
Mojawapo ya mambo mazuri ambayo yanatokea nchini Tanzania hivi leo ni kuibuliwa kwa vipaji mbalimbali miongoni mwa vijana na kitu kinachoitwa Tanzania House of Talent (THT).Kama umewahi kuhudhuria shughuli ambapo miongoni mwa watoa burudani walikuwa ni vijana wanaotokea THT bila shaka utakubaliana nasi tunaposema kwamba vipaji vipo nchini Tanzania.Kinachotakiwa ni uongozi na mikakati mizuri ya kuviboresha na kuvionyesha ulimwenguni.
Miongoni mwa vipaji vilivyowahi kuibuliwa na THT ni mwanadada Mwasiti(pichani).Msikilize hapa katika wimbo wake mpya uitwao Nalivua Pendo kwa kubonyeza hapo chini.Kazi nzuri Mwasiti!
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Page 1 of 3 | Next page