chokinyotabc

Yupo mwanamuziki mmoja wa zamani kidogo aliwahi kuimba kwamba “wivu katika mapenzi ni lazima….japo kidooogo”. Alimaanisha kwamba wivu ni sehemu ya mapenzi ingawa pia aliashiria kwamba ukizidi unaweza kuwa kero na wakati mwingine kuleta balaa kabisa. Si ushasikia mtu kamchinja mwenzake kisa wivu?

Swali la kujiuliza ni je nini husababisha wivu? Ni kutojiamini,kupenda kumiliki kitu mwenyewe au ni kweli kwamba mapenzi ndio husababisha wivu?Na kama jibu ni ndio je hayo huwa mapenzi ya dhati au ndio tulivyo tu sisi wanadamu?

Huo ni upande mmoja.Upande wa pili ni kuhusu “mpenzi wa zamani”. Hivi watu wakishaachana bado huwa wanaachana kweli au huwa wanapeana nafasi? Na inakuwaje unapoona mpenzi wako wa sasa anaendeleza sana mawasiliano na mpenzi wake wa zamani? Ni sababu tosha ya kuwa na wivu?

Ali Choki akishirikiana na msanii Nyota Ndogo anayetokea nchini Kenya maeneo ya Mombasa(Naamini unamkumbuka kutoka katika kibao chake Watu na Viatu) wanaimba kuhusu mambo ya wapenzi wa zamani na “wivu”. Mmoja anakuwa haelewi,wivu unamtatiza.Mwenzake anamwambia tulia,usiwe na papara wala wasi,hakuna kitu. Mwenzake anamsihi kwamba asimfiche na ndio maana wimbo unaitwa Usinifiche. Mimi najiuliza;akiambiwa ukweli ataweza kuhimili? Can he handle the truth? Usikilize wimbo Usinifiche kwa kubonyeza player hapo chini.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Feedback / Comments

2 Responses to ““USINIFICHE”-ALI CHOKI ft NYOTA NDOGO”

  1. Comment by priscar on April 30th, 2009 11:29 am

    KAZI NZURI SANA. CHOKI BIG UP

  2. Comment by Vyne on May 1st, 2009 12:20 am

    when I heard choki na Nota nilikuwa nasubiri mashairi mazito dah kazi nzuri but could be longer than that hamjamalizia hadithi.

Leave a Reply