JAJI EUSEBIA N.MUNUO

Miongoni mwa wanawake wanaofahamika na kuheshimika katika fani ya sheria nchini Tanzania ni Jaji Eusebia Nicholas Munuo(pichani).Hivi leo yeye ndio Makamu wa Rais Mteule wa Chama Cha Majaji Wanawake Duniani(IAWT).Mbali ya cheo hicho,Jaji Munuo pia ndio Mwenyekiti wa Chama Cha Majaji Wanawake nchini Tanzania(TAWJA).Yeye ndio Hakimu wa kwanza mwanamke nchini Tanzania na pia Jaji wa kwanza mwanamke katika Mahakama ya Rufaa nchini Tanzania.

Miezi kadhaa iliyopita Jaji Munuo alifanya mahojiano maalumu na mwandishi Happy Katabazi kuhusiana na mambo mbalimbali ya kijamii,kisheria na pia kumhusu yeye binafsi.Je ni kweli kwamba Jaji huyu aliwahi kuamuru kwamba mumewe atiwe ndani kutokana na kuidharau mahakama?Ili kupata jibu la swali hilo na mengine mengi kumhusu Jaji Eusebia Munuo,bonyeza hapa uitembelee blog ya Happy Katabazi.

Photo/Happy Katabazi

Page 1 of 3 | Next page