
Bila shaka unalikumbuka kundi maarufu la Hard Blasterz Crew(HBC).Hilo ni mojawapo ya makundi ambayo tunaweza kabisa kusema yalichangia kwa kiasi kikubwa kuuweka muziki wa kizazi kipya hapo ulipo.Sasa kuna habari njema ambazo zimeripotiwa na Full Shangwe kwamba huenda mwaka 2009 ukashuhudia kurudi kwa kundi hilo baada ya miaka kadhaa kutokuwepo hewani ingawa mwenzao Prof.Jay aliendelea na game kwa muda wote huu.
Kundi lile lilikuwa linaundwa na Joseph Haule aka Prof.Jay,Willy Shundi aka Big Willy na Terry aka Fanani lilikuwa na makazi yake maeneo ya Upanga jijini Dar-es-salaam.Tunawatakia kila la heri HardBlasterz.BC itaendelea kufuatilia maendeleo ya kuundwa upya kwa kundi hilo.
Pichani juu kutoka kushoto ni Big Willy,katikati ni Profesa Jay na kulia ni DJ Choka ambaye ni mmojawapo miongoni mwa producers wanaotarajiwa kuwatoa upya HBC.Kwa undani wa habari unaweza kubonyeza hapa.
Page 1 of 3 | Next page