BERNIE MAC AFARIKI DUNIA

Kwa wale ambao mnafuatilia habari au kuangalia vipindi mbalimbali vya vichekesho kutoka nchini Marekani, habari ambazo si za kufurahisha ni kwamba mchekeshaji (comedian) na muigizaji filamu maarufu Bernie Mac(pichani) amefariki dunia.Bernie Mac ambaye alijizolea umaarufu kutokana na kipindi chake cha televisheni cha The Bernie Mac Show amefariki leo asubuhi katika hospitali ya Northwestern Memorial Hospital ya jijini Chicago nchini Marekani alipokuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa pneumonia.Wengine mtamkumbuka Bernie Mac kwa uigizaji wake wa hivi karibuni katika filamu kama vile Ocean Thirteen na Transformers.Bernie Mac alikuwa na umri wa miaka 50.Kwa undani zaidi wa habari hii unaweza kubonyeza hapa.

Page 1 of 3 | Next page