makassybc

Naam. Wikiendi tena. Wakati wa burudani. Wakati wa vikao vya kiti kirefu,familia,harusi,ubatizo,ubarikio,mwali kutolewa ndani nk.Ni muda mwingine wa kupumzisha akili.Hata kama unafanya kazi weekend hii bila shaka utakubaliana nami kwamba hata huko mabarabarani hali huwa shwari. Zile vurugu za foleni,msururu wa watu nk huwa hakuna.Ukiitazama Samora Avenue unaweza kuona kutokea Askari Monument mpaka Clock Tower.Unabisha? Hebu jaribu uone.

Kikubwa wiki hii ni kwamba tumetimiza miaka miwili. Kwa maana hiyo bado tupo kwenye mauzamauza ya kufurahi,kujipongeza na katika semina elekezi ili kuweka mstakabali wa nini kinachofuata. Kwa upande mwingine umemsikia mwenyewe mkuu wa nchi.Anasema habari za uraia wa nchi mbili hazina budi kusubiri. Anasema wasomi wamemshauri kwamba mpango wa kula huku na kule sio mzuri. Mwenyewe akasita kuleta habari za “wivu”. Wakati huo huo mkuu anasema mjenge na kuwekeza “nyumbani”. Nyumbani tena? Sijui wewe unasemaje lakini mimi naona kazi kubwa bado ipo. Washauri wasomi najua wamenielewa. Kama hawajaelewa basi tena.

Turudi kwenye burudani kwani kama ujuavyo leo ni Ijumaa. Ni mambo ya sakayonsa. Mambo ya zilipendwa. Enzi zile ambapo ugonjwa ulikuwa ni mafua tu! Wimbo unaitwa Binadamu Hatosheki kutoka kwao Orchestra Makassy. Bila shaka utakubaliana na kina Mzee Makassy.Binadamu sijui umpe nini aridhike. Hivi kwanini tupo hivyo tulivyo? Kama wanavyoimba; ukimpa jua anataka mvua. Ukimpa mvua anataka jua!Kha. Ukimpenda sana anataka kuchukiwa na ndio maana atakuletea madharau,visa,vituko na visasi.Enewei,wasikilize mwenyewe Orchestra Makassy. Pata burudani na furahia weekend yako.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Subiri kidogo. Kwa sababu wikiendi hii tunaweza kusema ni wikiendi ya BC kwa maana ya kutimiza miaka miwili sidhani kama kuna ubaya kama tukiweka kibao kingine kama zawadi….sikiliza hapo chini;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Feedback / Comments

7 Responses to ““BINADAMU HATOSHEKI”-ORCHESTRA MAKASSY”

  1. Comment by Daily News About Wikis : A few links about Wikis - Thursday, 21 May 2009 20:02 on May 21st, 2009 11:05 pm

    [...] “BINADAMU HATOSHEKI”-ORCHESTRA MAKASSY [...]

  2. Comment by Peter on May 22nd, 2009 3:11 am

    kwa kweli bongo celebrity ni noma, nimekuwa nawafatilia sana na hasa hivi vibao mnavyotoa vya zamani vinanikumbusha sana, nyie ni noma, ningefurahi kama mnazo nyimbo za vijana jazi enzi za maneti na nyinginezo kama hizo hapo chini ningefurahi sana kupata

    ni
    Mfaume waniliza – DDC mlimani park

    Solemba – Juwata Jazz band

    Kipipa Ayubu – Dar international

    Jirani – Africa International

    Masikitiko – Tancut Almas

    Yaliyopita – Washirika stars

    Mwenyekiti mwalimu Nyerere – DDC

    Usinifinyie jicho – OSS

    Kimbunga kimenisonga – OSS

    Asia – Bima Lee

    Tulia mama – Bima Lee

    Dunia Haina siri – Bima lee

    Kwa mjomba – Urafiki Jazz

    Tutafunga ndoa Asmaha- Urafiki Jazz

    Barua nyingi nilikutumia- Western Jazz

    Ewe mpenzi Christina – Western Jazz

    Yamewafika wenzenu – Dar international

    Maneno mengi nimesikia – KIko kids

    Mimi Hanipati ng’o – Kiko kids

    Mwenzeni niko taabani – Western Jazz

    Mtoto wa Mjini – Masantula

    Hangaika – Masantula

    Gubu la mume – Vijana Jazz

    Shemeji – Vijana Jazz

    Bujumbura – Vijana Jazz

    Magaidi wa Msumbiji- Vijana Jazz

    Epuka Jambo lisilokuhusu – DDC

    Jiko Limenuna – Vijana Jazz

    Paulina – Dar international

    Milima ya kwetu – Orchestra super rainbow

    Ogopa tapeli – Vijana Jazz

    Natoa Onyo – Dr. Remmy

    watoto wamekuja juu – washirika stars

    Nalila masumanda – washirika stars

    Penzi la Ulaghai – washirika stars

    Nimebaki nashangaa – Washirika stars

    Kayumba- washirika stars

    Kisa- washirika stars

    Nyongise – Vijana Jazz

    Siri ya ndani – Vijana Jazz

    Heshima ya mtu – Vijana Jazz

    Malaine – Vijana Jazz

    Usicheze na bahari – Vijana Jazz

    VIP – Vijana Jazz

    Shoga – Vijana Jazz

    Ni Mashaka – Patrick Balisidya

    Zinduna – Zahoro Ally

    kama kawaida bongo celebrity, hebu tuburudishe na vibao hivyo

  3. Comment by chapombe on May 22nd, 2009 9:07 am

    mi naomba mniwekee kile kibao wanachoimba,bomu limeshapasuka wanguzi wanatapata,sijui wanaitaje ule wimbo na nisahau bendi pia,labda mnikumbushe kidogo

  4. Comment by chapombe on May 22nd, 2009 9:10 am

    i mean walanguzi

  5. Comment by KBC..Kwanza UNiT. on May 22nd, 2009 12:12 pm

    CLASSIC CLASSIC CLASSIC BONGO MUSIC

    Shukrani zimfikie Mzee makassy kwa miaka yoote aliyotuzawadia hii Muziki Munene..Hii SANTURI Inazunguka kila siku hapa Nyumbani Kwangu..Ilirecordiwa na Virgin records miaka ya Sabini..Maybe the 1st TZ Artist on a MAJOR LABEL??..

  6. Comment by Yoyoo on May 25th, 2009 4:12 pm

    Wow! It has been a while since I heard “Kasongo … Mobali na Ngai”! Inanikumbusha enzi hizo na vijana wa Bwiru/Sengerema katika visiwa vya Sanane – Those were the days, life was good, and love was plenty!! No sex, BUT real innocent Love! Thanks BC-:)

  7. Comment by Barrack Nyakundi. on December 4th, 2011 7:34 am

    Can i buy some of the mentioned music above.

Leave a Reply