HAPPY WOMEN’S DAY

womens_day_greeting

Leo ni siku ya Wanawake Duniani(Women’s Day).Ni siku ambayo husheherekea mafanikio na mchango wa wanawake katika nyanja zote za maendeleo ya binadamu iwe ni kiuchumi,kijamii au kisiasa.Ni siku ambayo inatukumbusha sote umuhimu wa kipekee wa wanawake duniani.Hapa tunawazungumzia mama zetu,dada zetu,wake zetu,watoto wetu,shangazi zetu,binamu zetu,majirani zetu wanawake,marafiki zetu,maadui zetu nk.

Mwanamuziki maarufu kutoka nchini Marekani,James Brown, aliwahi kuimba “It’s A Man’s World but It Would Be Nothing Without a Woman”. Hilo halina ubishi.Dunia tuionayo leo kama dunia,inatokana na mchango mkubwa wa wanawake.Dunia si dunia bila mwanamke.Haipo.

BC inaungana na wote katika kusheherekea siku hii na pia kuwasihi wanawake,popote pale ulimwenguni, waendelee kufanya ambacho wamekuwa wakikifanya tangu mwanzo wa dunia hii.Happy Women’s Day.

Mtizame James Brown na Luciano Pavarotti hapo chini wakiimba Its A Man’s World.Mungu azilaze roho zao mahali pema.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Page 1 of 3 | Next page