iluminata2009bc

Kama kuna mashindano ya urembo ya kimataifa ambayo Tanzania inaweza kujivunia bila shaka ni mashindano ya Miss Universe. Bila shaka bado tunakumbuka jinsi mrembo Flaviana Matata alivyoipeperusha vyema bendera ya Tanzania huko nchini Mexico mwaka 2007. Flaviana sio tu alishika mojawapo ya nafasi za juu bali style yake ya kuwa “mrembo mwenye upara” ilikuwa gumzo la dunia nzima kitu ambacho kwa namna yake kiliitangaza sana Tanzania.Kila mtu alikuwa akitaka kujua yule mrembo mwenye upara anatokea nchini gani? Jibu walilipata.

Mashindano ya mwaka huu yanatarajiwa kufanyika tarehe 23 August huko katika visiwa vya Atlantis Paradise ndani ya Nassau,Bahamas.Jumla ya warembo 84 wanatarajiwa kushiriki mashindano ya mwaka huu.

Tumaini letu na mwakilishi wetu huko ni binti unayemuona pichani. Anaitwa Illuminata James Wize. Bila shaka tayari waandaaji wa Miss Universe Tanzania walio chini ya uongozi hodari wa Maria Sarungi tayari wameshaanza maandalizi makali ili kuhakikisha kwamba kwa mara nyingine tena Tanzania inakwenda kushindana na sio kushiriki.BC inamtakia kila la kheri Illuminata James.

Page 1 of 3 | Next page