Leo ni siku ya ukimwi duniani.Ni mwaka wa ishirini sasa tangu maadhimisho ya siku hii yaanze hapo mwaka 1988.Ni siku ambayo dunia nzima inajumuika kukumbuka ndugu,jamaa na marafiki zetu wote walioathirika na hata kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huu hatari ambao mpaka hivi leo bado unaendelea kuwa tishio.
Lakini muhimu kabisa ni kwamba maadhimisho ya siku hii hutumika pia kutafakari mambo mbalimbali kuhusiana na ugonjwa huu.Ni siku ya kutizama kwa makini maendeleo ya tafiti mbalimbali za tiba kuhusiana na ugonjwa huu,hatua ambazo tumeshapiga katika mapambano ya kuutokomeza ugonjwa huu na mipango ya mbeleni katika vita hii.Zaidi ya watu milioni 33 duniani wanaishi na virusi vya ukimwi.Ni siku nzuri pia kudhamiria,wewe na mimi,kwamba tutaongoza mapambano dhidi ya ugonjwa huu.
Takwimu mbalimbali za kitaalamu zinaonyesha kwamba maambukizi ya ukimwi yameanza kupungua ikilinganishwa na miaka kadhaa nyuma. Hili ni jambo la kujivunia ingawa halitakiwi kuachwa kuwa kama mafanikio ya mbalamwezi ambayo hupotea pindi tu jua linapoanza kuchomoza.Kazi kubwa bado ipo.Ukimwi bado upo,ni hatari na unaua.Sote tuna jukumu la kujilinda,kuwalinda tuwapendao na kuilinda dunia yetu.Dunia bila watu si dunia!Kama unampenda,utamlinda!
You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video
Page 1 of 3 | Next page