Muimbaji nyota wa nyimbo za Injili Tanzania mwenye album za JIPE MOYO, UNIFICHE, FURAHA YAKO,Flora Mbasha pichani (akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha) ambapo kwa sasa anasikika na wimbo wake wa WANAWAKE ulioimbwa katika mahadhi ya mchiriku,ndiye msanii pekee wa muziki wa Injili atakayetumbuiza kwenye tamasha la uzinduzi wa album ya MSETO WA WAHAPAHAPA litakalofanyika Juni 7 2009 viwanja vya Coco Beach, mbali na yeye kushiriki tamasha hilo, waimbaji wengine watakaokuwepo kwenye tamasha hilo ni pamoja na Mzee Yusuph (Muimbaji wa Taarabu kutoka kundi la Jahaz Modern Taarab) Banana Zoro (kutokana B-Band), Enika (Muziki wa kizazi kipya) Calora Kinasha na Wahapahapa Band watatumbuiza kwa siku hiyo.
Pia WAHAPAHAPA ni tamthilia ya mchezo unaosikika kila jumatatu kwenye Radio Free Africa (RFA) na Radio One, lengo lao likiwa ni kuangalia athari za VVU/UKIMWI kwa vijana.
Page 1 of 3 | Next page
