
Huyu ndiye mbunge mpya wa jimbo la Tarime.Huyu ndiye aliyekitoa kamasi chama tawala cha CCM katika uchaguzi wa hivi karibuni kutafuta mrithi wa Marehemu Chacha Wangwe.Anaingia bungeni akikabiliwa na kibarua kizito cha kuziba pengo lililoachwa na Wangwe.
Pichani ndipo alipokuwa akila kiapo bungeni Dodoma hapo juzi.Anaitwa Mwera Charles Nyanguru. Je na yeye atakuwa na cheche alizokuwa nazo Marehemu Wangwe?Tusubiri kuona na kusikia.
Picha kwa hisani ya ofisi ya Waziri Mkuu
Feedback / Comments
12 Responses to “MBUNGE MPYA WA TARIME ALA KIAPO!”
Leave a Reply


sending...
KARIBU NDANI YA JUMBA.
Haya baba mikoba ya chacha wangwe ndio hiyo unakabidhiwa sasa ukiwachanganya tu wale wana tarime ahhh mbona utawakoma hawaoni hasara kukuchinjia baharini
Mwenyezi Mungu amlinde katika kazi yake!Ameeen
Kila la kheri!Usijisahau tu!
Namkumbuka marehemu Wangwe wakati wa uhai wake alikuwa wakipelekeshana sana mh Spika.
Siku moja kwenye kikao cha bunge aliambiwa aombe radhi kwa kauli yake ya kusema serikali inaua wananchi Tarime.
Mh Wangwe alipoona maji yamefika shingoni hakukubali kujisalimisha aliona bora afe na tai shingoni kama wakina Mkwawa jibu alilompa Spika alisema.
“mh Spika nimefuta kauli ILA MESSAGE DELIVERY!” …
Hakika Ras Wangwe ambaye alikuja nyoa rasta zake baadaye alijitahidi sana kuwakilisha sauti za mamia ya wananchi wake waliokuwa wananyanyaswa na kuporwa haki zao kwenye Mgodi wa North Mara unaomilikiwa na East African Mines.
RIP Wangwe..Mwera usije jisahau alafu utegemee 2010 ukawaulize Tarime hivi kweli mlisema mnavaa viatu saidi ngapi?
Kumbuka visima vya kale havifukiwi mjomba…
Ndimi kwangu pakavu nakusalimu salaaam Mwera
Tutafika tu
tata amang’ana ghao mura.Nina wasiwasi hapo alikuwa anakandamiza kikurya kwa kwenda mbele.Karibu sana mjengoni
eeeh Mheshimiwa Mwera Charles Nyanguru.
Tafadhali katuwakilishe vema huko bungeni sisi wananchi wako. Usicheke kabisa na mafisadi na vibaraka wao! Kafanya kazi bila woga wala kuchoka.
Nasubili kuona cheche zako mheshimiwa
Nami nasema kama Edwin Ndaki….Kumbuka visima vya kale havifukiwi mjomba…
Stay Blessed.
Peace out!
tunataka changamoto Bungeni,siyo khrrrrrrrrrrrrrro,khrrrrrrrrrrrro.Nafikiri wadau mmenipata.
Mura heheeheheheh mtani wangu huyo i love u hahahaha ila sasa pls usituangushe wanainchi wako, fuata nyayo za Chacha wangwe.
Kila la heri bro!
-hope hutakuwa mmojawapo wa wale walalavi ndani ya mjengo….kila la kheri….
Tunasubiri tu hiyo CCM itengane maanake tayari mtungi ni wamoto saizi. ANC wameshaonyesha njia. Hapo ndo tutapata at least Upinzani wa maana Tanzaia…maana watakuwa wanasemana wao kwa wao, maanake njia za wizi wanazijua ati wenyewe. Kwa sasa bado wanaogopana sababu wameshindiliwa wote ndani ya mtungi mmoja ambao tayari umeshapigwa mtikisiko na nyufa zimeshaonekana. RIP baba wa Taifa!!
is gonna get there Gervas! Watch!.