Weekend ndio imewadia tena. Kama ulidhani wiki hii ingekuwa kavu kavu nchini Tanzania bila mikikimikiki basi ulikosea.Ilikuwa ni wiki ya “mipasho”. Ilikuwa ni rusha kombora nirushe kombora au kama vile alivyowahi kuimba Prof.Jay ukimwaga ugali mimi namwaga mboga!
Bahati nzuri ni kwamba nadhani watu wazima wamejiona ovyo na kuamua kufuata njia zinazostahili. Mchezo sasa umegeuka kuwa wa kudaiana “vijisenti”. Bila shaka umesikia mmoja kadai fidia ya Tshs Bilioni 10 huku mwingine akidai fidia ya Tsh 1 tu. Kama ingewezekana huenda angedai ile ya mkoloni kabisa iliyokuwa na tundu katikati. Sijui tugange yajayo au bado tuendelee na nguvu ya hoja,uchambuzi nk.
Tuyaache hayo.Leo ni burudani ya kale.Wenyewe mnaziita Zilipendwa. Natamani tungeziita Tunazozipenda kwani ukweli ni kwamba bado nyimbo hizi zina mafundisho kemkem na ni kama zilitungwa jana. Leo tunaye Gwiji Marijan Rajab(RIP). Wimbo unaitwa Ndoa ya Mateso. Binti karudi kwao.Anasema ndoa imemshinda.Mume anamtesa.Pesa zote anamalizia kwenye makuku ya kukaanga akiwa na “vimwana’ wake huko nje wakati familia inakufa kwa njaa.Binti hana msaada wowote,hana ndugu wala jamaa hapo alipo.Kwa masikitiko anauliza kwani kuolewa ni utumwa? Binti anaomba talaka yake.Mjumbe ndie anaombwa kuwa shahidi. Kwa uchungu na aibu anasimulia yaliyokuwa yanamsibu.Anataka kurudi nyumbani kwao kwani anasema hakuzaliwa juu ya miti bali ana kwao.Ana baba na mama. Mateso.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Pata burudani,pata ujumbe na furahia weekend yako. Maisha mafupi haya.
Feedback / Comments
7 Responses to ““NDOA YA MATESO”-MARIJANI RAJAB”
Leave a Reply


wimbo mzuri ila naomba kuuliza kwanini hawa kina marijani na mbaraka nyimbo zote za bendi zao walikua wanaimba wenyewe mwanzo mapaka mwisho hamna kupokezana ni kweli walika wabinafsi au? waliwabania chipukizi kwa kuogopa kufunikwa? vijana wa zamani hebu fafanueni hapa!
10th May 2009 once again it a big day for all types of “MOTHERS”
All whom we are or hope to be we owe to our “ANGELS” mother. Mother is the name in the lips and heart of all Childrens.
I thank my mama for being their for me
through out in my life and became whom I am today. You are a such wonderfully mama in this world the “EXEPTIONAL” gift that God has given me. There is no day of the year that you are not special for me mama. You are my “INSPIRATION” I love you mama with whole my HEART.
Wishing all the MOTHERS a HAPPY MOTHERS day with full of joy, and thank them for being their for us.
Have a nice week end all BC contributors + BC staff.
Take care………………!
Mr Degree,swali lako nzuri, Marijani kwanza alikua na sauti ya biashara,yaani yeye ndo ilikua Nyota ya bendi… n’takupa mfano wa Bob Marley alikua akiimba nyimbo zote za bendi akina Rita Marley wanaiitikia,Marijani pia akina Fresh Jumbe..
walikua wanafanya backing vocals ilikua sio ubinafsi ilikua ni nani katika group ataleta maketi ya BENDI
Umenikuna Jeff vilivyo,enzi hizi mambo yalikuwa du kinaa! kama sio Kimara Stop Over basi labda waungwana hawa walikuwa wakimvisha mtu kandambili mfuko wa nyuma Wami Bar Mwananyamala….ya kale kweli dhahabu.
Hi guys kutoka Helsinki
Kwa kweli mimi ni mpenzi na mshabiki wa nyimbo za zamani, content ya wimbo huu wa marijani unatukumbusha sisi wanaume tusiwatese wake zetu kwa sababu za ulevi wa pombe, na hii inakuja wakati tukikumbuka siku ya mama, mkeo ni mama wa watoto wako, sasa kwa nini unafanya mambo husingependa afanyiwe mama yako, asante marijani na pia asante BC, wadau weekend njema
Frateline
Sio siri Jeff ….”maisha ni mafupi”….you dont need anything under this sun to be happy and enjoy this shortest life.
Nimeburudika na wimbo, asante. Wadau wenzangu…(wale vijana wa zamani)…naona nanyi mmepata raha ya roho….
maisha mafunzo,musik ni skuli