
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Khadija Shaban a.k.a Keisha.Binti huyu hivi karibuni alikaririwa akielezea masikitiko yake juu ya kuuawa kwa ma-albino nchini Tanzania kutokana na imani za kishirikina.Keisha anasoma nchini Uganda.
Photo/Global Publishers.
Feedback / Comments
15 Responses to “KEISHA”
Leave a Reply


binti umejaaliwa sauti mashAllah!
kuhusu mauaji ya maalbino serikali inafuatilia kwa umakini na itawadhibiti tuu.
washirikina wana akili basi, ni maramoja tuu watakwama na serikali itawatia mikononi na kuwadhibiti, kwani shetani anawachezea tuu, itafikia wakati hao maalbino hawatafaa kwenye mambo yao na kuingia kwenye mambo mengine ( kwa kifupi watashindwa tu) na tutakuwa huru na kizazi chetu cha maalbino.
Binti mrembo sana huyu,anashepu kama ya kule kwetu Kaitaba na anasauti nzuri kwa kweli, kuna ule wimbo aliimba na Bushoke nauzimia sana umetulia.
Nayaonea huruma sana maisha yako honeyy ohhhh honey
sitaki kupoteza uhai wako honeyyyyy ohhh honey heeee mimi simo kabisa kwenye kuimba ngoja niishie hapa.
Ila mimi nalia na wanaoua maalbino na wanaotoa viungo vya siri vya binadamu ili wapate utajiri mungu awalaani kwa kweli!
Usijali Keisha Mungu atakulinda tu!
poleni sana jamani…sijui kwanini binadamu tumekuwa hivyo….nirudi kwako wewe mdada….napenda shape yako sana una shape ya kufa mtu….mungu hakunyimi vyote na hakupi vyote…nakupendaga sana.
dada kazi unaiweza sauti unayo,usiogopeshwe na hao wanaoua mwili bali mwogope anayeweza kuua mwili pamoja na roho ambaye ni Mungu.
Maskini weee!!! wanatiaga huruma kweli hawa watu then wanawaua, kwa kweli hizi ni siku za mwisho.
Du, lakini Keisha uongo mbaya shost una shepu nzuri hakuna mfano mtoto hiha……
It is a shame on the Tanzanians who practice such uncouth and vulgar actions. Now, what a lovely lady! May I know if she has a fiancé, else I wish to propose her!!!
Ushirikina upo ila serikali inajidai haiutambui, na kheri umeshalitikisa Bunge tayari, Albino, ulaji nyama watu n.k, Hawa ma-albino ni wachache saana kwenye Jamii yetu na inawezekana kabisa kuwalinda. Narudia tena washirikina wanajulikana wananchi wakihusishwa. Hebu sungusungu irudishwe. Elimu ya msingi mpaka secondary inatakiwa iwe bule na lazima, ni njia mahususi ya kutokomeza dhana hii ya ujinga wa kuwanga. Nyerere kabla ya kufa alisema nawaachia maadui Ujinga, Umaskini na maradhi. Maadui hawa wamefugwa na wamenenepa na awamu zilizofuatia na sasa wamezaa adui mwingine Ufisadi……haki ya nani Bongoland.
Mimi sijawahi kumsikia. Lakini maadamu wengi mnamsifia basi nampa hongera. Wahenga walisema wengi wape!.
Keisha! GOD BLESS AND PROTECT YOU FROM ALL THEM DEMON POSSESSED PEOPLE!.
Huyu ni mwanamke mwenzangu lakini acheni tu nikiri jamani huyu dada nimzuri. yaani kaumbika kibantu hasaaaaa na ana sauti nzuri pia. Kwa ufupi ni kajaaliwa. Ingawa ni aalbino, still ana sura mvuto “A” na ana roho nzuri sana.
Hi guys, kutoka Helsinki-Finland
Kwanza ninampongeza huyo dada kwa kweli simjui vizuri wala nyimbo zake sizijui lakini napenda kutumia nafasi hii kulaani mauaji ya maalbino nimesoma habari hizo kwenye internet ebu jamani angalieni hii video http://video.on.nytimes.com/?fr_story=f1cf6d2330fb3aa5aca8fc3d8d08ca128b1366b6
Pia waweza google ”(Albinos killings in Tanzania)” utapata picha ya ajabu, hivi kwa nini Kikwete asitangaze kampeni ya Kitaifa dhidi ya huu unyama wa kutisha, pia Albinos wanabaguliwa, dunia imekuwa inalaani ubaguzi wa rangi sasa Tanzania tunawabangua ndugu zetu kwa kuwa ni Albinos, Ninawaomba watanzania na wapigania haki za binadamu tuungane na BC kulaani kwa nguvu sote, eti imani za kichawi kutaka kupata utajili, nimesoma eti wavuvi na wachimba madini ndiyo wanaongoza hasa hasa Mwanza na Shinyanga, nie wasukuma vipi?, mmetoka kuwaua vikongwe na sasa mmehamia kwa maAlbinos acheni imani za kijinga za ujima na uchawi nyie mnaishi dunia gani?Askofu Kakobe nenda kawaubilie habari za Yesu.
Bora ya hao MAFISADI wanatumia uwongo na akili kupata pesa,kuliko nyinyi mnaoua watu mpate pesa,hivi nyie waganga na wagangwa mko binaadam wa haina gani?mnajua kweli samani ya binaadam?i wish huko kiyma mungu atanipa kazi ya kuchochea moto wenu!
Big up Keish!!
Nasikitika pia na haya mauwaji ya maalbino. Kweli hata nchi nyingine watu wanashangaa kwanini watu na akili zao wanawauwa viumbe wa mungu bila makosa. Tuombe mungu wastop hawa watu wakatiri jamani.
ukweli siku za mwisho ndio zimewadia maana haileti akili eti umuuemwenzio kisa utajiri na hao wanaowaelekeza kuua watu sio waganga ni wachawi wkubwa walaaniwe
basi na wenye homa tuwaue … wenye vipele nao…. na wenye makomwe!
uzeruzeru is just a state of health.. upungufu wa pigments basi…
keisha we binti mzuri mwanawanee
she’s doing great!!