Mwimbaji maarufu wa muziki wa mwambao(taarab) nchini Tanzania,Bi.Nasma Khamis Kidogo,amefariki dunia. Kwa mujibu wa gazeti la Habari Leo,Bi.Nasma alifariki dunia usiku wa kuamkia juzi kutokana na ugonjwa wa malaria. Vyombo vingine mbalimbali vya habari vimeripoti kwamba Bi.Nasma ameiaga dunia kutokana na ugonjwa wa moyo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu.
Kifo cha Nasma ni pigo kubwa kwa ulimwengu wa taarab.Ilikuwa ni Bi.Nasma na shoga yake Khadija Omar Kopa ambao waliifanya taarab kupendwa zaidi hususani walipoanzisha style iliyokuja kujulikana kote Afrika Mashariki kama “mipasho”. Hapo ndipo nyimbo zake kama Taarab Iko Huku na Salamu la Michelini zilipokuwa gumzo na kivutio cha kila sikio.
Mojawapo ya nyimbo zake ambazo pia zilipendwa ni ule ulioitwa Mwanamke Mazingira. Usikilize hapo chini..Pole kwa ndugu,jamaa,marafiki na wapenzi wote wa sanaa na muziki popote pale ulimwenguni.Pumzika Kwa Amani Bi.Nasma Khamis Kidogo!
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Feedback / Comments
11 Responses to “PUMZIKA KWA AMANI BI.NASMA KHAMIS KIDOGO”
Leave a Reply


Jamani enzi zile za kidudu mtu mh! Nilikuwa si kurembua macho kumuiga mama Nasma. Kweli walifanya taarabu iwe tamuuuuuuuuuuu.Pumzika kwa amani Nasma.
INNA LILAHI WAINA LILAHI RAJUUUNI KILA NAFSI LAZIMA IONJE UMAUTI MOLA AIWEKE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU AMINA INSHALLAH
Pumzika kwa amani kwani kila mtu ataonja mauti na kila mtu ana siku yake.
Tumetoka kwake na kwake tutarejea, mwenyezimungu akuondolee adhabu ya kaburi. amin
Kifo cha nasma kimeniuma sana ! masikini, pumzika salama kwani mbele yako nyuma yetu sisi.
Mungu ampumzishe mpendwa wetu Nasma kwa amani,raha ya milele umpe ee bwana. PENGO LAKE HALITOZIBIKA… Jamani Khadija Kopa utajibishana na nani ikaleta raha kama ilivyokua zamani na Mpendwa wetu Mamaa Nasma Hamisi Kidogo. REST IN PEACE MY MOM.
Bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe
R.I. P. Nasma
We are missing you already.
My condolences to the bereaved family and friends.
Pumzika kwa amani Mama Nasma.
Pole sana kwa msiba ulio wapata.
Hili ni pigo kubwa kwa wanataarabu kote ulimwenguni.
walah imeniuma sana kweli binadanu cki2 mungu amuondole athabu ya kaburi na sisi sote amin