MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

comedi-orijinobc

Naam!Xmas kwa mwaka 2008 ndio imeshaisha.Kwa bahati mbaya siku kama hizi huwa hazirudi tena.Ilivyokuwa Xmas mwaka huu sivyo itakavyokuwa mwaka ujao na mingine itakayofuata.Ulipokuwa mwaka huu si ajabu hutokuwepo mwakani.Ndio maana huwa tunasisitiza kwamba Make The Most Use of It when/whenever you can(nimetia kizungu hapo kuonyesha msisitizo).

Najua wengi wenu bado mpo kwenye hali ya sikukuu.Wengine nasikia bado wanatibu mning’inio wa ziada(hangover).Kwa wengine huu ni wakati wa kutafakari jinsi matumizi yalivyokwenda.Ni wakati wa kukagua risiti huku macho yakiwa yamekutoka na simanzi likiwa limetanda usoni.Usijali,ndio maisha.Si ushasikia ule msemo usemao Ponda Mali kwani Kufa Kwaja?Sasa?

Lazima pia nikiri kwamba hata sisi wenyewe tupo kwenye holiday mood bado.Ndio maana mwendo kidogo unakuwa taratibu ingawa sio kama wa kinyonga.Bahati nzuri hatubadiliki rangi pia.Tunajongea huku tukiandaa mambo makubwa zaidi kwa ajili ya mwaka ujao ambao kimsingi tunataka uwe mwaka wa BC!

Sikukuu ilikuwaje?Uliserebukia wapi?Mambo yalikwendaje?Tungependa kusikia kutoka kwako msomaji.Wakati unatafakari jinsi sikukuu ilivyokwenda,hatungependa kukuacha hivi hivi.Burudika na wimbo Ndoa Fungo la Imani kutoka kwa Bima Lee.Pata burudani

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Tumeshindwa kupata maelezo au caption ya hiyo picha.Unaweza kutusaidia?

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

18 Responses to “SIKUKUU ILIKUWAJE?”

  1. Comment by Majita on December 30th, 2008 5:08 pm

    BC athante ama avacha kwa kichina kwa hii picha na kupiga kimombo.Uwe una kandamiza bwana kiingilishi,si unajua ndo kimefanya mimi nikapewa Phd?????

    Caption ya picha iko hapo kwenye kufungua soda hapoooo.
    Yaani hapo ndo penyewe.Mengine tisa ila kumi hilo kopo lilivyoshikwa na kufunguliwa hope yataandikwa mengi.bwaaaaa hahahahah.
    Either Heri ya mwaka mpya ndg zangu woote hapa BC
    Dr.Majita

  2. Comment by hombiz on December 30th, 2008 6:20 pm

    joyous

  3. Comment by papuu on December 31st, 2008 12:02 am

    dah naona huyu mpoki anabonyeza kizenji.. mashallah

  4. Comment by Mattylda on December 31st, 2008 3:42 am

    mimi make up za mpoki ndo zinanimaliza khaaaaaaa!

    wishing u all a happy new year!

  5. Comment by viola on December 31st, 2008 4:16 am

    mbona mwashangaza watu na yote uloyasema ni kweli dhahiri

  6. Comment by DUNDA GALDEN on December 31st, 2008 5:05 am

    HOME SICK
    SIKUKUU ILIKUWA SAFI
    JÄTTE FIN SOM FAN

  7. Comment by rasto on December 31st, 2008 6:04 am

    bc jina la wimbo kama sijakosea ni Ndoa ni fungo la hiari.ni burudani safi la wana magnet tingisha.x-mas ilikuwa poa tu labda leo.all the best katika mwaka mpya wadu wote.iwe ya mafanikio mema na afya njema

  8. Comment by BLACKMANNEN on December 31st, 2008 4:11 pm

    “Roy”=Rweyemamu, niliwahi kuimba naye katika moja ya bendi za hapo Dar, ni mwimbaji mzuri sana. Aliiacha kidogo Bimalee na kujiunga nasi katika bendi yetu. Baada ya hapo alirudi tena Bimalee na alitunga na kuimba ule wimbo wa “Sophy”.

    Black=Blackmannen

  9. Comment by binti-mzuri on January 1st, 2009 9:18 am

    jamani blackmanen kumbe we musician.. i always knew there was something about you..tukumbukane basi lool

  10. Comment by FIFI on January 1st, 2009 10:17 am

    SKUKU ILIKUWA SAFIIIIIIIIIIIII SANA.
    NAWATAKIYA WANAINCI WOTE UYU MWAKA UWE WA KHERI NA AFYA NJEMA:

  11. Comment by Mattylda on January 2nd, 2009 3:14 am

    Blackmannen kumbe unaimba?safi sana kaka mimi natamani kuimba ila sina sauti ya kuimbia!

  12. Comment by angel jk on January 2nd, 2009 4:19 am

    huyo mpoki angebadili mekups coz watoto wanaogopa

  13. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on January 2nd, 2009 9:55 am

    hizo make-up zao zimeniacha mbavu sina…(teh teh teh…)….nakipenda saana kipindi chao hao mabwana…kuna wakti kulikuwa kunatokea kama coincidence hivi…kwani kila kipindi kikikaribia umeme unakatika….not sure if it was a black out in all places…or what…whether a planned one….not sure….ila nondo zao kali….wana ujumbe mzito kila wakati…lol

  14. Comment by bugi on January 2nd, 2009 10:53 am

    sikuku muhimu lakini tusije tukasahao sababu ya kuisherehekea

  15. Comment by cityboy on January 4th, 2009 12:01 am

    Mmmmm!! Mattylda wacha longo longo!!!nimekusia ukiimba kule uwani!!! unasauti nzuri bana!!!hahahaaaaa

  16. Comment by cityboy on January 4th, 2009 5:44 am

    Mattylda, yaaaaani ndo tuseme make up za Mpoki zimekua hoi bin taabani!!!, hahahahaaaaaa!!!!!

  17. Comment by Mattylda on January 5th, 2009 4:35 am

    Cityboy cityboy visa hivyo ninaimba uani kivipi??fafanua hahahahaha,nakwambia mimi make ups za mpoki sina usemi utadhani anataka kukata roho hahahahah!

  18. Comment by maggie on October 7th, 2009 2:44 pm

    yani iyo eye shadow umependeza

Leave a Reply