MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Jina lake kamili ni Godfrey Tumaini. Kwa wengi anajulikana kama “Dudu Baya”. Ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao waliwahi kutamba na kujipatia umaarufu ingawa mara kwa mara amekuwa akiandamwa na sifa ya ‘ugomvi’ jambo ambalo ni vigumu kulithibitisha bila kusikia pande mbili za shilingi.

Albamu yake ya kwanza aliitoa mwaka 2000 na aliipa jina la Siku ya Kufa Kwangu. Mwaka mmoja baadaye yaani 2001 alitoa albamu nyingine iliyokwenda kwa jina Amri Kumi Za Mungu. Hiyo ilifuatiwa na albamu ya Mpangaji mwaka 2002 kabla ya Papo Kwa Hapo mwaka 2003 na kisha Kiwango mwaka 2005. Mwaka 2006 alifyatua albamu aliyoiita Manundu.

Kwa muda sasa Dudu Baya amekuwa kimya kidogo katika mfufululizo wake wa kufyatua albamu mpya takribani kila mwaka.Miongoni mwa nyimbo zake zinazofahamika zaidi ni ule wa “Nakupenda Tu”. Unaweza kuutizama wimbo huo kwa kubonyeza hapa.

Photo/Global Publishers.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

7 Responses to “DUDU BAYA”

  1. Comment by Matty on July 28th, 2008 3:03 am

    Huyu Jamaa anaimbaga fresh,naupenda ule wimbo “NAKUPENDA MPENZI USIOPENDA CHAPAAA…HALAAAAA BABYYYYYY” aliomshirikisha Vivian (RIP VIVIAN & COMPLEX) ila sasa anatalent nyingine ambayo ni kuarest wenzake a.k.a mkono mtu!!

  2. Comment by any on July 28th, 2008 11:11 am

    mbona hajamjoin TID!

  3. Comment by Pearl on July 29th, 2008 9:14 am

    mi sina hata la kusema ila mi namjua zaidi kama mtu mpenda ugomvi.

  4. Comment by binti-mzuri on July 29th, 2008 12:11 pm

    tentementeeee …. i loveee that song

  5. Comment by Gervas on July 29th, 2008 2:16 pm

    The dudubaya ni kijana mzuri tu, tena nakumbuka alikuwa Mseminaristi kule Makoko-Musoma. The dudu yeye ana sifa moja bwana mtu akijipendekeza kwake anampa manundu tu basi. He is not a violent guy anyway. Walianza kuimba nakumbuka na bwana Edwin Ndaki enzi hizo…ukwayani.

  6. Comment by Dunda Galden on July 30th, 2008 8:01 am

    Ngumi mkononi that why people call dudu baya
    ukileta shobo la uzushi chapa ngumi kisawasawa
    maana baadhi ya wabongo kuna wengine wanapenda
    kujishembendua wanapoona watu
    kula tano Tumaini
    chaigoda

  7. Comment by Amina on September 23rd, 2008 6:42 am

    mi namjua huyu jamaa hakawii kuku chenjia..dar skendo baby hallllaaaa

Leave a Reply