
Mshambuliaji hatari wa timu ya soka ya Yanga, Mrisho Ngassa hapo jana alijipatia “jiko”. Amemuoa Latifah Abdulhaman. Ndoa ilifungiwa huko Tabata Kisiwani.
Hivi karibuni Ngassa alikuwa nchini Uingereza kufanya majaribio ya kuchezea timu ya West Ham. Habari zinapasha kwamba sehemu ya kwanza ya majaribio hayo ilikwenda vizuri na kwamba kunako majaaliwa Ngassa atarejea tena nchini Uingereza kwa majaribio mengine.
BC inawatakia Mr.& Mrs Ngassa kila la kheri katika ndoa yao.
Photo/Michael Jamson via Charaz
Page 1 of 3 | Next page