uzeenibc

Katika maisha ya kawaida utakuwa hujakosea kabisa ukiwaita “vijana”.Lakini katika game la muziki ambao leo hii tunauita wa kizazi kipya,unaweza kabisa kuwaitwa “wakongwe”.Wamekuwepo toka enzi zileee…na bado wapo.

Si unakumbuka enzi zile Mr.II alipoanza muziki? Nina maana enzi zile alipokuwa akiitwa 2 Proud kabla hajawa Mr.II mpaka kufikia hapa alipo hivi leo ambapo tunamuita Sugu. Si unakumbuka enzi za Nigga Jay ambaye leo hii tunamuita Prof.Jay? Enzi zile akiwa na washikaji zake ndani ya Hard Blasterz. Na si unakumbuka alipoanzia MwanaFalsafa ambaye leo ukisema Binamu kila mtu anakuelewa unamuongelea nani?

Naam vichwa hivyo ndio vilivyoshirikiana katika wimbo huu uitwa Nazeeka Sasa. Wimbo umetengenezwa na Producer Hermy B. Sikiliza ujumbe uliomo kisha utoe maoni yako.Pata burudani.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Feedback / Comments

28 Responses to ““NAZEEKA SASA”-MwanaFA ft SUGU & PROF.JAY”

  1. Comment by Lukwilinga on June 1st, 2009 6:01 pm

    eeeeeehhh,haka kanyimbo ni balaa ndugu wananchi. hawa ni legends kweli sababu hata mashairi yao yamepangwa yakapangika,sio kama mashairi ya vijana wa siku hizi,unaweza ukasikia mtu anasema “baby” karibu nusu ya wimbo wote. Mwanafa kazi nzuri sana kaka pamoja na wenzako. na haka kakijana kalipewa tuzo ya uproducer bora tukahisi amependelewa lakini kusema ukweli hermy b is so talented and very creative. nafurahi kwa kazi zako nzuri sababu haujirudii kama wengine na karibu kila wimbo uliotoa unashika namba moja au kuwa gumzo miongoni mwetu. kazi nzuri hermy b tunategemea mengi zaidi kwako.

  2. Comment by kindamba on June 1st, 2009 6:44 pm

    sasa kama kuna m2 anabisha kuhusu ivi vichwa!!! basi anachuki binafsi awa ni wakali wabongo jamani!!!!! nani anabisha?????¿¿¿¿¿¿

  3. Comment by b87 on June 1st, 2009 6:56 pm

    Duh hawa jamaa walikua wanasubiri nini siku zote???Maana hivi vichwa ni noma vyote!!!Ebwana bonge la colabo si la kitoto!!

  4. Comment by kili on June 2nd, 2009 3:41 am

    imekaa poa hiyo

  5. Comment by Nas on June 2nd, 2009 6:02 am

    Tune limetulia sema inaonekana kama ni Diss kiaina….na Colabo limetulia kwani wote wakali, Ila naona jimbo liko kimaugomvi ugomvi tu

  6. Comment by Nas on June 2nd, 2009 9:51 am

    Ebwana nimelisikiliza tena ili tune, ucpme kwenye mziki mnee ni full Bang ebwana yani ivi vichwa vitatu vime smash mazima
    (3HEADS SMASHER)

  7. Comment by b87 on June 2nd, 2009 11:45 am

    Duh Sugu jamaa walikua wanadhani umezeeka!!!Kumbe mzee bado unaongeza mzuka.Bado unakula kuku na M kwako kama book!!!Hahaha waambie mkuu!!!
    Uwiii…FA ni zaidi ya mtambo!!!Huyu ni kaka mkubwa bwana msibishane wadogo zake!!!Kusoma hawajui basi hata picha jamani hawaoni??Nashangaa!!!Wanavaa saa na hajui kuisoma…Ni wa pumbavu haswaaa!!!Achana na Makenge kama kina Inspectar…Waone wajinga tu waliokubali kua nguruwe then wanaomba mabawa!!!Hhehee!!!Prof,mzee wa mitulinga;Mkali wa rymes!!!Walisahau kua uzi unafuata sindano hawo!!!Wakitaka kujua umuhimu wa matako na wajaribu kukalia kichwa tuwaone!!!
    Hili fataki ni noma wazazi!!!Asiekubali akapimwe akili!!

  8. Comment by jongo on June 2nd, 2009 12:00 pm

    Ni kweli hawa jamaa wanazeeka sasa,hawatanii..

  9. Comment by badu on June 2nd, 2009 1:44 pm

    hili dude ni la kisawasawa sana.watu wazima wameamua kufanya kweli naona,hongereni sana

  10. Comment by ezekiel on June 2nd, 2009 3:55 pm

    duuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,yani jamani wengine mlikaaa redioni mkawa mnabishana kua uyu dogo Hame B wamempendelea? we marco wewe, mi naona ubishi unaoleta ni kama unataka ngono gesti afu umesahau uume home. we lamar ndo ukacheze marede na makahaba wa kino. Bitz zako zinajirudia kila kukichaa. Dnt hate jamani,diz guyz wanafanya kazi. Ivi F.A c yupo nje amerekodi vp? teknolojia bwana. Jize umeipa nyimbo maisha kiukweli na supu yako ya dafu. F.A naona wimbo umehakikisha ni wako, u murdered the minits u got.BY th way kuna m2 anaitwa manecky anajiita produza, hebu nenda kaombe lebo kwa hame B kama msanii labda atakufundisha production. co mnakaa na mapimbi wenzako kina pingu na desso mnarekodi utumbo afu mnakibilia kushoot video mjilambe midomo kama warembo wa kike wakati ni pumba tupu.Kama mmeshindwa kufanya hii ki2, tengezeni vigari mtembeze tepu na cd. Shwine Nyie

  11. Comment by mark on June 2nd, 2009 6:54 pm

    Mimi sio mpinzani wala hater ila kawa wanajiona wanazeeka wakae pembeni au watafute shughuli nyingine ,kwa mfano producer sugu sikaoa marekani mwan fa vipi masomo jay kwanini usimpe nafasi black chata ,anyway nimesikiliza nyimbo yakawaida sana wanajisifia sijasikia ujumbe wa maana mafumbo ndio mengi ikuwapi watetezi wa wanyonge mimi nafikiri hiphop ni watetezi wa wanyonge na maisha thug ya mtaani sio mill kama buku nguruwe mabawa au matako kichwa ,my opinion i ddnt feelng this trak lakini labda ni mimi,mdau wa wanyonge

  12. Comment by Adelyn on June 2nd, 2009 7:49 pm

    Whoever is the producer ni nomaaaaa. siamini mziki wa kibongo ukawa na quality hivi. i am so amazed. again whoever produced it amefanya kazi nzuri. I am going to put this in my playlist for a very longtime. Natamani sana kurudi nyumbani kwa kweli. I love this song.

  13. Comment by Bob Sambeke on June 2nd, 2009 8:01 pm

    E bwana uCPME M2 WNG C MCHEZO TRAK LIMESTAND
    KINOMA FATHER ANGU! c UNAJUA SUGU HATA ASIPOIMBA DILI ZAKE NI MILLION NDO MAANA ANKWAMBIA MILLION KWAKE NI KAMA BUKU! C MCHEZO BABA! FA-BINAMU-B:UNATISHA BRO KAMUA
    TU KAMA M2 ANAWEZA AKUDISS KAMA INSPECTOR NDO ATAJUA WHO IS THE DON? HEAVY WEIGHT MC
    UNATISHA BABA! KWELI NI MA-LEGENDS KATIKA FANI….NA WEWE JONGO WANAVYOKWAMBIA WAMEZEEKA WANAMAANISHA WAMEKOMAA KTK FANI!

    IT’S ME BOB SAMBEKE-YOUNG MILLIONAIRE

  14. Comment by Jsixty on June 3rd, 2009 3:08 am

    Safi watu wazima kazi nzuri sana, inapendeza kuteam up ili kuongeza ladha kwenye game wazee keep it up guyz

  15. Comment by Boss Mtoto on June 3rd, 2009 4:39 am

    Eee bwana sasa mziki wa bongo unaelekea kwenye level nyingine, Hermy B hapo kichwa umekitumia haswaa ipasavyo, na hii colabo kweli si ya kitoto, FA, Jize na Sugu!!anaebisha lazima ni hater, nafikiri Mark hapo juu is one of them, if not basi hauelewi wimbo wenyewe, lakini kama kusoma huwezi hata picha huioni? Big up sana FA, they should hate you more cause unazidi kuwaacha mbali katika kila nyanja…..”pumbavu haswaaaaaaaa”

  16. Comment by Sajjo on June 3rd, 2009 4:51 am

    All has been said. Track imesimama yaani Hermy kanyonga Beat mbaya halafu hawa three legends wakakandamiza kiukweli. Mark u need to understand hip hop kabla ya kutoa such lame comments! Unaongelea RHYO na Jizze ni sawa na mtu una watoto darasa la tano na la saba na just coz wa la saba got brains unataka amuachie mwenzake? Sugu kuoa na habari hapa hazihusiani na this track.

    Hip ni majigambo na mafumbo. Unatakiwa uwe mwerevu kuyafumbua maama hufumbiwa wajinga. Jicheki Mark uone kama u mjinga ama mwerevu. This z my fav track yaani been at it toka juzi..! Big up Homiez.

  17. Comment by mac carlos on June 3rd, 2009 5:11 am

    kibokooo

  18. Comment by kanyelamomo on June 3rd, 2009 1:08 pm

    uuuuuuuuuuuuuuuuuwi! Vijana mmedinda!Hamjapotelea hewani kama dege la ufaransa!

  19. Comment by akihito on June 3rd, 2009 3:55 pm

    duh!
    hawa jamaa wametulia sana..ujumbe unaeleweka kabisaa kuwa wapo juu,wengine wanafuata..ninapoongelea wengine nina maana wote wasiokuwepo kwenye nyimbo hii! wao sio tu kwa kuimba bali pia ni wakongwe kabisa..anayebisha basi aangalie hata picha ,sio kwa kubadilisha majina tu bali picha pia zinasomeka vyema…for haters..keep on hating,once u hate,u make them think different way to change ur opinion so we will still have more good to come..aight!

  20. Comment by Kindo on June 4th, 2009 2:39 am

    Nawapa hongera wote Sugu, Mwana FA, Prof. J, na Hermy B kazi ni nzuri.

    Muziki ni mchanganyiko wa ujumbe na melody. Haijalishi kama ni mafumbo,sifa au utetezi wa wanyonge vyote ni kheri mradi ujumbe unafika, unaeleweka na umepangangiliwa vizuri bila kashfa au matusi. Mimi sioni tatizo kuhusu wimbo huu, mashairi ni mazuri, vina vinamiminika na melody haichushi. Big up!

  21. Comment by bingo on June 4th, 2009 2:58 am

    kwa nini hamkumshirikisha sister P??

  22. Comment by Danila on June 4th, 2009 3:13 am

    ucpime kama unabisha kalia kichwa ndio utaona umuhimu wa makalio hahahhahahahaahha
    mko juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

  23. Comment by Bonta on June 5th, 2009 7:28 am

    Hii ni fulanaz ya Michuzi.

  24. Comment by chitalula on June 5th, 2009 5:46 pm

    da mzuka sana,track imesimmama sana…..!!ujumbe nmeukubali,ni wa wazee kimuzik ila bado wanashaini kwenye game.FA umepatia sana kuwapa shavu jizze for prof na sugu
    wasanii wachanga mliheshimu game ‘hao ndo waliwashawishi baba zenu ili nanyi muimbe’
    angalieni hamuwezi mkakwea mnazi ili mgeme SUPU,hahaa ni noma..!!
    acyeipenda hii bila shaka naye ni mabana pua,hip 2 hipohop daima

  25. Comment by kika on June 5th, 2009 11:55 pm

    download hii nyimbo bure http://www.shwari.com ,halafu
    nenda ktk link ya download

  26. Comment by juma on June 6th, 2009 8:58 am

    ebwana cyo mchezo m kuwa bok.mr 2?

  27. Comment by juma on June 6th, 2009 9:01 am

    ivi prof jay ulikuwa unawajibu kikosi au?

  28. Comment by lady s on June 14th, 2009 3:40 pm

    KWELI MMEZEEKA, LAKINI BADO MPO. LOVE THE SONG.

Leave a Reply