mradi umbo linaruhusu, tehe tehe kaaazi kweli kweli!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! hapo utasikia wana miaka 18 kila mmoja mimi sitashangaa kbs.
kekue kwani una umri gani? maana hujataja umri wako.lakini jaribu usikate tamaa.
Jamila hongera sana umejitahidi mwana wane.
hongera amanda,mie nakuombea Mungu ufanye vizuri huko uendako.Haya Jamila vipi tena mamaa,mambo yameshindikana tena na huko!!!!???? usife moyo kuna miss tourism inakuja tena jaribu bahati,halafu kuna miss tz,miss malaika zote jaribu tu.
Mtoto umependeza sana.wanaohiji miaka yako ni wajinga tu kwani ungekuwa umezidi umri kamati ya shughuli hizo isingekuacha ushiriki.just dont let us down in Vietnam,na uchunge risasi huko kwani kwao ni vita milele.All the best.
mwisho wa umiss miaka 24,usiwe na mtoto,hujaolewa wala hujatoa mimba
haha..but ni wangapi,wanasema ukweli,that i dont know
hahahahahah binti mzuri you made my day …utamtambuaje ambaye hajatoa mimba?
binti-mzuri hiyo ya mimba umeiongezea au?lol
afazali zis taim ameshinda ‘mzawa’.siku hizi wanashinda wahindi tunasema ni watanzania. wakati mwingine tunaangalia ‘weupe’ na pua za kihindi! Hivi hao ndo wananchi? Miss wa mwaka jana kuiwakilisha TZ sikuona kama ni vema.
Anyway ni mawazo yangu tu jamani si ‘ubaguzi’.
Ila kuna siku raisi wa Tanzania atakuwa mhindi kama miss na mbunge wanawezakuwa wahindi!
DU!
mamiss wengi sio wa kweli kwani wengi ninaowajua wana umri mkubwa lakini akiwa stejini utasikia miaka 18 19 20 wajaribu kuwa wa kweli pia mngekuwa mnaagalia vyeti vya kuzaliwa
Vyeti vya kuzaliwa wanatengenezewa kwa shilingi elfu 20. Hata wewe ukihitaji kinachoonesha una miaka 8 utakipata kaka. Bongo”tambarare”!
hivi huyu amanda si alikuwa miss arusha?au nimemfananisha jamani.