Leo tunapenda kuwashukuru wadhamini wetu kampuni ya Zara Tours ambao wanaongoza kwa huduma zote zinazohusiana na utalii nchini Tanzania.Zara Tours ndio inayoongoza pia kwa kuandaa safari za kupanda Mlima Kilimanjaro.Shukrani nyingi kwa udhamini wenu.
Kwa habari zaidi kuhusu huduma za utalii zitolewazo na Zara Tours,bonyeza hapa ili kutembelea tovuti yao.
NB: Kama na wewe una biashara au kampuni na ungependa kuwa mmoja wa wadhamini wa BC,usisite kuwasiliana nasi kupitia bongocelebrity at gmail dot com au kupitia kwenye fomu inayopatikana katika ukurasa wa “Kuhusu BongoCelebrity” hapo juu.
Feedback / Comments
4 Responses to “SHUKRANI WADHAMINI”
Leave a Reply


go ZARA, go ZARA!
ZARA TOURS,
Mimi pamoja na wanachama wenzangu wa BC wanaopenda kushirikiana na mimi, katika kutoa shukrani hii ya dhati kwenu. Tunawashukuru sana kwa kuwadhamini Bongocelebrity. Udhamini wenu kwa Bongocelebrity ni manufaa sana kwetu sisi Watanzania.
Bongocelebrity, imeturudisha nyumbani Tanzania, watu wote tulioko nje ya nchi yetu na inatufanya tuwe na moyo wa kufuatilia matukio mbali mbali yanayotokea nchini kwetu. Bongocelebrity inatupa burudani za aina nyingi, ikiwemo miziki mbali mbali ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Kuwepo Bongocelebrity kumenifanya mimi na watanzania wenzangu kukutana hapa, kubadilishana mawazo ya kisiasa, kijamii na hata kimahusiano. Nimekutana na watu wenye mawazo endelevu, na ya kuona mbele na watu wenye mawazo finyu pia wapo.
Bongocelebrity, nimekutana na watu wabishi kwa kila kitu, ambao wanaweza kukuambia kuwa rangi hii nyeusi ni nyeupe na wakakomalia kwa hilo mpaka kesho. Lakini kwa vile maoni yetu hapa ni mtazamo wa kila mtu na mawazo yetu ni tofauti. Mimi imenifanya nijifunze kuishi na watu wenye mitazamo tofauti na yangu.
Hapa BC, ni kioo cha kujiona mwenyewe, na sehemu ya kujipima kama unakubalika na jamii ya Watanzania wenzako. Utaona, kupitia katika kauli zako unazoandika hapa, kama zinakubalika na wenzako, utaona kutoka kwao, watakavyokuwa wakikujibu au kukulalamikia.
Pamoja nasi katika uwanja wa BC, nimekutana na wasanii wa maisha, ambao wanaweza kukufanya kuwaamini kuwa, maisha yao ni bora kuliko unayoishi wewe, lakini ukijitahidi kuwafatilia utawagundua kuwa maisha yao ni taabani kuliko hata maisha unayoishi wewe. Lakini, taratibu tutafika tu.
Kwa kumalizia, nawaomba “Bongocelebrity”, wajaribu kuiboresha zaidi Blog yetu hii, kwa kuiongezea vitu vipya, siku hazigandi, kila siku vitu vipya vinatokea. Napendekeza kitu kipya, kama vile kutuwekea sehemu(Private), ambayo tunaweza kuachiana E-Mail na Telephone namba zetu, badala ya kuzianika hapa kwenye “Kuku Wengi, Mtama Kidogo”, kunguru pia wapo wataula mtama. Ni hayo tu kwa leo!
Bond=James Bond………..NO,…….. I Mean Black=Blackmannen
ZARA muishi milele
Sisi binadamu ni “Viumbe Wa Ajabu” kweli. WanaBC wapo wengi sana, lakini ninashangaa kuona hapa ni sisi watatu tu, ndiyo tuliotoa neno la “AHSANTE” kwa ZARA!
Kumbe alivyoimba rafiki yangu “Zakaria Danile (RIP)” (Tenda Wema Wende Zako), alipokuwa na kundi lake la Shinyanga Jazz Band – 1968, ni kweli tupu. ZARA ndiyo wadhamini wa BC, lakini binadamu (WanaBC wenzangu), badala ya kushukuru, wanaipita “page” hii mkuku, kwenda page zingine!
Mie kwa kweli wameniacha hoi bin taabani. Lakini hata hivyo neno AHSANTE, ni muhimu pia litoke moyoni. Isije ikawa, watu waonyeshe shukrani za aina ya “Heshima Ya Kijeshi”.
Hata hivyo mimi bado nasema, Ahsante sana ZARA kwa kuwadhamini Bongocelebrity, tunajisikia tuko nyumbani Tanzania. Endeleeni na moyo wenu huo.
This Is Black=Blackmannen