Maisha yetu yanaboreshwa kwa pesa ambazo zinapatikana nyakati za malipo (kwa wafanyakazi, wafanyabiashara n.k).Malipo hayo huwa yanatokea kwa nyakati tofauti. Lakini uwe unalipwa mwisho wa siku, ama mwisho wa wiki, ama mwisho wa kila baada ya wiki ama mwisho wa mwezi, dalili ni kwamba siku ya leo wengi watakuwa wamelipwa maana sio tu mwisho wa siku,na wiki, bali ni Mwisho wa mwezi.Tumeingia ngwe ya lala salama ya mwaka 2008.Unaweza dhani utani vile ukiwambiwa karibuni watu tunakula Xmas.
Unakumbuka vituko vya mwisho wa mwezi?Binafsi nakumbuka kisa cha mzee mmoja ambaye ilikuwa kila mwisho wa mwezi unapofika haonekani nyumbani mpaka alizonazo zikishamuishia.Siku moja mke wake akagundua kule jamaa anapoenda akishakamata “mshiko”. Kilichotokea huko mpaka hivi leo ni simulizi lenye mafunzo.Kwa kifupi jamaa alitoka huko bila sehemu muhimu ya viungo vyake vya uzazi!
Wasikilize Vijana Jazz wakizungumzia mambo ya mwisho wa mwezi katika kibao chao kilichotamba saana cha MWISHO WA MWEZI. Wikiendi njema kwenu nyote.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Burudani ya leo imeletwa kwenu kwa hisani ya www.changamotoyetu.blogspot.com
NB: Kwa wasomaji na wapenzi wote wa BC ambao walimiss burudani ya kila Ijumaa kwa majuma kadhaa,tunawaomba radhi.Hiyo yote ilitokana na sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wetu.Tekinolojia ya 3G ilituangusha kwa majuma kadhaa tulipokuwa hukooo kwenye semina elekevu.

Huyu ndiye mbunge mpya wa jimbo la Tarime.Huyu ndiye aliyekitoa kamasi chama tawala cha CCM katika uchaguzi wa hivi karibuni kutafuta mrithi wa Marehemu Chacha Wangwe.Anaingia bungeni akikabiliwa na kibarua kizito cha kuziba pengo lililoachwa na Wangwe.
Pichani ndipo alipokuwa akila kiapo bungeni Dodoma hapo juzi.Anaitwa Mwera Charles Nyanguru. Je na yeye atakuwa na cheche alizokuwa nazo Marehemu Wangwe?Tusubiri kuona na kusikia.
Picha kwa hisani ya ofisi ya Waziri Mkuu

Anaitwa Ambwene Yessayah.Kwa wengi anafahamika kama AY huku wengine wakiendelea kumuita “Mzee wa Commercial”.Kwake muziki ni burudani na pia ni kazi.Mafanikio yake katika game ni mfano wa kuigwa na wengi hususani wasanii wanaochipukia.Ni miongoni mwa “mabalozi” wazuri wa Tanzania nje ya nchi kupitia sanaa ya muziki.Kwa mara nyingine tena mwaka huu anawania tuzo maarufu za Kisima za nchini Kenya.
BC ina furaha kuutambulisha kwako wimbo mpya kutoka kwa AY.Wimbo unaitwa FREEZE.Amewashirikisha P.SQUARE kutoka nchini Nigeria. Wimbo umetayarishwa na kurekodiwa na Producer Hermy B kutoka Tanzania.Tayari wimbo huu unakamata chart katika vituo mbalimbali vya radio.Unaweza kuusikiliza kwa kubonyeza player hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Siku moja baada ya kuishuhudia Yanga ikiichapa Simba bao 1-0, mfadhili mkuu wa klabu hiyo, Yusuf Manji ameugua ghafla na kukimbizwa Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam kwa matibabu. SIKU moja baada ya kuishuhudia Yanga ikiichapa Simba bao 1-0, mfadhili mkuu wa klabu hiyo, Yusuf Manji ameugua ghafla na kukimbizwa Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam kwa matibabu.Kwa undani wa habari hii bonyeza hapa.
Pichani ni Mfadhili huyo,Yusuf Manji(kulia) akiwa na Rais Mstaafu wa Yanga,Francis Kifukwe(kushoto).Hii ilikuwa kwenye hafla ya kutiliana mkataba wa udhamini kati ya club za Yanga na Simba na kampuni ya bia nchini.TBL miezi michache iliyopita.
Picha na Issa Michuzi

Ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao hivi leo wanaweza kujiita “wakongwe”.Kwa miaka nenda rudi wamekuwepo katika “game”.Jina lake anaitwa Inspekta Haruni…jina la kisanii likiwa limelifunika jina lake halisi la.Tangu enzi za Gangwe Mob(pale alikuwa na mwenzake Luteni Kalama)
Hivi karibuni ametangaza kujitoa katika kundi la Wanaume Halisi lililo chini ya Sir Juma Nature.Lakini kabla ya kujitoa gumzo kuelekea upande wake lilikuwa kuhusu wimbo wake wa hivi karibuni uitwao Ndoa Haina Doa.
Wimbo huu ni majibu ya wazi kwenda kwa MwanaFA ambaye hivi karibuni umekuwa sio tu msemo maarufu bali “kisingizio” cha vijana wengi kuhusu ndoa au mahusiano ya kudumu.Wimbo wa MwanaFA unaitwa Bado Nipo Nipo akiwa amemshirikisha mrembo Flaviana Matata katika kiitikio(chorus).Unaweza kuusikiliza wimbo wa MwanaFA kwa kubonyeza hapa na kisha kuusikiliza wimbo wa Ndoa Haina Doa kwa kubonyeza player hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Mrembo Miriam Odemba(pichani) ambaye yuko nchini Philippines akiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Earth amefanikiwa kuingia katika tano bora katika shindano la kutafuta mrembo aliyependeza katika vazi la ufukweni katika kundi lake.
Mashindano haya yalijumuisha baadi tu ya warembo 90 ambao wanashiriki katika mashindano ya Miss Earth 2008 kwani fainali ya mashindano ya vazi la ufukweni yatafanyika tarehe 1 Novemba. Katika kundi lake, Miriam aliweza kuwapiku warembo wenzake takriban 30 kwa kupita jukwaani kwa kujiamini katika vazi hili la ufukweni.
Washindi wengine ni Columbia, France, Greece na Canada. Mshindi wa kwanza alikuwa Canada ambaye alijinyakulia zawadi ya dola 1,500.


Baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari wameandamana leo asubuhi jijini Dar es salaam,maandamano hayo yalianzia mtaa wa Lugoda na kuelekea wizara ya habari utamaduni na michezo,ambako walikabidhi barua kwa Waziri wa wizara hiyo Mh George Mkuchika,aidha madhumuni ya maandamano hayo yalikuwa ni kupinga kufungiwa kwa gazeti la mwanahalisi na serikali kwa muda wa miezi 3 na pia kuishinikiza serikali ifanye marekebisho ya sheria ya uhuru wa vyombo vya habari ya mwaka 1976
Mfalme wa Rhymes Afande Sele akiwapagawisha mashabiki wake jana usiku ndani ya ukumbi wa mambo club
pamoja na kujiramba watu walikuwa ile full mizuka mbaya
Qchila nae akikamua vilivyo mbele ya wakazi wa Moro,Chila bila hiyana aliutambulisha wimbo wake mpya kabisa uitwao Paparazi ambao ulionekana kuwakuna mno washabiki waliotinga ukumbini humo
Watu kibao ndani ya tamasha la fiesta jirambe mkoani Morogoro ilililofanyika ndani ya ukumbi wa Mambo Club jana usiku,Fieata leo inafanyika pale Dodoma na baade jpili itafayika uwanja wa jamhuri.
Mojawapo ya makampuni nchini Tanzania ambayo yanafanya kazi nzuri ya huduma kwa jamii (corporate social responsibility) ni Vodacom kupitia kitengo chao cha Vodacom Foundation.Hivi karibuni BC ilishuhudia uzinduzi wa mradi wa “Voda Kompyuta” kwa shule za sekondari Tanzania ambapo walikabidhi kompyuta 22 kwa Meya wa Arusha-Lawrence Hedi.Hizo ni kwa ajili ya kompyuta mbili za sekondari mkoani Arusha.
Pichani juu ni Mkurugenzi wa Utawala (Africa) wa Vodafone,Bob Collymore akimkabidhi Meya wa Arusha,Mh.Lawrence Hedi kompyuta hizo.Kwa habari kamili kuhusu tukio hili endelea kusoma hapo chini.BC inaunga mkono vitu kama hivi. (more…)



