
Wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakiwajibika wakati wa uzinduzi wa Dar-es-salaam.

Safu ya wanenguaji wa kiume wakiwa kazini.
Bendi maarufu ya muziki wa dansi nchini Tanzania, African Stars au maarufu kama Twanga Pepeta, majuzi walizindua albamu nyingine ambayo ni ya kumi tangu bendi hiyo ianze kuwapa burudani wapenzi wa muziki. Albamu hii wameipa jina Mwana-Dar-es-salaam. Sijajua kwanini wameipa jina hilo lakini nahisi ni kutokana na ukweli kwamba kwa muda sasa Twanga Pepeta wamekuwa wafalme wa burudani hususani jijini Dar-es-salaam yalipo makao yao makuu.Hongera Twanga Pepeta.
Lakini wakati albamu zinazinduliwa,muziki unakonga roho,watu wanaburudika yapo maswali ambayo baadhi ya watu wamekuwa wakiuliza. Tumeona nasi tuyalete hapa ili kama kawaida kila mtu atoe maoni au mapendekezo yake; Swali la kwanza ambalo lilianzia pale kwa Michuzi JR linauliza Eti Ni Kwanini Madensa Wengi wa Kibongo Wana Vitambi? Unaweza kusoma post hiyo na maoni yaliyotolewa kwa kubonyeza hapa. Kabla mada hiyo haijatulia msomaji wetu mmoja akatutumia e-mail akihoji kwanini wanenguaji wa kike huwa wanapenda kuvaa “nusu uchi” wakati wenzao wa kiume wakiwa wameficha karibu kila sehemu ya miili yao?
Kwa sababu tunaamini kwamba sisi hapa BC hatuwezi kuwa na majibu ya kutosheleza,hatuna budi kuomba msaada kutoka kwako msomaji.Unasemaje?Eti ni kwanini? Picha za hapo juu zikusaidie katika majibu.
Picha zote kwa hisani ya Charahani.
Feedback / Comments
10 Responses to “UZINDUZI WA TWANGA PEPETA + SWALI KWA JAMII”
Leave a Reply


sending...
Maswali Rahisi kabisa;
1: Ktk Jamii yetu Bongo Kitambi ni dalili ya afya, Pesa, Heshima kwa watu, nirahisi hata kupewa mkopo…hata mimi ninacho
2: Wanenguaji wasipovaa nusu uchi, watu wachache wataingia kwenye shoo, Show hazitalipa tena, hata bia hazitanyweka sawasawa.
3. Swali juu ya Swali:…Kwa nini wanapotaka kupata “miss” katika ngazi yeyote lazima kuna hatua apite amevaa “Bikini”/chupi tu? huwa majaji wanaangalia nini hapo? inamaana akivaa nguo inayofunika mwili hawatauona uzuri wake?
Ni uzazi wa kila leo jamani, halo halo teh teh!!
BC bwana ina maana hujui kuwa biashara matangazo?
Sasa mimi nauliza swali, hiyo biashara ni kwa wanawake na matangazo ni kwa wanawake tu au vipi? manake hii imekaje, wanaume wamevaa vizuri nguo za kujisiri hata vitambi vyao wamevificha.
Ni aibu kubwa sana kwa hawa wadada kutokana na mavazi yao, kwa mtazamo wangu hao wanenguaji wa kike wao wenyewe wanafurahia hayo mavazi coz hapo hakuna mtoto mdogo ambaye ameshikiwa fimbo au amelazimishwa kuvaa nusu uchi.
Cheki hapo na hivyo vitambi vyao kama vya chibuku ovyoooooooo!!!!!!!!
semeni ukweli wanawake wanatangaza biashara ndiyo maana wanavaa nusu uchi,kama wazaramo wasemavyo “wewe binti mbona unakalia uchumi hakuna kula hapa nyumbani kama hauleti chumvi” wenye akili wameisha jua, hata kuna msemo wa kizungu unasema “women have powers between their legs” lakini wanaume wanavaa nguo zinafunika mwili mzima maana wao ndiyo wateja wanunua biashara zinazotangazwa na wanawake yaani k
Wabongo Bana Kweli M`mechoka kwanini msijadiliane mambo ya maana,Hizo ni evolution tu…Je dunia ingekuwa kama zamani ungesema nini sasa..wakati babu ya Babu yako anajifunika Mbele tu na mwili wote upo wazi….Kuhusu Vitambi ni michipsi Mixer Bia wanakula mazoezi hawana
hivyo vifreza ni vya beere na miviazi na mikuku
I recommend this ladies do some crunches.
nitasema wanawake wavue nguo na kucheza na bikini kwasababu inaleta jambo le ku atttract watu na kunywa pombe freshi na wazidishe kitambi kwasababu ya kuitigisha no kuleta dumu asante. i love u