MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

nasma-khamisbcMwimbaji maarufu wa muziki wa mwambao(taarab) nchini Tanzania,Bi.Nasma Khamis Kidogo,amefariki dunia. Kwa mujibu wa gazeti la Habari Leo,Bi.Nasma alifariki dunia usiku wa kuamkia juzi kutokana na ugonjwa wa malaria. Vyombo vingine mbalimbali vya habari vimeripoti kwamba Bi.Nasma ameiaga dunia kutokana na ugonjwa wa moyo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu.

Kifo cha Nasma ni pigo kubwa kwa ulimwengu wa taarab.Ilikuwa ni Bi.Nasma na shoga yake Khadija Omar Kopa ambao waliifanya taarab kupendwa zaidi hususani walipoanzisha style iliyokuja kujulikana kote Afrika Mashariki kama “mipasho”. Hapo ndipo nyimbo zake kama Taarab Iko Huku na Salamu la Michelini zilipokuwa gumzo na kivutio cha kila sikio.

Mojawapo ya nyimbo zake ambazo pia zilipendwa ni ule ulioitwa Mwanamke Mazingira. Usikilize hapo chini..Pole kwa ndugu,jamaa,marafiki na wapenzi wote wa sanaa na muziki popote pale ulimwenguni.Pumzika Kwa Amani Bi.Nasma Khamis Kidogo!

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

11 Responses to “PUMZIKA KWA AMANI BI.NASMA KHAMIS KIDOGO”

  1. Comment by Vyne on June 22nd, 2009 11:53 pm

    Jamani enzi zile za kidudu mtu mh! Nilikuwa si kurembua macho kumuiga mama Nasma. Kweli walifanya taarabu iwe tamuuuuuuuuuuu.Pumzika kwa amani Nasma.

  2. Comment by SaLaMa on June 23rd, 2009 4:15 am

    INNA LILAHI WAINA LILAHI RAJUUUNI KILA NAFSI LAZIMA IONJE UMAUTI MOLA AIWEKE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU AMINA INSHALLAH

  3. Comment by munira on June 23rd, 2009 5:48 am

    Pumzika kwa amani kwani kila mtu ataonja mauti na kila mtu ana siku yake.

  4. Comment by zaina on June 23rd, 2009 12:34 pm

    Tumetoka kwake na kwake tutarejea, mwenyezimungu akuondolee adhabu ya kaburi. amin
    Kifo cha nasma kimeniuma sana ! masikini, pumzika salama kwani mbele yako nyuma yetu sisi.

  5. Comment by Moinnan on June 24th, 2009 5:37 am

    Mungu ampumzishe mpendwa wetu Nasma kwa amani,raha ya milele umpe ee bwana. PENGO LAKE HALITOZIBIKA… Jamani Khadija Kopa utajibishana na nani ikaleta raha kama ilivyokua zamani na Mpendwa wetu Mamaa Nasma Hamisi Kidogo. REST IN PEACE MY MOM.

  6. Comment by halima on June 24th, 2009 7:49 am

    Bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe

  7. Comment by Mwanamke wa Shoka (UK) on June 24th, 2009 4:07 pm

    R.I. P. Nasma
    We are missing you already.

    My condolences to the bereaved family and friends.

  8. Comment by Dinah on June 24th, 2009 4:49 pm

    Pumzika kwa amani Mama Nasma.

  9. Comment by LYDIA on June 26th, 2009 6:15 am

    Pole sana kwa msiba ulio wapata.

  10. Comment by Amoro on June 29th, 2009 12:54 pm

    Hili ni pigo kubwa kwa wanataarabu kote ulimwenguni.

  11. Comment by ismail mohamedy on July 3rd, 2009 11:08 am

    walah imeniuma sana kweli binadanu cki2 mungu amuondole athabu ya kaburi na sisi sote amin

Leave a Reply