Zimebakia siku chache tu tuumalize mwaka 2008.Weekend inapojongea namna hii ni kuashiria kwamba ni wakati wa kuburudika,kupumzisha akili,kutembeleana,kuhudhuria vikao vya harusi,mwali kutolewa ndani,vikao vya familia,kiti kirefu(cha kaunta),nyama choma nk.
Kwa wengine huu ndio wakati wa maandalizi ya krismas.Ni wakati wa kuwaza na kuwazua kuhusu zawadi za x-mas.Ni wakati wa kupamba miti ya x-mas.Wakati wa kuweka pamba kwenye miti eti kuashiria barafu!Ama kweli wenzetu wanatupata.Hapo sijajiuliza kuhusu mambo ya Santa Claus na jinsi ambavyo wabongo tunamshobokea bila hata kujua au kudadisi chanzo na mwisho wake.Ajabu tukiambiwa kwamba tuna kautumwa ka akili tunakuja juu ile mbaya!Hivi ni lazima kila siku tuige kila kitu wanachofanya “wa magharibi”?Wao wanaiga nini kutoka kwetu?
Anyway,ngoja niyaache hayo kwa sababu kadri ninavyozidi kujiuliza ndivyo ninavyoshindwa kujizuia kumkumbuka rafiki yangu Ampeninimungu aliyewahi kunionya kuhusu madhara ujinga.Leo ni Ijumaa,ni siku ya kuburudika.Ndio jadi yetu hapa BC.
Wiki hii Rais ametangaza msamaha kwa wafungwa 4,306.Miongoni mwao ni mwanamuziki TID.Msamaha huo ndio ulionifanya nikumbuke wimbo kutoka kwa FM Academia(Wajela jela Gwa) au The Dream Team.Enzi zilee za kina Ndanda Kosovo(pichani).Wimbo ni Jela.Wasikilize hapo chini.Wanasema jela…jela…jela ni mbaya.Wikiendi njema.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Burudani ya leo imewezeshwa na DJ Dennis ambaye huwa kila jumamosi anavurumisha midundo pale Bongo Radio
Feedback / Comments
9 Responses to “JELA-FM ACADEMIA ORIGINAL”
Leave a Reply


sending...
Duh!!!!!!!!!
Yani umenikumbusha mbali Jeff……………….
Nilikua namzimikia huyu jamaa na nyimbo zake,
Anyway I miss my home, I miss Tanzania……..
Rebbygod
Nimependa sana hilo dongo la Santa Claus, kuna Krismasi ya mwaka fulani nilipata kumshuhudia muigizaji mkongwe wa hapa nyumbani, Mzee Small, akiwa amevaa yale manguo mazito ya Santa huku akigawia watoto peremende pale mnara wa askari, mchana wa jua kali eti. Nikajiuliza, “Hawa jamaa waliomvalisha huyu mzee wa watu haya manguo na joto lote hili wanamtakia heri kweli?”
Sasa leo ndio nimegundua kuwa kuiga kubaya. mtu unaweza ukafa hivihivi.
Tusherehekee sikukuu ya Noeli, lakini kwa namna yetu sisi.
Hi guys
Nimekumbuka wakati wa uzinduzi wa hiyo album yao ya wimbo wao huo, nilikuwepo pale pool side ya zamani kilimanjaro hotel kwa sasa hakuna tena hiyo pool side wala kilimanjaro , najua kwa sasa kuna Kempisk-Kilimanjaro Hotel- Wimbo wao ulikuwa ume tulia sana,
Hongera sana BC yakale ni mazuri kukumbushana
Frateline
Chozi la munyonge malipo kwa mungu babaaaaa!
Acha waseme sisi ni kazi babaaaa!
Jela…jela ni mbaya
jela…jela ni shida
Jela…jela mateso
Week end yangu imekamilika.
Kazi muzuri kabisa FM-A!
Thankz BC
Thanx BC leo umenikumbusha mbali sana, huyu ndanda Kosovo namkumbuka mwaka 2001nilimuona live jamani mkaka aliwekaga brichi kichwani ya msalaba lol!,aluuuuuuu(Uko wapi Hilarya Ng’oma???unamkumbuka Ndanda Kosovo????) naizimia hii nyimbo ya JELA NI MBAYA!!sijui yuko wapi jamani huyu mtu!
Mhhh, jamani BC mnenikumbusha mbali kweli mwanawane!
mwanzo ni mugumu
Hivi bongo imekuwa Zaire?. Kwanini miziki inapigwa kama ya Zaire?. Heri miziki ya Kingwendu.
ivi hawa si ndio waliimba ule mwimbo wa kidedea..kichezaji shoo chao kilikua kinakatika..